Kikwete Mbeya: Mgongano na wananchi na mwitikio wa serikali

Mzee Mwanakijiji,

Hii habari kama ni kweli si Dr. Mwakyembe aende kuwatetea na kuwatoa hao vijana? Kama mbunge ana wajibu wa kulinda maslahi ya wapiga kura wake.

Ungewashauri waliokutumia ujumbe waufikishe pia kwa mbunge wao ili kama hana habari basi achukue hatua.

Itakuwa ni ukichaa kuwakamata vijana kwasababu tu wanalalamikia uongozi uliopo.

Hivi kati ya Mbunge na Mkuu wa Mkoa nani ana madaraka zaidi mkoani? Nani anasimamia polisi na magereza?
 
PICHA%2BYA%2BUSHAHIDI%2BYA%2BFANCY%2Bna%2BKIPANYA.jpg


subirini katuni ya kesho
 
Huyu Mwakipesile anajifanya mungu mtu?. Wananchi wa mkoa wa mbeya hawakutaki kwanini wasiseme?. Mwakipesile na kundi lake waachilieni vijana hao mara moja ama na wewe watoto wako hawatakwenda shule ama popote pale.

Mkuu Kidatu,

Huyu RC naye ni jirani yangu kule Kinyerezi, ninamjua toka akiwa Manager Dawa ya Mbu, na Mwalimu CBE, sijui huko Mbeya lakini ninavyomjua huyu mkulu huwa hata kijijini kwangu wote tunamuogopa sana maana huwa haongei na mtu kabisa, never! The best he can do ni anaweza kukupa lift katika gari lake lakini asikusemeshe mpaka anakushusha!

Nakumbuka hadithi moja pale kijijini kwetu kua siku moja aliwapa lift katika gari lake wanyakyusa flani ambao hawakujua kuwa huyu mkulu naye ni wahuko, wakaanza kumponda kwa kinyakyusa ndani ya gari lake kua hili lijitu ni la namna gani ambalo hata haliongei, jeusi kama mkaaa, walipofika wanaposhuka likawaaaga kwa kinyakyusa wakaanza kuliomba msamaha,

My point ni kwamba kama hao wananchi wamewekwa ndani, basi kwa amri yake huyu, maana ndiye rais wa mkoa, na jinsi ninavyomjua hawata toka huko ndani soon, hapa ni kumuomba Mwakyembe amuombe rais wachiliwe, am sivyo wafwileeee mwee!
 
Sasa naelewa kwa nini JKN alikuwa hachagui mtu wa Mara kuwa kiongozi wa mkoa wa Mara. Haya matatizo yangeepushwa Mbeya.
 
Tanzania tunarudi nyuma kidemokrasia sasa. Gazeti linafungiwa, watu wanatiwa ndani bila sababu.... Anyway, ngoja tusubiri ukweli wa hii habari udhibitike kwanza ndio tutaongea zaidi.
 
Sasa naelewa kwa nini JKN alikuwa hachagui mtu wa Mara kuwa kiongozi wa mkoa wa Mara. Haya matatizo yangeepushwa Mbeya.

Thank You Jasusi;

Ukweli utabaki palepale, Ukichagua Mchagga kuongo za Kilimanjaro; Mnyakyusa Mbea nk. itakua tatizo na mifano iko mingi kama ya yule mmasai aliekua Arusha miaka ya nyuma na kuharibu sekei, sakina mpaka tengeru kwa kutatua masuala ya serikali kimila na hadi leo Arusha imeathirika kwa kukosa good city plan
 
Ni haki yao kuonyesha bango....wanaonyeshwa hata viongozi wazito na wakubwa dunaiani sembuse Jk...kuwatesa waseme kuwa wametumwa na MWakyembe au Mwandosya ni kuwaonea na kuwakose aheshima..kila mtu ana uhuru wa kusema maoni yaoo..wakumbuke kuwa watu wameenda shule siku hizi........wasahau kabisa mawazo mgando ya kusema wametumwa........na hao CCM wajiandae sana maana watu tumewachoka kabisa na kulindana kusikovumilika........
 
Kwani Mwakipesile ilikuwaje akaupata Ukuu wa Mkoa?

Mwanakijiji mbona unamkumbusha machungu mwanamtandao mwakipesile!
najua kwamba unajua ila kwa faida ya wengine ambao watakuwa hawajui huyu mwakipe alifikaje kwenye u-RC, ni baada ya kubwagwa vibaya vibaya na mh.dr.Mwakyembe huko kwao kyela kwenye uchaguzi, i mean kura za maoni ndani ya ccm ndipo mkulu akaamua kumpoza machungu kwa kumtupia u-RC.

Nakumbuka siku JK anawaapisha ma RC, moja ya kioja ni mwakipesile kutetemeka na kushindwa hata kusoma kiapo chake kwa umakini.

anyways,kama wasemavyo wenyewe hizo ndio siasa za mbeya,inawezekana jamaa ana hasira za tukio la mwanjelwa sasa mara tena kyela nao wanamuibukia bila soni kaamua kuwafanyia kweli.
 
Duh nimesikia tena wameupiga mawe msafara wa JK huko Chunya kijiji kimoja sikumbuki magari sita yameharibika mawili ya mawaziri...kazi kweli wanayo.
 
Jana usiku kuna wananchi wa chunya wameletwa Hospital ya Rufaa Mbeya baada ya kupigwa na polisi walipovamia msafara wa Jk kwa mawe. Muungwana amekatisha ziara ghafra alikuwa anaelekea Mbozi akitokea chunya, Nitawaletea habari zaidi
 
Sishabikii fujo wala vurugu, ila nasema ................

............. "NA BADO!!"

Watu wameshachoka, wanaona viongozi hawashughulikii matatizo yao, kutwa kuchwa kupiga politiki na kufanya ziara tu, mara leo Mbeya kesho Marekani keshokutwa Mexico wakati nchi ina matatizo yanayohitaji kupatiwa solution.
 
Kama na hili ni la kweli,bado hizi ni habari kwao.Wanachotakiwa kufanya ni kujumlisha tuu.Tarime + Mgomo wa walimu+ Muungwana kufanyiwa fujo +............... kwa sababu najua bado watanzania hawajaamua kuweka alama ya sawasawa,bado wanaendelea kujumlisha.Tutafika tuuu.
 
Akitaka akagombee urais Marekani,Zimbabwe,Sudan,au akawe rais wa Real Madrd.

Yes,Hasira zinaanza kulipuka taratibu.Watakiona cha mtemakuni,kama hataki aachie mamlaka!
 
Sishabikii fujo wala vurugu, ila nasema ................

............. "NA BADO!!"

Watu wameshachoka, wanaona viongozi hawashughulikii matatizo yao, kutwa kuchwa kupiga politiki na kufanya ziara tu, mara leo Mbeya kesho Marekani keshokutwa Mexico wakati nchi ina matatizo yanayohitaji kupatiwa solution.
mara wezi wa EPA wamepewa siku 72, mara mitihani kuvuja kuliko kawaida,
 
Kwa nini msafara wasafiri usiku?Halafu wanadanganya waliotupa mawe eti ni walevi,
Maana nasikia hadi gari la Salma Kikwete limevunjwa kioo na baadhi ya waandishi wamejeruhiwa
 
Mungu ibariki Tanzania,
Wabariki viongozi wake,
Heshma, umoja na Amani,
Hizi ni Ngoa zetuuuuuuuuu,
Tanzaniaaa na watu wakeeee,
Ibariki, Tanzania Ibariki.
 
Kwa nini msafara wasafiri usiku?Halafu wanadanganya waliotupa mawe eti ni walevi,
Maana nasikia hadi gari la Salma Kikwete limevunjwa kioo na baadhi ya waandishi wamejeruhiwa

Aisee hii kali walevi wapige mawe msafara wa Mhe. rais! hii haijawahi kutokea. By the way, muungwana anapata ujumbe stahili siyo zile jumbe za Rweyemamu salva eti "atang'olewaje Rais mwenye mafanikio makubwa... anayependwa na wananchi... anayeng'ara duniani kote na kuigwa na Marais wengine! wapi bana!
 
Back
Top Bottom