Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
UCHUNGUZI WATHIBITISHA

Wangwe: Siyo risasi

*Uchunguzi wathibitisha jeraha lake ni la ajali
*Waonyesha alipasuka fuvu, ubongo ulimwagika
*Profesa Wangwe asikitishwa na habari za uzushi
*Akana Mbowe kuokolewa, kunusurika mapanga

*Zitto Kabwe aziita taarifa hizo kuwa za kizushi


Na Joseph Senga, Tarime


HATIMAYE mazishi ya Mbunge wa Tarime, Chacha Wangwe (Chadema) aliyefariki dunia kwa ajali ya gari, Jumatatu wiki hii, yamefanyika jana baada ya matokeo ya uchunguzi uliofanyika kutangazwa.
Mazishi hayo ambayo awali yalikuwa yafanyike juzi, yalikwama baada ya wanafamilia kutaka ufanyike uchunguzi mwingine huru kutokana na kuwapo kwa utata katika mazingira yaliyosababisha kifo cha mbunge huyo.
Uamuzi huo wa wanafamilia kutaka kufanyika kwa uchunguzi huo, ulikwenda sambamba na kuibuka kwa hali ya wasiwasi na kutishia kuibuka kwa vurugu katika Kijiji cha Kemakerere.
Akitangaza matokeo ya uchunguzi huo jana, mbele ya wananchi waliofurika, Profesa Samuel Wangwe ambaye ni kaka wa marehemu, alisema uchunguzi huo ulifanywa na daktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, ambaye hata hivyo hakutajwa kwa sababu za kiusalama.
Profesa Wangwe alisema uchunguzi huo uliofanyika kwa zaidi ya saa mbili, ulibainisha kuwa, ajali ilisababisha mdogo wake apasuke fuvu la kichwa kutokana na kujigonga kwa juu na kisha ubongo ukamwagika sambamba na taya kuvunjika.
Uchunguzi huo ulioanza jana asubuhi majira ya saa 5:15, ulifanyika chini ya uwakilishi wa wanafamilia watatu, Jeshi la Polisi na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliyekiwakilisha Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Profesa Wangwe aliwaeleza wananchi waliokuwa wakimsikiliza kwamba, yeye na wanafamilia wenzake walikuwa wamekubaliana na kuridhishwa na taarifa hiyo ya uchunguzi, na hivyo kukubali kumzika ndugu yao.
Mbali ya hilo, alisema daktari alikuwa akitarajia kuiwasilisha taarifa kamili ya maandishi ya uchunguzi alioufanya akiambatanisha na picha zilizopigwa.
Baada ya taarifa hiyo ya uchunguzi iliyotolewa nje ya Hospitali ya Wilaya ya Tarime ulikofanyika, safari ya kwenda Kemokerere kwa ajili ya mazishi ilianza.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi wa Tarime waliitaka familia hiyo kuahirisha mazishi hadi leo, ili kuwapa fursa watu wengine ambao walikuwa wameshaondoka kuhudhuria, ombi ambalo hata hivyo halikukubaliwa na wanafamilia.
Mwili wa marehemu ulipofika nyumbani kwake, shughuli za mazishi zilianza kwa salamu za rambirambi kutolewa kwanza na umoja wa vyama vya upinzani vinavyoshirikiana na Chadema; NCCR Mageuzi, TLP na CUF.
Akizungumza kwa niaba ya vyama hivyo, Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema aliwataka wananchi wa Tarime kushikamana na kuendeleza mema yote aliyoyatenda marehemu Wangwe wakati wa uhai wake.
Mbali ya kutoa ubani wa shilingi 300,000 Mrema aliwataka kuanza kuangalia wanachama kutoka katika kambi hiyo ya upinzani ili kumtafuta mtu atakayerithi mikoba ya ubunge ya Wangwe.
Wengine waliotoa salamu za rambirambi ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Luteni Kanali mstaafu, Issa Machibya aliyetoa ubani wa shilingi 100,000 na kilo 50 za mchele kusaidia shughuli za msiba.
Ibada ya mazishi ya Wangwe iliendeshwa kwa mahubiri ya Kikristo na Nancy Msafiri na ikahudhuriwa na wananchi wa Tarime, viongozi wa kisiasa, ndugu, jamaa, marafiki, watoto na wake watatu wa marehemu waliojulikana kwa majina ya Gati, Dotto na Mariam.
Jeneza la marehemu Wangwe lilianza kuteremshwa kaburini saa 11:50 jioni.
Awali, muda mfupi kabla ya kuanza kwa uchunguzi jana, Profesa Wangwe alizungumza na wanahabari na akaeleza kusikitishwa kwa familia yao na taarifa za uzushi zilizoripotiwa katika vyombo kadhaa vya habari juzi na jana, kuhusu hali ya usalama wakati wa msiba huo.
Profesa Wangwe alisema yeye na wanafamilia wenzake, walikuwa wamesikitishwa na taarifa zilizokuwa zikidai kwamba, kulikuwa na kikundi cha watu wenye mapanga waliokuwa wakimuwinda Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Mbali ya hilo, Profesa Wangwe alieleza kushangazwa kwake na taarifa alizozielezea kuwa zisizo sahihi, zilizokuwa zikidai kuwa Mbowe alilazimika kuondolewa uwanjani chini ya ulinzi mkali wa polisi ili kumnusuru na mapanga hayo.
'‘Hakuna mapanga yaliyokuwa pale, wala hakukuwa na vurugu za kutumia silaha na wala Mwenyekiti wa Chadema Mbowe (Freeman) hakuondolewa chini ya ulinzi wa polisi," alisema Wangwe huku akiyataja baadhi ya magazeti (si Tanzania Daima) ambayo yaliandika taarifa hizo.
Akifafanua, Profesa Wangwe alisema, Mbowe aliondolewa uwanjani hapo juzi akiwa na viongozi wengine wa juu wa kiserikali na kisiasa kutokana na ushauri uliotolewa na Mkuu wa Mkoa baada ya mabishano kuhusu uhalali wa kumzika marehemu ulipoibuka.
Hata hivyo, taarifa ambazo Tanzania Daima ilizipata baadaye juzi jioni na jana kutoka Musoma na Tarime zinaonyesha kwamba, kulikuwa na kikundi maalum kilichokuwa kimeandaliwa kwa malengo ya kisiasa na watu wasiojulikana, kwa lengo la kumdhuru Mbowe.
Wakati Mbowe akiwasili katika Kijiji cha Kemakorere hiyo juzi, hali ilikuwa ni tofauti kwani alilakiwa na vijana wa Chadema ambao walimuongoza hadi katika jukwaa kuu.
Katika hali ambayo si rahisi kuielezea, pamoja na Mbowe kuwasili na kuondoka uwanjani hapo salama, tena pasipo kusindikizwa na polisi, vyombo kadhaa vya habari vilianza kuripoti kuhusu kunusurika kwake kwa mapanga hata kufikia hatua ya kuokolewa na polisi.
Akizungumza na Tanzania Daima juzi, Zitto alizielezea taarifa hizo za mwenyekiti wake kunusurika kuwa ni za uzushi uliokuwa umeandaliwa kwa malengo ya kisiasa na kwa nia ambayo haikuwa nzuri.
'‘Huku hakukuwa na kinachoitwa vurugu, wala hakukuwa na hali ya hatari dhidi ya mwenyekiti. Kuna propaganda kali inasambazwa kuwa mwenyekiti kaokolewa na polisi. Hizi ni taarifa za uongo," alisema Zitto alipoulizwa kuhusu nini kilikuwa kimetokea.
Akizungumza na Tanzania Daima kutoka Musoma jana, Mbowe pasipo kutaka kuingia kwa undani, alieleza kusikitishwa na taarifa hizo na akasema baada ya kufanya mashauriano na washauri wake na viongozi wengine wa chama hicho, alikuwa ameamua kurejea Dar es Salaam.



Freeman Mbowe
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jump to: navigation, search
Freeman Aikaeli Mbowe (born 14 September 1961) is a Tanzanian politician and chairman of Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA – Party for Democracy and Development). Mbowe is a member of the Chaga ethnic group.


Mbowe CampaigningMbowe was elected to the National Assembly in 2000 representing Hai Constituency (Kilimanjaro Region). He won 64.5% of the vote, which was the highest percentage of votes won among constituencies with opposition MP's.

In preparation for the 2005 elections, Mbowe was nominated as CHADEMA's presidential candidate. Jumbe Rajab Jumbe, a Zanzibari was chosen as his vice-presidential candidate. The election was originally scheduled for 30 October 2005, but was postponed until 14 December due to the death of Jumbe.


Mbowe and Komu CampaigningMbowe criticized the lengthy postponement, saying a week's delay would have sufficed and that his party cannot afford to finance extra campaigning. Chadema eventually settled on Anna Komu to be the running mate.

He placed third out of ten candidates in the 14 December 2005 presidential election, winning 5.88% of the vote.

Mbowe is the owner of Club Bilicanas, one of the best nightclubs in Dar es Salaam. He is also the owner of Tanzania Daima, a national daily newspaper, as well as Protea Hotel Aishi Machame, a hotel in his native town of Machame, in Kilimanjaro region, Tanzania.

Mbowe is married to Lillian Mtei (daughter of Edwin Mtei, the first Governor of Bank of Tanzania). They were married on 17 August 1991. The two live happily with their children in Mikocheni A, a suburb of Dar es Salaam, Tanzania. Mbowe has three children: Dudley A. Mbowe (15), Nicole A. Mbowe (11) and Dennis E. Mbowe (8). All their children go the Dar es Salaam Independent School (D.I.S.), also in Mikocheni.
 
Huu uchuguzi umefanywa ni kiini macho tu tumenyimwa habari mhimu wange mwacha huyo Daktari kutoka Kenya afanye uchunguzi wake asinge fungamana na upande wowote.Tambueni kuna kitu kimesha tendeka nyuma ya pazia news zitaliki tu nyie subilini sisi ni watu wazima.
 
Jamana mbona sijaona comments za ASHA ABDALA, MWAFRIKA WA KIKE on this issue?? Come on girls hebu jitokezeni huko mlipo......

Pumba za Yona Maro na zenyewe nimezimiss kidogo lakini nilipata habari kuwa amekamatwa sasa jijui ni kweli au ndo usanii wake tu,, nway ngoja tusikilizie hii issue itaishia wapi maana ni mengi yamesemwa mengi yamefikiriwa na mengi yamezushwa.
R.I.P Wangwe z. Chacha
 
Naendelea kulifuatilia hili kwa ukaribu mkubwa sana kwani linaweza kutoa ushahidi fulani na watu wakatakiwa kuisaida polisi na haswa Rostam Azizi kwanini alijihusisha kiasi hicho?

Magazeti ya leo wameshindwa kusema kuwa juzi Mbowe alikoswakoswa na mapanga na mishale kama walivyosema jana .

Waandishi walioandika habari jana ni hawa;

1.Nipashe-Bigambo Jeje-PST.

2.Majira-George John -Tarime na Reuben Kagaruki DAR.

3.Habari Leo -Makubo Haruni

4.Uhuru -Mwandishi wetu

5.Mtanzania-George Mwita.


Waandishi walioandika leo ni hawa;

1.Nipashe-Mary Edward PST.

2.Habari Leo-Halima Mlacha.

3.Majira -George John

4.Mtanzania-Christopher Gamaina

5.Uhuru-Mwandishi wetu.

Maswali ya kujiuliza ni kuwa je?waandishi hawa walipelekwa jana huko Tarime?
Majina yaliyoripoti juzi inamaana hawaaminiki tena ama wamefukuzwa kazi?
Habari za leo kila gazeti limekuwa na maandishi yake na hakuna kufanana kama jana japo wameripoti tukio hilohilo .
Kikao cha jukwaa la wahariri kinaendelea sasa ,ntawapa yatakayojiri huko punde.

Ndugu yangu umeweza kung'amua kitu hapo. Lakini nakushauri kama unataka kujua mambo kuhusu yanayotokea hapa bongo, you are better much much better here at JF hapa sio rahisi kuwahonga members ni hoja zako. Usiwaamini waandishi ambao hupokea bahasha na kupelekwa kuandika habari baada ya wao kuchimba habari.
 
.'...Adv na disadv' ya uhuru wa vyombo vya habari.

Serikali yetu imejifikishaje hapa pa kutokuaminiwa karibu katika kila jambo? Itarudishaje IMANI kwa Wananchi wake? Hatima ya hali kama hii ni nini huko tuendako? Binafsi namshukuru Muumba wetu haya mambo yamemalizika hivyo yalivyomalizika.

...Swali/hoja nzuri...

CONSPIRACY THEORIES,i fear for this country,at every turn,we come with these theories,most of them unfounded,this monster which has taken hold of our medulla's is throwing this once proud nation deeper down the abyss.the damage of most of these unfounded allegations divides us further.HITTING the keyboard immediatly,before proper gathering facts only to be proved otherwise,to any patriot is worse then any FISADI,for the damage cannot be reversed.its time we sit down,take stock of our actions,FOR ABUSING THE FREEDOM OF SPEECH GRANTED TO US IS THE WORST SIN OF ALL

...jibu/hoja nzuri sana.

...kuna haja kubwa watanzania tukajihadhari na mikono ya waandishi, la sivyo ipo siku damu itakuja mwagika iwapo kuna wataochochewa kuamini taarifa zisizothibitishwa. Wahariri wa magazeti will be accountable, na hata JF Very Senior members ambao mara nyingi kutokana na utashi na ushawishi mkubwa credibility ya 'source of info' na posting 'zao/zetu/zenu' zinaaminiwa na wengi.

ni tahadhari tu, nothing personal.
 
Zito Kabwe aliwasilisha malalamiko rasmi kwa Jukwaa la Wahariri kuhusiana na jinsi vyombo vya habari vilivyopotosha kilichotokea tarime. Jukwaa la wahariri ndio limemaliza kikao chake punde na imeundwa kamati inayowajumuisha Sakina Datoo, Nevil Meena, Saed Kubenea, Danny Mwakiteleko na Joseph Kulangwa kulshughulikia malalamiko hayo.
Malalamiko makubwa yalikuwa juu ya magazeti na timu hiyo imepewa SIKU CHACHE kukamilisha kazi yake
 
Jamana mbona sijaona comments za ASHA ABDALA, MWAFRIKA WA KIKE on this issue?? Come on girls hebu jitokezeni huko mlipo......

Pumba za Yona Maro na zenyewe nimezimiss kidogo lakini nilipata habari kuwa amekamatwa sasa jijui ni kweli au ndo usanii wake tu,, nway ngoja tusikilizie hii issue itaishia wapi maana ni mengi yamesemwa mengi yamefikiriwa na mengi yamezushwa.
R.I.P Wangwe z. Chacha
Labda wamekwenda Likizo na na ubavu wa kupata hela ya kuvamia mtandano sio mchezo.
 
Freeman Mbowe
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jump to: navigation, search
Freeman Aikaeli Mbowe (born 14 September 1961) is a Tanzanian politician and chairman of Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA – Party for Democracy and Development). Mbowe is a member of the Chaga ethnic group.


Mbowe CampaigningMbowe was elected to the National Assembly in 2000 representing Hai Constituency (Kilimanjaro Region). He won 64.5% of the vote, which was the highest percentage of votes won among constituencies with opposition MP's.

In preparation for the 2005 elections, Mbowe was nominated as CHADEMA's presidential candidate. Jumbe Rajab Jumbe, a Zanzibari was chosen as his vice-presidential candidate. The election was originally scheduled for 30 October 2005, but was postponed until 14 December due to the death of Jumbe.


Mbowe and Komu CampaigningMbowe criticized the lengthy postponement, saying a week's delay would have sufficed and that his party cannot afford to finance extra campaigning. Chadema eventually settled on Anna Komu to be the running mate.

He placed third out of ten candidates in the 14 December 2005 presidential election, winning 5.88% of the vote.

Mbowe is the owner of Club Bilicanas, one of the best nightclubs in Dar es Salaam. He is also the owner of Tanzania Daima, a national daily newspaper, as well as Protea Hotel Aishi Machame, a hotel in his native town of Machame, in Kilimanjaro region, Tanzania.

Mbowe is married to Lillian Mtei (daughter of Edwin Mtei, the first Governor of Bank of Tanzania). They were married on 17 August 1991. The two live happily with their children in Mikocheni A, a suburb of Dar es Salaam, Tanzania. Mbowe has three children: Dudley A. Mbowe (15), Nicole A. Mbowe (11) and Dennis E. Mbowe (8). All their children go the Dar es Salaam Independent School (D.I.S.), also in Mikocheni.

haya yote tunayajua siku zote umeweka hapa ya nini? au ndiyo muenedelezo wa bahasha za RA?
 
Leo asubuhi kumefanyika kikao baina ya viongozi wa CHADEMA na jukwaa la wahariri. Kikao hicho kimemalizika yapata saa 7 mchana.

Katika jukwaa hilo Mhe. Zitto Zuberi Kabwe na John Mnyika waliokiwakilisha chama walitumia muda huo kuwasilisha malalamiko yao kuhusu habari zilizokuwa zikitolewa kutoka msibani. Malalamiko yao ambayo ilionekana kabisa kuwa wahariri walikuwa wakijua kuwepo kwayo yalihusu kutungwa hadithi ya kukimbizwa kwa Mbowe kwa kutishiwa marungu na mikuki na ya kuwa vurugu zilizotokea Kemakorere Tarime zilitokea mara baada ya Mbowe kufika hapo msibani. "Habari hii si ya kweli hata kidogo, Hata wakazi wa Tarime wameshangaa ilikotoka hii habari" amesema Zitto.

Lalamiko jingine ambalo litatumika pia kwa ajili ya rejea ya uchunguzi ni habari hiyo kuwekwa kwenye vyombo 5 vya habari na kufanana kabisa. Hata makosa yaliyofanyika katika uandishi wa habari hiyo yanafanana.

Wahariri wameunda kamati ya watu wachache ambao watalishughulikia jambo hili kwa kufanya uchunguzi wa kina kujua kulikoni. Kwa nini habari hizi zitoke kama zilivyotoka? Nani aliziandika? Nani alikuwa nyuma akisukuma habari hizi ziandaliwe na zitoke? Alitumia kishawishi gani? Nani hasa walioshawishiwa?

Kamati hiyo inawainclude: Sakina Datoo, Nevil Meena, Saed Kubenea, Danny Mwakiteleko na Joseph Kulangwa
Itaibidi pia kamati hii ichunguzi/ihoji role ya TBC1 katika maziko hayo

Kamati imepewa muda mfupi kukamilisha kazi yake na itatoa release hadharani.

Stay tuned
 
Leo asubuhi kumefanyika kikao baina ya viongozi wa CHADEMA na jukwaa la wahariri. Kikao hicho kimemalizika yapata saa 7 mchana.

Katika jukwaa hilo Mhe. Zitto Zuberi Kabwe na John Mnyika waliokiwakilisha chama walitumia muda huo kuwasilisha malalamiko yao kuhusu habari zilizokuwa zikitolewa kutoka msibani. Malalamiko yao ambayo ilionekana kabisa kuwa wahariri walikuwa wakijua kuwepo kwayo yalihusu kutungwa hadithi ya kukimbizwa kwa Mbowe kwa kutishiwa marungu na mikuki na ya kuwa vurugu zilizotokea Kemakorere Tarime zilitokea mara baada ya Mbowe kufika hapo msibani. "Habari hii si ya kweli hata kidogo, Hata wakazi wa Tarime wameshangaa ilikotoka hii habari" amesema Zitto.

Lalamiko jingine ambalo litatumika pia kwa ajili ya rejea ya uchunguzi ni habari hiyo kuwekwa kwenye vyombo 5 vya habari na kufanana kabisa. Hata makosa yaliyofanyika katika uandishi wa habari hiyo yanafanana.

Wahariri wameunda kamati ya watu wachache ambao watalishughulikia jambo hili kwa kufanya uchunguzi wa kina kujua kulikoni. Kwa nini habari hizi zitoke kama zilivyotoka? Nani aliziandika? Nani alikuwa nyuma akisukuma habari hizi ziandaliwe na zitoke? Alitumia kishawishi gani? Nani hasa walioshawishiwa?

Kamati hiyo inawainclude: Sakina Datoo, Nevil Meena, Saed Kubenea, Danny Mwakiteleko na Joseph Kulangwa
Itaibidi pia kamati hii ichunguzi/ihoji role ya TBC1 katika maziko hayo

Kamati imepewa muda mfupi kukamilisha kazi yake na itatoa release hadharani.

Stay tuned
Naamini hawa kwa kiasi kikubwa wataleta ukweli na kuwafunua nguo hao majibwa yanayovuruga habari za kila siku maana sio leo tu haya majibwa yamevuruga habari
 
haya yote tunayajua siku zote umeweka hapa ya nini? au ndiyo muenedelezo wa bahasha za RA?


yawezekana ni bahasha la RA maana huyu RA mnapandisha chati wenyewe .

Hapo mimi nahoji TANZANIA DAIMA kumilikiwa Na Mbowe harafu na uhalali wake wa habari kuhusu Mbowe .

Lakini Majira ,mwanainchi,mtanzania ,ippmedia,michuzi wakiandika wao wamenunuliwa na hawakusoma sijui hao wa tanzania daima wamesomea wapi?

Yani hapa nataka kusema hakuna chombo cha habari kitakachonishawishi ni amini yaliyotokea tofauti na wale wananchi waliokuwepo pale.

Uzoefu unaonyesha kila muwamba ngoma ngozi hujivutia kwake.
 
yawezekana ni bahasha la RA maana huyu RA mnapandisha chati wenyewe .

Hapo mimi nahoji TANZANIA DAIMA kumilikiwa Na Mbowe harafu na uhalali wake wa habari kuhusu Mbowe .

Lakini Majira ,mwanainchi,mtanzania ,ippmedia,michuzi wakiandika wao wamenunuliwa na hawakusoma sijui hao wa tanzania daima wamesomea wapi?

Yani hapa nataka kusema hakuna chombo cha habari kitakachonishawishi ni amini yaliyotokea tofauti na wale wananchi waliokuwepo pale.

Uzoefu unaonyesha kila muwamba ngoma ngozi hujivutia kwake.

Kile mlichopanga hakikufanikiwa sasa huyu RA naye aende kuwahonga hawa;

Sakina Datoo, Nevil Meena, Saed Kubenea, Danny Mwakiteleko na Joseph Kulangwa

Hii ni kamati iliyoundwa na jukwaa la wahariri kufuatilia uzushi wote huo ulikuwa na maana gani na ulikuwa unataka kufanya nini na kwa nini?Who was behind all this?
 
yawezekana ni bahasha la RA maana huyu RA mnapandisha chati wenyewe .

Hapo mimi nahoji TANZANIA DAIMA kumilikiwa Na Mbowe harafu na uhalali wake wa habari kuhusu Mbowe .

Lakini Majira ,mwanainchi,mtanzania ,ippmedia,michuzi wakiandika wao wamenunuliwa na hawakusoma sijui hao wa tanzania daima wamesomea wapi?

Yani hapa nataka kusema hakuna chombo cha habari kitakachonishawishi ni amini yaliyotokea tofauti na wale wananchi waliokuwepo pale.

Uzoefu unaonyesha kila muwamba ngoma ngozi hujivutia kwake.

Naona mkuu unazungumza utani katika swala ambalo lingehatarisha maisha ya watanzania, hasa TARIME. Hapa hakuna swala la kuvutiangozi kwake au la.JE WATU WA TARIME WANASEMAJE UTUELEZE? KAMA USIPOWEZA UNAWEZAJE KUPATA TAARIFA??

HIVI TAARIFA KUANDIKWA NA MTU MMOJA, WOTE WAKIFANYA MAKOSA SAWA, NUKTA,KOMA SAWA HAIKUINGII AKILINI? TENA VIKIWA NA WAMILIKI TOFAUTI WAKITUMIA MAJINA TOFAUTI.

MIMI SIDHANI KUWA KUNA SWALA LA MWAMBA NGOMA HUJIVUTIA KWAKE.

KITU GANI KITAKUFANYA UAMINI KUWA TANZANIA DAIMA WALIANDIKA HABARI YA KWELI? NA JE NI KITU GANI NA UNA UTHIBITISHO GANI KUELEZA KUWA UNA WASIWASI NA TANZANIA DAIMA-MKUU NASUBURI MAJIBU

''Suspicion is a mental picture seen through an imaginary keyhole”
 
Pumzika kwa amani chacha zakayo wangwe!Tulikupenda ingawa wapo waliokuchukia kwa kusema ukweli!MUNGU AKUALAZE MAHALI PEMA!
AMEN!
 
Huo mkono wa RA utafika kote lakini JF hawezi
 
Huo mkono wa RA utafika kote lakini JF hawezi

Upo na kama juzi ulikuwa unafuatilia ulikutana na wagagagegigiii, na wengine kama huyu anayetetea hapa hivyo upo ila ni kwa individuals ,ila JF kama taasisi kamwe hawateweza kufika.
 
Huko Dodoma naambiwa kuwa TBC wanaaibika sana kwani imebidi fundi mitambo wao aweke vifaa kwenye hema na studio imekuwa ni kwenye hema huko Bungeni kutokana na kuwa gari lao ama studio yao OB VAN haijawasili ikiwa inatokea Tarime ilikoenda kufuatilia na bila mafanikio ya kile ambacho walifikiri wataweza kukirusha kilikposhindikana sasa wameweka hema na vifaa vyao vipo hapo ndio studio.

Tido mhando angalia hao mtandao watakumaliza muda sio mrefu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom