Mkuu kuhani,
Sina nia ya kumhukumu mtu, bali kama ilivyosema misahafu, utawajua kwa metendo yao. Kama nilivyoeleza hapo awali kuna dalili kubwa za kuonyesha kuwa kuna mtandao ndani ya CHADEMA ambao lao ni moja. Sasa ni juu ya kila mtu kuwa na conclusion yake ya kitovu cha huo mtandao kama ni madaraka au ni urafiki tu. Mimi napata hisia za uchu wa madaraka.
Kama ni kweli wote walikuwa wanavuruga, sasa ilikuwaje akaadhibiwa Wangwe peke yake? Ugomvi ulikuwa kati ya Mbowe na Wangwe, sasa ilikuwaje Dr. Slaa, Zitto n.k., wakaamua kuwa upande mmoja tu kama kweli Wangwe naye alikuwa ana point? Kama tulivyojadili hili hapo awali, mengi ya aliyopigania Wangwe yalikuwa ya kweli lakini hayakukubalika na Mbowe (Mtandao) na hicho ndio chanzo cha Wangwe kuitwa fisadi.
Sidhani kama walijaribu ku-accomodate maoni ya Wangwe. Walipojaribu kufanya hivyo kwa kuunda kamati, ripoti yake ilikataliwa na mwenyekiti wa hiyo kamati (Mziray) pamoja na Wangwe wote wakabambikiziwa sifa za kuwa vibaraka wa RA. Mtandao wa CHADEMA ukikukataa tu basi wewe unabatizwa kuwa fisadi.
Dissent ni sehemu muhimu sana ya Demokrasia, kama alivyofanya bwana mdogo Nape huko UVCCM. Haya ya zidumu fikra za mwenyekiti ndio yaliyotufikisha hapa tulipo. Dr. Slaa nafikiri amejitahidi kuwa mkali dhidi ya CCM lakini amefeli sana ndani ya CHADEMA. Tusimuonee aibu kama tunataka awe kiongozi bora.