Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
mkikubali hiki ni kifo cha kawaida na uchunguzi ulio huru na wa kihalifu kutofanyika; mkikubali kuwa ni "ajali tu kama zingine" na ya kuwa ni "mapenzi ya Mungu"; mkikubali kuwa hakuna haja ya kuangalia ukweli wote ule, siyo tu mtakuwa hamumtendei haki Chacha na jitihada zake za kuwa mkweli na muwazi, lakini yawezekana tutakuwa tumetoa kibali cha mambo haya kuendelea kutendeka kwa kisingizio cha "mapenzi ya Mungu" au "ajali ni ajali tu".

Sasa hivi katika Tanzania lolote linawezekana na hasa linapokuja suala la fedha na madaraka. Mkikubali kuwa hiki kifo ni mapenzi ya Mungu, basi inabidi mkubali pia kuwa yote yanayoendelea nchini ni mapenzi ya Mungu, wizi wa EPA ni mapenzi ya Mungu, ubadhirifu ni mapenzi ya Mungu n.k Kwani kimsingi kwa wale wenye imani, hakuna kitu kinachotokea ambacho si mapenzi ya Mungu. Hivyo tukubali tu yaishe kwani mafisadi nao ni mapenzi ya Mungu kwetu. Sisi ni nani hata tuwapinge?
 
Waryanchoka V/S Waanryichoki? hapo nasikia halufu ya damu

hakuna cha damu.... kuwa fair ndugu yangu. Hakuna kitu kama waanryichoki kwenye koo za Tarime.

Haikugharimu kitu ukiacha dharau dhidi yetu watu wa Tarime.

Heshima ni kitu cha bure ndugu yangu.
 
Familia ya marehemu, imesibitisha, uchunguzi utafanyika kesho asubuhi na maazishi yatafanyika mara baada ya uchunguzi (Source;Wanachi kutoka kijiji cha Kimakolele, TBC1 na Prof. Wangwe.)
Pitia thread zote mkuu, kuna mkulu kasema Mbowe amenusurika kuuwawa baada ya Dr. kutoka Kenya kufanya ukaguzi wa mwili na kugundua jamaa alikufa kwa kupigwa risasi mbili.
 
makubwa haya?
Kama ni jeraha la risasi ni kwa nini Polisi wafiche?
Mimi siamini kama seikali, CCM au hata Chadema wahusike na hili ana nini cha muhimu anachokijua mpaka wamuue, jamani hiki kifo kimegeuzwa mno. Ila kama kauawa na majambazi inawezekana na hapo sasa ni kwa nini kama nio hivyo vyombo vya dola vifiche?
Hii stori ya risasi sitashangaa kusikia kuwa ni stori za vijiweni
 
Ina maana Mazishi yatafanyika Lini?hao ndugu zangu wakurya watakuwa wanagombania Mali tu na hizo Rambi rambi,nakujua huko..

kutakuw ana ishu nzito,nitampigia ndugu yangu mmoja ambaye yuko karibu na familia ya Wangwe na atanipa feedback na nitawahabarisha

Gembe fanya heshima kwa wenzako.

Una hakika kuwa watu wa Tarime watakuwa wanagombania mali. Unadhani kuwa wakurya ni wanyama au watu wasio na akili kiasi hiki. Heshimu wengine na wewe utaheshimiwa.

Maneno ya kashfa kama haya si mazuri wakati wenzako tunahuzunika kwa kifo hiki cha mbunge wetu Wangwe.
 
Mnamkumbuka Robert Ouko na the original story...? Mnakumbuka kifo cha Benazir Bhutto na original story?
 
makubwa haya?
Kama ni jeraha la risasi ni kwa nini Polisi wafiche?
Mimi siamini kama seikali, CCM au hata Chadema wahusike na hili ana nini cha muhimu anachokijua mpaka wamuue, jamani hiki kifo kimegeuzwa mno. Ila kama kauawa na majambazi inawezekana na hapo sasa ni kwa nini kama nio hivyo vyombo vya dola vifiche?
Hii stori ya risasi sitashangaa kusikia kuwa ni stori za vijiweni

Hii sio stori ya kijiweni.... hii ndio sababu kubwa iliyopelekea mazishi yasifanyike leo na wabunge na viongozi wa serikali kufukuzwa toka Tarime.
 
Inabidi sasa vinara wetu wawe makini,ZITO,KUBENEA,SLAA etc M.KIJIJI wapewe ulinzi hata kama utakua ni INVISIBLE lakini wasiwe tena kama wananchi wakawaida.Maana sasa wasi wasi utakua unatuingia.
 
Tunaomba wabunge wetu wapatiwe Ulinzi na pia taarifa hizo zifanyiwe kazi kwa kina.

Mtu ambaye anapaswa kuombewa ulinzi wa polisi kabla ya wote kwenye hili sakata ni Bw. George Mwiguni, kwa kusema hayo aliyoyasema ni wazi kwamba maisha yake pia yapo hatarini pengine kuliko mtu yoyote sasa. Hivi Bongo tuna witness protection program au huu bado ni msamiati?
 
mkikubali hiki ni kifo cha kawaida na uchunguzi ulio huru na wa kihalifu kutofanyika; mkikubali kuwa ni "ajali tu kama zingine" na ya kuwa ni "mapenzi ya Mungu"; mkikubali kuwa hakuna haja ya kuangalia ukweli wote ule, siyo tu mtakuwa hamumtendei haki Chacha na jitihada zake za kuwa mkweli na muwazi, lakini yawezekana tutakuwa tumetoa kibali cha mambo haya kuendelea kutendeka kwa kisingizio cha "mapenzi ya Mungu" au "ajali ni ajali tu".

Sasa hivi katika Tanzania lolote linawezekana na hasa linapokuja suala la fedha na madaraka. Mkikubali kuwa hiki kifo ni mapenzi ya Mungu, basi inabidi mkubali pia kuwa yote yanayoendelea nchini ni mapenzi ya Mungu, wizi wa EPA ni mapenzi ya Mungu, ubadhirifu ni mapenzi ya Mungu n.k Kwani kimsingi kwa wale wenye imani, hakuna kitu kinachotokea ambacho si mapenzi ya Mungu. Hivyo tukubali tu yaishe kwani mafisadi nao ni mapenzi ya Mungu kwetu. Sisi ni nani hata tuwapinge?

Mzee Mwanakijiji,

Nakuhakikishia kuwa familia ya Wangwe na wananchi wa Tarime wamekataa kukubali kuwa hiki ni kifo cha kawaida. Yanayoendelea Tarime sasa hivi ni zaidi ya maelezo ya kawaida.

Uchunguzi binafsi umeanza na inaonesha kabisa kuwa inawezekana Wangwe aliuawa kwa kitu kingine (risasi?) na sio ajali kama ilivyotolewa. Kuna maelfu na maelfu ya watu wa Tarime wamekuja kumuaga Wangwe na wamesema kuwa hawatakubali longo longo na propaganda za TBC1 na magazeti ya Rostam Azizi kuhusu kifo cha Wangwe.
 
Habari kutoka ndani kabisa zinasema kuwa ilikutwa risasi kichwani kwa Wangwe na kuwa impact ya jeraha lake kichwani sio consistent na madhara ya ajali ya gari bali ya risasi.

Uchunguzi wa maiti unafanywa na dakitari kutoka Nairobi ..... sort of....

Habari zaidi kutoka ndani ya Tarime zitakuja accordingly.

Hapo sasa mm ndo nilikuwa nataka hapo tu yule dogo amebeba siri nzito waendelee kumzuia kabisa atasema yote.
 
mkikubali hiki ni kifo cha kawaida na uchunguzi ulio huru na wa kihalifu kutofanyika; mkikubali kuwa ni "ajali tu kama zingine" na ya kuwa ni "mapenzi ya Mungu"; mkikubali kuwa hakuna haja ya kuangalia ukweli wote ule, siyo tu mtakuwa hamumtendei haki Chacha na jitihada zake za kuwa mkweli na muwazi, lakini yawezekana tutakuwa tumetoa kibali cha mambo haya kuendelea kutendeka kwa kisingizio cha "mapenzi ya Mungu" au "ajali ni ajali tu".

Sasa hivi katika Tanzania lolote linawezekana na hasa linapokuja suala la fedha na madaraka. Mkikubali kuwa hiki kifo ni mapenzi ya Mungu, basi inabidi mkubali pia kuwa yote yanayoendelea nchini ni mapenzi ya Mungu, wizi wa EPA ni mapenzi ya Mungu, ubadhirifu ni mapenzi ya Mungu n.k Kwani kimsingi kwa wale wenye imani, hakuna kitu kinachotokea ambacho si mapenzi ya Mungu. Hivyo tukubali tu yaishe kwani mafisadi nao ni mapenzi ya Mungu kwetu. Sisi ni nani hata tuwapinge?

Mwanakijiji,
I take this
Sasa hivi katika Tanzania lolote linawezekana na hasa linapokuja suala la fedha na madaraka.

Mhe. Mbowe yuko Msibani?
 
mkijiji una hoja,naungana nawe hata kama ni mapenzi ya MUNGU bado yatubidi tufanye uchunguzi tujue ni nini hasa kilitokea ambacho kingeweza zuilika
 
Mwanakijiji,
I take this
Sasa hivi katika Tanzania lolote linawezekana na hasa linapokuja suala la fedha na madaraka.

Mhe. Mbowe yuko Msibani?

Ndio,

Mheshimiwa Mbowe, Zitto na viongozi wa vyama vya upinzani na baadhi ya viongozi wa chama tawala wengine wako kwenye msiba ila viongozi wengi wa serikali na baadhi ya wabunge wamekimbia na kuna habari kuwa wanaondoka kurudi walikotoka maana hakuna aliye tayari kutoa maelezo ya kilichotokea kwa mbunge wetu.
 
Gembe fanya heshima kwa wenzako.

Una hakika kuwa watu wa Tarime watakuwa wanagombania mali. Unadhani kuwa wakurya ni wanyama au watu wasio na akili kiasi hiki. Heshimu wengine na wewe utaheshimiwa.

Maneno ya kashfa kama haya si mazuri wakati wenzako tunahuzunika kwa kifo hiki cha mbunge wetu Wangwe.

Kwa taarifa yako,

huu msiba unanihusu,tena sana mno..usinione niko kimya ila i know everything,mmoja wa wanafamilia wa Wangwe ameoa katika Familia yangu hivyo mie nimmoja wa wanafamilia,na nitaenda huko baada ya MAzishi kutoa Pole
 
Gombe. hii habari ya risasi nami nimeisikia kutoka Tarime.Ndugu wa marehemu wamegundua tundu la risasi baada ya kukagua mwili wa marehemu ulipofika kijijini kwake.(lakini mpaka sasa nachukulia ni uvumi). Mpaka wenye habari za kweli watakapotufahamisha zaidi.
 
Kibiti,
Tumeelezwa daktari anakuja toka Nairobi, that mean hajafika na kuufanyia uchunguzi mwili, sasa hizi risasi mbili zinatokea wapi? Kama kauawa kwa risasi waliouona mwili wa kwanza yaani wanakijiji nafikiri hilo wangeliona kwa sababu jeraha la risasi ni tofauti saana na mkumbuke wanavijiji wengi ni wawindaji hivyo wanajua majeraha ya risasi.
 
Wana JF,
Naomba muangalie maelezo kuwa jamaa walinunua voucher ya simu. Nafikiri kuna haja ya kwenda hapo dukani na kuuuliza kama wanakumbuka chochote.

Pia naomba muangalie UKURASA WA 15 AU ANWANI hiyo chini ya MPOKI na mchunguze jinsi damu ya Wangwe iliyodondokea kwenye shati la Mallya. Inaonekana upande wa kulia tu na inaonekana KUMRUKIA kama vile ilirushwa baada ya au Wangwe kurushwa na kuvutwa tena na mkanda nyuma na damu ikamrukia Mallya. Au ilimrukia baada ya kuwa Wangwe kichwa chake kimetobolewa na damu kuruka.

Sijui kitu gani kilisababisha damu kutoka ila ukweli ilitoka. Sasa ni kwambakwa sababu damu iko upande wake wa kulia, hapa utata unaanza. Kwa muono wangu ni huu, jamaa anatumia mkono wa kulia. Ili amdhuru Wangwe aliyekaa UPANDE WA KUSHOTO mwa gari kama abilia na yeye kama dereva, ilibidi anyenyua mkono huo na kuuelekeza kwa Wangwe, na hivyo hii sehemu ikawa imerukiwa damu. Kama si hivyo basi itakuwa alikaa upande wa nyuma wa kiti cha abilia na mtu aliyemdhuru Wangwe alimdhuru pia upanda e wa kulia na hii imesababisha huo upande wa kulia wa Malya uwe na damu. Labda kama shati lake jamaa lilikuwa na damu pande zote. Naomba wengine pia muangalie na mtoe maoni yenu.

Pictures Credit: http://mpoki.blogspot.com/
 
Kwa taarifa yako,

huu msiba unanihusu,tena sana mno..usinione niko kimya ila i know everything..

Gembe,

kama habari inakuhusu je utatoa maneno ya kashfa dhidi ya wakurya kama ulivyofanya hapo juu? hayo maneno sio mazuri na kashfa dhidi ya kabila fulani sio kitu kizuri.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom