Kigamboni: Watuhumiwa kutandaza mabomba na kuiba mafuta yanayoenda bandarini

2019

JF-Expert Member
Dec 31, 2018
2,982
4,457
Mkuu wa wilaya ya Kigamboni, Sarah Msafiri akiwa na kamati ya Ulinzi na usalama wamebaini nyumba iliyopo mtaa wa Ugindoni iliyotandazwa mashine zinazotumika kuchimba visima vya maji lakini badala ya kuchimba chini kuelekea maji yalipo, wanachimba kuelekea usawa yalipo mabomba ya mafuta yanayotoka baharini kuelekea bandarini.

Mafuta hayo yanachukuliwa baada ya 'flow meter' kusoma na kutambulika yamepokelewa nchini lakini kabla ya kufika kituo cha mwisho ndipo mabomba hayo yanapoelekea.

Ndani ya nyumba hiyo kuna mashine na mipira ambayo inavuta mafuta na kujazwa. Nyumba hiyo ina ulinzi mkubwa na taarifa za awali zinasema muhusika amepangisha eneo hilo lenye kodi ya milioni 60 kwa mwaka huku akiwa amelipa miaka miwili na hakuna shughuli inayoendelea zaidi ya kisima ambacho mabomba yake yanaelekea baharini.

=========




Nchi ilitafunwa na watafunaji wakafichwa ila sio na serikali. Wafichuaji walizibwa midomo. Inasikitisha sana
 
Yaaaan mwendazake aliwa fool wapumbavu na wajinga kwamba hakuna upigaji kumbe....kunaaa jamaa angu ni hawa wakula vitu aka unga..nmewahi kumuuliza mtapata wapi hiyooo ktu ..jamaaa alijibu hakunaaa kipindi unga unaingia kwa wingi kama zama hizi za mwendazake..
Huo ni ujambazi siyo wizi wa serikalini. Huyu siku zake zilikuwa zinahesabiwa tu, angekamatwa. El-Chapo alikamwata itakuwa huyu
 
Duh... Nchi hii!!! Mafuta yana faida sana! Manake gharama iliyo tumika kukamilisha huo wizi sio ndogo! Wangeweza kupata kifaa chao chenye security footage, nadhani ingekuwa bora zaidi.

Pili, kama wametoboa baada ya flow meter, ina maana kuna wahusika wa ndani ya bandari. Kwahiyo nao wachunguzwe!

List ni ndefu!

Sent from my S20 Ultra using JamiiForums mobile app
 
Sio rahisi upigaji kama huo kusiwe na mkono wa vigogo serikalini.

Halafu wale teeth wa kipindi Cha mwenda zake walikuwa wapi? Maana tunaambiwa walikuwa hatari balsa

Hivi kwa mfano wangekuwa ni magaidi na kuamua kulipua hayo mapipa ya mafuta si walikuwa washafanikiwa.
 
Nimetaza video hii zaidi ya mara tatu.kwanza huyu mtu anapesa ndefu maana mitambo na vifaa sio vya kitoto.pili inaonesha kuna mtu kachoma hii ishu,. inatakiwa wabaini mtandao wote.haiwezekani kila mwaka rais alikuwa anasema nchi haina kitu kumbe wengine ilikuwa ni neema kwao?πŸ€”πŸ€”
 


Nchi ilitafunwa na watafunaji wakafichwa ila sio na serikali. Wafichuaji walizibwa midomo. Inasikitisha sana
π™ΊπšŽπšœπš’ πš”πšŠπš–πšŠ πš‘πš’πš’πš˜ πš‘πšžπš πšŽπš£πš’ πš”πšžπš–πšžπš‘πšžπšœπš’πšœπš‘πšŠ πš–πš πšŽπš—πšπšŠπš£πšŠπš”πšŽ πš£πšŠπš’πšπš’ πš”πšŠπš–πšŠ πšŠπš—πšπšŠπš•πš’πš”πšžπš πšŽπš™πš˜ 𝚊𝚘 πš πšŠπš—πšπšŽπšŽπš—πšπšŠ πš“πšŽπš›πšŠ πš–πšŠπš•πš’ 𝚣𝚊𝚘 πš”πšπšŠπš’πšπš’πšœπš‘πš πšŠ πš—πšŠ πšŠπšŒπšŒπš˜πšžπš—πš 𝚣𝚊𝚘 πš”πšžπšπšžπš—πšπš’πš πšŠ πšπš‘πšŽπš— πšŠπš—πšπšŽπš”πšžπš“πšŠ 𝙼𝙰𝙼𝙰 πš‘πšžπš›πšžπš–πšŠ πš—πšŠ πš”πšžπšŠπš–πšžπš›πšž 𝙰/𝙲 πš‰πš’πšπšžπš—πšπšžπš•πš’πš πšŽ πš—πšŠ πš”πšŽπšœπš’ πš”πšŠπš–πšŠ πš‘πš’πš’πš˜ πš’πš”πšŠπš“πšžπš–πšžπš’πšœπš‘πš πšŠ πš”πšžπš πšŠ πš—πš’ πš”πšŽπšœπš’ 𝚒𝚊 πš”πšžπš‹πšŠπš–πš‹πš’πš”πš’πš£πš πšŠ πš”πšŠπšπš’πš”πšŠ πš£πš’πš•πšŽ 147. πš’πš—πšπšŽπšœπš˜πš–πšŠ 148.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa Magufuli anahusikaje hapo. Hao si wezi Kama wezi wengine au kosa lake ni kule kupiga vita wizi kwa maslahi ya taifa. Lazima tukubali alijitahidi kwa uwezo wake ila haizuii ukweli kwamba kuna wachache walikuwepo bado ambao mmoja wapo ni hawa
 
Mimi najiuliza kama aliiba muda wote bila kujulikana au hasara kupatikana basi mafuta yana faida sana
Duh... Nchi hii!!! Mafuta yana faida sana! Manake gharama iliyo tumika kukamilisha huo wizi sio ndogo! Wangeweza kupata kifaa chao chenye security footage, nadhani ingekuwa bora zaidi.

Pili, kama wametoboa baada ya flow meter, ina maana kuna wahusika wa ndani ya bandari. Kwahiyo nao wachunguzwe!

List ni ndefu!

Sent from my S20 Ultra using JamiiForums mobile app
 
π™ΊπšŽπšœπš’ πš”πšŠπš–πšŠ πš‘πš’πš’πš˜ πš‘πšžπš πšŽπš£πš’ πš”πšžπš–πšžπš‘πšžπšœπš’πšœπš‘πšŠ πš–πš πšŽπš—πšπšŠπš£πšŠπš”πšŽ πš£πšŠπš’πšπš’ πš”πšŠπš–πšŠ πšŠπš—πšπšŠπš•πš’πš”πšžπš πšŽπš™πš˜ 𝚊𝚘 πš πšŠπš—πšπšŽπšŽπš—πšπšŠ πš“πšŽπš›πšŠ πš–πšŠπš•πš’ 𝚣𝚊𝚘 πš”πšπšŠπš’πšπš’πšœπš‘πš πšŠ πš—πšŠ πšŠπšŒπšŒπš˜πšžπš—πš 𝚣𝚊𝚘 πš”πšžπšπšžπš—πšπš’πš πšŠ πšπš‘πšŽπš— πšŠπš—πšπšŽπš”πšžπš“πšŠ 𝙼𝙰𝙼𝙰 πš‘πšžπš›πšžπš–πšŠ πš—πšŠ πš”πšžπšŠπš–πšžπš›πšž 𝙰/𝙲 πš‰πš’πšπšžπš—πšπšžπš•πš’πš πšŽ πš—πšŠ πš”πšŽπšœπš’ πš”πšŠπš–πšŠ πš‘πš’πš’πš˜ πš’πš”πšŠπš“πšžπš–πšžπš’πšœπš‘πš πšŠ πš”πšžπš πšŠ πš—πš’ πš”πšŽπšœπš’ 𝚒𝚊 πš”πšžπš‹πšŠπš–πš‹πš’πš”πš’πš£πš πšŠ πš”πšŠπšπš’πš”πšŠ πš£πš’πš•πšŽ 147. πš’πš—πšπšŽπšœπš˜πš–πšŠ 148.

Sent using Jamii Forums mobile app
Shida ya mwendazake alikuwa anatuficha mno ili asichafuke
 
Back
Top Bottom