Kikwete akagua Mradi wa Maji!

Kikwete akagua Mradi wa Maji!

@
Nadhani hii haikuwa rasmi....!
=======================
Hata hivyo bado naye ni mtanzania ana haki ya kufuatilia kinachondelea katika maeneo anayoweza kufika.
si Kaz yake apumzike anapenda safari asubiri msiba ,maulid na shughuli km hizo!!!
 
sina kumbukumbu za kumuona mkapa akizurura na msafara kama huu baada ya uraisi aliokaa mpaka alipokuja kutuita malofa
Mkapa aliishindwa nguvu ya wanamtandao na Ikulu waliingia kwa nguvu yao kwa hiyo mkapa alikuwa hana chake lakini huyu Ikulu amepelekwa kwa nguvu ya kikwete na ndio maana unamuona mpaka sasa ana nguvu kama utaludisha kumbu kumbu zako nyuma kama vile enzi za nyerere Rais akiwa mzee MWINYI baadae mkapa si unajua rimoti alikuwa nani
 
Anakagua mradi huo wa maji akiwa kama nani katika serikali hii ya awamu ya tano?
 
Katika hiyo picha tuonyeshe aliyevaa hata t shirt ya chama.
mkuu wewe ndo umefilisika hoja kabisa,yani mpaka mtu avae shati ya chama ndo anakuwa mwenyekiti wa chama!!kama ni mfuatiliaji mzuri wa politics Mwl Nyerere enzi zake akiwa mwenyekiti wa chama kuna vikao alikuwa anaviongoza bila hata kuvaa uniform za chama.Nenda kapekue katiba ya ccm utuoneshe kipengele kinachomtaka mwenyekiti avae shati ya chama anapokuwa katika shughuli za kichama.Mwenyekiti wa chama hakomi kuwa mwenyekiti kwa kuvua shati ya chama.UMEKURUPUKA MKUU!
 
dhamana ya kuishauri na kuisimamia serikali iko mikononi mwa Bunge kikatiba na sio chama.

Kama mwenyekiti akakague miradi ya CCM serikali ni ya wa TZ sio ya chama
Usijidanganye ndugu yangu ccm ndio chama dola magufuli akikosea tunasema chama tawala kimekosea
 
Ukisoma comment za watu utaona ni kwa namna gani watu wanachuki na JK na hii yote ni kwa sababu ya ile shughuli ya pale dodoma goli la dakika ya tisini,, mkiendelea kumjadili JK ni kuendelea kumuongezea umaarufu na hata wale wasiojua kwanini anasakamwa watajua sasa,, endeleeni kupambana jamani jamaa yenu bado ananafasi nyingine 2020, mkiendelea kumsakama JK 2020 mambo yatawaendea kombo tena maana mtakuwa mmetumia muda mwingi kumzomea JK asiye na madhara tena na kusahau kumjenga mtu wenu...

Haya sasa pigo lingine hili tena,, JPM kateua makatibu na naibu kamishna, dah kawatupa mbali jamaa fulani kutoka sehemu fulani hivi maana tabia yao ya wizi, unafiki na tamaa ya kuigeuza tanzania nchi ya watumwa wao imeshajulikana na kila mtu anawachukia sasa,,, game bado mbichi kabisa ndio kwanza asubuhi..
Sababu ya shughuli ya Dodoma? Sio ajabu ndugu yetu umelogwa! Yaani hayo yote anayoyavumbua na kuyaweka wazi Magufuli juu ya serikali iliyopita bado unajipendekeza kwa Mkwere? Hujui upotevu huu wa pesa nyingi ndio uliochangia elimu kuzorota, Mahospitalini kukosekana dawa na vifaa tiba hivyo kusababisha maelfu ya ndugu zetu kufa!
Wewe mtu aliyesababisha kifo cha ndugu yako anaweza kuwa rafiki yako kweli? Basi utakuwa na matatizo ya kiakili wapaswa kupata tiba.
 
Ukisoma comment za watu utaona ni kwa namna gani watu wanachuki na JK na hii yote ni kwa sababu ya ile shughuli ya pale dodoma goli la dakika ya tisini,, mkiendelea kumjadili JK ni kuendelea kumuongezea umaarufu na hata wale wasiojua kwanini anasakamwa watajua sasa,, endeleeni kupambana jamani jamaa yenu bado ananafasi nyingine 2020, mkiendelea kumsakama JK 2020 mambo yatawaendea kombo tena maana mtakuwa mmetumia muda mwingi kumzomea JK asiye na madhara tena na kusahau kumjenga mtu wenu...

Haya sasa pigo lingine hili tena,, JPM kateua makatibu na naibu kamishna, dah kawatupa mbali jamaa fulani kutoka sehemu fulani hivi maana tabia yao ya wizi, unafiki na tamaa ya kuigeuza tanzania nchi ya watumwa wao imeshajulikana na kila mtu anawachukia sasa,,, game bado mbichi kabisa ndio kwanza asubuhi..
ficha ujinga wako,kikwete hakumtaka magufuli kikwete alimtaka kaka yake membe,wafuasi wa lowassa ndio waliomchagua magufuli ili membe akose sio unarukiarukia mambo kama wadada wauza bar,huyo jk akipumzika msoga atakosa nini anakagua mradi kama nani,waziri wa maji anafanya kazi gani,mijitu ya pwani mijinga sana ndio maana magufuli kaitosa kwenye uongozi najua na wewe kwa akili zako zinakutosha kuvukia barabara tu ubongo umejaa makamasi kushabikia ujinga ,watanzania dizaini yako mnaongeza idadi ya watu wasio na tija kwa nchi yao tunaonekana tuko mil 45 kumbe kuna mijitu kama bure kabisa,
 
Anakagua maji ambayo hakuyaacha.
anatakiwa achunguzwe kuhusu uraia wake ,mtu gani asiye na huruma ,alitakiwa awe amejifungia msoga huko kwa uzembe na uzururaji aliofanya akiwa rais
 
Hili ni janga la kitaifa.Mswahili hadi awe mstaarabu inabidi ufanye kazi ya ziada

Kweli Watanzania ni waoga sana kustaafu ............. mpaka mafisadi waoga pia!!!

Kuna jamaa alikwa karani wa masijara kwenye wizara flani ............. jamaa pamoja na kufanya kazi kwa muda wa miaka 25 by then bado faili lake lilikuwa linaonyesha kuwa ana miaka 36 tu!! Jamaa alikuwa anachakachua file kuavoid retirement!!
 
Hakuna kitu kinaitwa "Serikali ya CCM" huo ni ujinga waliolishwa watu kwa muda mrefu sana na wakauamini. Chama cha siasa mwisho wake ni kututafutia wagombea lakini si kuisimamia Serikali. Wajibu wa kuisimamia serikali ni wajibu wa Bunge na CCM huko inao wabunge wa kutosha wa kufanya kazi hiyo

Halafu Rais ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM kama wanataka kujua serikali yake inafanyeje kazi si wakamuulizie huko kwenye vikao vyao na kina Nape? Mambo ya chama kushika hatamu ni mifumo ya Kikomunisti na kishoshalisti ambayo kwa sasa haina nafafsi kwenye siasa zetu. CCm imejaa wafanyabishara na mabepari na tunapomuona Mwenyekiti wake Taifa anajifanya kufanya mambo kishoshalist sisi wengine tunajua hizo ni mbinu za siasa za Kmazingaombwe!
 
IMG-20151230-WA0103.jpg


IMG-20151230-WA0101.jpg


IMG-20151230-WA0096.jpg

IMG-20151230-WA0102.jpg

IMG-20151230-WA0100.jpg


IMG-20151230-WA0098.jpg


IMG-20151230-WA0107.jpg

Mkuu hizi ni picha ambazo hazina maelezo.

Je, alikagua kipindi kipi. Wakati akiwa Rais au baada ya kustaafu????

Fafanua tuelewe ili tuweze kusema neno!!!!!!!!!!
 
@Obuma,
Mtumbua majipu anapaswa kutumia akili nyingi Sana..kwanza kutengeneza mfumo wake kuanzia kwenye usalama i.e jeshi!!..pia kama hatoweza kuleta tume huru ya uchaguzi basi aipangue ile..na mwisho kabisa afanye yale aliyokusudia kuyafanya kwa kujamini huku akitengeneza mahusiano mazuri na chama kimojawapo cha upinzani au vyote!!!

Binafsi namshangaa Magufuli na sera ytake anayoiita KUTUMBUA MAJIPU!!!!!

Mbona anatumbua vijipu uchungu na ikiwa majipu mfano TUME YA UCHAGUZI ZA BARA NA VISIWANI (NEC & ZEC) hawatumbui??????

Tunamsifu kwa kutumbua jipu la TAKUKURU majipu yaliyobaki ni NEC & ZEC. mengine vijipu uchungu.
 
Anawaambia wana chalinze, ubunge umemshinda Rizione, aliingia ubunge apate nafasi ya kuwa msemaji apige dili, sasa nafasi za dili na warabu zimefika ukomo, kachanganyikiwa baba mtu kaona aokoe jahazi wananchi waisje andamana hawamtaki mbunge.
 
Back
Top Bottom