Mzee Mwanakijiji,
Hii habari kama ni kweli si Dr. Mwakyembe aende kuwatetea na kuwatoa hao vijana? Kama mbunge ana wajibu wa kulinda maslahi ya wapiga kura wake.
Ungewashauri waliokutumia ujumbe waufikishe pia kwa mbunge wao ili kama hana habari basi achukue hatua.
Itakuwa ni ukichaa kuwakamata vijana kwasababu tu wanalalamikia uongozi uliopo.
Hivi kati ya Mbunge na Mkuu wa Mkoa nani ana madaraka zaidi mkoani? Nani anasimamia polisi na magereza?