GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

Ni kweli amedondoka madodyguard wa bongo ni wa hovyo wamemwacha hadi mzee mzima analamba mchanga badala ya kumwahi asidondoke jumla!
Duh!!

Ingawa mimi siyo shabiki sana wa K. Kwete tangu avunje ahadi aliyoniahidi mwaka 2005 ya ari mpya, nguvu mpya na maisha bora kwa kila mtanzania, lakini bado namheshimu sana kama kiongozi wa taifa langu. Hao walinzi wake inabidi waadabishwe kama kweli walimwacha mzee mpaka akala dafrao kwanza ndipo wakamuokota ingawa pia inawezekana hawakujua kuwa mzee atarudia tena mchezo huo.

BTW: Mbona K. Kwete amekuwa rais wa kukolapsikolapsi mara kwa mara wakati wa kampeini? Je huku kukolapsi kwake kunaonyesha upungufu wanguvu mwilini na ubongoni mwake kukabiliana na majukumu mazito ya kuongoza taifa maskini kama hili?? Je hii inaweza kuwa inaonyesha kwa nini tangu akamate madaraka hajaweka vizheni imara ya taifa hili bali tunakwenda na upepo tu kama vile hatuna dereva? Je inawezekana kuna sababu ya msingi kutafuta dereva mwingine mwaka huu wa elfu mbili na kumi?

Mimi siyo mtaalamu wa historia ila ni mpenzi mkubwa sana wa historia. Kwa marekani, historia ya karibu inatuambia kuwa Rais Kennedy alikuwa na matatizo sana ya kiafya lakini alikuwa imara sana mbele ya umma na vile vile alikuwa na akili sana kiasi kuwa maumivu yake ya mwilini hayakuingiliana na uwezo wake wa kufanya maamuzi magumu kama yale ya mvutano kuhusu merikebu za Urusi kwenda Kyuba; kwa hiyo raia wa kawaida hawakujua lolote kuhusu matatizo ya kiafya ya Kennedy hadi baada ya kuwa ameuwawa ndipo watu wake wa karibu wakayatoa nje. Kwa huyu mzee wetu kuanguka anguka hadharani mara kwa mara bila hata kuwa ameweka mataputapu kunaonyesha kuwa huenda ana matatizo makubwa sana kuliko tunavytaka kuamini, na matatizo hayo yanaweza kuwa yanaingiliana na uwezo wake wa kufanya maamuzi magumu ya kitaifa.

History will tell..............
 
...mmm, taratibu mkuu! mimi nimeona kama ni kidole kilichojitokeza cha kiganya cha yule sekurity mwenye kisogo mbele ya yule aliyevaa mawani, au??:confused2:

Nadhani ishu hapa ni hicho kidole nilichowekea mduara. Sijaweza kuamini kama kweli ni gumba la mguu wa mheshimiwa K. Kwete.



2yz9yxh.jpg
attachment.php
 
Je hawa jamaa wanajua wanachofurahia au wanafanya kazi kwa vile wamelipwa? Si hawa jamaa ndio waliotumika pia kwenye mradi wa Maralia kwa kutumiwa na Januari Makamba?? ( Mwenzao leo ni mbunge na waziri mtarajiwa na wao bado waburudishaji au wasindikizaji tu!!)


IMG_0049.jpg



Inawezekana akina mama hapa chini wanaoata uchungu wa wazazi kuona mmoja wa atoto wao anapata dhahama kama iliyomkumba mtukufu mhesimiwa rais, ila sidhani kama kuna cha zaidi ya huo ubinadam kuwafanya wasikitike kama vile eti kuona kuqa mwanga wa kueleka kwenye maisha bora kwao na kwa kila mtanzania unataka kuzimika. Siyo kweli, kwa sera za CCM watabaki vivyo hivyo


5yhkip.jpg

 
VIJANA JAZZ BAND...NAO WALITUMBUIZA....ukiacha kina BITCHUKA.....NA WENGINE KIBAO....KWA KWELI WASANII WENGI WANAKIKUBALI HIKI CHAMA.........aaaaaahh nilitaka kusahau.. CHEGE NA MHESHIMIWA TEMBA NAO WALIKUWEPO HASA NYIMBO YAO YA MKONO MMOJA WEKA JUU...WEKA JUU....... it was colourful day for CCM SUPPORTERS.......!
 
I believe here in JF is where we dare to talk openly. Nimeambatanisha video iliyokuwa imeondolewa ya JK kuanguka jangwani 2010.
 
Last edited by a moderator:
Naomba MKUU yeyote mwenye picha za video na mnato zinazoonyesha JK alikpokua anaanguka pale jangwani, ili ambao hatukuwa kwenye TV za bongo tuweze kushuhudia

Nawakilisha hoja
 
Last edited by a moderator:
jamani tuachane na huu udini, Hali ya mgonjwa ni aje? yupo muhimbili/nyumbani kwake anapumzika au wamempeleka nje ya nchi?
Nakubaliana nawewe mkuu,
Hivi JK kwa sasa yuko wapi?
Anafanya nini?
Na hali yake vipi?
 
Nadhani ishu hapa ni hicho kidole nilichowekea mduara. Sijaweza kuamini kama kweli ni gumba la mguu wa mheshimiwa K. Kwete.



ukiangalia hiyo picha utaona makosa mengi mno ya hawa jamaa zetu wa UWT,
1) wote wamejitofautisha kabisa na Target (raisi), dress code yao inatoa mwanya mkubwa kwa snipers kujua nani ni nani, na hapo maana halisi ya bodyguard inapotea, ingekuwa busara kwa baadhi ya hao jamaa kuvaa nguo zinazofanana na Target,

2) ukiangalia hiyo picha, hicho kijiji chote cha UWT kimeconcentrate kwa Mgonjwa, na hakuna hata mmoja anaeangalia upende mwingine wowote, zaidi ya kuangaika kumbeba

3) Afya ya rais nadhani inajulikana zaidi na watu wa UWT, hivi kweli wanaweza kuja hapo au kutembea na raisi bila kuwa na kikosi cha Paramedics?, as far as i know hao jamaa wako trained kumguard huyo Rais, kwa hiyo palipaswa kuwa na kikosi kingine cha UWT ambacho kingefanya kazi hiyo ya kumzoa na kumshughulikia Mgonjwa wakati hao Bodguards wakiendelea na zoezi lao la ulinzi kama kawaida

4) nasema hao jamaa hawako trained kwa first aid, maana kwa ugonjwa wa kuanguka na hicho kiwingu kiasi hata huyo mgonjwa anakosa hata pa kupumulia

4) kunakuwaga na askari mwenye kitambi kikubwa nyuma ya raisi mara nyingi, vipi kwenye hii tukio hakwepo?, maana nadhani yeye ndio angekuwa wa kwanza kumdaka kabla hajafika chini, au yeye ni wa mapambo tu?
 
VIJANA JAZZ BAND...NAO WALITUMBUIZA....ukiacha kina BITCHUKA.....NA WENGINE KIBAO....KWA KWELI WASANII WENGI WANAKIKUBALI HIKI CHAMA.........aaaaaahh nilitaka kusahau.. CHEGE NA MHESHIMIWA TEMBA NAO WALIKUWEPO HASA NYIMBO YAO YA MKONO MMOJA WEKA JUU...WEKA JUU....... it was colourful day for CCM SUPPORTERS.......!


......ishu sio kwamba wasanii wanakikubali CHAMA ..... JK ameshaongea na don wa wasanii ..CLOUDS ...hakuna msaniii ambaye CCM itamtaka akatumbuize imkose....wanawalipa vizuri...na wanawapa deal nyingine ie malaria no more!!!

...siku wakipanda chadema au CUF ....kama kuna msanii atakayedhubutu kupanda basi ni wale ambao ....wameshajitoa muhanga......kama kina mkoloni,john walker,etc ambao hawapo kwenye ufalme wa ruge na kusaga!!
 
I believe here in JF is where we dare to talk openly. Nimeambatanisha video iliyokuwa imeondolewa ya JK kuanguka jangwani 2010.


That's what I'm talkin' bout....zama hizi sio zama za mwaka '47....

Walijidai wametoa kumbe kuna machizi wameshainyaka....ahahahahahahahaaaaaa......
 
Last edited by a moderator:
Halafu nna swali la kizushi, hivi ukiwa UWT bongo shurti uvae Kaunda suti??????????????????????



2yz9yxh.jpg


Ha ha ha
Mkuu Nyambala, the guys wa PSU are so distinct utawaona bila kuuliza
1 Kaunda suit nyeusi au kijivu
2 wanamapanki
3 wote viuno vimetuna(silaha)
4 kutokana na mazoezi nafikiri wote ni weusi tii
Bahati mbaya kuna wenye vitambi uchwara, wangeshauriwa wabadili muonekano, you can smell them a mile away.
 
Pole sana Mhe Jakaya Kikwete.Watanzania waoga sana huyu mtu aliamua kutoa video kwa nini kwani si kila mtu alifika jangwani.walishaanguka watu wengi hata rais wa marekani George Bush mwaka 1992 alianguka lakini hawafichi hizo picha ,huyu JK ni rais wa watanzania wote hata matibabu anayoweza kupewa ni kutokana na kodi za wa tanzania.Nchi hii imeharibika kwani watu hawajiamini kabisa kwani hata kuchukua fomu za kugombea urais ndani ya sisi emu, ccm watu wengine waliogopa lakini Bwana Shibuda akajitokeza na baadaye sijui kilichotokea ndipo alipo withdraw forces zake na akaamua kumchangia kikwete hela .Tukumbuke kuwa JK aliyokuwa anayaaongea kabla ya kuanguka yote yalikuwa yana msuta kuanzia kupunguza gharama za matumizi ,kutegemea misaada ,kukusanya mapato hadi kupambana na rushwa japo mafisadi hata hakuthubutu kuwataja maana yeye ni mmojawapo kwani alichota mahela ya walipa kodi akafanyia kampeni na kuiba kura mwak 2005 na huyo aliye chota hizo heal katika watu waliomba kazi shirika la nyumba kama GM alipewa kwa lazima japo kuna taratibu za kuajiri zilikuwa zinafuata lakini alilipwa fadhila mzee chilig akiwa ndiye aliyefanikisha zoezi hilo.Jangwani ni sehemu takatifu pia kuanzia hapo hapo watanzania wanaoishi mabondeni wana maisha duni kabisa lakini huyu mhe anawaongopea watu.Tayari amezunguka dunia nzima na hata first lady anazunkuka na msafara mkubwa na wanatumia fedha za walipa kodi kama ni kiongozi kumbe ni 1st lady tu.
 
Halafu kweli kutoka Jangwani anaenda Mwanza? I hope siyo Kirumba. Rais Kikwete akianguka tena wakati huu wa kampeni aamue kujitoa tu kwani mtu unaweza kuijaribisha fate kwa kiasi fulani lakini at the end fates win. Na mimi nitawawajibisha hawa enablers wake kama wale wa Michael Jackson!!!
 
Halafu kweli kutoka Jangwani anaenda Mwanza? I hope siyo Kirumba. Rais Kikwete akianguka tena wakati huu wa kampeni aamue kujitoa tu kwani mtu unaweza kuijaribisha fate kwa kiasi fulani lakini at the end fates win. Na mimi nitawawajibisha hawa enablers wake kama wale wa Michael Jackson!!!

Yaani what I see in our country is more than this problem, hawa apologists wa Muungwana nadhani hata akizimia wiki, God forbid, wataendelea tu kutuaminisha the guy has a sound health! Tunakuwa kama vile tuko China?

What do you think angekuwa Lipumba au Dr. Slaa ameanguka hivyo hadharani???????

Kwa kifupi bongo hamna nuwz organizations, they are just apologists and funny enough unaweza kukuta hakuna mtu aliyetoa maelekezo ya kuzuia hiyo coverage bali uwoga wa hao wapiga picha na anchors wao!!!!!!!!!!!!!!!!! Halafu JK anasema eti ktk utawala wake amewezesha uhuru wa vyombo vya habari............ This was a test and better jus in the beginning, U just failed it buddy!!!!!!
 
Kuanguka si tatizo, tatizo ni kuanguka mara nyingi. Pia kusingizia saumu, kama saumu unakufanya uanguke kwanini kufunga? Siaache.

Wengine hawataki tumjadili lakini wajue tunamjadili kwa kuwa anatuhusu kama rais wa nchi na mgombea wa urais.

Ajitoe kwenye nafasi hizo ili tusijadili afya yake.
 
Back
Top Bottom