Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Malya.. ana historia kidogo na viongozi wa Chadema; historia pekee inayokosekana ni uhusiano wake na Wangwe, hili linaonekana ni la siku za karibuni sana. Ka nzi ka KLHN ambako kamepeperuka kwa muda maeneo ya DDM na Dar kanaeleza pasipo shaka kuwa Malya amejaribu kujiweka karibu na viongozi wa Chadema kwa muda sasa na amefika makao makuu kama mjasiriamali akatolewa nje. Baada ya kutolewa nje akawa ameandika barua kadhaa za malalamiko kwa kiongozi mmoja wa juu wa Chadema.

Siku chache zilizopita alimkaribia kiongozi mwingine na kutoa wazo kuwa angependa kuandika biograph yake;

inatosha kwa usiku huu: ka nzi kameenda kulala.

one more.. siku moja aliwahi kujitokeza akiwa amebadili rangi za nywele zake akidai kuwa alikuwa ameigiza kwenye mchezo mmoja wa luninga..!!
Huyu ni robot, kazi ni kujua ni nani controller wa huyu robot. Naamini polisi wanajua vyema lakini hawatasema. Je, tutajuaje...??? Tushushieni data... natamani hako kanzi ka KLHN kama kangeweze kuendelea kurukaruka maana kanaonekana kanaleta news za moto sana.
 
Kwa wakati huu, nadhani imetosha kuwapa clues Polisi, wanajua pa kuanzia na ninatarajia watatangaza kesho mwanzo wa mpango wa uchunguzi wa tukio zima hasa baada ya habari za kukinzana ambazo tulizoweka leo ni ncha tu ya mlima uliofichika majini. Vinginevyo natumaini siku ya Ijumaa tutakwenda on the offensive and on record.

Samahani wale wengine ambao tulikuwa tunajibizana mengine nimewasahau kwa muda kwani hii habari ndiyo ilikuwa moto na ambayo ilikuwa inahitaji huduma za kijiji chenu. Tutarudi huko kwingine inshallah.

By the way; nimekoswa koswa na gari mwenyewe leo kwenye traffic light, jamaa ka run red light akakata kona almost at the same time I'm getting to the thick stop line. Nikabreki. Vinginevyo, mngekuwa na simulizi la mwaka. Na jamaa hakuwa na dalili zote za kifisadi; mtasha, gari kubwa SUV, na alikuwa ana kitambi ni miwani ya jua. LOL
 
Mzee Mwanakijiji,

Be carefull my brother. Mafia ni dunia nzima na haichagui rangi wala kabila. IGP mwenyewe alisema nchi imetekwa na magaidi kwahiyo tuiendee taratibu, ina maana washenzi wanaovuruga mambo wana connection dunia nzima ikiwamo wazungu, wahindi na fisi wengine walio tayari kula nchi yetu kila ipatikanapo nafasi.

Sio lazima ulikuwa unafuatwa au unawindwa, ila kuwa mwangalifu maana bado tunakuhitaji Mkuu.
 
Mzee Mwanakijiji,

Be carefull my brother. Mafia ni dunia nzima na haichagui rangi wala kabila. IGP mwenyewe alisema nchi imetekwa na magaidi kwahiyo tuiendee taratibu, ina maana washenzi wanaovuruga mambo wana connection dunia nzima ikiwamo wazungu, wahindi na fisi wengine walio tayari kula nchi yetu kila ipatikanapo nafasi.

Sio lazima ulikuwa unafuatwa au unawindwa, ila kuwa mwangalifu maana bado tunakuhitaji Mkuu.

Ni kweli..Mambo si mazuri na issue hii ni nzito...Siasa si kitu kizuri....Ni afadhali nijirudie zangu shule maana harufu ya damu kila mahali.
 
zamani, habari zilikuwa zinatoka Polisi, zikichujwa na kuzungushwa; hili la Wangwe watapata kazi sana. Na walifanya jambo baya sana kumtaja kwa jina yule shahidi mzee aliyejitokeza hadharani. Wamuhatarisha sana.

Mwanakijiji siku zote mnasema kuwa Wangwe amenunuliwa na CCM na kundi la Rostam Aziz, sidhani kama CCM kumuua Wangwe itakuwa advantage kwao,wasingemnunua kama nia yao kumuua.

kama ambavyo Chadema wamekuwa wakisema kuwa Wangwe ni rafiki wa CCM hasa DR.AMAN KABOUR, vizuri ni kuwa shutuma hizi bwana Mwanakijiji ulimuuliza kwanini yuko karibu na CCM na akakujibu kwenye mahojiano yenu.

Sioni connection ya Wangwe kuuliwa na CCM wala serikali, na sina ushahidi wa kusema kuwa alikuwa na ugomvi na wana CCM au serikali, wagomvi wake wanajulikana kama alivyofariki mtoto wa Malecela aliyekuwa akigombea uenyekiti wa umoja wa vijana wa UVCCM, mchawi wake alitafutwa katika chama chake, hakuna aliyehusisha kifo cha mtoto wa Malecela na chama cha upinzani wala serikali, shutuma zote zilielekezwa kwenye chama chake.
Wangwe nae alikuwa na nia ya kugombea Uenyekiti Chadema na alikuwa na kundi kubwa la maadui Chadema.

Rostam anaweza kuhuusishwa na Mtikila kama angekufa Mtikila tungesema kuwa Rostam ndio mtu wa mwisho kujibizana na Marehemu,
CCM kama kweli wlimnunua Wangwe basi ni pigo kwao, kwani uhai wa Wangwe ungesaidia sana kuisambaratisha Chadema.

Naamini ni kazi ya Mungu haina makosa lakini kama tukiamua kutafuta mchawi atakuwa anatoka eneo alikokwaruzana na watu.
 
Mwanakijiji siku zote mnasema kuwa Wangwe amenunuliwa na CCM na kundi la Rostam Aziz, sidhani kama CCM kumuua Wangwe itakuwa advantage kwao,wasingemnunua kama nia yao kumuua.

kama ambavyo Chadema wamekuwa wakisema kuwa Wangwe ni rafiki wa CCM hasa DR.AMAN KABOUR, vizuri ni kuwa shutuma hizi bwana Mwanakijiji ulimuuliza kwanini yuko karibu na CCM na akakujibu kwenye mahojiano yenu.

Sioni connection ya Wangwe kuuliwa na CCM wala serikali, na sina ushahidi wa kusema kuwa alikuwa na ugomvi na wana CCM au serikali, wagomvi wake wanajulikana kama alivyofariki mtoto wa Malecela aliyekuwa akigombea uenyekiti wa umoja wa vijana wa UVCCM, mchawi wake alitafutwa katika chama chake, hakuna aliyehusisha kifo cha mtoto wa Malecela na chama cha upinzani wala serikali, shutuma zote zilielekezwa kwenye chama chake.
Wangwe nae alikuwa na nia ya kugombea Uenyekiti Chadema na alikuwa na kundi kubwa la maadui Chadema.

Rostam anaweza kuhuusishwa na Mtikila kama angekufa Mtikila tungesema kuwa Rostam ndio mtu wa mwisho kujibizana na Marehemu,
CCM kama kweli wlimnunua Wangwe basi ni pigo kwao, kwani uhai wa Wangwe ungesaidia sana kuisambaratisha Chadema.

Naamini ni kazi ya Mungu haina makosa lakini kama tukiamua kutafuta mchawi atakuwa anatoka eneo alikokwaruzana na watu.

Ndugu zangu wana jf...Hatuna budi kuiheshimu kauli hii ya mgagagigikoko...Na hivyo kwa mara nyingine narudia tena tena...Bwana ametowa na bwana ametwaa..RIP WANGWE.
 
Mwanakijiji siku zote mnasema kuwa Wangwe amenunuliwa na CCM na kundi la Rostam Aziz, sidhani kama CCM kumuua Wangwe itakuwa advantage kwao,wasingemnunua kama nia yao kumuua.

kama ambavyo Chadema wamekuwa wakisema kuwa Wangwe ni rafiki wa CCM hasa DR.AMAN KABOUR, vizuri ni kuwa shutuma hizi bwana Mwanakijiji ulimuuliza kwanini yuko karibu na CCM na akakujibu kwenye mahojiano yenu.

Sioni connection ya Wangwe kuuliwa na CCM wala serikali, na sina ushahidi wa kusema kuwa alikuwa na ugomvi na wana CCM au serikali, wagomvi wake wanajulikana kama alivyofariki mtoto wa Malecela aliyekuwa akigombea uenyekiti wa umoja wa vijana wa UVCCM, mchawi wake alitafutwa katika chama chake, hakuna aliyehusisha kifo cha mtoto wa Malecela na chama cha upinzani wala serikali, shutuma zote zilielekezwa kwenye chama chake.
Wangwe nae alikuwa na nia ya kugombea Uenyekiti Chadema na alikuwa na kundi kubwa la maadui Chadema.

Rostam anaweza kuhuusishwa na Mtikila kama angekufa Mtikila tungesema kuwa Rostam ndio mtu wa mwisho kujibizana na Marehemu,
CCM kama kweli wlimnunua Wangwe basi ni pigo kwao, kwani uhai wa Wangwe ungesaidia sana kuisambaratisha Chadema.

Naamini ni kazi ya Mungu haina makosa lakini kama tukiamua kutafuta mchawi atakuwa anatoka eneo alikokwaruzana na watu.
Hapo mimi nakataa mkuu, hatujafika kuamua kama ni CHADEMA au CCM walihusika juu ya hili, lakini Bw. Mallya atakuwa na majibu yote kuhusu nani haswa amehusika na msiba huu.

Kuhusu vyama kwa ujumla CCM haina hasara kwa lililotokea ukilinganisha na hasara iliyoipata CHADEMA, kwanza CHADEMA wamepoteza jimbo ambalo sasa CCM wanapiga kambi kuliiba, pili watu wa madini ambao ni CCM watapumzika, tatu kama usemavyo wewe CHADEMA itachafuka kwakuwa itaonekana imehusika. Kwa ujumla CCM sanasana labda wamepoteza pesa ambazo sio shida kwa mafisadi...! Pia CCM ina namna, mbinu na watu wengine ambao wanaweza kutumika kuwachanganya CHADEMA...! Time will tell maana binadamu tuwaone tu usoni lakini mioyoni mwao hatuwajui wako vipi, ni hatari kuliko Simba wala watu...!
 
Nazidi kushangazwa na watu wanaosema kuwa WANGWE kahujumiwa na CCM au Serikali.

watu hao hao siku si nyingi walisema kuwa WANGWE afukuzwe uanachama chadema kwa vile ni mzigo ndani ya Chadema na ni pandikizi la CCM.

SWALI KAMA CCM walimnunua Wangwe kupitia kwa Rostam na wakasema kuwa walikutana MOVENPICK ili awe Mwanaccm na mtu aliyekuwa akimpa siri za Chadema ni mbunge Aman Kabour,vipi leo CCM wamuue pandikizi lao? kitu ulichokinunua mwezi uliopita ukijua thamani yake kwanini leo ukiue kabla hujarudisha gharama zako?

ushahidi mwingi wa wazi Wangwe alikuwa na maadui nje ya CCM na serikali na alikuwa na nia ya kugombea Uenyekiti Chadema, hili lilitokea kwa mtoto wa Malecela kutaka kugombea uenyekiti wa vijana wa CCM na akapata ajali ya gari na kufariki, katika maneno ya mtaani haikusemwa kuwa kauliwa na wapinzni wa CCM ,bali uvumi ulikuwa kwamba kauliwa na wana CCM wenzake waliokuwa wakiutaka Uenyekiti wa UVCCM, hata Marehemu Chifupa ilisemwa kuwa ni watu waliokuwa hawataki awe mwenyekiti au ashiriki uchaguzi wa UVCCM wa mwaka huu ndio wamemuhujumu, walitajwa watu ambao wako ndani ya CCM hawakutajwa wapinzani, kifo cha Kolimba kilihusishwa na wana CCM kwa vile aligongana nao kimaneno, sas kwani kipimo cha Wangwe kiwe tofauti? inajulikana kuwa kuna genge kubwa linamchukia Wangwe ndani ya Chadema kwani ni uzushi wetu usianze huko? kama tunazipa nguvu imani za kishirikina na kimafia. kwa CCM wangwe angekuwa asset why wamuue?
 
Hapo mimi nakataa mkuu, hatujafika kuamua kama ni CHADEMA au CCM walihusika juu ya hili, lakini Bw. Mallya atakuwa na majibu yote kuhusu nani haswa amehusika na msiba huu.

Kuhusu vyama kwa ujumla CCM haina hasara kwa lililotokea ukilinganisha na hasara iliyoipata CHADEMA, kwanza CHADEMA wamepoteza jimbo ambalo sasa CCM wanapiga kambi kuliiba, pili watu wa madini ambao ni CCM watapumzika, tatu kama usemavyo wewe CHADEMA itachafuka kwakuwa itaonekana imehusika. Kwa ujumla CCM sanasana labda wamepoteza pesa ambazo sio shida kwa mafisadi...! Pia CCM ina namna, mbinu na watu wengine ambao wanaweza kutumika kuwachanganya CHADEMA...! Time will tell maana binadamu tuwaone tu usoni lakini mioyoni mwao hatuwajui wako vipi, ni hatari kuliko Simba wala watu...!

Horace Kolimba alikuwa katibu mkuu wa CCM akagongana na wenzake na muda si mrefu akafariki, uvumi ulioenezwa ni kuwa wale aliogongana nao kimawazo ndani ya chama chake wamemkolimba, haikusemwa kuwa wapinzani wamemkolimba ilitizamwa kuwa kabla ya kufa Marehemu alikuwa na ugomvi na watu gani.

mfano wa pili wa kifo cha Marehemu Amina Chifupa hakikuusishwa na Chadema wala CUF, uvumi wote ni kuwa Amina alikuwa na nia ya kugombea uenyekiti wa CCM kundi la vijana mwaka huu na baadhi ya wana CCM wenzake hawataki agombee ndio wamemfupishia maisha yake.

hakuna aliyesema kuwa CUF wamehusika na kifo cha Amina,

kama alivyopania Marehemu Wangwe kuchukua uenyekiti wa Taifa Chadema,jee wamezima azima yake? kwani Wangwe alisema kuwa uamuzi wa mwisho juu ya hatima yake wanayo wanachama wa Chadema wa nchi nzima sio kundi la wahuni wa makao makuu ya Chadema, na uzoefu unaonesha kuwa Wangwe kwenye chaguzi ni ngumu kumzuia kama alivyopita kwenye umakamu wa Mwenyekiti na kwenye uenye kiti kulikuwa hakuna cha kumzuia.

Mfano wa tatu ni wa Junior Malecela aliyekuwa kwenye sakata la uchaguzi wa vijana na akapata ajali kama WANGWE,alipokufa kifo chake kilihusishwa na chama chake si vyama tofauti.

Wangwe alikuwa na mgongano wa kimawazo na wana Chadema wengi hadi wengine wakasema kuwa afutwe uanachama, wengine wakasema apigwe risasi humu humu JF,wengine wakasema ni Pandikizi la CCM kupitia kwa Rostam na alinunuliwa akiwa Movenpick hotel.

kama CCM walimnunua kwanini wamuue? kama kipimo cha kumpimia Kolimba kilikuwa alikolimbwa na wana CCM wenzake kwa kugongana kimtazamo kama alivyogongana Wangwe na wana chadema wenzake,kwanini tusihusishe kifo chake na mgongano wa kimawazo na wenzake ndani ya chama chake?

katika vita ya ufisadi anayesema kauli hiyo ni Slaaa sio Wangwe basi wangemuua Slaa,lakini Mwanakijiji ana msemo wake kuwa kipimo kiwe kimoja nakubaliana nae,kuwa kipimo cha Kolimba aliyekuwa na mgongani wa kimtazamo na kimawazo na wanaccm,kinafaa kutumika kwenye kadhia hii ya Wangwe, alipofariki DR.OMAR ALI JUMA haiukuhusishwa CUF ni wana CCM wenzake ndio waliovumishiwa ubaya na hilo hadi kwa marehemu Sokoine. mchawi siku zote ni jirani au mtu wako wa karibu hamlijui hilo?
 
Kwa wakati huu, nadhani imetosha kuwapa clues Polisi, wanajua pa kuanzia na ninatarajia watatangaza kesho mwanzo wa mpango wa uchunguzi wa tukio zima hasa baada ya habari za kukinzana ambazo tulizoweka leo ni ncha tu ya mlima uliofichika majini. Vinginevyo natumaini siku ya Ijumaa tutakwenda on the offensive and on record.

Samahani wale wengine ambao tulikuwa tunajibizana mengine nimewasahau kwa muda kwani hii habari ndiyo ilikuwa moto na ambayo ilikuwa inahitaji huduma za kijiji chenu. Tutarudi huko kwingine inshallah.

By the way; nimekoswa koswa na gari mwenyewe leo kwenye traffic light, jamaa ka run red light akakata kona almost at the same time I'm getting to the thick stop line. Nikabreki. Vinginevyo, mngekuwa na simulizi la mwaka. Na jamaa hakuwa na dalili zote za kifisadi; mtasha, gari kubwa SUV, na alikuwa ana kitambi ni miwani ya jua. LOL
Huwezi kuwalekeza Polisi pa kuanzia, wewe uko miles away na Tanzania halafu uwape instructions polisi? hata SFO wa UK walimfuata Chenge na kupitia vitu mbali mbali hawakuamua tu wakina mbali na matukio. usiwangilie Polisi.
 
sasa Malya si mwanachama wa Chadema? au una info zinaonesha kuwa siyo....?

Wasemaji wa Chadema wapo, wanaweza kuja na jibu zuri kama ni mwanachama wao au laa, hapa hakuna mtu mwenye REGISTER ya wana chama wa Chadema labda useme uko hapa kupindisha au kuficha kitu fulani katika uchunguzi huu. kama unataka kujua fulani ni mwanachama wa chama fulani wapige simu au tuma email kwa wahusika kuliko kusubiri jibu la hapa ambako huna uhakika na wasemaji wa vyama husika.
 
Kolimba aligongana kimtazamo na wana CCM ikavumishwa kuwa amekolimbwa na wana ccm wenzake, kipimo hicho hicho tukitumie kwa Wangwe aliyegongana na wanachadema wenzake juu ya mwenendo wa chama chao.
 
Marehemu alikuwa anakula kote kote..ccm na chadema...Huku akipeleka siri kote kote...Yani hata siri za ccm unawezakuta ni yeye alikuwa akiwapa chadema and vice versa...So inawezekana kifo chake kikawa pigo pande zote.
Ila connection iko pande zote kama ni kweli huyo kijana na yeye ni mwana chadeccm...Kwa maana na yeye anakula kote kote.
Mchezo mchafu wenye madhara huo!
Mungu amrehemu tu.

NB:The only thing pia ni kujiuliza kuhusu kauli ya Mkumbo aliposema marehemu alikutana naye na walizungumza bila kupata nafasi ya kula wala kunywa...Na alisema wazi kuwa marehemu alidai kuwahadhi yake imeshushwa na sasa alikuwa na hasira sana kwani umaarufu wake ulikuwaa matatani.

Sasa nauliza...Umaarufu wa mtu huu ni kweli ulikuwa chini?
 
Kuna ushahidi mwingi kuhusu mengi yaloyotokea, ni kweli. Kwasababu issue bado ni ya moto nadhani tutaendelea kupata clues mingi zaidi muda ukisonga maana naona bado kuna nyuz mingi zitamwagwa hapa. Kwanza leo ndio tutaona mazishi yataendaje, na kawaida ya issue kama hizi kwenye shughuli huibuka na kufanyika mambo mengi yaliyokuwemo ama yasiyokuwemo kwene ratiba.

Naamini tutapata mengi kutokea Tarime yakiambatana na mazishi ya huyu Kamanda, hasa ukichukulia serikali ilivyokipa uzito kifo hiki. Kituo kimoja cha TV kimediriki kusema yanafanana na ya Baba wa Taifa (Nyerere) kwa mengi.

Mimi niko makini kushudia kupitia vyombo vyote vya habari nipate ukweli kupitia utafiti wangu wa jumla, Asanteni.
 
Horace Kolimba alikuwa katibu mkuu wa CCM akagongana na wenzake na muda si mrefu akafariki, uvumi ulioenezwa ni kuwa wale aliogongana nao kimawazo ndani ya chama chake wamemkolimba, haikusemwa kuwa wapinzani wamemkolimba ilitizamwa kuwa kabla ya kufa Marehemu alikuwa na ugomvi na watu gani.

mfano wa pili wa kifo cha Marehemu Amina Chifupa hakikuusishwa na Chadema wala CUF, uvumi wote ni kuwa Amina alikuwa na nia ya kugombea uenyekiti wa CCM kundi la vijana mwaka huu na baadhi ya wana CCM wenzake hawataki agombee ndio wamemfupishia maisha yake.

hakuna aliyesema kuwa CUF wamehusika na kifo cha Amina,

kama alivyopania Marehemu Wangwe kuchukua uenyekiti wa Taifa Chadema,jee wamezima azima yake? kwani Wangwe alisema kuwa uamuzi wa mwisho juu ya hatima yake wanayo wanachama wa Chadema wa nchi nzima sio kundi la wahuni wa makao makuu ya Chadema, na uzoefu unaonesha kuwa Wangwe kwenye chaguzi ni ngumu kumzuia kama alivyopita kwenye umakamu wa Mwenyekiti na kwenye uenye kiti kulikuwa hakuna cha kumzuia.

Mfano wa tatu ni wa Junior Malecela aliyekuwa kwenye sakata la uchaguzi wa vijana na akapata ajali kama WANGWE,alipokufa kifo chake kilihusishwa na chama chake si vyama tofauti.

Wangwe alikuwa na mgongano wa kimawazo na wana Chadema wengi hadi wengine wakasema kuwa afutwe uanachama, wengine wakasema apigwe risasi humu humu JF,wengine wakasema ni Pandikizi la CCM kupitia kwa Rostam na alinunuliwa akiwa Movenpick hotel.

kama CCM walimnunua kwanini wamuue? kama kipimo cha kumpimia Kolimba kilikuwa alikolimbwa na wana CCM wenzake kwa kugongana kimtazamo kama alivyogongana Wangwe na wana chadema wenzake,kwanini tusihusishe kifo chake na mgongano wa kimawazo na wenzake ndani ya chama chake?

katika vita ya ufisadi anayesema kauli hiyo ni Slaaa sio Wangwe basi wangemuua Slaa,lakini Mwanakijiji ana msemo wake kuwa kipimo kiwe kimoja nakubaliana nae,kuwa kipimo cha Kolimba aliyekuwa na mgongani wa kimtazamo na kimawazo na wanaccm,kinafaa kutumika kwenye kadhia hii ya Wangwe, alipofariki DR.OMAR ALI JUMA haiukuhusishwa CUF ni wana CCM wenzake ndio waliovumishiwa ubaya na hilo hadi kwa marehemu Sokoine. mchawi siku zote ni jirani au mtu wako wa karibu hamlijui hilo?

Maneno yako yana mantiki fulani na wala siwezi kukupinga kwa vile bado tunatafuta ukweli. Hata hivyo kulingana na jinsi ushahidi unavyojitokeza pole pole, huenda tafsiri ya mambo haiko straight namna hiyo. Tuendelee kusubiri na kuchukua kila ushahidi unaojitokeza kama ulivyo bila kutafuta mchawi hadi habari zote zitoke nje.
 
Kolimba aligongana kimtazamo na wana CCM ikavumishwa kuwa amekolimbwa na wana ccm wenzake, kipimo hicho hicho tukitumie kwa Wangwe aliyegongana na wanachadema wenzake juu ya mwenendo wa chama chao.
Hapo nadhani tutakuwa tumeenda haraka mkuu, maana yake Mbowe na Dr. Slaa wapigwe mishale/mawe wakati wa mazishi... HAIFAI...tuipe hii issue muda kidogo wakati huyu Kamanda wa hawa wana-tarime anazikwa leo. Naamini tutapata mengine mengi leo mkuu.
 
sasa Malya si mwanachama wa Chadema? au una info zinaonesha kuwa siyo....?

MKJJ...Si umekuwa msitari wa mbele kusema kuwa ninapenda kutoka nje ya topic?
Sasa heading hii inasema kuwa ni kwanini alijifanya INVISIBLE...Sasa kujifanya invisible ndio kuwa mwanachama wa chadema?
Ama hii haistahili thread yake?
Unapingana na Slaa kuwa huyo kijana hajulikani na chadema na kwamba alishajaribu kujiunga akakataliwa?
Ama there's something tunamisss hapo kwenye u invisible vs uanachama wa chadema?

NB:Naomba urejee kauli kutoka kwa katibu mkuu kuwa makao makuu haimtambui huyo Deus Mallya...Sasa ni chadema mkoani waliokuwa wakimtabuwa?
Je ni kweli kuna chadema mtandao na jf mtandao kama anavyopenda kusema NN?
Maana hata Kuhani ameshindwa kuniambia kama yeye ni SILENCER...Sasa ndugu yangu unayependa kusema ninatoka off topic...Je kwanini watu kama ni ma mod wawe na status hiyo moja na si kuwa na status mbili?
Yani kama kuhani ni mod..Basi ijulikane na isije kuwa kuhani huyo huyo ndiyo silencer maana hapo kutakuwa hakuna haki.
Huu si mtandao huo?
Mtu kuwa flani halafu uwe na status nyingine na kujiita silencer?
Wapi haki?
 
Kama ni kauli ya chadema hii hapa...

C/HQ/ADM/SG/02/185 30 Julai, 2008


MKUU WA JESHI LA POLISI,
P.O.BOX DAR ES SALAAM ,
TANZANIA.

YAH; KIFO CHA MHESHIMIWA CHACHA ZAKAYO WANGWE MBUNGE WA TARIME.

Kutokana na ajali iliyotokea tarehe 28 Julai 2008 katika eneo la Pandambili Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma na kusababisha kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime Marehemu Chacha Zakayo Wangwe, ninalazimika kukuandikia rasmi kuhusiana na taarifa mbalimbali ambazo zimekuwa zikiripotiwa na vyombo mbalimbali vya Habari hapa nchini juu ya utata ambao umekighubika kifo hicho na haswa mazingira ya ajali yenyewe. Katibu Mkuu wa CHADEMA, katika mahojiano yake na TBC1 katika mahojiano yake kwenye kipindi cha Jambo Tanzania alielezea pia utata huo na kutaka Jeshi la Polisi lifanye uchunguzi wa kina.

Maelezo ya Ndugu Deus Mallya ameyatoa kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusiana na jinsi ajali hiyo ilivyotokea na eneo ambalo yeye alikuwa amekaa wakati ajali inatokea , pamoja na kusema kuwa yeye alikuwa amekaa kiti cha nyuma huku Dereva wa Gari akiwa ni Marehemu Chacha Wangwe yameongezea kwenye utata huo.

Taarifa ambazo zimetolewa na watoto wa Marehemu kama walivyohojiwa na vyombo mbalimbali vya habari na kuripotiwa na vyombo hivyo na haswa maelezo yaliyorushwa na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), na vituo vingine vya Television, pamoja na Habari za Magazeti mbalimbali ya tarehe 30-07-2008 ,kama vile Magazeti ya The Guardian, Nipashe, Tanzania Daima ,Mwananchi na mengineyo ambayo yaliandika kuhusiana na maelezo aliyotoa Ndugu Deus Mallya pamoja na watoto wa Marehemu yakilinganishwa na maelezo ya Deus Mallya yanahitaji kupatiwa majibu ya kina, jambo ambalo CHADEMA kama mwathirika wa ajali hiyo isingeliweza kulifumbia macho.

CHADEMA , tumefuatilia kwa kina sana kuhusiana na maelezo hayo ambayo yametolewa kwa nyakati tofauti na watu tofauti kuhusiana na ajali hiyo na hatimaye msiba huo.


Hivyo basi , Chadema kama Chama kilichoathirika kwa kumpoteza Mbunge wake, Mwenyekiti wake wa Mkoa na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti na hivyo kuwa na maslahi ya karibu sana katika uchunguzi huu, tunalitaka Jeshi la Polisi wakishirikiana na vyombo vingine vya Usalama kufanya uchunguzi wa kina kuhusiana na mambo yafuatayo;

1. Kujua huyu ambaye alikuwa (Deus Mallya) na Marehemu kwenye gari lake wakati anafariki ni nani na anafanya shughuli gani.
2. Deus Mallya alienda Dodoma kufanya shughuli gani na ana uhusiano gani na Marehemu na au Familia ya Marehemu.
3. Ndugu Deus Mallya alikuwa amekaa kwenye kiti gani wakati ajali inatokea.
4. Ni nani alikuwa anaendesha Gari wakati ajali na hatimaye umauti unamkuta Mheshimiwa Chacha Wangwe.
5. Ni mazingira gani yaliyopelekea na au kusababisha ajali hiyo kutokea .
6. Tunataka Polisi wachukue hatua stahiki za kisheria ili Deus Mallya akaisaidie Polisi na kuhojiwa kwa kina juu ya suala hili kwani maelezo yake yana utata mkubwa sana.
7. Jeshi la polisi liitoe ripoti ya uchunguzi huo mapema na kuiweka ripoti hiyo hadharani.

Tunapendekeza hatua hizo zichukuliwe mara moja kwani tunaamini kuwa kifo hiki kimeghubikwa na utata mkubwa sana na haswa kutokana na maelezo ambayo yamekuwa yakitolewa na aliyeshuhudia ajali (Deus Mallya) pamoja na watoto wa marehemu.


Tunaamini kuwa utatupatia ushirikiano wa kina ili kuhakikisha kuwa hatua za haraka na za dharura zinachukuliwa mara moja kwa ajili ya kuujua ukweli wa kifo hiki tata.

Pamoja na hayo, hivi karibuni wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakipata taarifa za vitisho pamoja na kuzushiwa vifo kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu za mkononi na ujumbe huo kusambazwa sana kama ilivyoripotiwa kwako na Mheshimiwa Zitto Kabwe (MB).

Tunaomba wabunge wetu wapatiwe Ulinzi na pia taarifa hizo zifanyiwe kazi kwa kina.

Nakutakia kazi njema.

Wako katika ujenzi wa Demokrasia na Utawala Bora.




……………………
John Mnyika - 0754694553,
Kaimu Katibu Mkuu,
Na Mkurugenzi wa Vijana Taifa ,

Nakala:
1. Mhe.Lawrence Masha – Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
2. Mhe.Dr. Willbrod Slaa (MB) - Katibu Mkuu CHADEMA .
3. Robert Manumba -Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom