Kikwete adai tatizo ni ujamaa!

Kikwete adai tatizo ni ujamaa!

Juma Kaseja (JK) ama unaimanisha Jakaya Kikwete? Huyu ana miaka 60 na ushee sasa yeye mwenyewe inabidi aondoke kwanza.....

Teh teh teh
Namaana ya Jakaya Harufan Mrisho Kikwete, duu sijui naye alirudia darasa la saba, maana kwa kawaida ukiona mtu kafikisha majina 3 kwa Tz anza kumtilia shaka na darasa la saba. Maana walikuwa wanachukua majina harafu wanaongeza yao katikati. Ndiyo hivyo, na ile katiba inabidi urais uwe miaka kama ya wabunge kuuwania.
 
Mbona wapo tu watanzania wengi tu wanaofanya vizuri iwe ulaya au hapa tanzania kuzidi watu wa mataifa mengine, iwe mthungu/mweusi. mbona sita na uzee wakee lakini anajua baya na zuri, mbona slaa na umri wake anajua anacho taka kufanya au anacho takiwa kusimamia na kutolea uamuzi.

Serikali iliyopo imeshindwa kwenye kila kitu sasa wanatafuta mti wa kushikilia na yote ina tereza, kwa mfano suala la uwekezaji katika umeme linatolewa uamuzi na cabinet ambao wameteuliwa na aliye toa kauli na yeye ndio mwenyekiti wao, wanashindwaje kuaamua leo kwenye suala hilo, mpaka maji yakauke ndio waanze sirikali itafanya kila kinachowezekana kuleta umeme. Kushindwa kukua kwa uchumi wetu ambao ndio una leteleza mishahara midogo hautokani na hawa wazee waliopo serikalini bali linatokana na uongozi mbovu tuliokuwa nao, mbona wakati wa mkapa hali ya nidhamu ilikuwa tofauti na sasa.

Ni kweli wapo wanaofanya vizuri lakini nenda ukaangalie ka chombo kanakowaunganisha upime jinsi walivyo ji-organizi. Haha ha ha unanitajia Slaa na Sita, mbona hawa kwangu wote ni ma thugs tu. Unakumbuka Sitta mwanzoni na Richmonds? Unakumbuka alichokipata Zitto wakati hawajadhurumiana?
 
Mkuu sio kutofautiana na itikadi ya chama chake tuu bali hata Katiba ya nchi.

Ibara ya 9 ya Katiba yetu inasema kuwa "Lengo la Katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au wa chochote kati ya vyombo vyake na udugu na amani kutokana na kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, amabyo inasisitiza utekelezaji wa misingi ya kijamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika Jamhuri ya Muungano.

Kwa hiyo, Mamlaka ya Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha pamoja na mambo mengine kwamba nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya demokrasia na ujamaa.

Yaani you said it all.

Katiba ndio nguzo kuu sasa huwezi kuhubiri kitu kinachopingana na katiba unless you change the constitution. Hivi utatungaje sheria inayopingana na katiba?? Mbona tunaanzia kwenye matawi badala ya mzizi mkuu. Pia nakubaliana na wote wanaosema ujamaa, au ubepari hauwezi kuwa suluhisho la umaskini tulionao.

Hivi mbona Rais anakuwa kama mtu anayechambua matatizo tu siku zote na sio mtoa soln???
 
tatizo la tanzania si ubepari wala ujamaa, bali ni uongozi dhaifu usio taka kufanya vitu vya maendeleo, kama tatizo ni ujamaa na hao wazee walio kaa miaka mingi basi wa kwanza kujichukulia hatua ni huyu aliye toa matamshi haya, na mtu yoyote hawezi kuniambia iptl, richmond, epa, rites , ttcl, vodacom, airtell, umetokana na ujamaa?
kenya ni majirani zetu wanafuata ujamaa lakini wana goldenberg, wana rift valley railways, wana serikali inayo watetea ocampo six, dhidi ya waathirika wa vuruga za uchaguzi nk nk nao utasema matatizo yao ni ujamaa.

wewe wasema...mengine yote hapa ni porojo tuuu..tatizo hilo hapo peusi,basi!
 
TATIZO LA TANZANIA SI UJAMAA WALA UBEPARI,BALI UONGOZI DHAIFU by August
Mkuu niruhusu nitumie hii kama signature!
 
TATIZO LA TANZANIA SI UJAMAA WALA UBEPARI,BALI UONGOZI DHAIFU by August
Mkuu niruhusu nitumie hii kama signature!

Tuwe tunaongea ukweli jamani
Ni kweli kabisa uongozi uliopo ni dhaifu bado ni tatizo, uongozi wa marehemu Mwalimu Nyerere ulikuwa dhabiti na imara kabisa usio na rushwa lakini Tanzania ilikuwa masikini mnooo, tulikuwa masikini sanaaaa tulikula ugali wa yanga, tulifulia majani ya miti, na tulijipaka magwanji kama sabuni.Jamani tatizo nini? Uzuri Tanzania imepata kupitia ktk uongozi wa aina yote waadilifu na wanyang'anyi lakini tatizo liko palepale, jamani tatizo ni nini???

UJAMAA NDO TATIZO
Kuna kitabu kimoja huwa nakisomasoma na kinauliza hivi kwanini TANZANIA ni masikini na ilikuwa na JUST leader(Nyerere), wakati malasia iliyokuwa na corrupt leader imeendelea, lakini wakati wa 1960 nchi hizi zote zilikuwa mahala pamoja.
 
Ujamaa siyo tatizo kwa sababu kuna nchi hadi leo bado ni za kijamaa na zimepiga hatua kubwa kimaendeleo, tatizo letu ni nidhamu katika uongozi, imefikia hatua taifa halina mtu mwenye sauti ya kumkemea mwingine kama ilivyokuwa enzi za Nyerere angalau na Mkapa kidogo, watu mnaweza kusema ulikuwa udikteta ndio ni bora uitwe hivyo wakati unahimiza uwajibikaji.

Kikwete ana kofia mbili ni m/kiti wa chama tawala ni rais alikuwa na nafasi nzuri sana kulielekeza taifa liende wapi (kijamaa/kibepari) badala yake yeye ndiye anayelalamika.

Hii inaonyesha weakness katika uongozi yuko weak katika maamuzi hana decision making power(uoga), sasa anatafuta sababu ku justify weakness yake kwa kusingizia ujamaa au kuwasingizia waliouenzi ujamaa, lakini sijui hasa lengo lake ni nini wakati yeye amekulia na kulelewa kwenye ujamaa inamaana hakuliona hilo leo ana 60s ndio anaona.
 
Tuwe tunaongea ukweli jamani.

Ni kweli kabisa uongozi uliopo ni dhaifu bado ni tatizo, uongozi wa marehemu Mwalimu Nyerere ulikuwa dhabiti na imara kabisa usio na rushwa lakini Tanzania ilikuwa masikini mnooo, tulikuwa masikini sanaaaa tulikula ugali wa yanga, tulifulia majani ya miti, na tulijipaka magwanji kama sabuni.Jamani tatizo nini? Uzuri Tanzania imepata kupitia ktk uongozi wa aina yote waadilifu na wanyang'anyi lakini tatizo liko palepale, jamani tatizo ni nini???

UJAMAA NDO TATIZO
Kuna kitabu kimoja huwa nakisomasoma na kinauliza hivi kwanini TANZANIA ni masikini na ilikuwa na JUST leader(Nyerere), wakati malasia iliyokuwa na corrupt leader imeendelea, lakini wakati wa 1960 nchi hizi zote zilikuwa mahala pamoja.
Kwani wewe unaamini Nyerere alikuwa kiongozi bora? Nani alikwambia kuwa wakati wa Nyerere hakukuwa na rushwa,ukiritimba na ugoigoi maofisini?Ni Nyerere aliyekuwa anahamisha watendaji wake wabovu kutoka ofisi moja kwenda nyingine au Nyerere mwingine?Hawa viongozi tulionao sasa ni product ya nani?
 
Ujamaa siyo tatizo kwa sababu kuna nchi hadi leo bado ni za kijamaa na zimepiga hatua kubwa kimaendeleo, tatizo letu ni nidhamu katika uongozi, imefikia hatua taifa halina mtu mwenye sauti ya kumkemea mwingine kama ilivyokuwa enzi za Nyerere angalau na Mkapa kidogo, watu mnaweza kusema ulikuwa udikteta ndio ni bora uitwe hivyo wakati unahimiza uwajibikaji.

Kikwete ana kofia mbili ni m/kiti wa chama tawala ni rais alikuwa na nafasi nzuri sana kulielekeza taifa liende wapi (kijamaa/kibepari) badala yake yeye ndiye anayelalamika.

Hii inaonyesha weakness katika uongozi yuko weak katika maamuzi hana decision making power(uoga), sasa anatafuta sababu ku justify weakness yake kwa kusingizia ujamaa au kuwasingizia waliouenzi ujamaa, lakini sijui hasa lengo lake ni nini wakati yeye amekulia na kulelewa kwenye ujamaa inamaana hakuliona hilo leo ana 60s ndio anaona.

Kwa hiyo enzi za Nyerere tulikuwa tumendelea? kumbuka wakati anang'atuka hali ilikuwa je? the so called madude ya ushirika sijui viwanda yalikuwa yakufa vibayaa. Hebu tuongee na tutafute tatizo hasa, nakubali uongozi legelege kama uliopo pia ni tatizo. Lakini je ndo mwalobaini? ukumbuke pia enzi za Mwalimu vizuri.
 
Kwani wewe unaamini Nyerere alikuwa kiongozi bora?Nani alikwambia kuwa wakati wa Nyerere hakukuwa na rushwa,ukiritimba na ugoigoi maofisini?Ni Nyerere aliyekuwa anahamisha watendaji wake wabovu kutoka ofisi moja kwenda nyingine au Nyerere mwingine?Hawa viongozi tulionao sasa ni product ya nani?

Nyerere naamini kabisa alikuwa kiongozi bora sana tena sana, ndio maana ktk ubora wake utaona ametu integrate watanzania sie hatuna tofauti , lakini umasiki wetu ni kutokana na Njia mbaya aliyochukua Mwalimu ya ujamaa, binafsi simlaumu yale yalikuwa maono yake akifikiri ndo njia sahihi lakini ukweli ilikuwa si njia sahihi.

Ni sawa na mtu anapojitolea kwenda kumuokoa mwenzake aliye zama ndani ya bahari kwa yeye kujitupa naye ktk bahari yumkini naye pia hafahamu kupiga mbizi, na ikitokea wakafa wote siwezi mlaumu maana huyu alikuwa na moyo wa dhati wa kumuokoa aliyetumbukia lakini njia aliyotumia si sahihi, na pia siwezi kusita kumwita kwamba alikuwa na moyo bora kabisa wa kujitolea.

Ndivyo vivyo kwa Nyerere, mengine alifanya kwa ufanisi lakini hili la ujamaa alipotea njia na ndilo bado linatafuna, ni ili kupunguza nguvu zake inabidi wazee kwa asilimia kubwa waondolewe madarakani.

Kitendo cha yeye Nyerere kutokuwa fisadi ni kigezo tosha kabisa kwamba alikuwa mtu bomba, angalia hata familia yake.Huwezi mhukumu yeye kwa sababu ya wanafunzi wake.
Mfano Yesu alikuja akituhubiria tusiibe, tusizini,tusiseme uongo nk lakini leo tunaiba,tunazini tunasma uongo nk, hivyo huwezi sema Yesu alifeli ama alikuwa mwizi kwa sababu sie tunaiba tunazini nk.
 
Ndiyo matatizo ya kukurupuka na kutoa kauli bila kutafakari kwa kina. Dunia ya sasa anayoizungumzia ndiyo ipi? ya kuwakaribisha wawekezaji wasiolipa kodi? Wanaoruhusiwa kuchimba rasilimali na kutuachia 3% tu!? Au wawekezaji wa kutoka Houston, Texas Richmond/Dowans ambao ni matapeli tu na kumbe ni wa Kariakoo tu? Au wale wahindi wa RITES ambao walipewa 51% ya hisa za TRC bila kutoa hate senti moja na sasa wanatakiwa kulipwa $87 millioni, au hawa Wahindi walionunua Zain na Serikali kukosa kodi ya shilingi bilioni 500 kwa uzembe wao wa kufikiri?

Ni aibu kuwa na mtu kama huyu katika nafasi yoyote ile ya uongozi.

Asante saaana mkuu, I salute you for your post, umetuliza sana machukizo ninayopata kwa kuwa na Rais kilaza namna hii!
 
Kwa hiyo nchi tajiri zinaendekeza starehe na uvivu kwa long weekends zao?

Hapana wala haziendekezi. Sisi ambao ni mafukara tunaendekeza hayo mambo zaidi kuliko kujibidiisha katika mambo yenye kuleta maendeleo. Nchi tajiri zinaweza kumudu kuwa wikendi ndefu.
 
Mkandara
Ujamaa ndo huo ukominist walioumodify. Ujamaa mie pia nauita ukoministi ndo ujinga wake huo wa kupumbaza watu wakati wachache wanajilimbikizia.
Mkandara unaongea nini, umeshifika moscow kwa waasisi wa ujamaa? kuna matajiri balaa na masikini balaaaaaaaaaaaaaaaaaaa wanaodanganywa na ujamaa aka ukoministi.
Wewe unafikiri viongozi wa urusi ni masikini, unafikiri akina PUTIN ni masikini , unafikiri Medvedved ni masikini? lakini nenda kule SEBERIA jimbo moja urusi utatoa machozi wewe.

Wewe unachanganya u-Conservative sio ujamaa/ukoministi, u-conservative ni kutokubali mabadiliko. Mfano kule NANSIO ukerewe kuna vijibabu ni vi-conservative ukiwapelekea mke wa kizungu wanakukana wewe sio mtoto wao. huo ndo ukosevertive, na ile mlengo mwingine ni kukubali mabadiliko kwendana na wakati, Mfano kwetu nikienda na mzungu wale mamba hawawezi kuleta fujo maana wanakubali mabadiliko kulingana na wakati.

Ukoministi ndo ujinga wake huo, umekaa kaa kuogopana kuchongeana ninyi kwa ninyi wakati maviongozi yanafaidika na huo ujinga, wajamaa wote Tanzania wakitupwa nje, tukaiingia vijana Tz itapaa.

Bila kupambana kwanza na rushwa /ufisadi, na bila kuyajali maslahi ya taifa kwanza, Tanzania kupaa haitawezekana. Umeingia kutoa maoni yako kabla ya kuielewa hoja ya Mpangala matokeo yake umeishia kubwata nakuubeba ujana wako ambao hauonyeshi hata chembe ya faida kwa taifa. Basi tujenge ubepari wetu wenye misigi ya kwetu badala ya kuwa makuwadi wa mabepari wa nje kama ilivyo sasa bwana mdogo.
 
Mkuu,
Tanzania sio tena makoministi/wajamaa. Tatizo ni kwamba wazee walio na hatamu wanamawazo ya kikoministi na kuendesha serikali kibepari basi wanapoteaaaaaaaaa jangwani. Ndio maana JK, anasema tuwaoondoa hawa wazee na tuweke vijana wenye mawazo ya kibepari kuongoza serikali kiperi. Namuunga JK kwa asilimia 100%. Fukuza wazeeeeee wotee.

Nenda kaombe kazi serikali, teh teh teh kwanza kwenye interview itakuja panel ya watu kama 15, hawa wanalipwa posho wote kufika ktk panel, watakupitisha. na ikitoka hapo itakuja kamati nyingine ya watu 30 ili kupitisha jina lako. ikitoka hapo watapeleka jina utumishi na utumishi watakaa watu 50 kujadili jinsi ya kuingiza jina lako ktk malipo.Utumishi watarudisha jina sehemu ulipoomba nao tena wataita kamati nyingine, upuuzi tupu.
Ujamaa huwezi kuudefine na jinsi serikali inavyoendesha shughuli zake,bali kwa kutumia takwimu za kiuchumi.Kwa mfano,ikiwa asilimia 12% ya uchumi wote unamilikiwa na serikali,maana yake ni kuwa watu binafsi wanamiliki asilimia 88% kwa hiyo hapo ujamaa hakuna! Ila kama serikali inamiliki angalau 40% hapo hiyo serikali huwa considered as a socialist state! kwani kuna fungu kubwa la mapato ya jamii linalomilikiwa na umma!
Kwa hivyo utaona nchi kama ufaransa ni ya kijamaa zaidi ya tanzania!
 
Kulaumu kila kitu bila kujilaumu mwenyewe ni dalili ya mtu aliyeshindwa kufanya tafakari ya ukweli. Umasikini wetu uta semwa ume sababishwa na kila kitu kasoro viongozi wetu. Kweli binadamu hakosi sababu.
 
Nyerere naamini kabisa alikuwa kiongozi bora sana tena sana, ndio maana ktk ubora wake utaona ametu integrate watanzania sie hatuna tofauti , lakini umasiki wetu ni kutokana na Njia mbaya aliyochukua Mwalimu ya ujamaa, binafsi simlaumu yale yalikuwa maono yake akifikiri ndo njia sahihi lakini ukweli ilikuwa si njia sahihi.

Ni sawa na mtu anapojitolea kwenda kumuokoa mwenzake aliye zama ndani ya bahari kwa yeye kujitupa naye ktk bahari yumkini naye pia hafahamu kupiga mbizi, na ikitokea wakafa wote siwezi mlaumu maana huyu alikuwa na moyo wa dhati wa kumuokoa aliyetumbukia lakini njia aliyotumia si sahihi, na pia siwezi kusita kumwita kwamba alikuwa na moyo bora kabisa wa kujitolea.

Ndivyo vivyo kwa Nyerere, mengine alifanya kwa ufanisi lakini hili la ujamaa alipotea njia na ndilo bado linatafuna, ni ili kupunguza nguvu zake inabidi wazee kwa asilimia kubwa waondolewe madarakani.

Kitendo cha yeye Nyerere kutokuwa fisadi ni kigezo tosha kabisa kwamba alikuwa mtu bomba, angalia hata familia yake.Huwezi mhukumu yeye kwa sababu ya wanafunzi wake.
Mfano Yesu alikuja akituhubiria tusiibe, tusizini,tusiseme uongo nk lakini leo tunaiba,tunazini tunasma uongo nk, hivyo huwezi sema Yesu alifeli ama alikuwa mwizi kwa sababu sie tunaiba tunazini nk.

Sikuelewi.Unasema Nyerere ametufanya watanzania tusiwe tofauti?Sijui unazungumzia usawa gani tulio nao Watanzania leo hii.Labda ufafanue-ni usawa wa fursa za kiuchumi na kimaendeleo au ni usawa upi tulionao watanzania leo hii?Au bado unaaamini propaganda ya Tanzania ni kisiwa cha amani,watanzania si wakabila na wadini,ni wamoja?
Unaamini Nyerere alikuwa Kiongozi bora,halafu unakubali kuwa fikra zake hazikuwa sahihi.Kiongozi anakuwaje mzuri wakati fikra zake mbovu?
Tusimlaumu Nyerere kwa sababu ya Wanafunzi wake?Kwahiyo Mwanafunzi akifeli,Mwalimu wake in all circumstances hawezi kuchukua blame?
 
Kulaumu kila kitu bila kujilaumu mwenyewe ni dalili ya mtu aliyeshindwa kufanya tafakari ya ukweli. Umasikini wetu uta semwa ume sababishwa na kila kitu kasoro viongozi wetu. Kweli binadamu hakosi sababu.

Na wananchi wenyewe hawana dhima yoyote katika umaskini wetu?
 
Na wananchi wenyewe hawana dhima yoyote katika umaskini wetu?

mindset za wananchi zimejazwa ghilba za chuki na majungu na wanasiasa; watu hawafanyi kazi na kama wanafanya hawafanyi kwa bidii na ufanisi.
Waliopewa dhamana wanajiona waungu watu (serikalini, taasisi za umma na binafsi na katika vyama vya siasa. Umaskini utaondokaje?
 
Back
Top Bottom