Kila mwaka tunaazimisha siku ya madaraka ya Rais. Je, hiki ni kipaumbele kipya?

Msanii

Platinum Member
Jul 4, 2007
22,606
29,754
Kila mwaka tangu mpendwa wetu ashike madaraka ya uraisi kumekuwa na maadhimisho ya kuazimisha madaraka yake.

Je, haya mabango, matangazo kwenye vyombo vya habari, Makongamano na dhifa zinazoandaliwa zipo kwenye bajeti ya serikali au kuna wafadhili wenye moyo mwema wanaochangia gharama za maadhimisho haya?

Tunasikia orodha ndefu zinatajwa za aliyoyafanya ambapo mengi hayaonekaniki kwa macho bali tunalazimishwa kwenye orodha kuwa yamefanyika na utukufu unaenda kwake. Ina maana Watanzania hawana taarifa ama ufahamu wa nchi yao? Je, aliapishwa madarakani ili akae tu na asifanye lolote kiasi kwamba akifanya hata jambo dogo zitatumika gharama kubwa kulitangaza?

Tumeshuhudia misafara mikubwa ya watendaji waandamizi wa serikali kwenda kuzindua matundu ya vyoo na kadhalika ambapo gharama za masurufu ya misafara hiyo zingetisha kupunguza vifo vya mama na mtoto wanaokosa tiba bora hususani kipindi hiki ambacho dada Ummy ameshikilia ofisi ya Afya.

Wakati tunakumbuka mema na mabaya ya Hayati JPM, kinachofuatia na kinafanywa kwa nguvu kubwa ni kuadhimisha miaka kadhaa ya utawala wa mama. Ninaomba kuelimishwa haya
  1. Umuhimu wake
  2. Taifa linapata tija gani kwenye hizi kumbukizi?
  3. Ni utekelezaji wa ilani?
Inawezekana tunaohoji labda hatuna hoja za msingi, basi wenye uelewa na hili jambo mtuelimishe labda tutaungamkono juhudi.
 
Na wanachotupendea ni kwamba tunaishiaga kulalama au kujihoji pembeni tu halafu tunaendelea na mambo yetu. 🤣 kichwa cha mwendawazimu n maiti
 
Hivi kwani hatuwezi kuungana wana jamii forums wote tunaopinga madudu ya gavoo tukaenda kuwapindua.

Au ndo sie akina keyboard warriors chini ya mwamvuli wa anonymity.
 
Hivi kwani hatuwezi kuungana wana jamii forums wote tunaopinga madudu ya gavoo tukaenda kuwapindua.

Au ndo sie akina keyboard warriors chini ya mwamvuli wa anonymity.
Kufanya kosa hakurekebishi makosa ya awali....

Tunawaondoa kwa sanduku la kura na kuirejesha nchi kwenye misingi yake
 
Kufanya kosa hakurekebishi makosa ya awali....

Tunawaondoa kwa sanduku la kura na kuirejesha nchi kwenye misingi yake
Unafikiri ni rahisi kuuondoa uongozi wa kidhalimu madarakani uliojichimbia mizizi kwa njia hiyo ambayo kila siku mnashindwa kwayo??
 
Unafikiri ni rahisi kuuondoa uongozi wa kidhalimu madarakani uliojichimbia mizizi kwa njia hiyo ambayo kila siku mnashindwa kwayo??
Kizazi hiki tunachoishi sisi hatutaweza na tusitarajie. Tunaweka misingi ya wajukuu zetu kuja kufanya mabadiliko
 
Kizazi hiki tunachoishi sisi hatutaweza na tusitarajie. Tunaweka misingi ya wajukuu zetu kuja kufanya mabadiliko
Asante kwa jibu lenye mwanga.

Kumbe kinachotakiwa ni kuwekeza katika kizazi kichanga ili wao waje kuwa wasahihishaji wa makosa yakiyokwisha kufanya na mababu zao.

Kama wameshindwa kuwa na huruma na kizazi hiki basi wakihurumie hata kizazi kinachofuata.
 
Kila mwaka tangu mpendwa wetu ashike madaraka ya uraisi kumekuwa na maadhimisho ya kuazimisha madaraka yake.

Je, haya mabango, matangazo kwenye vyombo vya habari, Makongamano na dhifa zinazoandaliwa zipo kwenye bajeti ya serikali au kuna wafadhili wenye moyo mwema wanaochangia gharama za maadhimisho haya? Tunasikia orodha ndefu zinatajwa za aliyoyafanya ambapo mengi hayaonekaniki kwa macho bali tunalazimishwa kwenye orodha kuwa yamefanyika na utukufu unaenda kwake. Ina maana Watanzania hawana taarifa ama ufahamu wa nchi yao? Je aliapishwa madarakani ili akae tu na asifanye lolote kiasi kwamba akifanya hata jambo dogo zitatumika gharama kubwa kulitangaza?

Tumeshuhudia misafara mikubwa ya watendaji waandamizi wa serikali kwenda kuzindua matundu ya vyoo na kadhalika ambapo gharama za masurufu ya misafara hiyo zingetisha kupunguza vifo vya mama na mtoto wanaokosa tiba bora hususani kipindi hiki ambacho dada Ummy ameshikilia ofisi ya Afya...

Wakati tunakumbuka mema na mabaya ya Hayati JPM, kinachofuatia na kinafanywa kwa nguvu kubwa ni kuadhimisha miaka kadhaa ya utawala wa mama. Ninaomba kuelimishwa haya
  1. Umuhimu wake
  2. Taifa linapata tija gani kwenye hizi kumbukizi?
  3. Ni utekelezaji wa ilani?
Inawezekana tunaohoji labda hatuna hoja za msingi, basi wenye uelewa na hili jambo mtuelimishe labda tutaungamkono juhudi
Siku 100 ndio kipimo hii ni mchongo wa kutaka kuua siku ya jpm!
 
Asante kwa jibu lenye mwanga.

Kumbe kinachotakiwa ni kuwekeza katika kizazi kichanga ili wao waje kuwa wasahihishaji wa makosa yakiyokwisha kufanya na mababu zao.

Kama wameshindwa kuwa na huruma na kizazi hiki basi wakihurumie hata kizazi kinachofuata.
Mkuu umenena mule mule.

Kati ya wapiga mbiu tuliomo humu, wapo ambao wanaamini mpaka washike madaraka ndiyo wanaweza kubadilisha mfumo huu mbovu. La hasha, bali sisi tuwaandae vijana waje kusahihisha makosa yetu bila kutoana macho.

Lakini jukumu la kumuita mwizi, muuaji, fisadi, asiyewajibika kwa jina lake siyo la kuwaachia vizazi vijavyo
 
Back
Top Bottom