Riwa
Platinum Member
- Oct 11, 2007
- 2,607
- 3,068
Wakuu hakuna siri chini ya jua!!!!
(Sitataja wapi kilikalika na nani walihudhiria, bali nitamwaga mikakati tu iliyoadhimiwa)
Intelijensia iliyopandikizwa katika kikao maalumu cha ccm leo jioni kinachotafuta ushindi wa hila Kalenga, imenasa mtiririko wa mikakati hii hapa chini,
1. Karatasi za kupigia kura ambazo zimewasili jana na leo kule Kalenga zimetengwa maalumu kwaajili ya kupewa wajumbe wa nyumba kumi na wanaccm waaminifu kila mmoja karatasi (tupu) kuanzia 10-100,
2. Jumapili wajumbe hao watakwenda kupiga kura huku wakiwa na karatasi hizi mifukoni mwao, wakifika watakabidhiwa vitendea kazi vya kupigia kura kama kawaida, wakifika kwenye chumba maalumu cha kupigia kura, watazitoa sasa zile karatasi na kuzipigia zote upande wa ccm na kuzikunja kwaustadi mkubwa sana kisha kuja kuzitumbukiza kwenye sanduku la kura,
Hapo kila mtu wao atakuwa na uhakika wakupiga kura kumi na kuendelea,
Katika kikao hiki wanajisifu kuwa mbinu hiyo imewaokoa sana kwenye chaguzi za madiwani wiki chache zilizopita,
NB
Tume ya uchaguzi mpaka leo hii haijui idadi halisi ya wapiga kura Kalenga, Lubuva ameanza mawenge anasema tayari wanalo daftari la wapiga kura la 2014 hivyo litatumika hilo badala ya lile la 2005/2010 linalotambuliwa na uuma wote, hebu jiulize ni lini yalifanyika maboresho ya daftari hilo kwa mwaka huu wa 2014?
PENDEKEZO LANGU,
Chadema ihakikishe inawaambia mawakala wao wahakikishe wanakuwa jirani kabisa na sanduku la kupigia kura, na kila anaetumbukiza kura waangalie kwa umakini kama kakunja karatasi mbili au moja?
Ama ikiwezekana kila mpiga kura akaguliwe kwa uangalifu kabla ya kuruhusiwa kwenda kupiga kura.
Chapeni kazi Yericko acheni kuomba sympathy hapa kijinga...kila siku oooh tunachezewa faulo, kila siku oooh tunaibiwa...hizi singo tushazichoka bana, toeni albam mpya yenye mashiko. Mbona mnaanza kutukatisha tamaa na Chadema yetu!? ka mmeshindwa kazi kubalini tu make pembeni nasi tuje kujaribu...bla bla blaaah kila siku!