GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

Ndio maana Zanzibar wamesitisha kampeni wakati wa mfungo wa Ramadhani.Hata hivyo mpiganaji anayeanguka na kuinuka kuendelea na vita ni mpiganaji shujaa aliyedhamiria kuendelea na vita na anayejiamini kwa analopigania./
 
Unajua huo mguu sikuuona aisee

Halafu yaani hakukuwa hata na stretcher ya kumbebea? Shameful..

Hii ndio shida ya Tanzania. Kwanza Rais hakutakiwa kubebwa, walitakiwa wamlaze chini wamzunguke.
Kumbeba mtu aliyekuwa karibu na kuzimia saa ingine kunaweza kuwa na madhara.

Halafu huyo Kinana na daktari wa Rais waache kutudanganya!! Toka lini SUKARI IKISHUKA INASABABISHA KUSHUKA KWA SHINIKIZO LA DAMU KIASI CHA KUZIMIA/KUKARIBIA KUZIMIA? Na kama ni kweli, mbona si kila wakati anapopatwa na hali hii anakuwa amefunga? Msifikiri watu wote ni mambumbumbu! Pili, kama ingekuwa kweli sukari imeshuka, Rais asingeweza kunyanyuka na kupanda ngazi mwenyewe kuingia kwenye mobile clinic kama tulivyoambiwa. Inawezekana Rais ana matatizo ya moyo, ndiyo huweza kuwa na dalili kama alizokuwa nazo: yaani kama uliangalia vizuri ile clip (kabla 'monster hajaitafuna' kama wadau humu wanavyosema), basi utakuwa ulimsikia na kumwona Rais akisema, 'Aisee!' na sura kubadilika kidogo na akaanza kuanguka - hiyo inaitwa pre-syncope, na mgonjwa huweza kuamka hiyo hali ikishapita.

Kama kweli sukari na shinikizo la damu vyote vilishuka, basi ni vizuri Rais akapimwa ufanyaji kazi wa mfumo wake wa tezi (endocrine system) kwani inawezekana ana tatizo la hormone - na labda ndio iliyokuwa maana yake mwaka jana aliposema kuwa amepimwa akili (labda walimfanyia MRI/ CT scan kuangalia tezi kuu mwilini inayoitwa pituitary (samahani sifahamu kwa Kiswahili).

Shida ni kwamba huyo daktari atakuwa na mwenyewe kajaa siasa tu.

Ni hayo tu. Kwa leo. Sina kawaida ya kutoa maoni ya kitiba lakini leo wamenitibua!
 
du, ahsante sana wote waliotuletea video katika Youtube..
pole JK. inabidi root cause ya tatizo hili la kuishiwa na nguvu na kudodoka litatuliwe na siasa iondolewe katika afya!!. Dr. Mfisi hebu toa ufafanuzi!!
 
yaani kama uliangalia vizuri ile clip (kabla 'monster hajaitafuna' kama wadau humu wanavyosema)

Mkuu injinia ile clip imetundikwa tena angalia post #516. It is important pia mods mkaitundika kwenye first post and this time iwe locally saved.
 
Ndio maana Zanzibar wamesitisha kampeni wakati wa mfungo wa Ramadhani.Hata hivyo mpiganaji anayeanguka na kuinuka kuendelea na vita ni mpiganaji shujaa aliyedhamiria kuendelea na vita na anayejiamini kwa analopigania./
Haya ndio mimi huwa naita maoni ya enzi za ujima! Mtu mgonjwa watu wanaleta ushabiki!!
 
Mkuu injinia ile clip imetundikwa tena angalia post #516. It is important pia mods mkaitundika kwenye first post and this time iwe locally saved.

Nimeona, asante. I wish ningekuwa naweza kui copy niweke kwenye kabrasha langu
Yaani jana nimeshangaa sana. Nilipiga simu nyumbani kuongea na ndugu zangu. Wakati Rais anapatwa na shida hii hawakufahamu kwani walikuwa safarini, kufika nyumbani jioni wameangalia taarifa ya habari, mimi nikapiga simu nikauliza kama wameona Mh Rais yaliyomsibu wakabaki kunishangaa. Yaani mimi niliye mbali na Tanzania ndio nimewataarifu walioko ndani ya Tanzania!!

Kweli mkono wa CCM mrefu. Ila namshukuru huyu mdau aliyerudisha clip hapa
 
Ndio maana Zanzibar wamesitisha kampeni wakati wa mfungo wa Ramadhani.Hata hivyo mpiganaji anayeanguka na kuinuka kuendelea na vita ni mpiganaji shujaa aliyedhamiria kuendelea na vita na anayejiamini kwa analopigania./

Acha hizo wewe, mtu anaumwa halafu unasifia ujinga badala ya kulaani wao kumrudisha kuongea wakati he was not fit... we hukuona alivyokua anashindwa kupanga hata karatasi??? When he came back, he was disoriented and that was not good

Ushujaa upi unaoutaka wakati mtu anateseke, kama ni ushujaa, basi angekuja na kusema wazi kwamba alizidiwa na aseme ukweli kuhusu hali yake

nimesoma sehemu wanasema huwa anakaidi baadhi ya ushauri wa madaktari... inabidi apate good washauri nasaha
 
Kwa mujibu wa Tanzania Daima;
Alipopanda jukwaani na kuanza kuhutubia tena, Kikwete alianza kwa kusema: ¡°Nimefungulia jamani¡*niliishia hapa kwenye¡*naona wamevuruga hotuba yangu¡±
Shida yangu ni hapo mwisho anaposema naona WAMEVURUGA hotuba yangu.Je mh. Rais anahisi kuwa kuna watu walio nyuma ya tukio la yeye kuanguka?Jus thinkin aloud.
 
Du! Naanza kuamini kwamba Jangwani kuna nguvu ya Upako wa Mungu. Atokaye kwa kina Sangoma S/wanga, B/moyo, Tanga na Pemba asitie mguu kamwe
Leo atapiga mzinga kule kwa wasuma maana alisha mtest wakaona mweupe...JK acha ubishi wako pumzika ulee...na sikia una mtoto mchanga
 
Kwa mujibu wa Tanzania Daima;
Alipopanda jukwaani na kuanza kuhutubia tena, Kikwete alianza kwa kusema: ¡°Nimefungulia jamani¡*niliishia hapa kwenye¡*naona wamevuruga hotuba yangu¡±
Shida yangu ni hapo mwisho anaposema naona WAMEVURUGA hotuba yangu.Je mh. Rais anahisi kuwa kuna watu walio nyuma ya tukio la yeye kuanguka?Jus thinkin aloud.
Hapa nadhani alikuwa anazungumzia zile purukushani za kumbeba... wali-mix up zile karatasi. Hili ni jambo la kawaida kwenye purukushani. Mimi ninachoshangaa ni kuwa ilikuwaje wamruhusu tena ajaribu tena kuendelea na hotuba?
 
Pole sana Mhe Jakaya Kikwete.Watanzania waoga sana huyu mtu aliamua kutoa video kwa nini kwani si kila mtu alifika jangwani.walishaanguka watu wengi hata rais wa marekani George Bush mwaka 1992 alianguka lakini hawafichi hizo picha ,huyu JK ni rais wa watanzania wote hata matibabu anayoweza kupewa ni kutokana na kodi za wa tanzania.Nchi hii imeharibika kwani watu hawajiamini kabisa kwani hata kuchukua fomu za kugombea urais ndani ya sisi emu, ccm watu wengine waliogopa lakini Bwana Shibuda akajitokeza na baadaye sijui kilichotokea ndipo alipo withdraw forces zake na akaamua kumchangia kikwete hela .Tukumbuke kuwa JK aliyokuwa anayaaongea kabla ya kuanguka yote yalikuwa yana msuta kuanzia kupunguza gharama za matumizi ,kutegemea misaada ,kukusanya mapato hadi kupambana na rushwa japo mafisadi hata hakuthubutu kuwataja maana yeye ni mmojawapo kwani alichota mahela ya walipa kodi akafanyia kampeni na kuiba kura mwak 2005 na huyo aliye chota hizo heal katika watu waliomba kazi shirika la nyumba kama GM alipewa kwa lazima japo kuna taratibu za kuajiri zilikuwa zinafuata lakini alilipwa fadhila mzee chilig akiwa ndiye aliyefanikisha zoezi hilo.Jangwani ni sehemu takatifu pia kuanzia hapo hapo watanzania wanaoishi mabondeni wana maisha duni kabisa lakini huyu mhe anawaongopea watu.Tayari amezunguka dunia nzima na hata first lady anazunkuka na msafara mkubwa na wanatumia fedha za walipa kodi kama ni kiongozi kumbe ni 1st lady tu.


ANOTHER Monster JOINED WITH PUMBA
 
Kumbe Mama Salma nae alianguka!Hiyo habari ni kwa mujibu wa Habari Leo.I just hope hawataiondoa.
 
Hapa nadhani alikuwa anazungumzia zile purukushani za kumbeba... wali-mix up zile karatasi. Hili ni jambo la kawaida kwenye purukushani. Mimi ninachoshangaa ni kuwa ilikuwaje wamruhusu tena ajaribu tena kuendelea na hotuba?

Nafkiri ni approach nzuri, maana asingerudi kumalizia hotuba, wananchi wangejua yupo katika hali mbaya sana, nadhani ilikuwa katika kuweka mambo saa ndo maana hakuongea kwa muda m refu aliporudi mara ya pili, na nahisi hotuba ilikuwa ndefu zaidi ya pale, ila ilibidi afanye hitimisho tu.
 
Kumbe Mama Salma nae alianguka!Hiyo habari ni kwa mujibu wa Habari Leo.I just hope hawataiondoa.

Ni kweli Habari leo imeandika Mama Salma pia alizidiwa wakati anaenda kumjulia hali mumewe.

" Wakati huo huo, katika hali isiyotarajiwa, mkewe Mama Salma naye alijisikia vibaya uwanjani hapo na kusaidiwa na kupelekwa kwenye zahanati hiyo, kupewa huduma ya kwanza.

Mama Salma wakati akielekea kwenye zahanati hiyo kumjulia mumewe hali, alipokaribia alidondoka na kudakwa na walinzi wake na wakati anaingizwa kwenye zahanati hiyo, alipishana na mumewe mlangoni akitoka. "


Sasa wote wagonjwa. Kazi kweli kweli, na mabody guard wanakazi ya kuwadaka kila wanapokaribia kudondoka
 
Wananchi wenzangu tunaojiuliza 'kulikoni raisi aanguke' naomba tujadili kwa dhati ya mioyo yetu kabisa na tutake majibu mazuri kabisa na kutoa ushauri na wanaopokea ushauri wautendee kazi. Ifike mahali taaluma za watu zifanye kazi na kazi hiyo ionekane. Watu waliopewa dhamana ya kuwa karibu na raisi waache mzaha na mambo ya kawaida tu. This is serious.

Mwaka 1997, Raisi Kikwete alipokuwa waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, alizidiwa ghafla na kuanguka uwanja wa ndege wa Brussels, Ubeligiji akiwa safarini kuelekea nchini Cuba.

Mwaka 2005 katika kampeni, alizidiwa hapo hapo viwanja vya Jangwani Dar Es Salaam na kuanguka ghafla ikabidi kupatiwa huduma ya dharura.

Raisi aliwahi pia kuanguka mjini Mwanza.

Majuzi hivi amepatwa na dharura ya kuishiwa nguvu.

Leo kuanguka tena Jangwani ni tukio la ngapi, la tano, hadharani, hatuna uhakika na ambayo hatujayaona.

Wananchi tulipodai kupatiwa taarifa ya afya ya raisi wetu, baadhi ya watu na watendaji walidhani ni kebehi au kutaka udadisi usiokuwa na sababu, wakasahau kuwa Wananchi ni waajiri wa Raisi na wanapokuwa na wasiwasi juu ya usalama wa afya ya Raisi wao, pia hukumbwa na kiwewe na maneno mengi yakasemwe 'ndivyo sivyo', hatimaye kilio chetu kilisikika, na daktari wa Raisi akazungumza. Kama tulivyo wengi, na mapokeo yalikuwa mengi, wapo waliohoji undani wa ripoti ile kuwekwa hadharani na wapo waliohoji ni kwa nini ifichwe.

Wanaotunyima kujua hali ya afya ya raisi wanashindwa kuelewa kuwa wanajidanganya wenyewe, wanatudanganya sisi na wanamdanganya raisi, mwishowe tumebabaishwa tu.

Mimi si daktari wala mshauri wa Raisi, ila kwa mtizamo wangu na kwa vigezo vya fani yangu, nitasema Raisi anahitaji Mtaalamu wa Saikolojia. That's what he needs right now. Nifafanue. Mtu yeyote anapokumbwa na tatizo ambalo ni vigumu kulikabili (out of control) mara nyingi tatizo hilo huwa kama jinamizi kwake, na aghalabu jinamizi ni hali ya kuteseka kisaikolojia kwa woga na hofu ilyiopindukia (exaggerated fear), hii hutokea punde tu unapokuwa katika mazingira yale au yanayofanana na yaliyosababisha ukapatwa na tatizo uliloshindwa kulikabili. Hivyo ni dhahiri kuwa utakapokwenda kwenye eno lile lile, utakumbwa na mfadhaiko na woga na hofu yako itakutawala na utajikuta umeangukia tatizo lile llile (succumb to the same problem). Hali hii ndiyo inayowapata hata watu wenye kifafa, akiwa katika mazingira fulani ndipo anaanguka au kuweweseka. Linawapata pia watu wenye phobia. Na tTatizo la saikolojia kuliondoa linahitaji mtaalamu wa Saikolojia.

Nimemaliza!
 
Ni kweli Habari leo imeandika Mama Salma pia alizidiwa wakati anaenda kumjulia hali mumewe.

" Wakati huo huo, katika hali isiyotarajiwa, mkewe Mama Salma naye alijisikia vibaya uwanjani hapo na kusaidiwa na kupelekwa kwenye zahanati hiyo, kupewa huduma ya kwanza.

Mama Salma wakati akielekea kwenye zahanati hiyo kumjulia mumewe hali, alipokaribia alidondoka na kudakwa na walinzi wake na wakati anaingizwa kwenye zahanati hiyo, alipishana na mumewe mlangoni akitoka. "


Sasa wote wagonjwa. Kazi kweli kweli, na mabody guard wanakazi ya kuwadaka kila wanapokaribia kudondoka


url
 
Yaani Mganyizi, kwa mara ya kwanza, hasa kuhusiana na maswala ya kisiasa, nakubaliana na wewe asilimia mia.

Umenena
 
Back
Top Bottom