Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Hebu naomba nisaidieni, wanaoharibu mustakabali wa nchi ni watu waliopo CCM au jina tu CCM?
ni mfumo wa ccm ndo hatari. mfumo wa ccm ndo unaowalea wezi na mafisadi. dawa ni kuuondoa huo mfumo na si kudeal na mtu mmojammoja.

pale ccm hata ukipeleka malaika hawezi kubaki safi sababu mfumo wote wa ccm ni mchafu kuanzia juu hadi chini.

embu nipe sababu za kwanini lowassa alipokuwa ccm ulitaka asiibe ili iweje? kwa nini asiibe wakati wenzake wote wanaiba? ambao hawaibi ccm imewapa heshima gani zaidi ya kuwatenga na kuwadhalilisha? kina warioba ambao si wezi wamefanyiwa nini na ccm?

wastaafu waliokuwa wanaitumikia ccm kiuadilifu, na hata watumishi waadilifu ndani ya serikali ya ccm leo hii, wamefanyiwa nini na ccm? ukiwa ccm kuwa mwizi si optional ni lazima.

Ukiwa ccm na ukataka kuacha wizi na uzembe hatua ya kwanza ni kutoka nje ya ccm kama alivyofanya lowassa.
 
Lazma tukubali jamani, dr.slaa, prof lipumba hawana nguvu ya kumshnda magufuli akiwa na ccm katika uraisi.

Na hata kama tukisema slaa au lipumba agombee uraisi , hawatashnda huo ndo ukweli. Na magufuli alishajua kashnda, ila kwa ujio huu wa lowasa lazma ccm ikune vichwa, na itawabidi wafanye kazi ya ziada kama kweli lowasa atagombea upinzani!

Kila mtu anamjua lowasa, na tuhuma zilizokuwa zinamsibu, lakini mambo ya siasa hatuwez jua ni nini kilichotokea kihalisia. Wananchi tunampenda lowasa, despite ya yote hayo wanayomsingizia.

Kiukweli 2010, uraisi nilimpa slaa. Na 2015 bada ya EL kukatwa nilipanga kumpa magufuli, lakini kama lowasa atagombea akyamungu, kura yangu anayo.

Siasa ina siri kubwa,
 
Sote tunakumbuka kuwa kwenye ile list of shame ya slaa ya watu 11 Lowassa alikuwa mmojawapo.

Leo hii Slaa itabidi aanze kwanza kumtoa kwenye ile list na kuwabakiza 10. Kwamba nilikosea kumtaja Lowassa, kwani majina niliyoletea na vijana wangu yalikuwa 10 shetani akaongezea na la Lowassa, ashindwe na alegee kabisa, hahaaaaa!

Ndugu wananchi nawahakikishia Lowassa ni kamanda na mtu msafi kabisa kuliko mnavyofikiria.

Pipoooooooooooooooz!!! Pawaaaaaaaaaaaaaaaa.

Wakati wale wa ESCROW wanasafishwa, tena bungeni, ulipata picha..??
 
Mkuu umezungumza kweli tupu na mimi naongeza kuwa kwa mwendo huu hakunachama cha kizalendo wote wapigaji tu! Dr.slaa na lisu wanachakutuambia wanachadema !

Naomba kama haya yasemwayo ni tetesi basi yabaki hivyo lkn dr.slaa ama mwingine yoyote lkn co huyo lowasa tutapoteza tena

Inatia huzuni sana,najiuliza mara mbili mbili sipati jibu.Wametuona watanzania wapuuzi sana.Yaani ninaumia nikikumbuka wanachama walivyojitoa muhanga kuitetea CDM,wamepoteza familia na wengine viungo vyao,leo wanamuweka mtu ambaye hata kuwatetea BUNGENI tu hakuthubutu,leo wanamuona wamaana kuliko hawa wanachama?

J J Mnyika atuambie Bungeni alikuwa anatetea nini?Na sasa anafanya nini?Ngoja nifanye maamuzi magumu sasa.

Watanzanzania wote wenye mapenzi mema sema HAPANAAAAAAAAAAAA kwa Lowassa
 
Hivi wewe kwa akili yako nusu kijiko, kati ya Lowassa na ccm nani kikwazo cha maendlleleo hapa nchini? Bora lowassa au ccm.

Lowassa as an individual sio hasara au hatari hata kama ni corrupt kuliko ccm as a system ambayo ni corrupt as whole.

Ccm ni hatari zaidi kuliko lowassa, kikwazo cha maendeleo nchi hii ni ccm sio Lowassa.

Baada ya kusoma user name yako nimegundua wewe ni mtu!
 
Nadhani sasa waelewa tutaelewa kazi ya Mh. Mabere Marado shushu maarufu wa CDM. Walifanikiwa kuwachonganisha na Zitto, na sasa wamemleta Fisadi ili kuzika chama. Sema roho inuma, kurudi tea nyuma. Maana sasa tulianza kuona wabunge wanaondoka kwenye u ndiyo mzee (mfano Mwigulu, Deo), je upinzani ukifa itakuwaje tena?

Alisema JKN chama IMARA cha upinzani kitatokana na CCM kuvunjika,nayo sina imani nayo,ila CDM wamenivunja moyo kabisa.
 
Tulia wewe lowasa hajaja ili kugombea urais alichosema anagombea ubunge huko monduli kwa tiketi ya cdm urais slaa anatosha
 
CHADEMA ghafla kimetekwa nyara na wahamiaji ambao wengine hata ukiwauliza kirefu cha CHADEMA ni nini hawajui.Hivi ni sahihi kisiasa kukabidhi chama kwa wahamiaji? Naomba kesho na keshokutwa CHADEMA msije lalamika kuwa CCM imehusika kuua CHADEMA au kuua UKAWA chonde chone mwenye masikio asikie wakiwemo wafadhili wenu wasije piga yowe kuwa hela zao zimezama bure kufanya kampeni hewa.Hasa wale matajiri wa Arusha na MOSHI.
 
Back
Top Bottom