GE2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

GE2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

Status
Not open for further replies.
Silaa tunakuombea , wenye roho mbaya ni wengi ila tanzania tunataka mtu kama wewe mwenye kuthubutu.
 
Umewaza niliyowaza. Kuna taarifa mbili za kifo cha yule dogo. Kafa ghafla na kajiua! Baada ya hapo hakuna taarifa nyingine iliyotoka hata ya mazishi. Poor boy was only 32 years. RIP kamanda!
.

Mstaafu mmoja wa UWT anasema kwamba, vifo vya hawa jamaa,UWT havitangazwa duniani kote kwa sababu ya asili ya kazi yao kwamba moja ya kiapo chao ni kuwa tayari kufa wakati wowote ukiwa kazini. Kiapo hiki ukikikataa siku ya kwanza tu ndio inakuwa ukomo wa kutafuta ajira huko. anasema kujiua pia ni kosa la kiamaadili kwa sababu wana vitengo vya kudhibiti saikolojia kwa kuwa muda mwingi wanahodhi silaha na kujua mambo nyeti. Wanaoweza kutangazwa ni wale viongozi wa juu ambao kanuni imewaweka wazi kwa umma.

Inaaminika kwao kwamba kufikiria kujiua ni jambo la hatari si kwa anayechukua uamuzi huo tu bali hata kwa watumishi wengine na raia wa kawaida wasio na hadhi ya kujitetea.Wakati wote wa kazi za utumishi mfanyakazi anatakiwa kuwa na akili timamu isiyotiliwa mashaka.Fikra za kujiua zinadhibitiwa wakati wote wa somo la saikolojia kwa kuwa kwao kutamani kujiua kunaweza kwenda sambamba na kuua na wengine kabla ya kufikia uamuzi huo.

Anasema taarifa alizonazo ni kwamba kifo cha mlinzi wa Chief Justice ni cha kawaida na ndio taarifa sahihi lakini watu hawawezi kuamini kwa sababu vifo vyao haviwekwi wazi kama ilivyo kwa raia wa kawaida.
 
Mhhh, hapo kweli kuna madudu mengi ya kufanya libichwa bovu lianze kuzunguka.

Taarifa ya kwanza inasema alikutwa amekufa nyumbani kwake baada ya majirani kuvunja mlango sasa 8.45 (sina hakika kama ana maana ya 8.45 AM au 2.45 PM). Hata hivyo hao majirani zake ni akina nani kama huyo juu alikuwa anaishi kweye Barracks za TISS? Na walikuwa wanatafuta nini au wanamtaka wa nini mtu ambaye ni bachelor?

Taarifa ya pili ndiyo inalikoroga kabisa. Hivi mtu akijipiga risasi (hata kama ni mdomo) mlio wa bunduki hautoki nje? Na hao wenzake walio mkuta amekufa ni akina nani na walikuwa wanatafuta nini?

Ukiwaza zaidi kuhusu hizi repoti 2 unazidi kupata kizunguzungu.....you end up smelling evil!
.

Waataalamu wa silaha mko wapi mtusaidie, nilipokuwa JKT nilifundishwa kwamba kuna pistol ziko kimya, hazitoi mlio kabisa kwa hiyo suala la mlio sio la msingi katika mjadala.
 
Hata kura za maoni nyingi zinazoendeshwa sasa zinaonesha Slaa anampita JK kwa mbali sana. Kama Slaa ataweza kuwateka watu wa vijijini basi mambo yatakuwa magumu kwa CCM. Chama cha Mafisadi kijiandae kwa anguko la kihistoria. Soon kitaanza kuwa chama cha upinzani. Watanzania wengi sasa wameshaishtukia CCM.

chadema hakina mtandao hadi vijijini hakiwezi kuwateka watu vijijini kwa mwendo huo
 
sehemu zote walizofanya tafiti zinaendana na hali ilivyo, ila ya dar nimeshangaa aisee!!!


...Of course Dar ndio chanzo cha matatizo yote ya nchi hii. Fikiria, kwa bunge lililoisha, hakukuwa na mbunge wa kuchaguliwa hata mmoja kwa mkoa mzima. Anzia hapa kwanza, ndipo ujue kwamba Dar ni kimeo sana kwa siasa.


Umewasiliana na mtu mwenye access na simu + TV. Embu watafute wale wasio na simu wala TV wanaoshinda kwenye maboda ya mpunga upate maoni yao

Si vijiji vyo vya nchi hii ambavyo havina TV. Siku hizi vijijini kuna jenereta za Mchina kibao sana, kuna umeme wa jua n.k. Hata kobe la dunia wengi walikuwa wanaangalia mechi kama kawa. Hali ya vijiji vya sasa si kama miaka ya nyuma, hivyo hizi taarifa huwa zinafika. Simu za Mchina nyingi zina redio, kwa hiyo taarifa zinafika kama kawa.
 
Wazee tusipuuze, tujaribu kucheck viashiria!!!!.....Kwanza jiulizeni kwanini majuzi kati CCM waliamua kuwatuma makada wake(wazee kwa vijana) kwenda kila jimbo ili Kuongeza kasi ya kampeni???? Na wale makada walioshinda kura za maoni lakini CC ikawaengua (akiwamo Bashe na Mwakalebela) CCM ishaanza kuwaangukia... Hali ni mbaya saaaana kwa CCM wazee!!! Kwahiyo tusimpuuze huyu jamaa, tutafiti.
 
Siku hizi flow of information haipo primitive kama mnavyozani....Wala mpango wa CCM kutegemea mabalozi wa nyumba kumi kumi ili ku-strenthen base yake vijijini hauna nafasi sana kwani inawezekana wakawa wasikivu midomoni tu lakini mioyo yao ikawa mbali sana na CCM. Isitoshe, katika ulimwengu wa sasa watu wana fikra huru zaidi kuliko ulimwengu wa enzi za mwalimu (huwezi kuwahadaa au kuwaburuza)
 
Wazee tusipuuze, tujaribu kucheck viashiria!!!!.....Kwanza jiulizeni kwanini majuzi kati CCM waliamua kuwatuma makada wake(wazee kwa vijana) kwenda kila jimbo ili Kuongeza kasi ya kampeni???? Na wale makada walioshinda kura za maoni lakini CC ikawaengua (akiwamo Bashe na Mwakalebela) CCM ishaanza kuwaangukia... Hali ni mbaya saaaana kwa CCM wazee!!! Kwahiyo tusimpuuze huyu jamaa, tutafiti.

Mdharau mwiba mguu huota tende CCM inaona itashinda tu hata leo nimesoma gazeti kuna mwakilishi mmoja wa CCM alisema hawawasumbui wazee wa CCM (Mwinyi na Mkapa) maana wanaona mambo mazuri. Wanasahau mwaka 2005 Mwinyi alikuwa akipita waziwazi kumnadi Kikwete sasa hivi hatuwaoni maana wanalifahamu joto au fukuto la wananchi waliochoka na ufisadi wa CCM. Tena wakijaribu kumsimamisha Mkapa ndio watakuwa washajitengenezea kaburi la kujizikia ndani
 
Issue ya REDET na Synovate waulize wenyewe... lakini ukitumia medula oblangata uliojaliwa na Mungu, ulizia uchaguzi wa serikali za mitaa CCM iliibuka na kura kiasi gani? Alafu jiulize ni kitu gani cha ajabu kimetongea tangu wakati huo mpaka sasa? Jiulize kipi CHADEMA imekuja nacho cha ajabu ambacho kitaweza kubadili matokeo kiasi hicho? Jiulize CCM inaowabunge wangapi? Niulize CCM inatarajia kupata wabunge wangapi? Jiulize wabunge na madiwani wa CCM ambao wametapakaa nchi nzima hawana mchango kwa kura za Rais wao.

Sisi waTanzania watu wa ajabu sana tunaamini mazingaombwe mno....




Noma Mkuu, hebu watendee haki watanzania yasije kupata yale ya mkuu wako Makamba kuhusu midahalo ya wagombea na uwepo wa watanzania wenye njaa kutoka mitaa ya kariakoo! au ni sehemu ya ilani ya CCM kuwatusi watanzania?
 
Si kweli thread zinazomsifia JK zinafutwa bali Zinakosa MVUTO sababu hazipendwi na kujikuta zikienda rank za chini kabisa kwa umaarufu humu JF. Scroll down sana ndo utazikuta!!
.

acha uongo thread zinazomsifia JK zinafutwa kila mwenye macho anaona. Tukizisoma baada ya muda zinafutwa nani kasema hatujui kuzitafuta hapa JF zinazoachwa kumsifu JK ni zile ambazo hazina uzito.
 
kukubalika vijijini kwa slaa kunatokana na matunda ya operesheni sangara. Pia ni baada ya wananchi wa huko kuanza kupima ukweli wa kile kinachoelezwa na wapinzani.


operesheni sangara haikufika vijijini na ilikatishwa kabla ya kufika nchi nzima ilikuwa ni opresheni iliyotembelea miji zaidi. impact yake kwa watu wa vijijini inaweza kuwa si kubwa kihivyo.
 
Mkuu, Kikwete hasimamiii sera za chama hata kidogo bali sera za ujangili wa Rostam Azizi na rafiki yake Richmonduli Edward Lowasa na maisha bora kwa wanamtandao na familia zao. Na usipuuzie taarifa hizi. Nakwambia ukweli sasa hivi nimetoka kupiga simu kijijini kwetu nimeongea na dada yangu aliyeko huko anasema mwaka huu watu wanachagua CHADEMA wamechoka na ahadi hewa na bla bla za CCM na kaniambia mambo mengine ya ndani sana (siwezi kuyaandika hapa). Kama watu wa vijijini wamepata mwamko huo basi ndo mwisho wa CCM.

Muhimu: CHADEMA wekeni mikakati ya kulinda wizi wa kura na kuingizwa kwa masunduku yaliyojaa kura za CCM kutoka usalama wa taifa. Hatika ukombozi wa Watanzania umewadia.

Hawa usalama wa taifa hawasingiziwi kweli kila jambo wao. Haya yote ni matunda ya kikwete, katoa uhuru wa mawazo. Ni maoni yangu tu.
 
Mwaka huu unaweza kutokea muujiza ya Mungu Huko Tanzania na pia kama ndio hivyo basi Mungu saidia sana
 
.

Mstaafu mmoja wa UWT anasema kwamba, vifo vya hawa jamaa,UWT havitangazwa duniani kote kwa sababu ya asili ya kazi yao kwamba moja ya kiapo chao ni kuwa tayari kufa wakati wowote ukiwa kazini. Kiapo hiki ukikikataa siku ya kwanza tu ndio inakuwa ukomo wa kutafuta ajira huko. anasema kujiua pia ni kosa la kiamaadili kwa sababu wana vitengo vya kudhibiti saikolojia kwa kuwa muda mwingi wanahodhi silaha na kujua mambo nyeti. Wanaoweza kutangazwa ni wale viongozi wa juu ambao kanuni imewaweka wazi kwa umma.

Inaaminika kwao kwamba kufikiria kujiua ni jambo la hatari si kwa anayechukua uamuzi huo tu bali hata kwa watumishi wengine na raia wa kawaida wasio na hadhi ya kujitetea.Wakati wote wa kazi za utumishi mfanyakazi anatakiwa kuwa na akili timamu isiyotiliwa mashaka.Fikra za kujiua zinadhibitiwa wakati wote wa somo la saikolojia kwa kuwa kwao kutamani kujiua kunaweza kwenda sambamba na kuua na wengine kabla ya kufikia uamuzi huo.

Anasema taarifa alizonazo ni kwamba kifo cha mlinzi wa Chief Justice ni cha kawaida na ndio taarifa sahihi lakini watu hawawezi kuamini kwa sababu vifo vyao haviwekwi wazi kama ilivyo kwa raia wa kawaida.

Aisee wewe na huyo mstaafu wako mnadanganyana, kifo kifanywe siri kwani huyo mlinzi alikuwa kwenye deep cover mission?
 
Huu ndiyo ukweli wa mambo. Hebu tulia kwenye luninga yako ufanye utafiti wa matangazo yote ya kuihamasisha jamii kuhusu uchaguzi mkuu 2010 pia fungulia redio yako fuatilia matangozo yote ya kuhamasisha jamii kuhusu uchaguzi mkuu kisha tuletee matokeo ya utafiti wako hapa JF. Ukumbuke kuwa matangazo haya yameandaliwa na taasisi mbalimbali za wanaharakati katika nyanja tofauti na mengine yameandaliwa na taasisi za umma. Nikudokeze tu, 99.9/% yanaikumbusha na kuhamasisha jamii na umma kwa ujumla kufanya mabadiliko ya utawala wa nchi, ili kuondoa ufisadi, ulevi wa madaraka, matumizi mabaya ya raslimali za taifa na kuleta na kujenga UADILIFU ULIOPOTEA katika miaka hii ya utawala unaojali FEDHA ZA MAFISADI.:glasses-nerdy:
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom