kikwete avuna aibu Sheikh Amri Abeid Stadium -Arusha

kikwete avuna aibu Sheikh Amri Abeid Stadium -Arusha

Mkuu sisi wakazi wa Arusha ndo tunajua kilicho tokea.....Ni aibu tupu...

Ina maana hapa Arusha hamna Wakereketwa wa CCM...?

Mwalimu wenu wa Propaganda hakufuzu shule, Rais amepokelewa Arusha kama anavyopokelewa mahali popote pale, wana Arusha wanampenda Rais wao kuliko muda wowote ule. Wahuni wanaomsapoti LEMA ni wachache kuzuia Rais asihutubie wananchi wazalendo. Kwahiyo hizi siasa Chafu hazitafua dafu.
Kikwete Songa Mbele!
 
Tazama Picha utuonyeshe hao "wanafunzi tupu" wa shule za msingi waliojaza uwanja wako wapi?


Wewe utadhubutu kuweka picha ya hao watoto wewe?
Nakwambia wadanganyeni waliolala tu ila wengine tumeshaamka kitambo sana!

Hapa A town tutakomaa mpaka kieleweke nakwambia.
 
Hawa bila kwenda nao kitaalamu wataipotosha sana Jamii ya wapenda Amani.

Mkuu hizo picha zako umepiga ule upande wa jukwaa kuu ambao makada wa CCM wa wilaya ya Arumeru waliamria kufunga ofisi leo ili wahudhurie uwanjani...

Manesi waliwekewa matent mbele kabisa......

Kama unaubavu piga majukwaa yote ya Stadium tuone...

JK leo amepata aibu ya mwaka..
 
Mkuu niko hapa Mnara wa Mwenge, Kuna jamaa amenitonya kuwa huyu Mleta mada ni mfanyakazi wa kazi za ndani nyumbani kwa LEMA huko Njiro.


Hapo mnara wa mwenge umeegeshwa? Ama umekuwa kati ya wale wale nini??
Pole sana!
 
kayika - KATIKA
anaeongoza - ANAYEONGOZA
kutembekea - KUTEMBELEA
aliotalajia - ALIYOTARAJIA
shighuli - SHUGHULI
maazimisho - MAADHIMISHO
ukilanja - UKIRANJA
wamelazomishwa - WAMELAZIMISHWA


Mkuu Crashwise hebu jifunze kuandika kwanza. Haya ya Kikwete yako juu ya uwezo wako
cc: FaizaFoxy
Kiandikio cha huyu lazima alitumia kisimu cha tachi screeni ndio maana kakosea kosea.unaedit kama ticha wa darasa la kwanza anafundisha mwandiko?
 
Kiandikio cha huyu lazima alitumia kisimu cha tachi screeni ndio maana kakosea kosea.unaedit kama ticha wa darasa la kwanza anafundisha mwandiko?
Hakuna cha "Touch Screen" wala nini. Elimu yake ndogo tu! Touch Screen inaweka "R" badala ya "L" na "L" badala ya "R" , wakati kwenye keyboard hizo letter hata hazikaribiani?
 
Back
Top Bottom