Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
MWanakijiji Uko tayari kuhojiwa kuelezea unachokijua kuhusu utata wa kifo cha Aliyekuwa Mwansiasa Nguli na Bora wa CHADEMA?
 
Mura mwita hapo umenikosha,
kama walizoea kuwatisha wengine na kuiba mabox ya kura mura hapo lazima kieleweke! Huwezi tumia vitisho kuminya haki ya walio wengi. wamezoea hao kuwatisha wa karatu wasijitokeze piga kura, yego mura jitokezeni muonyeshe ukomavu wenu. Tunawaombea mura mpate haki yenu na sikuyumbishwa na kutishwiwa nyau!

Rwabugiri

Inaaminika kuwa hakuna haki hata kama unastahili haki hiyo ila ni vema wahusika wakazingatia mazingira ya hapa nyumbani, nashukuru hata wao wenyewe zile mbwembwe zao hatuzioni kabisa, nadhani(CCM) wanaendelea kutathimini jinsi ya kututia mchanga wa macho.

Tunawatahadharisha kuwa huo mchanga wa macho wajitiwe wenyewe na kisha ndipo fikra wazielekeze kwetu, hapa nitakuwa sieleweki sana, ila wenye akili wananisoma.
 
Mtazamo wa Masatu inaelekea ni wa kweli kwani Fikra tulizotaka kupata toka kwa Mbowe kupitia kwa MMJJ - KLHNews, zinaelekea kukwama kila wakati. Itabidi tutafiti kuwa pengine ni kweli MMJJ amekalia tawi.


Kubwajinga

Nadhani kuna ile thread yanyu niliwahi kupost hapa nikimshauri Mbowe ajiweke pembeni(ajiudhuru) watu wakanishambulia, wakasema kuwa mimi fikra zangu ni finyu, zimetawaliwa na jazba na hamaki.

Kubwajinga nadhani baada ya uchaguzi tutaandaa maandamano ya Kumshinikiza Mbowe ajiudhuru kwa sababu zinazojulikana, tunathubutu kusema hivyo kwa sababu CHADEMA ndiyo chama chenye sura ya kitaifa kwa sasa, sasa hatuwezi kumuogopa mtu kwa sababu ya maslahi binafsi.

Kubwajinga unajua bado watu hawajaweza kutenganisha CHADEMA na huyu Mbowe, watanzania wanadhani hiki ni chama chake, lakini napenda watu wasilichukulie hivyo, hapo wakati utakapo timu tutamtaka ajiweke pembeni ili tuwe na upinzani wa kweli 2010.
 
Imetolewa mara ya mwisho:
21.09.2008 0457 EAT

Kitendawili kifo cha Wangwe chateguliwa

Na Mwandishi Wetu
Majira

MKURUGENZI wa Upelelezi wa Mashitaka ya Jinai nchini (DCI), Kamishna Robert Manumba, amedokeza juu ya kilichobainika katika uchunguzi kuhusu utata wa kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Tarime, marehemu Chacha Wangwe.

Akizungumza katika mahojiano maalum na Majira Jumapili ofisini kwake juzi juu ya hatua ambazo ofisi yake imezichukua kuhusu wito wa kutakiwa kuunda Tume Maalum ya Vifo (Inquest), DCI Manumba amesema wao walishakamilisha uchunguzi wao.

Akizungumza wiki iliyopita, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Wilbroad Slaa alisema kutokana na uvumi mwingi unaoendelea nchini Kamati Kuu ya Chama hicho imeagiza Jeshi la Polisi liulizwe iwapo uchunguzi uliokuwa ukifanyika unahusu utata wa kifo cha Wangwe ili kama si hivyo waombe Tume Maalum ya Uchunguzi wa Vifo.

Saa 12 tu baada ya kauli hiyo ya Dkt. Slaa, mwanasiasa ambaye katika siku za karibuni amekuwa akizua mkanganyiko katika kambi ya upoinzani, Mchungaji Christopher Mtikila aliibuka na madai mazito akikihusisha kifo hicho na kile alichokiita njama alizodai zilipangwa na baadhi ya viongozi wa juu wa CHADEMA na mfanyabiashara mmoja maarufu nchini.

Katikati ya mjadala mkali unaoendelea katika jamii kuhusu tuhuma hizo za Mtikila na wito huo wa CHADEMA, Kamishina Manumba amelithibitishia gazeti hili kuwa uchunguzi wao umeonesha kuwa Wangwe hakuuawa.

Alipoulizwa kuhusu wito wa kuunda Tume Maalum ya Kuchunguza Vifo Tata, DCI Manumba, alisema ofisi yake haihusiki na uundwaji wa tume hiyo na kwamba kazi yake ilikuwa kufanya upelelezi wa chanzo cha kifo hicho ambao matokeo yalionesha kuwa ni ajali ya kawaida.

Kamishna Manumba aliliambia Majira Jumapili kuwa, pamoja na upelelezi huo kuonesha kuwa kifo hicho kilitokana na ajali, ofisi yake bado iko wazi kwa mtu mwingine mwenye taarifa tofauti kuhusu kifo hicho kuzipeleka na zitafanyiwa uchunguzi.

"Nimesikia taarifa zilizotolewa na tunazitafakari, hatukatai taarifa kutoka kwa mwananchi, tutaipokea na kuifanyia kazi ili tuone kama zitabadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya," alisema.

Alifafanua kwamba taarifa zilizotolewa na Mchungaji Mtikila kuwa kifo hicho hakikusababishwa na ajali, ni sehemu ya taarifa ambazo zinaweza kutumika kufanya uchunguzi zaidi ili kubaini ukweli kuhusu taarifa hizo.

Alisema taarifa zilizotolewa na Mchungaji Mtikila kwa kuwa zimetuhumu baadhi ya watu, zinaweza kuongeza wigo wa eneo la kufanyia uchunguzi huo.

"Tunaamini kuwa Mchungaji anaweza kutusaidia, anaweza kutoonesha watu waliompa taarifa hiyo, hao nao watakuwa eneo la kufanyia uchunguzi na hata yeye mwenyewe (Mtikila) atachunguzwa. Pia tutafanyia kazi maeneo mengine tutakayopata kadri yatakavyojitokeza," alifafanua DCI Manumba.
 
Bubu shukran kwa makala hii...Ila nina swali kuhusiana na kichwa cha habari....Je kitendawili hicho nani alikitega?
 
Mjumbe hauawawi, mimi nimeiweka tu hapa hiyo article, sijui mwandishi kwa nini alichagua kichwa cha habari kama hicho lakini kama sikosei kitendawili kilitegwa na chama cha mafisadi na wao walitaka sana wakitegue wenyewe kwamba kuna ushahidi wa kutosha unaonyesha Wangwe hakufa kwa ajali bali aliuawawa na waliofanya hivyo ni viongozi wa juu wa CHADEMA. Sasa nyuso zimewashuka.
 
Mjumbe hauawawi, mimi nimeiweka tu hapa hiyo article, sijui mwandishi kwa nini alichagua kichwa cha habari kama hicho lakini kama sikosei kitendawili kilitegwa na chama cha mafisadi na wao walitaka sana wakitegue wenyewe kwamba kuna ushahidi wa kutosha unaonyesha Wangwe hakufa kwa ajali bali aliuawawa na waliofanya hivyo ni viongozi wa juu wa CHADEMA. Sasa nyuso zimewashuka.

Na kama ingekuwa CHADEMA basi Manumba na timu yake wasingesita kueleza ukweli huo,! lau kama CCM-Mafisadi walihusika basi ngoma droo, aliyegeuza akili za watanzania waseme ni Chadema alifanya bonge la teknic, maana watu walikuwa wanasubiria CHADEMA wapatikane, hata kama waliokuwa wamemuua sio CHADEMA!

Waberoya
 
Kwanza nashukuru hii kubandikwa hapa ili tuweze kuichambua, namshukuru sana Mkuu Bubu mwenzangu.

Hata hivyo mimi nina wasiwasi na matamshi ya DCI Manumba yeye kama Mkurugenzi wa Makosa ya jinai anasema uchunguzi wao ulisha kamilika na ilionekana Mh Chacha Wangwe hakuuawa. Hapo sipingani naye. Lakini ninapingana naye na kuona hii taarifa yake haijakamilika pale anaposema wako tayari kutoa ushirikiano na mtu yeyote mwenye taarifa zitakazobadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya. Namnukuu toka majira.....
"Nimesikia taarifa zilizotolewa na tunazitafakari, hatukatai taarifa kutoka kwa mwananchi, tutaipokea na kuifanyia kazi ili tuone kama zitabadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya," alisema.

Nasema sikubaliani na uchunguzi anaosema ulisha kamilika kwani bado anaonyesha uchunguzi wake huo haupokamili.
Yeye kama Mkurugenzi anatakiwa kutoa taarifa kamili na abaki na msimamo huo bila kutuchanganya wananchi. Kufanya hivyo bila kujua athari zake atasababisha wananchi kujikita zaidi kuamini taarifa za udaku badala ya taarifa tunazoziamini kwamba ni za kitaalamu toka Jeshi letu la Polisi.
 
Kwanza nashukuru hii kubandikwa hapa ili tuweze kuichambua, namshukuru sana Mkuu Bubu mwenzangu.

Hata hivyo mimi nina wasiwasi na matamshi ya DCI Manumba yeye kama Mkurugenzi wa Makosa ya jinai anasema uchunguzi wao ulisha kamilika na ilionekana Mh Chacha Wangwe hakuuawa. Hapo sipingani naye. Lakini ninapingana naye na kuona hii taarifa yake haijakamilika pale anaposema wako tayari kutoa ushirikiano na mtu yeyote mwenye taarifa zitakazobadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya. Namnukuu toka majira.....
"Nimesikia taarifa zilizotolewa na tunazitafakari, hatukatai taarifa kutoka kwa mwananchi, tutaipokea na kuifanyia kazi ili tuone kama zitabadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya," alisema.

Nasema sikubaliani na uchunguzi anaosema ulisha kamilika kwani bado anaonyesha uchunguzi wake huo haupokamili.
Yeye kama Mkurugenzi anatakiwa kutoa taarifa kamili na abaki na msimamo huo bila kutuchanganya wananchi. Kufanya hivyo bila kujua athari zake atasababisha wananchi kujikita zaidi kuamini taarifa za udaku badala ya taarifa tunazoziamini kwamba ni za kitaalamu toka Jeshi letu la Polisi.


Bubu asante kumpa ushauri wa bure Manumba, ni kuchanganya wananchi yeye anapodai wamekamilisha uchunguzi ambao bado yeye anaona kuna taarifa zaidi zinazo weza ubadilisha! Basi aseme tu uchunguzi unaendelea na mwenye ushahidi wa kusaidia aupeleke! vinginevyo kama umekamilika na ausimamie milele!
 
Bubu asante kumpa ushauri wa bure Manumba, ni kuchanganya wananchi yeye anapodai wamekamilisha uchunguzi ambao bado yeye anaona kuna taarifa zaidi zinazo weza ubadilisha! Basi aseme tu uchunguzi unaendelea na mwenye ushahidi wa kusaidia aupeleke! vinginevyo kama umekamilika na ausimamie milele!

Mwandishi keshasema kuwa Manumba amefanikiwa kutegua kitendawili cha awali.
Sasa ni wazi kuwa Manumba huyo huyo katega kitendawili kingine kipya.
Nadhani hawajachoka na bado wanaweza wakawa na madhumuni ya kukitumia kifo hicho kisiasa huko mbeleni.
 
katika nchi hii hakuna kifo kinachotokea kwa amri ya MUNGU, bali kwa uchawi, kuuawa, au kupelekwa msukule, wako watu wanaosubiri akina sokoine, chifupa, nk warudi toka misukuleni
 

Kamishna Manumba aliliambia Majira Jumapili kuwa, pamoja na upelelezi huo kuonesha kuwa kifo hicho kilitokana na ajali, ofisi yake bado iko wazi kwa mtu mwingine mwenye taarifa tofauti kuhusu kifo hicho kuzipeleka na zitafanyiwa uchunguzi.

"Nimesikia taarifa zilizotolewa na tunazitafakari, hatukatai taarifa kutoka kwa mwananchi, tutaipokea na kuifanyia kazi ili tuone kama zitabadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya," alisema.

Alifafanua kwamba taarifa zilizotolewa na Mchungaji Mtikila kuwa kifo hicho hakikusababishwa na ajali, ni sehemu ya taarifa ambazo zinaweza kutumika kufanya uchunguzi zaidi ili kubaini ukweli kuhusu taarifa hizo.

Alisema taarifa zilizotolewa na Mchungaji Mtikila kwa kuwa zimetuhumu baadhi ya watu, zinaweza kuongeza wigo wa eneo la kufanyia uchunguzi huo.

"Tunaamini kuwa Mchungaji anaweza kutusaidia, anaweza kutoonesha watu waliompa taarifa hiyo, hao nao watakuwa eneo la kufanyia uchunguzi na hata yeye mwenyewe (Mtikila) atachunguzwa. Pia tutafanyia kazi maeneo mengine tutakayopata kadri yatakavyojitokeza," alifafanua DCI Manumba.

Hiki ni kitendawili kipya au kile kile cha zamani?
 
Kimeteguliwa vp kama madaktari wawili tofauti walisem ni ajali?

Maswali najiuliza mimi mara nyingi nisomapo habari za hayati Wangwe ni haya - kuna sababu gani zilizofanya "auwawe"? What kind of a threat did he pose to upinzani and/or sisiemu?
 
Kimeteguliwa vp kama madaktari wawili tofauti walisem ni ajali?

Maswali najiuliza mimi mara nyingi nisomapo habari za hayati Wangwe ni haya - kuna sababu gani zilizofanya "auwawe"? What kind of a threat did he pose to upinzani and/or sisiemu?

Nadhani wale wanaoamini kuwa ameuawa, watakuja kutusaidia kujibu swali hili
 
Kwanza nashukuru hii kubandikwa hapa ili tuweze kuichambua, namshukuru sana Mkuu Bubu mwenzangu.

Hata hivyo mimi nina wasiwasi na matamshi ya DCI Manumba yeye kama Mkurugenzi wa Makosa ya jinai anasema uchunguzi wao ulisha kamilika na ilionekana Mh Chacha Wangwe hakuuawa. Hapo sipingani naye. Lakini ninapingana naye na kuona hii taarifa yake haijakamilika pale anaposema wako tayari kutoa ushirikiano na mtu yeyote mwenye taarifa zitakazobadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya. Namnukuu toka majira.....
"Nimesikia taarifa zilizotolewa na tunazitafakari, hatukatai taarifa kutoka kwa mwananchi, tutaipokea na kuifanyia kazi ili tuone kama zitabadilisha matokeo ya upelelezi tulioufanya," alisema.


Nasema sikubaliani na uchunguzi anaosema ulisha kamilika kwani bado anaonyesha uchunguzi wake huo haupokamili.
Yeye kama Mkurugenzi anatakiwa kutoa taarifa kamili na abaki na msimamo huo bila kutuchanganya wananchi. Kufanya hivyo bila kujua athari zake atasababisha wananchi kujikita zaidi kuamini taarifa za udaku badala ya taarifa tunazoziamini kwamba ni za kitaalamu toka Jeshi letu la Polisi.


Hawajafnya uchunguzi wowote hao.wameketi mda ukafika wakasoma waliyoandika .
 
Wakuu wote heshima mbele sana, ninapenda kuwakumbusha kuwa bado tulikuwa tunaendelea na uchunguzi wa kifo hiki, na tuliahidi kua pole pole siku moja tutasema tulipofikia kuhusiana na uchunguzi, naomba kusema kuwa bado tupo on top of this thing na kwamba soon tutaleta tuliyokwisha yapata,

It does not look good to some of our friends here JF, kuna ambao inaonekana kuwa kumbe mnajua something kuhusiana na hiki kifo na tuko wote hapa kila wakati, sasa why don't you come forward and clean of what you know and what you do not kuhusiana na hiki kifo?

Nilisema huko nyuma na ninarudia tena kua marehemu Wangwe, hakufa kwa ajali ya gari, na niliapa kuwa sitachoka kufuatilia ukweli wa kilichotokea na kuuweka hapa, kwa sababu from mwazo nilikuwa ninaamini kuwa hii haikuwa ajali ya kweli, kwa sababu tumethibitisha kwamba:-

1. Kwenye gari kulikuwa na watu watatu, Wangwe (RIP), na wengine wawili.

2. Mahali ilipotokea "ajali", kulikuwa na gari lingine standby somewhere, baada ya "ajali" ambalo mmoja wa abiria alilitumia kuondoka nalo baada ya kumuacha mwenziwe ambaye alichanganyikiwa baada ya "ajali" na kusahau the original plan ya kukimbilia gari la standby baada ya "ajali".

3. Mzee wa kigogo, aliyekimbilia kusaidia baada ya kusikia kilio cha msaaada baada ya "ajali", ni 100% fact kuwa aliwakuta watu wawili aliwaona wakiu-search mwili wa marehemu aliyekuwa ndani ya gari, ambalo mwanzoni aliliona likienda huku watu wale wawili wakiwa nje ya gari lile la "ajali" wakilifutia kwa pembeni mpaka liliposimama.

4. Mmoja hawa watu wawili, alichukua "something" kutoka mwilini mwa marehemu, ikiwa ni pamoja na laptop, ambayo kwa mzee wa kigogo it looked like a little black box, na later aliskia gari likiondoka karibu na hapo lakini hakuliona gari hilo.

5. Simu ya kijana aliyekamatwa ambaye sasa yuko ndani, ilikutwa ikiwa na ujumbe mwingi sana wa back and forth, kati yake na mbunge mmoja maarufu sana, sasa why don't you come forth na kutuambia hapa JF the whole story kuhusu mawasiliano yenu na huyu kijana?

- Kumbe ulikuwa unamjua huyu kijana aliyekamatwa? tuambie sasa who is he? Wewe ulimjua lini? How? Je baada ya "ajali" did you volunteer info on your own to authorities of knowing and having sometype of communications with this kid? Kama hukufanya hivyo why? Je mlikuwa na mawasiliano ya aina gani na huyu kijana? Who is huyu kijana anyways?

6. Kwa wale mlioshirki ku-deal na mwili wa marehemu, kuanzia bungeni mpaka kwenye mazishi, kwa nini msitueleze ukweli kuhusu the state ya mwili wa marehemu, na hasa ni kwa nini mnafikiri kuwa nyuma ya kichwa cha marehemu kati ya shingo na kichwa kuna sehemu kubwa ya kiuongo ina-miss?,

- na hata kuwafanya madakitari maalum waliokuwepo kuuweka vizuri mwili bungeni kupata shida sana kukirudisha kichwa ambacho kilikuwa kinaning'inia tu na mwili pamoja, rais alipokuja kutoa heshima zake kwa marehemu?

7. Kaka wa Wangwe ni kwa nini baada ya mazishi amekana kuwa ndugu yake hakufa kwa ile "ajali?" ila yeye na familia yake walitaka kama alivyosema "kuokoa jahazi?"

Kwa leo ni hayo tu, lakini sooon tutakuja na mengi zaidi na kwa ukaribu zaidi.

Ahsante Wakuu.
 
Mkuu,Heshima mbele comrade!

Nahisi hizo dataz zinaweza kushtua kwa kiasi kikubwa,tunakusubiri komandoo because it is the right time sasa tuanze kufanya siasa za kibinadamu.Yeyote atakayekua amehusika hata kam ni kiongozi ninayemhusudu,nitatangaza kutokua na heshima nae kuanzia sasa. Maanke hata sisi wanasiasa wachanga tunaochipukia yatakuja kutukuta haya haya.Hapa ni makombora tu mpaka jamii iinuke ipate hasira na kudai majibu ya kuridhisha kutoka kwa wale wenye nayo lakini wameyashikilia.Si Tanzania ni Jamhuri?
 
Kazi nzuri Marshall,
Hapo kwenye namba 5, kama hautajali, unaweza kutufahamisha hizi simu zilikuwa na line za makampuni gani?
 
Wakuu wote heshima mbele sana, ninapenda kuwakumbusha kuwa bado tulikuwa tunaendelea na uchunguzi wa kifo hiki, na tuliahidi kua pole pole siku moja tutasema tulipofikia kuhusiana na uchunguzi, naomba kusema kuwa bado tupo on top of this thing na kwamba soon tutaleta tuliyokwisha yapata,

It does not look good to some of our friends here JF, kuna ambao inaonekana kuwa kumbe mnajua something kuhusiana na hiki kifo na tuko wote hapa kila wakati, sasa why don't you come forward and clean of what you know and what you do not kuhusiana na hiki kifo?

Nilisema huko nyuma na ninarudia tena kua marehemu Wangwe, hakufa kwa ajali ya gari, na niliapa kuwa sitachoka kufuatilia ukweli wa kilichotokea na kuuweka hapa, kwa sababu from mwazo nilikuwa ninaamini kuwa hii haikuwa ajali ya kweli, kwa sababu tumethibitisha kwamba:-

1. Kwenye gari kulikuwa na watu watatu, Wangwe (RIP), na wengine wawili.

2. Mahali ilipotokea "ajali", kulikuwa na gari lingine standby somewhere, baada ya "ajali" ambalo mmoja wa abiria alilitumia kuondoka nalo baada ya kumuacha mwenziwe ambaye alichanganyikiwa baada ya "ajali" na kusahau the original plan ya kukimbilia gari la standby baada ya "ajali".

3. Mzee wa kigogo, aliyekimbilia kusaidia baada ya kusikia kilio cha msaaada baada ya "ajali", ni 100% fact kuwa aliwakuta watu wawili aliwaona wakiu-search mwili wa marehemu aliyekuwa ndani ya gari, ambalo mwanzoni aliliona likienda huku watu wale wawili wakiwa nje ya gari lile la "ajali" wakilifutia kwa pembeni mpaka liliposimama.

4. Mmoja hawa watu wawili, alichukua "something" kutoka mwilini mwa marehemu, ikiwa ni pamoja na laptop, ambayo kwa mzee wa kigogo it looked like a little black box, na later aliskia gari likiondoka karibu na hapo lakini hakuliona gari hilo.

5. Simu ya kijana aliyekamatwa ambaye sasa yuko ndani, ilikutwa ikiwa na ujumbe mwingi sana wa back and forth, kati yake na mbunge mmoja maarufu sana, sasa why don't you come forth na kutuambia hapa JF the whole story kuhusu mawasiliano yenu na huyu kijana?

- Kumbe ulikuwa unamjua huyu kijana aliyekamatwa? tuambie sasa who is he? Wewe ulimjua lini? How? Je baada ya "ajali" did you volunteer info on your own to authorities of knowing and having sometype of communications with this kid? Kama hukufanya hivyo why? Je mlikuwa na mawasiliano ya aina gani na huyu kijana? Who is huyu kijana anyways?

6. Kwa wale mlioshirki ku-deal na mwili wa marehemu, kuanzia bungeni mpaka kwenye mazishi, kwa nini msitueleze ukweli kuhusu the state ya mwili wa marehemu, na hasa ni kwa nini mnafikiri kuwa nyuma ya kichwa cha marehemu kati ya shingo na kichwa kuna sehemu kubwa ya kiuongo ina-miss?,

- na hata kuwafanya madakitari maalum waliokuwepo kuuweka vizuri mwili bungeni kupata shida sana kukirudisha kichwa ambacho kilikuwa kinaning'inia tu na mwili pamoja, rais alipokuja kutoa heshima zake kwa marehemu?

7. Kaka wa Wangwe ni kwa nini baada ya mazishi amekana kuwa ndugu yake hakufa kwa ile "ajali?" ila yeye na familia yake walitaka kama alivyosema "kuokoa jahazi?"

Kwa leo ni hayo tu, lakini sooon tutakuja na mengi zaidi na kwa ukaribu zaidi.

Ahsante Wakuu.


Mkuu ES maandiko yako kidogo yamenishitua sana sana .Nakuamini sana kwa data lakini kwenye hizi I will be very skeptical na nitakuja na majibu yako .Sote tuko graundini tunatafuta data za ukweli .Kuna harufu fulani lakini sitaki kubishana but we are all at work .

Swala hili linataka kukuzwa na watu walikosa la kusema mwanzoni na soon wataibuka na hoja namba 2.

Tupo na tutasema yunayo yajua .
 
Mkuu ES maandiko yako kidogo yamenishitua sana sana .Nakuamini sana kwa data lakini kwenye hizi I will be very skeptical na nitakuja na majibu yako .Sote tuko graundini tunatafuta data za ukweli .Kuna harufu fulani lakini sitaki kubishana but we are all at work .

Swala hili linataka kukuzwa na watu walikosa la kusema mwanzoni na soon wataibuka na hoja namba 2.

Tupo na tutasema yunayo yajua
.

Mkuu Lunyungu,

Heshima mbele sana, ninakuomba kuwa kama una anything you know kuhusu hii ishu uuweke hapa ili tuweze kulisaidia hili taifa na ukweli, this is a very serious ishu ambayo hatuwezi kucheza na facts, ndio maana I am being very careful kwenye kila neno ninalolisema, na nina sababu za msingi kwa kila neno ninalolisema na sina personal ishu na anybody kuanzia hapa wala nje ya hapa, ninayaamini maneno ninayoyasema kwa 100%, na sina agenda yoyote zaidi tu ya committment yangu na taifa, na hasa heshima ya hii forum,

Now some more points kutoka kwenye investigation yangu,

1. - Ninamsafisha DR. Slaaa kwa 100%, kuwa hahusiki na kifo cha Wangwe, na wala hakujua kilichotokea na mpaka leo hajui kilichotokea, ninasema hivi kwa sababu kwangu hii investigation ninaifanya na open eyes na with open mind,

2. - Simu-Isolate anybody na wala simshuku anybody, lakini anybody is anybody, nilipoianza hii investigation nilikuwa na one thing in mind, kwamba hii "Ajali" imefanywa na individuals kutoka vyama vya siasa, Vyama kama vyama haviuhusiki waliohusika wamefanya on personal level kwa faida za binafsi,

- On that line ninaanza kuwa wasi wasi kuwa kunaweza kua kulikuwa na a cross over kati ya viongozi wa vyama hivi vya siasa kwenye kutimiza huu uovu, lakini ninaliifanyia kazi to the end kujua ukweli, my point ni kwamba nina some leads ambazo zinanifanya niwe na wasi wasi kuwa kulikuwa na njama iliyofanywa kwa mchanganyiko wa viongozi kutoka upinzani na CCM, kwa kushirikiana.

- Kwangu viongozi wote wa vyama vya siasa nchini ni target of my investigation na as I move forward nitakuwa very open, ndio maana natangaza rasmi kumsafisha DR. Slaa kuwa hahusiki kwa 100%, sikusema wengine ambao sijawataja wanahusika, lakini mpaka nitakapowasafisha nitasema wazi kama ninavyosema sasa again kua Dr. slaaa hakuhusika na wala hahusikia na wala hakujua anything tena kwa 100%.

Ninarudia tena kua anayetaka tulisaidie taifa na hiki kitendawili please join me, lakini binafsi sina agenda yoyote wala sina interest yoyote, zaidi tu ya kulisaidia taifa, na kuweka heshima ya JF meble, na ninaomba niseme ukweli tena kua, binafsi nina exeprience kubwa sana na Criminal Investigations, kutokana na elimu nzito niliyonayo kwenye hiyo fani, kwa hiyo sio kwamba ninababaisha au ninakurupuka, na kama kawaida siahidi time limit on this, pole pole hakuna haraka, na wala sina muda wa kubishana na anybody.

Mkuu Lunyungu, kama kuna anything unakujua naomba ukiweke hapa tulinganishe tupo wapi na huu uchunguzi.

Ahsante Wakuu!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom