GE2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

GE2010 Kikwete apewa report ya kura za Slaa

Status
Not open for further replies.
Hata kura za maoni nyingi zinazoendeshwa sasa zinaonesha Slaa anampita JK kwa mbali sana. Kama Slaa ataweza kuwateka watu wa vijijini basi mambo yatakuwa magumu kwa CCM. Chama cha Mafisadi kijiandae kwa anguko la kihistoria. Soon kitaanza kuwa chama cha upinzani. Watanzania wengi sasa wameshaishtukia CCM.
 
Yesterday 02:54 PM #1
Hutaki Unaacha
  • profile.png
    View Profile
  • forum.png
    View Forum Posts
  • message.png
    Private Message
  • article.png
    View Articles
  • add.png
    Add as Contact
user-offline.png

Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
Join DateSun Sep 2010Posts1Thanks0Thanked 58 Times in 1 PostRep Power0
Hapa zinatafutwa sababu za kukataa matokeo?
 
Kwamba Dr. Slaa anapendwa hili halina ubishi.. kuna makosa ambayo CCM wameyafanya kwenye kampeni hii ambayo sikutarajia kwa chama kikongwe na chenye kujua propaganda kingeweza kuyafanya. Makosa haya yanaweza kuigharimu CCM vibaya sana. Ninaamini matokeo makubwa ya kushangaza yatatoka Tanzania vijijini ambako kuna watu wameendelea kutuambia kuwa "ati wanakijiji hawajui tuwape elimu". Watu ambao watatudisappoint sana nina wasiwasi inabakia Dar! Hawa watu wa Dar ndio tatizo kubwa sana la mabadiliko nchini...
Mkuu, Dar imeamka sana sasa hivi. Watu wengi walikuwa hawaoni kuwa upinzani umekuwa kiasi cha kuaminika kuongoza nchi. Ila pia, wapinzani hawakuwahi kuonyesha seriousness ya kutoa mgombea/wagombea wanaoonekana kukubalika kwa miaka mingi. Lakini kubwa zaidi ambalo limebadilisha watu wengi wa Dar, ni utendaji wa serikali inayoomba ridhaa kwa mara ya pili.

JK alipata kura nyingi sana mwaka 2005 kwa kuwa watu wengi waliamini angeendeleza ufanisi wa serikali ya awamu ya tatu. Na kwakuwa alikuwa mmoja wa askari wa miamvuli, alionekana kufaa zaidi. Watu wamegundua kuwa walikosea. Dar haina wajinga Mkuu. Watu wanapiga kampeni ndani ya familia, kwenye vikao vya ndani ili Dr. Slaa achaguliwe. Sijawahi kuona kitu kama hiki katika siasa za Tanzania. Wengi wamekuwa hawajali sana nani anakuwa Rais, au Mbunge.

Mwaka huu, vijana wengi sana wamejiandikisha kupiga kura kwa mara ya kwanza. Na wengi wanasema imetosha sasa, lazima wabadilishe uongozi.
 
Wewe si wa Aug 2010.
Sishangai!!!



KAZIMOTO
Member

Join Date
Thu Aug 2010
Posts
15
Thanks
0
Thanked 1 Time in 1 PostRep Power
0
 
Issue ya REDET na Synovate waulize wenyewe... lakini ukitumia medula oblangata uliojaliwa na Mungu, ulizia uchaguzi wa serikali za mitaa CCM iliibuka na kura kiasi gani? Alafu jiulize ni kitu gani cha ajabu kimetongea tangu wakati huo mpaka sasa? Jiulize kipi CHADEMA imekuja nacho cha ajabu ambacho kitaweza kubadili matokeo kiasi hicho? Jiulize CCM inaowabunge wangapi? Niulize CCM inatarajia kupata wabunge wangapi? Jiulize wabunge na madiwani wa CCM ambao wametapakaa nchi nzima hawana mchango kwa kura za Rais wao.

Sisi waTanzania watu wa ajabu sana tunaamini mazingaombwe mno....

Mkuu Kasheshe, wanachokisema wengi sio u-CCm wala u-Chadema. Watu wanasema JK amewaangusha, amewadanganya na wanachotaka ni kumuondoa yeye tu. Wabunge na madiwani wao, wanaweza kuendelea kuchagulika. Hasira za wengi ni kwa JK ambae anaonekana kutojali maslahi ya wengi na kuendekeza ushikaji.

Ukweli ni kuwa hayo unayoita mazingaumbwe, mwaka huu yatatokea. CCM inaweza kushinda sana Ubunge, ila u-Rais watu wanaelekea kuchoshwa na aliepo.

Kwa mara ya kwanza watu wanasema, CCM ni ya watanzania, Chadema, CUF na vingine vyote ni vya watanzania. Wagombea wote ni watanzania na hawaoni ubaya kumchagua wa upinzani mwaka huu.

Watu wengi walitoa angalizo wakati wa kumtafuta mgombea wa uRais wa CCM. Wakaomba washindanishwe wengi. Ukweli ni kuwa, kama wangekuwa makini wakati ule, JK angeshinda angeweza kupewa nafasi ya kushinda uchaguzi mkuu kwa kishindo pia.
 
mwananchi ukishapiga kura yako kaa mbali na kituo cha kupiga kura umbali wa mita 5! Kwani si kazi yako kuchunga kura bali ni kupiga tu! Kazi ya kuhesabu na kuhakiki kura ni ya wasimamizi wa vituo, hivyo kudai ati mutalinda kura musahau au vinginevyo yatawakuta kama yale yaliyowakuta cuf 2001! Yaani mtu akileta fujo ni mkon`goto tu!!
 

Mkuu Kasheshe, wanachokisema wengi sio u-CCm wala u-Chadema. Watu wanasema JK amewaangusha, amewadanganya na wanachotaka ni kumuondoa yeye tu. Wabunge na madiwani wao, wanaweza kuendelea kuchagulika. Hasira za wengi ni kwa JK ambae anaonekana kutojali maslahi ya wengi na kuendekeza ushikaji.

Ukweli ni kuwa hayo unayoita mazingaumbwe, mwaka huu yatatokea. CCM inaweza kushinda sana Ubunge, ila u-Rais watu wanaelekea kuchoshwa na aliepo.

Kwa mara ya kwanza watu wanasema, CCM ni ya watanzania, Chadema, CUF na vingine vyote ni vya watanzania. Wagombea wote ni watanzania na hawaoni ubaya kumchagua wa upinzani mwaka huu.

Watu wengi walitoa angalizo wakati wa kumtafuta mgombea wa uRais wa CCM. Wakaomba washindanishwe wengi. Ukweli ni kuwa, kama wangekuwa makini wakati ule, JK angeshinda angeweza kupewa nafasi ya kushinda uchaguzi mkuu kwa kishindo pia.

..... mahubiri ya jana sehemu flani Kinondoni yalienda hivi, nanukuu..... MWAKA HUU NI MWAKA WA UCHAGUZI. UCHAGUZI WA MWAKA HUU NI TOFAUTI SANA NA CHAGUZI NYINGINE KWANI SASA HIVI KUNA MAKUNDI MAKUU MAWILI YA WAGOMBEA. WALE WACHA MUNGU NA WAUMINI WA NGUVU ZA GIZA. HATA HUKO BUNGENI MAKUNDI HAYO AHYO YATAKUWEPO. BASI TUMWEMBE MUNGU SANA....

Haya ni baadhi tu yasemwayo. Watanzania wanaelekea kukataa kuendelea kudanganywa. Sasa ukichanganya na wenye access na TEKNOHAMA bila kusahau mobile phones msione ajabu UJUMBE ukawafikia wengi, nao wakaweza pia kutafakari na kusoma alama za nyakati.

Otherwise, STATISTICS hizo hapo ni signicant if the sampling is that random. They will eventually normalize, and as expected, SLAA wins, NGUVU za GIZA na DOLA notwithstanding.
 
Hata kura za maoni nyingi zinazoendeshwa sasa zinaonesha Slaa anampita JK kwa mbali sana. Kama Slaa ataweza kuwateka watu wa vijijini basi mambo yatakuwa magumu kwa CCM. Chama cha Mafisadi kijiandae kwa anguko la kihistoria. Soon kitaanza kuwa chama cha upinzani. Watanzania wengi sasa wameshaishtukia CCM.
Uwezo wa kuhimili kuwa chama cha upinzani CCM hawana kabisa, ni baada ya kubweteka kuwa chama Dola kishicho fikiri namna yeyote ya ku survive kihalali zaidi ya kulazimisha michango ya matajiri na kuchukua fedha za mgawo toka kwa mafisadi.
Ukiona chama cha upinzani kinakuwa kila siku katika hali hii,ujue ndani yake kuna watu wastahimilivu na vichwa hasa sio vya panzi.
 
Chadema: Dk Slaa kinara utafiti wa Synovate
Mwananchi Monday, 20 September 2010 08:10

mbowechadema.jpg

Mwenyekiti wa Chadema ambaye ni mgombea ubunge jimbo la Hai, mkoani Kilimanjaro, Freeman Mbowe, akiwahutubia wananchi wa kitongoji cha Isanja, Sanya Juu, katika mkutano wa kampeni wa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Dk. Willibrod Slaa uliofanyika jana Picha na Edwin Mjwahuzi

Boniface Meena,Siha

MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe amedai kuwa ana taarifa za matokeo ya utafiti uliofanywa na taasisi ya Synovate zinazoeleza kuwa mgombea wa chama chake, Dk Willibrod Slaa aliongoza kwa kukubalika, lakini taarifa hizo hazikuwekwa bayana.

Wiki iliyopita Synovate, ambayo imekuwa ikifanya tafiti mbalimbali za kisiasa, kijamii na kiuchumi, ilitangaza matokeo ya utafiti wake juu ya jinsi ambavyo vyombo vya habari vimekuwa vikiripoti habari za uchaguzi mkuu, lakini taarifa hiyo haikuwa na kipengele ambacho kinazungumzia umaarufu wa wagombea na nani angeweza kushinda kama uchaguzi ungefanyika sasa.


Lakini Mbowe amesema anazo taarifa kuwa Synovate wamefanya utafiti unaoonyesha kuwa Dk Slaa anaongoza kwa asilimia 45 na kufuatiwa na mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete ambaye Mbowe alidai amepata asilimia 41.


"CCM haitaki matokeo haya yatangazwe," alidai Mbowe wakati akihutubia umati mkubwa wa watu kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Isanja ulio Sanya Juu mkoani hapa.


"Synovate haitakiwi iiogope CCM, itangaze matokeo ya utafiti wake bila ya kubadili ukweli.


"Tuna hizo taarifa na niwaambieni tu, Synovate walifanya utafiti kujua ni mgombea gani na chama gani kinakubalika na utafiti wao unaonyesha kuwa Chadema inaongoza kwa asilimia 45 na CCM ina asilimia 41. Lakini, CCM inawatishia wasiitoe ripoti hiyo."
 
""YES, IT IS""
watanzania sio viziwi, wamefunguka! Haiwezekani JK asimame hadharani na kumnadi Lowasa! Hii itaniuma milele.
 
""YES, IT IS""
watanzania sio viziwi, wamefunguka! Haiwezekani JK asimame hadharani na kumnadi Lowasa! Hii itaniuma milele.

Yaani kwa hili nimemuona mkuu wa kaya kweli yuko mfukoni mwa Rostam Azizi na swahiba wake Lowasa. Alitakiwa asome nyakati na kwa hekima kabisa alitakiwa ayaruke majimbo ya Lowasa na Rostam badala ya kwenda kujichafua huko. Hii inatosha kabisa kuwaambia watanzania kuwa tunachezewa akili na huyu rais wetu na hana uchungu na umaskini wa watanzania na hana mpango wa kuutoa uchumi wetu mikononi mwa Rostam na Lowasa na wana mtandao na familia zao.
Nimefurahi sana kuona ndugu zangu wa "Sukumaland" wakiwa wamefunguka macho na kusema "No to CCM". Mwisho wa CCM umeshafika. Kilio cha Watanzania kimefika kwa muumba wao naye amesikia.
 
mwananchi ukishapiga kura yako kaa mbali na kituo cha kupiga kura umbali wa mita 5! Kwani si kazi yako kuchunga kura bali ni kupiga tu! Kazi ya kuhesabu na kuhakiki kura ni ya wasimamizi wa vituo, hivyo kudai ati mutalinda kura musahau au vinginevyo yatawakuta kama yale yaliyowakuta cuf 2001! Yaani mtu akileta fujo ni mkon`goto tu!!

Kwani what is mita 5? Watu watasimama umbali wa mita 5 kutoka kituo cha kura na kuizingira kituo, na hakuna masunduku kuingia wala kutoka! Unafikiri huko Pemba walifanyaje? Mpaka wanapotangaza matokeo ya kura hata usiku wa manane watu hawaondoki.
Na usitake kuwatisha watu na eti matukio ya 2001.. unafikiri tunaogopa? Tumeshafunguka macho na hatuogopi vitisho :mad2: Mnataka kuwatisha watanzania million 40? Hatuwezi kutwaliwa na genge la wahuni wachache! Maneno kama ya kwako ni hamasa tosha kwa wananchi kujitokeza na kulinda kura zao!
 
mwananchi ukishapiga kura yako kaa mbali na kituo cha kupiga kura umbali wa mita 5! Kwani si kazi yako kuchunga kura bali ni kupiga tu! Kazi ya kuhesabu na kuhakiki kura ni ya wasimamizi wa vituo, hivyo kudai ati mutalinda kura musahau au vinginevyo yatawakuta kama yale yaliyowakuta cuf 2001! Yaani mtu akileta fujo ni mkon`goto tu!!

Acha kutufundisha nini cha kufanya wewe, hao mapolisi nao pia wamechoka nenda makambini kwao mpaka leo bado wanakaa kwenye nyumba za bati chini juu, Dr slaa kawaambia atafuta kodi ya vifaa vya ujenzi ili na wao wakae kwenye nyumba nzuri, kwani unadhani wao wanapenda shida..????
 
mwananchi ukishapiga kura yako kaa mbali na kituo cha kupiga kura umbali wa mita 5! Kwani si kazi yako kuchunga kura bali ni kupiga tu! Kazi ya kuhesabu na kuhakiki kura ni ya wasimamizi wa vituo, hivyo kudai ati mutalinda kura musahau au vinginevyo yatawakuta kama yale yaliyowakuta cuf 2001! Yaani mtu akileta fujo ni mkon`goto tu!!

Wewe acha kutishia watu. Unafikiri kila mtu ana akili iliyoganda kama wewe? Mpigakura kulinda kura yake ni haki na ndio maana ya demokrasia. Kama umetumwa kueneza propaganda za vitisho, endeleeni kutishiana huko kwenye vikao vyenu
 
Nimemwona muungwana leo yaani amezeeka mpaka basi.
Nadhani gharama ya UONGO inaanza kulipa deni sasa.
Baada ya NOV ndo ataona akina RA watakavyolala mbele na kumkana kana kwamba hawamjui.

Tufike mahala tuheshimu watu na kuweka UTU MBELE bila hivyo madhara yake si mazuri kabisaaaa
 
Nawaheshimu sana wapiga kura na maamuzi yao. ILa kama ikitokea tofauti na yale ambayo system imeyazoea, nani anaweza kuzuia bao la mkono kama lile la maradona dhidi ya England lisiivushe timu ya upinzani kwenda kileleni?
 
Nimemwona muungwana leo yaani amezeeka mpaka basi.
Nadhani gharama ya UONGO inaanza kulipa deni sasa.
Baada ya NOV ndo ataona akina RA watakavyolala mbele na kumkana kana kwamba hawamjui.

Tufike mahala tuheshimu watu na kuweka UTU MBELE bila hivyo madhara yake si mazuri kabisaaaa

Hebu tuwekee basi picha ya Muungwana basi tumwone na uchovu wake maana alijisahau na alikuwa anakula raha sana miaka 5! :becky:
Na hao akina RA ni kweli watakuwa wa kwanza kumtosa maana hawana principle!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom