Kikwete Mbeya: Mgongano na wananchi na mwitikio wa serikali

Salva ni kituko cha mwaka... ni heri arudi kwenye fani yake ambako anaweza kupata muda wa kuandika facts.... hizi hoax stories hazimsaidii yeye wala Rais wala mtanzania wa kawaida. Eti ametamka, nimesikia leo asubuhi kuwa wanaolalamika maisha magumu ni watanzania wachache walioko mijini tu... wale wa vijijini hawana maisha magumu kwani neema ya maisha bora, akataja... elimu bora, huduma bora za afya, barabara safi zipo vijijini.

!

Whaaaaat? Give me a break,
Maisha bora yako vijijini? wakati mafuta yataaa ambayo ndo chanzo kikuu cha nishati vijijini kwa sasa yanauzwa elfu 2 kwa rita ukilinganisha na mjini ambako ni 1400? naelekea kuamini kwamba Salva kumlinganisha na Comical ni kumuonea huyo Comical the guy is insane than Comical

Kama kijijini kungekuwa na maisha bora machinga wangefata dhoruba za vipigo vya mgambo wa jiji kila siku? na wale omba omba walio furika si wangerudi kwao vijijini ku enjoy maisha bora?

No wonder JK kawa 'ze comedy' kwa kuwa na msemaji wa aina hii.
 
Comical Salva sasa hawakitena jina lake bali kurugenzi ya mawasiliano Ikulu

Imetolewa mara ya mwisho: 20.10.2008 0122 EAT
• Mawe Mbeya:Ikulu sasa yajikanganya

*Rais asema kupigwa mawe hakukumsumbua
*Tamko la Ikulu lasema: Hili ni tukio lililomkera

Na Mwandishi Wetu
Majira

SIKU moja baada ya Rais Jakaya Kikwete kusema kuwa tukio la baadhi ya magari kwenye msafara wake kupigwa mawe kwenye kijiji cha Kanga, wilayani Chunya, Mbeya halikumsumbua na kuwapa moyo viongozi wa mkoa huo wasijisikie huzuni, Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeonesha kupingana na kauli hiyo ya Rais kwa kusisitiza kuwa tukio hilo lilimkera.

Kwa mujibu wa taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana jioni, Ikulu pia imekanusha masuala kadhaa yaliyoripotiwa na vyombo vya habari wakati Rais akiwa ziarani mkoani humo ikidai yalikuzwa huku ikisisitiza kuwa hata magari yaliyoshambuliwa, hayakuwa kwenye msafara mkuu wa Rais.

"Rais anaamini kuwa tukio hilo la kijiji cha Kanga ni tukio la uhalifu. Kamwe haiwezi kutokea Rais Kikwete asisumbuliwe na tukio lolote la uhalifu katika nchi yetu. Hili ni tuko lililomkera, lakini kama alivyoeleza jana kazi hiyo waachie polisi waendelee nayo," ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Juzi akijumuisha ziara yake ya siku 10 mkoani humo, Rais Kikwete kwa mara ya kwanza alilizungumzia tukio hilo tangu lilipotokea ambapo alifafanua kuwa lilitokana na wananchi kuwa na hamu ya kumuona kiongozi wao na kwamba lisitafsiriwe kuwa linawasilisha msimamo wa watu wote wa Mbeya ambao aliwasifu kuwa wamoja na wenye mawazo ya kimaendeleo.

Jana vyombo vya habari likiwemo gazeti la Serikali, Habari Leo Jumapili, vilimkariri katika habari zao kuu za ukurasa wa mbele Rais akizungumza katika hotuba yake hiyo ya majumuisho kwenye ukumbi wa Benjamin Mkapa ambapo alionesha kutokerwa na tukio hilo.

Katika habari yenye kichwa kinachosema, Kikwete> Mawe hayakunisumbua, iliyoanzia ukurasa wa mbele na kuendelea hadi ukurasa wa pili, gazeti la Habari Leo Jumapili, lilimkariri Rais Kikwete akisema:

"Hili tukio la kushambuliwa kwa mawe lilimfadhaisha sana Mkuu wa Mkoa. Hili tukio lisikufadhaishe, lisiwasononeshe watu wa Mbeya, haliwasilishi hali halisi ya watu wa Mbeya.

"...Hili mimi halinisumbui, wale watu wameshinda pale tangu asubuhi, wamekunywa kinywaji chao na kisha ndio wanaona usiku na watu wanapita. Jambo baya ni vyombo vya habari mka-criminalise mkoa mzima..."

Aidha, taarifa hiyo ya Ikulu ikizungumzia tukio hilo ilisema kuwa msafara ulioshambuliwa haukuwa ule wa Rais na kwamba hata yeye mwenyewe hakufahamu mara moja kutokea kwa tukio hilo.

"Magari ya Rais, kwa maana ya magari yote yanayotengeneza sehemu kuu ya msafara wa Rais, hayakutupiwa hata jiwe moja. Na wala Rais mwenyewe hakupata habari za tukio hilo mpaka alipokuwa amewasili Ikulu ya Mbeya.

"Na alipopata habari hizo alitoa maelekezo maalum kuwa zisije zikachukuliwa hatua za kipolisi kusumbua kijiji kizima na kutaka upelelezi wa suala hilo ufanyike kwa uangalifu mkubwa bila jabza.

"Magari yaliyotupiwa mawe ni yale yaliyokuwa nyuma katika sehemu ya pili ya msafara, yaani nje ya sehemu kuu ya msafara. Na mpaka Rais anaondoka Mbeya jana, ni watu watano tu walikuwa wametiwa mbaroni, tofauti na habari za kubuni za magazeti kuwa wamekamatwa watu 60.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa tukio hilo lilitokana na tahayuri ya wananchi hao kukaa muda mrefu bila kuweza kumuona na kuzungumza na Rais wao.

"Ilikuwa ni hamu hiyo hiyo ambayo wananchi wa kijiji cha Kanga walikuwa nayo wakati Rais anafanya ziara ya Wilaya ya Chunya ambako alipitia na kuhutubia mikutano mikubwa ya wananchi katika maeneo ya Chunya Mjini, Makongolosi na Mkwajuni.

"Kwa bahati mbaya wakati anawasili katika kijiji cha Kanga tayari ilikuwa usiku kati ya saa moja na saa mbili kwa sababu ratiba ya maeneo mengine ilikuwa imecheleshwa mno na hamu ya wananchi wa maeneo hayo kumsimamisha na kumwona Rais wao. Hivyo, msafara wake ukapita bila kusimama katika kijiji hicho," ilisema taarifa hiyo iliyokanusha pia madai kwamba Rais alikatisha ziara hiyo.

Tukio la kupigwa mawe msafara huo wa Rais limeibua mjadala katika jamii huku wananchi wengi wakisema kitendo hicho hakikuwa cha kiungwana hata kama wananchi wa eneo husika walikuwa na madai ya msingi.
 
Jamani Salva anakosa gani?. Kuna watu lazima waseme kuhusu watu?.
Simple mind discuss people.
Ordinary mind discuss events.
Great mind discuss ideas.

Whatever Salvz Says, that is his version. Everone is free to have his own version for his own ends. He is a Director of Communication-wa Ikulu. What do you expect his version to be!?.
What matters most was suppossed to be the media version of the story. That is what is suppossed to be nothing but the truth.
Kusema ukweli mimi nawahurumia hao watu zaidi ya 60 waliotiwa mbaroni kwa kadhia hiyo, kuna uwezekano mkubwa wasitendewe haki.
Mungu ibariki Tanzania.

Pasco, lakini Salva is not just mtu! Ni msemaji wa Rais! Kwa hiyo kumjadili Salva sio kujadili people, ni kujadili issue (integrity ya mkurugenzi wa mawasiliano)! To me, he is nothing less than Comical Ali! Watu wakiwa nje ya serikali wanaonekana wanaakili sana akipewa cheo tu anageuka madudu! Huyu bwana alikuwa pundit alipokuwa na habari corporation lakini leo amekuwa afadhali ya afadhali ya Makamba! Ndio haohao akina Njelu Kasaka, kelele usipokuwa na cheo, ukipata unafiki mtupu. Naamini hata JK atakuwa anamshangaa Salva, maana ni lazima alipomchukua alikuwa na impression tofauti na huyu wa sasa! Hawa ndio wa kutimuliwa kazi halafu wabaki mtaani!
 
Tanzania Ikulu Rais amejaza wachekeshaji tupu. Yeye anadhani mazingira ya 2005 bado yatafanya kazi.
Amekosea. Na asipogundua hili na kubaki akidanganywa na akina Rweyemamu na wenzao....... amekwisha. 2010 haitakuwa rahisi kiasi alivyokuwa 2005.
Believe me.
Maana sasa ni propaganda ndio zimeamia ikulu badala ya facts.
Shauri zao!!!!
 
Kikwete hakukatisha ziara Mbeya - Ikulu

*Ni chokochoko za magazeti, ilikuwa na mafanikio makubwa

Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete hakukatisha ziara katika mkoa wa Mbeya, kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Salva Rweyemamu, ilisema kuwa ziara hiyo ya siku 10 ilifanyika kama ilivyokuwa imepangwa, na ilikuwa na mafanikio makubwa.
Taarifa kamili ya Ikulu ni kama ifuatavyo:
Rais Jakaya Kikwete alihitimisha ziara yake ya siku 10 yenye mafanikio makubwa katika Mkoa wa Mbeya juzi mchana.
Kwa bahati mbaya sana, baadhi ya vyombo vya habari nchini, na hasa magazeti, vimeandika baadhi ya matukio ya ziara hiyo, kwa namna ya wazi ya kuwapotosha wananchi kuhusu ziara hiyo, ambayo Rais alitembelea wilaya zote saba zenye halmashauri nane.
Taarifa hii inalenga kuweka bayana ukweli ulivyokuwa katika ziara hiyo ambako, kwa mara nyingine, Rais alipata nafasi nyingine nzuri ya kufanya kile ambacho hukifurahia sana kukifanya, yaani kukutana na wananchi, kusikiliza kero zao, karaha zao, raha zao, mafanikio yao, na mahitaji yao ambayo wanaamini Rais wao anaweza kusaidia kuyatafutia majawabu.
(a) Rais akatisha ziara ya mkoa
Rais alipanga kukaa katika Mkoa wa Mbeya kwa siku 10. Amefanya hivyo. Hakukatisha ziara hiyo kama ilivyoandikwa katika baadhi ya magazeti. Aliingia Mbeya Oktoba 9, akaondoka Oktoba 13 jioni kwenda Tanga kuzima Mwenge, na alirejea jioni ya Oktoba 14 na kuondoka jana (juzi), Oktoba 18, jumla ya siku 10 kamili.
Ni vyema kujua kuwa kila Rais anapoweka mguu katika mkoa wowote, iwe ni asubuhi, mchana ama jioni ni siku kamili ya kuwapo kwake katika mkoa ama eneo hilo.
Kilichotokea ni kwamba kwa sababu ya ratiba kuwa na shughuli nyingi, ziko shughuli mbili ambazo hakuweza kuzifanya. Ameahidi atapata nafasi ya kwenda tena Mbeya kuzifanya.
(b) Mkutano wa majumuisho ya ziara kwenye Uwanja wa Sokoine
Na wala Rais hakuahirisha kuhutubia wananchi wa Mbeya kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine wakati wa majumuisho yake ya Mkoa huo kama inavyodaiwa.
Rais hakupangiwa kuhutubia mkutano kwenye uwanja huo kwa sababu alikuwa amekwisha hutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja huo, Februari 19, 2006, alipokwenda kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kukichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuongoza nchi yetu.
Na wala Rais hafanyi majumuisho ya ziara za mikoa kwenye mikutano ya hadhara. Huifanya kazi hiyo kwa kukutana na viongozi wa kisiasa, kijamii, kiuchumi, kidini, na kiusalama wa mikoa katika mkutano wa viongozi. Ndivyo alivyofanya jana (juzi) katika Ukumbi wa Mkapa mjini Mbeya.
(c) Kutotembelea Mbeya Vijijini
Kama nilivyoeleza, Rais alitembelea wilaya zote saba za mkoa huo zenye halmashauri nane kwa sababu Mbeya yenyewe ni wilaya moja lakini ina halmashauri mbili, moja ya mjini na nyingine ya vijijini.
Wakati mwingine uelewa wa waandishi wetu unapumbazisha kabisa. Jana, kabla ya kuingia kwenye mkutano wa majumuisho, Rais alitembelea kiwanda cha kutotoa vifaranga vya kuku katika eneo la Songwe, ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa Songwe, pamoja na kuzindua hospitali teule ya wilaya ya Ifisi, vyote vikiwa katika eneo la Wilaya ya Mbeya, lakini maeneo ya vijijini.
(d) JK akiri Mbeya ni pagumu
Huu pia ni upotoshaji mwingine. Kama kuna kitu Rais amekisema wakati wa majumuisho ya ziara yake jana ni kuumwagia sifa sana mkoa huo kwa jitihada za maendeleo ya wananchi - iwe katika elimu, iwe katika afya, iwe katika kilimo, iwe ni katika huduma za maji, iwe ni katika ufugaji, iwe katika umwagiliaji na maeneo mengine muhimu ya maendeleo.
Kile kinachoelezwa kuwa Mbeya ni pagumu, ni pale alipowasihi viongozi kujenga tabia na mwenendo wa uongozi wa pamoja akisisitiza kuwa viongozi hao wanajenga nyumba moja na hivyo hawana sababu ya kugombea fito kwa sababu ya tofauti zilizopo miongoni mwa baadhi ya viongozi wa mkoa huo.
Tofauti miongoni mwa viongozi wachache wa mkoa huo haziufanyi mkoa mzima wa Mbeya kuwa mgumu.
(e) Msafara wa Rais kupigwa mawe
Mwenendo mzima ambao uongozi wa Mkoa wa Mbeya unaweza kujivunia ni kujitokeza kwa wingi mno kwa mamia ya wananchi wa mkoa huo kila alipopita Rais ama kwenda kwa shughuli za maendeleo wakati wa ziara hiyo.
Kila sehemu, wananchi walimtaka asimame, wamwone, awasalimie. Na kama ilivyo ada, hakusita, hata sehemu moja, kufanya hivyo.
Hamu ya wananchi wa Mbeya kumwona na kumsikiliza Rais wao ndiyo ilimfanya Mhe. Rais kusema kuwa alikuwa ameondoka Mkoa wa Mbeya akiwa na kumbukumbu nzuri za wema, ukarimu na upendo wa wananchi wa Mbeya.
Ilikuwa ni hamu hiyo hiyo ambayo wananchi wa kijiji cha Kanga walikuwa nayo wakati Rais anafanya ziara ya Wilaya ya Chunya ambako alipitia na kuhutubia mikutano mikubwa ya wananchi katika maeneo ya Chunya Mjini, Makongorosi na Mkwajuni.
Kwa bahati mbaya wakati anawasili katika kijiji cha Kanga tayari ilikuwa usiku kati ya saa moja na saa mbili kwa sababu ratiba ya maeneo mengine ilikuwa imecheleshwa mno na hamu ya wananchi wa maeneo hayo kumsimamisha na kumwona Rais wao. Hivyo, msafara wake ukapita bila kusimama katika kijiji hicho.
Kile kitendo cha kiongozi wao kutosimama katika kijiji hicho ambako wananchi walikuwa wamejitokeza kwa mamia, wakasimama barabarani kwa saa nyingi wakiwa na hamu kumwona Rais wao, kikachochea na kusisimua tahayari (frustration) kwa vijana ambao wakaanza kurusha mawe kwenye baadhi ya magari yaliyokuwa kwenye msafara.
(d) Magari ya Rais
Magari ya Rais, kwa maana ya magari yote yanayotengeneza sehemu kuu ya msafara wa Rais, hayakutupiwa hata jiwe moja. Na wala Rais mwenyewe hakupata habari za tukio hilo mpaka alipokuwa amewasili Ikulu ya Mbeya.
Na alipopata habari hizo alitoa maelekezo maalum kuwa zisije zikachukuliwa hatua za kipolisi kusumbua kijiji kizima na kutaka upelelezi wa suala hilo ufanyike kwa uangalifu mkubwa bila jabza.
Magari yaliyotupiwa mawe ni yale yaliyokuwa nyuma katika sehemu ya pili ya msafara, yaani nje ya sehemu kuu ya msafara. Na mpaka Rais anaondoka Mbeya jana (juzi), ni watu watano tu walikuwa wametiwa mbaroni, tofauti na habari za kubuni za magazeti kuwa wamekamatwa watu 60.
Rais anaamini kuwa tukio hilo la kijiji cha Kanga ni tukio la uhalifu. Kamwe haiwezi kutokea Rais Kikwete asisumbuliwe na tukio lolote la uhalifu katika nchi yetu. Hili ni tukio lililomkera, lakini kama alivyoeleza jana (juzi) kazi hiyo waachiwe polisi.
Muhimu kusisitiza hapa ni kwamba tukio hilo siyo linalowakilisha taswira ya wananchi wa Mkoa wa Mbeya ambao wameonyesha mapenzi makubwa kwa kiongozi wao mkuu.
Ni makosa kwa kuuchukulia mkoa mzima wa Mbeya kama mkoa wa wahalifu kwa sababu ya tendo lililotendwa na watu wachache katika kijiji kimoja tu.


Na Gazeti La Uhuru!
Hii Habari Imenifurahisha Sana Nikaona Si Mbaya Kuwashirikisha!
 
Kevo,
Kuna jambo moja nimegundua katika hii habari na utendaji mzima wa hii inayoitwa Kurugenzi ya mawasiliano ya ikulu. Hata kama itaonekana kuna habari yenye ukweli inayomuhusu JK, kurugenzi ya habari lazima wai-neutralize.....Kwa hiyo Ndugu yangu Salva anajitahidi sana kutaka kufunika kombe hata mahali ambapo hapafunikiki....
 
spin za Salva. Na hayo mawe je ? Hayakuwashtua wa usalama na kushauri ziara iishie hapo?
 
Kikwete hakukatisha ziara Mbeya - Ikulu


(a) Rais akatisha ziara ya mkoa
Rais alipanga kukaa katika Mkoa wa Mbeya kwa siku 10. Amefanya hivyo. Hakukatisha ziara hiyo kama ilivyoandikwa katika baadhi ya magazeti. Aliingia Mbeya Oktoba 9, akaondoka Oktoba 13 jioni kwenda Tanga kuzima Mwenge, na alirejea jioni ya Oktoba 14 na kuondoka jana (juzi), Oktoba 18, jumla ya siku 10 kamili.
Ni vyema kujua kuwa kila Rais anapoweka mguu katika mkoa wowote, iwe ni asubuhi, mchana ama jioni ni siku kamili ya kuwapo kwake katika mkoa ama eneo hilo.
Kilichotokea ni kwamba kwa sababu ya ratiba kuwa na shughuli nyingi, ziko shughuli mbili ambazo hakuweza kuzifanya. Ameahidi atapata nafasi ya kwenda tena Mbeya kuzifanya.
(b) Mkutano wa majumuisho ya ziara kwenye Uwanja wa Sokoine
Na wala Rais hakuahirisha kuhutubia wananchi wa Mbeya kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine wakati wa majumuisho yake ya Mkoa huo kama inavyodaiwa.
Rais hakupangiwa kuhutubia mkutano kwenye uwanja huo kwa sababu alikuwa amekwisha hutubia mkutano wa hadhara kwenye uwanja huo, Februari 19, 2006, alipokwenda kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa kukichagua Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuendelea kuongoza nchi yetu.
Na wala Rais hafanyi majumuisho ya ziara za mikoa kwenye mikutano ya hadhara. Huifanya kazi hiyo kwa kukutana na viongozi wa kisiasa, kijamii, kiuchumi, kidini, na kiusalama wa mikoa katika mkutano wa viongozi. Ndivyo alivyofanya jana (juzi) katika Ukumbi wa Mkapa mjini Mbeya.
(c) Kutotembelea Mbeya Vijijini
Kama nilivyoeleza, Rais alitembelea wilaya zote saba za mkoa huo zenye halmashauri nane kwa sababu Mbeya yenyewe ni wilaya moja lakini ina halmashauri mbili, moja ya mjini na nyingine ya vijijini.
Wakati mwingine uelewa wa waandishi wetu unapumbazisha kabisa. Jana, kabla ya kuingia kwenye mkutano wa majumuisho, Rais alitembelea kiwanda cha kutotoa vifaranga vya kuku katika eneo la Songwe, ujenzi wa uwanja wa kimataifa wa Songwe, pamoja na kuzindua hospitali teule ya wilaya ya Ifisi, vyote vikiwa katika eneo la Wilaya ya Mbeya, lakini maeneo ya vijijini.
(d) JK akiri Mbeya ni pagumu
Huu pia ni upotoshaji mwingine. Kama kuna kitu Rais amekisema wakati wa majumuisho ya ziara yake jana ni kuumwagia sifa sana mkoa huo kwa jitihada za maendeleo ya wananchi - iwe katika elimu, iwe katika afya, iwe katika kilimo, iwe ni katika huduma za maji, iwe ni katika ufugaji, iwe katika umwagiliaji na maeneo mengine muhimu ya maendeleo.
Kile kinachoelezwa kuwa Mbeya ni pagumu, ni pale alipowasihi viongozi kujenga tabia na mwenendo wa uongozi wa pamoja akisisitiza kuwa viongozi hao wanajenga nyumba moja na hivyo hawana sababu ya kugombea fito kwa sababu ya tofauti zilizopo miongoni mwa baadhi ya viongozi wa mkoa huo.
Tofauti miongoni mwa viongozi wachache wa mkoa huo haziufanyi mkoa mzima wa Mbeya kuwa mgumu.
(e) Msafara wa Rais kupigwa mawe
Mwenendo mzima ambao uongozi wa Mkoa wa Mbeya unaweza kujivunia ni kujitokeza kwa wingi mno kwa mamia ya wananchi wa mkoa huo kila alipopita Rais ama kwenda kwa shughuli za maendeleo wakati wa ziara hiyo.
Kila sehemu, wananchi walimtaka asimame, wamwone, awasalimie. Na kama ilivyo ada, hakusita, hata sehemu moja, kufanya hivyo.
Hamu ya wananchi wa Mbeya kumwona na kumsikiliza Rais wao ndiyo ilimfanya Mhe. Rais kusema kuwa alikuwa ameondoka Mkoa wa Mbeya akiwa na kumbukumbu nzuri za wema, ukarimu na upendo wa wananchi wa Mbeya.
Ilikuwa ni hamu hiyo hiyo ambayo wananchi wa kijiji cha Kanga walikuwa nayo wakati Rais anafanya ziara ya Wilaya ya Chunya ambako alipitia na kuhutubia mikutano mikubwa ya wananchi katika maeneo ya Chunya Mjini, Makongorosi na Mkwajuni.
Kwa bahati mbaya wakati anawasili katika kijiji cha Kanga tayari ilikuwa usiku kati ya saa moja na saa mbili kwa sababu ratiba ya maeneo mengine ilikuwa imecheleshwa mno na hamu ya wananchi wa maeneo hayo kumsimamisha na kumwona Rais wao. Hivyo, msafara wake ukapita bila kusimama katika kijiji hicho.
Kile kitendo cha kiongozi wao kutosimama katika kijiji hicho ambako wananchi walikuwa wamejitokeza kwa mamia, wakasimama barabarani kwa saa nyingi wakiwa na hamu kumwona Rais wao, kikachochea na kusisimua tahayari (frustration) kwa vijana ambao wakaanza kurusha mawe kwenye baadhi ya magari yaliyokuwa kwenye msafara.
(d) Magari ya Rais
Magari ya Rais, kwa maana ya magari yote yanayotengeneza sehemu kuu ya msafara wa Rais, hayakutupiwa hata jiwe moja. Na wala Rais mwenyewe hakupata habari za tukio hilo mpaka alipokuwa amewasili Ikulu ya Mbeya.
Na alipopata habari hizo alitoa maelekezo maalum kuwa zisije zikachukuliwa hatua za kipolisi kusumbua kijiji kizima na kutaka upelelezi wa suala hilo ufanyike kwa uangalifu mkubwa bila jabza.
Magari yaliyotupiwa mawe ni yale yaliyokuwa nyuma katika sehemu ya pili ya msafara, yaani nje ya sehemu kuu ya msafara. Na mpaka Rais anaondoka Mbeya jana (juzi), ni watu watano tu walikuwa wametiwa mbaroni, tofauti na habari za kubuni za magazeti kuwa wamekamatwa watu 60.
Rais anaamini kuwa tukio hilo la kijiji cha Kanga ni tukio la uhalifu. Kamwe haiwezi kutokea Rais Kikwete asisumbuliwe na tukio lolote la uhalifu katika nchi yetu. Hili ni tukio lililomkera, lakini kama alivyoeleza jana (juzi) kazi hiyo waachiwe polisi.
Muhimu kusisitiza hapa ni kwamba tukio hilo siyo linalowakilisha taswira ya wananchi wa Mkoa wa Mbeya ambao wameonyesha mapenzi makubwa kwa kiongozi wao mkuu.
Ni makosa kwa kuuchukulia mkoa mzima wa Mbeya kama mkoa wa wahalifu kwa sababu ya tendo lililotendwa na watu wachache katika kijiji kimoja tu.


Na Gazeti La Uhuru!
Hii Habari Imenifurahisha Sana Nikaona Si Mbaya Kuwashirikisha!


Hizo tarehe na hesabu miminapata siku siku kumi nikihesabu tangu anaingia yaani tarehe 9 na nahesabia na siku aliyokuwa Tanga napata siku kumi nikiitoa siku ya kuzima mwenye napata siku 9 sina uhakika na maneno ya Salva especial anaposemakupigwa mawe kwa Rais ni watukuonyesha upendo kwa JK kama watu wale walionyesha mapenzi kwa JK mbona wamekamatwa na kuswekwa lock up? sisi waungwana tuna msemo wema/mapenzi hulipwa kwa mapenzi/wema sasa mapenzi hayo waliyokuwa nao hao wananchi mbona yanalipwa kwa ubaya na undava?
Tafakari
 
Kikwete hakukatisha ziara Mbeya - Ikulu

*Ni chokochoko za magazeti, ilikuwa na mafanikio makubwa

Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete hakukatisha ziara katika mkoa wa Mbeya, kama ilivyoripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari.

Ni choko choko za magazeti? Sasa magazeti yamekua maadui wa Mtandao? Kweli ushirika wa wachawi haudumu.
 
Yawezekana hakuhutubia sababu ya kiusalama.

Raisi akichokwa na wananchi walinzi wake kuanzia wa misafara hadi wale wa kuzagaa mitaani huwa wanapata taabu mno.Gharama za ulinzi huwa kubwa mno.Hakuna kulala.Ndio maana watu huhimiza Raisi ajitahidi kufanya kazi yake vizuri ili angalau walinzi walale na gharama za ulinzi zipungue na wao waone raha ya kufanya kazi ya ulinzi.Lakini wakiona kasheshe ni kubwa waweza amua kuwa hawataki kuendelea kukosa usingizi kumlinda mtu asiyependwa na watu kwenye eneo husika na hivyo kuamuru Raisi akatishe ziara zake ili nao wapate usingizi.

Raisi wa nchi akiwa dhaifu kiutendaji ndani ya nchi huwa ni mzigo mkubwa usiobebeka kwa vyombo vya ulinzi na usalama.Kutwa wanakuwa wakikimbizana kama vichaa huku na huko na waitwao adui wa Raisi badala ya kushughulikia mambo mengine.

Kama walinzi wake waliona wamshinikize akatize ziara Mbeya warudi nawapongeza kwani nao kama binadamu wana haki ya kulala usingizi na sio kukesha na kufukuzana tu na wananchi wanaozomea Raisi waliyemchoka.Kama waliamwamrisha Mbeya akatize ziara tunawaomba vyombo vya ulinzi na usalama kwa ujasiri huo huo siku ingine wakimwona bado legelege na dhaifu kiutendaji wasisite kumwambia ACHIA NGAZI JIUZULU PISHA WENGINE.

Raisi akiwa ana udhaifu katika utendaji waandishi wake pia huwa na kazi kubwa ya kukesha wakitunga porojo za uwongo .

Kutunga uwongo ni kazi sana .Kufanya uwongo huo ukubalike kwenye press release ni kazi kubwa zaidi.
 
Ni choko choko za magazeti? Sasa magazeti yamekua maadui wa Mtandao? Kweli ushirika wa wachawi haudumu.

Nguvu kubwa iliyokuwa imewekezwa kwenye magazeti na vyombo vingine vya habari ili kuijenga serikali (hasa Kikwete binafsi) mbele ya umma, imepwaya kwa sababu maisha halisi ni magumu kuliko makala tamu tamu za wapenzi wa serikali na chama tawala.

Nguvu ya mashushu wanaojipendekeza kwa serikali imepwaya kwa sababu nao ni binadamu; wanafika mahali wanaona ukweli. Maisha magumu yanawaathiri wao na ndugu zao vile vile.

Pesa za wizi na halali zilizo mikononi mwa vyombo vya dola na chama tawala zina kikomo. Haziwezi kununua kila kitu. Walau hadi sasa, zimeshindwa kununua mapenzi ya wananchi kwa serikali.

Haziondoi chuki yao dhidi ya watawala walioahidi maisha bora ambayo hayajapatikana, na dalili hazionyeshi kama yatapatikana wakiwa madarakani.

Vitisho dhidi ya wakosoaji wa serikali havifajua dafu kwa sababu serikali haina nidhamu; mambo ya kukosoa yanaongezeka. Woga wa wananchi kwa watawala umepungua kwa kiasi kikubwa, na uelewa wao wa masuala ya kisiasa umeongezeka.

Propaganda za CCM na wapambe wake zimeshindwa kufanya kazi kwa sababu wananchi wa kizazi hiki ni waelewa kuliko wale waliokabidhiwa jukumu la kueneza propaganda za CCM. Matokeo yake, serikali haikubaliki kwa wananchi, na kizazi hiki kimeanza kujitambulisha zaidi na siasa zinazoitaka CCM ipumzike.

Ni kizazi kinachotaka, na kimedhamiria, kuona CCM ikiachia madaraka katika ngazi za halmshauri, bunge na serikali kuu. Na wanaoyaona haya si wapinzani tu. Hata ndani ya CCM wamo watu wenye akili nzuri, waliochoka siasa za maigizo, wanaotaka kuendana na siasa zinazoakisi hisia na matarajio ya wananchi".
[/COLOR]
 
Kikwete hakukatisha ziara Mbeya - Ikulu

*Ni chokochoko za magazeti, ilikuwa na mafanikio makubwa

(e) Msafara wa Rais kupigwa mawe
Mwenendo mzima ambao uongozi wa Mkoa wa Mbeya unaweza kujivunia ni kujitokeza kwa wingi mno kwa mamia ya wananchi wa mkoa huo kila alipopita Rais ama kwenda kwa shughuli za maendeleo wakati wa ziara hiyo.
Kila sehemu, wananchi walimtaka asimame, wamwone, awasalimie. Na kama ilivyo ada, hakusita, hata sehemu moja, kufanya hivyo.
Hamu ya wananchi wa Mbeya kumwona na kumsikiliza Rais wao ndiyo ilimfanya Mhe. Rais kusema kuwa alikuwa ameondoka Mkoa wa Mbeya akiwa na kumbukumbu nzuri za wema, ukarimu na upendo wa wananchi wa Mbeya.
Ilikuwa ni hamu hiyo hiyo ambayo wananchi wa kijiji cha Kanga walikuwa nayo wakati Rais anafanya ziara ya Wilaya ya Chunya ambako alipitia na kuhutubia mikutano mikubwa ya wananchi katika maeneo ya Chunya Mjini, Makongorosi na Mkwajuni.
Na Gazeti La Uhuru!
Hii Habari Imenifurahisha Sana Nikaona Si Mbaya Kuwashirikisha!

"Wananchi hawa si vichaa. Hata sababu zilizotolewa na serikali kwamba wananchi walishambulia msafara wa rais kwa kuwa walikuwa na kiu ya kumuona lakini hakusimama kijijini kwao kwa sababu ya giza, hazieleweki kwa watu wenye kupenda kufikiri na kutafakati kidogo.

Wananchi wanaompenda kiongozi wao hawamrushii mawe kumdhuru yeye au watu walioambatana naye. Najua serikali yenyewe haiamini kauli yake, ndiyo maana imemwaga mashushushu mahali hapo kuchunguza sababu za kitendo hicho.

Hata hivyo, tunapaswa kujiuliza. Kwanini sasa wananchi wanaonekana kushabikia urushaji mawe? Huu ndio ukomo wa uvumilivu wao wa siku nyingi? Ndiyo njia mpya ya kujieleza kwamba wamechoka kupuuzwa?

Ndiyo njia ya kuwafanya wakubwa wawasikilize? Je, baada ya mawe watatumia silaha gani? Je, wakubwa wapo tayari kujifunza kutokana na mawe wanayorushiwa na wananchi? Au wataendelea kuwatuma polisi warushe risasi kudhibiti mawe hayo? Je, watafanikiwa?"
 
"Wananchi hawa si vichaa. Hata sababu zilizotolewa na serikali kwamba wananchi walishambulia msafara wa rais kwa kuwa walikuwa na kiu ya kumuona lakini hakusimama kijijini kwao kwa sababu ya giza, hazieleweki kwa watu wenye kupenda kufikiri na kutafakati kidogo.

Wananchi wanaompenda kiongozi wao hawamrushii mawe kumdhuru yeye au watu walioambatana naye. Najua serikali yenyewe haiamini kauli yake, ndiyo maana imemwaga mashushushu mahali hapo kuchunguza sababu za kitendo hicho.

Hata hivyo, tunapaswa kujiuliza. Kwanini sasa wananchi wanaonekana kushabikia urushaji mawe? Huu ndio ukomo wa uvumilivu wao wa siku nyingi? Ndiyo njia mpya ya kujieleza kwamba wamechoka kupuuzwa?

Ndiyo njia ya kuwafanya wakubwa wawasikilize? Je, baada ya mawe watatumia silaha gani? Je, wakubwa wapo tayari kujifunza kutokana na mawe wanayorushiwa na wananchi? Au wataendelea kuwatuma polisi warushe risasi kudhibiti mawe hayo? Je, watafanikiwa?"

Nadhani shida ni uvivu wa kufikiri kwa hawa viongozi wetu, mawe hayawezi kuwa nikuonyesha kiongozi huyo anapendwa sana, suppose wangekuwa na silaha za moto ingekuwaje?

Ushi
 
[(e) Msafara wa Rais kupigwa mawe
Mwenendo mzima ambao uongozi wa Mkoa wa Mbeya unaweza kujivunia ni kujitokeza kwa wingi mno kwa mamia ya wananchi wa mkoa huo kila alipopita Rais ama kwenda kwa shughuli za maendeleo wakati wa ziara hiyo.
Kila sehemu, wananchi walimtaka asimame, wamwone, awasalimie. Na kama ilivyo ada, hakusita, hata sehemu moja, kufanya hivyo.
Hamu ya wananchi wa Mbeya kumwona na kumsikiliza Rais wao ndiyo ilimfanya Mhe. Rais kusema kuwa alikuwa ameondoka Mkoa wa Mbeya akiwa na kumbukumbu nzuri za wema, ukarimu na upendo wa wananchi wa Mbeya.
Ilikuwa ni hamu hiyo hiyo ambayo wananchi wa kijiji cha Kanga walikuwa nayo wakati Rais anafanya ziara ya Wilaya ya Chunya ambako alipitia na kuhutubia mikutano mikubwa ya wananchi katika maeneo ya Chunya Mjini, Makongorosi na Mkwajuni.
Kwa bahati mbaya wakati anawasili katika kijiji cha Kanga tayari ilikuwa usiku kati ya saa moja na saa mbili kwa sababu ratiba ya maeneo mengine ilikuwa imecheleshwa mno na hamu ya wananchi wa maeneo hayo kumsimamisha na kumwona Rais wao. Hivyo, msafara wake ukapita bila kusimama katika kijiji hicho.
Kile kitendo cha kiongozi wao kutosimama katika kijiji hicho ambako wananchi walikuwa wamejitokeza kwa mamia, wakasimama barabarani kwa saa nyingi wakiwa na hamu kumwona Rais wao, kikachochea na kusisimua tahayari (frustration) kwa vijana ambao wakaanza kurusha mawe kwenye baadhi ya magari yaliyokuwa kwenye msafara.
(d) Magari ya Rais
Magari ya Rais, kwa maana ya magari yote yanayotengeneza sehemu kuu ya msafara wa Rais, hayakutupiwa hata jiwe moja. Na wala Rais mwenyewe hakupata habari za tukio hilo mpaka alipokuwa amewasili Ikulu ya Mbeya.
Na alipopata habari hizo alitoa maelekezo maalum kuwa zisije zikachukuliwa hatua za kipolisi kusumbua kijiji kizima na kutaka upelelezi wa suala hilo ufanyike kwa uangalifu mkubwa bila jabza.
Magari yaliyotupiwa mawe ni yale yaliyokuwa nyuma katika sehemu ya pili ya msafara, yaani nje ya sehemu kuu ya msafara. Na mpaka Rais anaondoka Mbeya jana (juzi), ni watu watano tu walikuwa wametiwa mbaroni, tofauti na habari za kubuni za magazeti kuwa wamekamatwa watu 60.
Rais anaamini kuwa tukio hilo la kijiji cha Kanga ni tukio la uhalifu. Kamwe haiwezi kutokea Rais Kikwete asisumbuliwe na tukio lolote la uhalifu katika nchi yetu. Hili ni tukio lililomkera, lakini kama alivyoeleza jana (juzi) kazi hiyo waachiwe polisi.
Muhimu kusisitiza hapa ni kwamba tukio hilo siyo linalowakilisha taswira ya wananchi wa Mkoa wa Mbeya ambao wameonyesha mapenzi makubwa kwa kiongozi wao mkuu.
Ni makosa kwa kuuchukulia mkoa mzima wa Mbeya kama mkoa wa wahalifu kwa sababu ya tendo lililotendwa na watu wachache katika kijiji kimoja tu.
Press Release ya Salva Rweyamamu ilitakiwa isomeke hivi:.

Kisa cha wananchi kushambulia msafara wa Raisi ni kuwa Raisi alikataa amri halali ya wapiga kura wake ambao walijitokeza kwa wingi mno barabarani wakimtaka asimame na msafara wake ili atoe maelezo kwa nini maisha ya wanakijiji wa Kanga ni magumu tofauti na ahadi ya Raisi ya maisha bora kwa kila mtanzania.

Raisi na msafara wake wakafanya jeuri wakakataa amri halali ya wananchi ambao ndio waliompa kura.

Wananchi wa Kijiji cha Kanga walipoona amekataa kusimama ndipo walipoamua kuuvurumishia mawe msafara wake kwa lengo la kumshinikiza asimame kitendo ambacho kilimfanya aongeze spidi ya kukimbia kwa mwendo wa kuua mtu kuwatoroka wapiga kura wenye hasira waliokuwa wakirusha mawe mfululizo.

Raisi akagoma kusimama hadi alipofika Mbeya ambako aliamuru wakamatwe wapiga kura walioamuru asimame na wakamrushia mawe waswekwe ndani.

Na hadi muda huu wapiga kura hao bado wako ndani na Raisi bado hajatoa maelezo kwa hata wapiga kura hao walioko ndani kwa nini maisha bora kwao na kwa kila mwanakijiji wa Kanga aliyerusha mawe na yule ambaye hajarusha mawe hayajawezekana.

Kitendo walichokifanya wananchi wa kijiji hicho ni cha kipekee hakilingani na sehemu zingine za Mbeya ambako wananchi hawakumpa amri ya kusimama ajieleze.
 
The Most ironical Part of these Article ni kuwa watu wengi walijitokeza kumlaki raisi wao!Hivi huyu Salva nataka kutuambia kuwa kumpiga raisi mawe ni njia ya kuonyesha upendo wao?Huyu Sala antaka kutuambia kwamba raisi kafurahi sana yaliyomkuta Mbeya?Nina uhakika right now he is feeling like shit coz he knows he is no longer the man of the people he was before!
 
Back
Top Bottom