Kilichotokea Kateshi, Hanang kitatokea tena Same na vitongoji vyake mara nyingine. Msije kushangaa

Tomaa Mireni

JF-Expert Member
Sep 8, 2015
2,330
2,283
Kwanza nawapa pole wote waliokumbwa na janga lililotokea wilaya ya Hanang mji mdogo wa Kateshi.

Jambo la kujiuliza tutaendelea na majanga ya aina hii mpaka lini kwanini hatujifunzi? Mwaka 2009 lilitokea janga kama hili kule Same. www.jamiiforums.com/threads/wafariki-kwa-kufunikwa-na-mlima-same.44706/%3famp=1
Serikali ilitoa rambirambi na mambo yakapita, sasa ni Kateshi, serikali imefanya mengi sana pia litapita.

Je ni mwisho? Hapana ukiangalia kwenye milima ya Same kuna ujenzi mwingi sana holela, hivi mtu unajenga juu ya mlima au kando ya mlima maeneo yameisha? Kwanini wanadamu wana sahau mapema hivi? Serikali iko wapi?

IMG_20230110_205335.jpg

Picha ya milima ya Same wakati wa usiku

Kosa si kosa, kosa kurudia kosa, serikali ichukue hatua sasa, ipime viwanja vya kutosha kila mji kila mtu anaetaka kujenga ajenge sehemu iliyopimwa na kuepukana na majanga haya.

Kawaida ya udongo ukiloa sana ni rahisi kumong'onyoka, kwa hiyo lazma ulete madhara kama kuna makaazi ya watu karibu.

Serikali iangalie sana hili.
 
Kwanza nawapa pole wote waliokumbwa na janga lililotokea wilaya ya Hanang mji mdogo wa Kateshi.

Jambo la kujiuliza tutaendelea na majanga ya aina hii mpaka lini kwanini hatujifunzi? Mwaka 2009 lilitokea janga kama hili kule Same. www.jamiiforums.com/threads/wafariki-kwa-kufunikwa-na-mlima-same.44706/%3famp=1
Serikali ilitoa rambirambi na mambo yakapita, sasa ni Kateshi, serikali imefanya mengi sana pia litapita.

Je ni mwisho? Hapana ukiangalia kwenye milima ya Same kuna ujenzi mwingi sana holela, hivi mtu unajenga juu ya mlima au kando ya mlima maeneo yameisha? Kwanini wanadamu wana sahau mapema hivi? Serikali iko wapi?

View attachment 2834793
Picha ya milima ya Same wakati wa usiku

Kosa si kosa, kosa kurudia kosa, serikali ichukue hatua sasa, ipime viwanja vya kutosha kila mji kila mtu anaetaka kujenga ajenge sehemu iliyopimwa na kuepukana na majanga haya.

Kawaida ya udongo ukiloa sana ni rahisi kumong'onyoka, kwa hiyo lazma ulete madhara kama kuna makaazi ya watu karibu.

Serikali iangalie sana hili.
Kuna maeneo mengi sana yatakumbw na kadhia.

Ninakumbuka mafuriko ya Isaka watu washasahau na washaanza Tena kujenga kwenye mkondo ule ule.

Changamoto hizi zitafika maeneo mengi sana ya miji yetu,.kwasababu Kuna kakiburi tumevishana wananchi kujiba uhuru uliopitiliza.

Ukiwaambia watu wahame maeneo hatarishi NGO zote na wanasheria uchwara watakutweet mpaka uhisi Kuna mahali unakosea.

Kikubwa sheria Na. 8, Cap 114 ya mwaka 2007 iwe in full effect. Wataalamu wa mipango miji wasimamie kweli shughuli za uendelezaji miji.

Wazitingie kanuni zote ikiwemo Kuona namna Gani makosa yake.yanaweza kuwa enforced. Kwa Sasa wanasiasa wanachukua kura kwa kuwaning'iniza watu kwenye milima na mabondeni ..ikija kadhia wanatoweka sawa na wanasheria uchwara (bush lawyers).

Hili tusaidiane kuelimishana, wananchi wote wuJue kesho ni ya kwao, wawekekze kw tahadhari na kwa namna ambayo majanga kama haya yatawaaacha salama.
 
Huwa napita miji mingi nchini yenye miamba ya mawe mengi, unakuta kuna mawe makubwa yalimeguka yakaangukia juu ya mawe menzake yakawa yamebebana na mengine ni kitisho huku chini ya mawe hayo wananchi wamejenga makazi. Je ikitokea tetemeko la ardhi lenye kipimo kikubwa cha ritcha na kusababisha mawe hayo kudondoka chini na kuangamiza makazi ya watu nani atalaumiwa? Mawe yanatisha huku watu wako chini yake wanaishi bila wasiwasi
 
Huwa napita miji mingi nchini yenye miamba ya mawe mingi, unakuta kuna mawe makubwa yalimeguka yakaangukia juu ya mawe menzake yakawa yamebebana na mengine ni kitisho huku chini ya mawe hayo wananchi wamejenga makazi. Je ikitokea tetemeko la ardhi lenye kipimo kikubwa cha ritcha na kusababisha mawe hayo kudondoka chini na kuangamiza makazi ya watu nani atalaumiwa? Mawe yanatisha huku watu wako chini yake wanaishi bila wasiwasi
Asee mkuu ww acha tu, wakaazi na serikali wote wakulaumiwa
 
Hayo majina ni Sudan Kusini, Somalia au Bongo maana nasikia tu Kotesh sijui Hanang mboni yamekaa kiSudan?
 
Lushoto hakuna ujenzi holela kwenye milima yao
Landslide na mudflow haisababishwi na ujenzi holela ni natural phenomenon jaribu kuwa makini na aina ya mada inayoongelewa.
However watu wa lushoto wako vulnerable na majanga kama haya sababu ya geography ya pale
 
Back
Top Bottom