Tangu mwishoni mwa miaka ya utawala wa Mkapa nimekuwa nikiiona ccm kama chama kinachozeeka na hatimaye kufa taratibu. Kifo cha ccm kimekuwa ni eminent. Jambo ambalo sikuliwazia ni muda, kuwa muda ungekuwa mfupi hivi. Kifo cha hili lichama kimekuja, kwa uhakika, ghafla na haraka sana.
Ni dhahiri sasa uwezekano wa Lowassa kuwa Rais wa Tano wa Tanzania ni almost 95% na hata asipokuwa Rais ni dhahiri ataondosha ule upuuzi wa ccm bungeni wa ndiyoooooooooooooooooooooo, kama ukichaa flani hivi.
ccm inawalazimu sasa muanze kufikiri na mnalazimika sasa kuajiri watu competent kwenye chama na serikali yenu ili waje wawasaidie kujenga upinzani imara. mkiendelea kujikusanya tu vilaza kiundugu na kirafiki hata huko kwenye kambi ya upinzani bungeni hamtaonekana.
Mabadiliko haya yanakaribishwa kwa mikono miwili na kila Mtanzania mpenda Haki, Amani, Maendeleo na Utulivu wa Nchi yetu.
Tanzania tunastahili kuwepo panapotustahili katika uwanja wa dunia hii. Tumedunishwa sana na Ma ccm kupitia ufisadi uliokithiri, uzembe kazini, incompetence, undugulization, unprofessionalism nk nk.
sasa ni wakati wa Taifa hili kukombolewa kutoka katika mikono ya mkoloni mweusi.