Umeongea maneno ambayo yanaumiza sana.Ninajiuliza kama Dr.Slaa ataendelea kuwa kiongozi ndani ya CDM sitakaa nimuamini au kumuheshimu kama mtu aliyeukataa ufisadi na akaonekana hivyo.
Sababu kama viongozi wameshindwa kutuheshimu watanzania tunaumia au tulioumia na uzembe,rushwa na ufisadi uliofanywa na viongozi wakiwa ndani ya uongozi ambao walishindwa hata kusema ni nani muhusika mkuu wa ufisadi ule,leo Wanamkaribisha Lowassa,atakuja na akina Rosatam na Chenge,utawa kimbiza hao?
Itabidi viongozi wa CDM watueleze vigezo walivyotumia kumteua Lowassa awe Mgombea urais,hivi pesa alizotapanya wakati akigombea kuteuliwa kuwa Mgombea kwa tiketi ya CCM anazirudishaje?Hivi viongozi wetu hata hili wameshindwa kuliona?
Ninajiuliza wamelipwa kiasi gani cha kutudhalilisha wanachama wa CDM kwa kiasi hicho?Hivi nani mwenye ubavu atakayekuja kumnadi Lowassa?
Kwa kweli kwangu KURA yangu sitompa FISADI hata siku moja.
Mbowe,Dr.SLaa na Tundu Lissu mtueleze mmelipwa kiasi gani na Lowassa?
Mkuu umezungumza kweli tupu na mimi naongeza kuwa kwa mwendo huu hakunachama cha kizalendo wote wapigaji tu! Dr.slaa na lisu wanachakutuambia wanachadema !
Naomba kama haya yasemwayo ni tetesi basi yabaki hivyo lkn dr.slaa ama mwingine yoyote lkn co huyo lowasa tutapoteza tena