Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Kifo cha Mhe. Chacha Wangwe na uchunguzi wake

Status
Not open for further replies.
Ni vema angalau umekubali kuwa wote ni waropokaji ingawa umechagua pumba za Dr.Slaa na kuachana na makapi ya Mtikila. Huu ni uamuzi wako. Wengine tusiofuata upepo, tunaangalia mambo kulingana na yaliyomo na sio kwa kumshabikia kiumbe fulani ambaye naye alizaliwa katika hali ya dhambi kama wengineo.
Kubwajinga,
Bado ningali hai kwa hiyo naomba usiniwekee maneno kinywani mwangu. Hakuna mahali popote pale niliposema au kukubali kuwa Mzee Slaa ni mropokaji.
 
Kati ya Mtikila na Mzee Slaa nitamwamini zaidi Mzee Slaa. Sijasikia mahali Mzee huyu alienda kuomba mkopo kwa fisadi.
Jasusi uko sawa na kaa upumzike ukate issues zingine zenye maana kuliko hii ya kumjadili Mwehu. Mahesabu ya MAFISADI siku zote tumeona wanavyokuja kwa kasi kupakazia jambo lakini baada ya muda pumba zinaonekana.
Kama alivyosema Mwita hapo juu,Mtikila aende Tarime akaitishe mkutano wa hadhara na aseme hayo aliyosema DSM. Ndio hapo atakapo jua ya kuwa UNAFIKI HAULIPI. Hii ni aibu kwa wote walioandaa mpango huu wa kutumia kifo cha mtu kujijengea majina na kuchafua wengine.
 
Kuwepo kwenye vyama vya upinzani hapa nchini mwetu ni kaazi ngumu kwelikweli haswa kutokana na hoja za baadhi ya wenzetu hapa.
Hawa viongozi wetu (baadhi) wamekuwa wakipigania hali bora lakini baadhi yetu mmekuwa mkizibeza lakini ni mojawapo ya changamoto, hivi wote mnataka tuwe CCM kwa hela mnazoziiba kwenye hazina yetu haya ni mambo ya ajabu kabisa na haitawezekana!!!!

Mkuu ngomanzito,

Tatizo tu sio kuwa kwenye chama tawala au chama cha upinzani. Kuna wengi ambao wanataka kuona maendeleo na mabadiliko Tanzania bila ya kuwa ndani ya ccm au chama chochote cha siasa - yaani kujenga nchi yao kama wananchi au wajenga nchi.

Kuna wengine wao kazi yao ni kujaribu kuleta machafuko na umwagaji damu ili kuendeleza status quo. Wakati ambao wananchi wa Tarime tunajiaanda na huu uchaguzi ili tupate mbunge atakayefikisha kilio chetu kuhusu sumu mbaya sana inayomwagwa kwenye vyanzo vya maji hapa Tarime na makampuni ya madini, wanafiki kina Mtikila na wenzake wanakuja na hoja ambazo wana wa Tarime tunajaribu kuziweka pembeni ili tuendelee na maisha yetu.

Wakati issue ya Wangwe ikiwa moto, Mtikila na wanafiki wenzake walifyata mikia na makopo yao. Wakati wana Tarime wakidai uchunguzi huru wa kifo cha Wangwe ili haya mambo yaishe, Mtikila na wanafiki wenzake walikuwa wanachukua mikopo toka kwa Rostam Azizi.

Leo hii wanatarime wamezungukwa na mamia ya polisi waliokuja "kuzuia fujo" hapa Tarime, ndio kina Mtikila wanaitisha press conf Dar es salaam kuongelea mambo yaliyopita badala ya kuongelea sera za wagombea wao Tarime na vile watasaidiana na wanaTarime ili kuwapatia maji safi yasiyo na sumu za madini.

Aibu kabisa.
 
Nimekuuliza swali rahisi tu linalohitaji jibu la ndiyo au hapana..... haya mengine yanakupelekea kwingine zaidi ya unavyojaribu kueleza hapa.

Narudia tena swali langu...

Ndugu yangu wewe ni msemaji wa Mtikila?

Ndugu yangu, wewe unamfuata Mtikila (kiumbe fulani) au ni msemaji wake?



Magabe Kibiti,
Ningekushauri mambo ya pr school usiyalete humu JF. Jaribu kuiheshimu JF maana sio kila mtu ana akili za ndio/hapana tu. Kama ukizidiwa hoja, kaa kimya na hakuna atakayekusumbua. Lakini kama ukitaka kunibatiza kuwa ati mimi ni msemaji wa Rev., you are welcome, ila usifikiri hiyo itanizuia kukemea ya Chadema. Wako wengi waliojaribu hiyo na wameshapoa sasa. Kama tunavyowashukia CCM kwa mang'amung'amu yao, hata Chadema nao wanapaswa kupewa dozi yao kulingana na ugonjwa unaowasibu.
 
Jasusi uko sawa na kaa upumzike ukate issues zingine zenye maana kuliko hii ya kumjadili Mwehu. Mahesabu ya MAFISADI siku zote tumeona wanavyokuja kwa kasi kupakazia jambo lakini baada ya muda pumba zinaonekana.
Kama alivyosema Mwita hapo juu,Mtikila aende Tarime akaitishe mkutano wa hadhara na aseme hayo aliyosema DSM. Ndio hapo atakapo jua ya kuwa UNAFIKI HAULIPI. Hii ni aibu kwa wote walioandaa mpango huu wa kutumia kifo cha mtu kujijengea majina na kuchafua wengine.

chakaza;

Hapo nimekuelewa mkuu, lakini mbona huyo Mtikila hajafika hapa nyumbani Tarime? tunamsubiri kwa hamu aje atujuze hayo anayoyafahamu na kisha tutamuuliza maswali akishindwa kuyajibu tu. hapo ndipo atujua kanga anafanana na kuku

mwambieni sisi wana tarime tuna msubiri sana.
 
Magabe Kibiti,
Ningekushauri mambo ya pr school usiyalete humu JF. Jaribu kuiheshimu JF maana sio kila mtu ana akili za ndio/hapana tu. Kama ukizidiwa hoja, kaa kimya na hakuna atakayekusumbua. Lakini kama ukitaka kunibatiza kuwa ati mimi ni msemaji wa Rev., you are welcome, ila usifikiri hiyo itanizuia kukemea ya Chadema. Wako wengi waliojaribu hiyo na wameshapoa sasa. Kama tunavyowashukia CCM kwa mang'amung'amu yao, hata Chadema nao wanapaswa kupewa dozi yao kulingana na ugonjwa unaowasibu.

Naona mkuu umeanza kashfa sasa,

Mambo ya Pr School?
Kuzidiwa hoja? hoja gani uliyonizidi hiyo?
Kubatiza wewe msemaji wa Rev?

Nimekuuliza swali rahisi tu lililohitaji jibu rahisi, hayo mengine na historia yako hapa JF ni juu yako mkuu lakini katika hii thread ambayo inahusu maisha ya wanaTarime mimi nitakemea unafiki wowote ninaoona bila kujali historia ya watu hapa JF (wewe) au Tanzania (Mtikila).

Natumaini tumeelewana katika hili, kama huwezi kujibu swali langu unaweza tu kusema hivyo na sio kuniambia cha kuandika hapa.

Asante.
 
Hapa hata Nyerere alijua kilichomuuwa licha ya kuwa na sababu za kitaalam Mtikila alikuja na zakwake....Nadhani polisi wafanye kazi yao Mtikila aonyeshe ushirikiano na kama anazusha habari kwa mtaji wa kisiasa basi adhibitiwe pia..

Well,

Kutokana na habari hii hapa chini polisi wanamuomba Mtikila aonyeshe ushiriakiano ili ushahidi wake usaidie katika swala la uchunguzi wa kifo cha Wangwe. Suala kubwa hapa je Mtikila atakubali manaake ameshasema hawaamini polisi.

*******************************
Mtikila kuhojiwa na polisi uwazi


Akizungumza na mwandishi wetu jana Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai nchini, Robert Manumba alisema Mtikila atahojiwa kama atatoa ushirikiano kuhusu ushahidi alionao wa madai ya kuuawa kwa Wangwe.

“Ikiwa atathibitisha hayo madai ya kuuawa kwa Wangwe sisi kama jeshi la polisi tutashughulikia, tutamuomba tu aoneshe ushirikiano,” alisema Manumba.

Juzi Jumapili Mchungaji Mtikila aliwaambia waandishi wa habari jijini Dare s Salaam kuwa, Wangwe aliuawa na watu kutoka Kenya kwa operesheni maalum iliyosukwa na vigogo (majina tunayahifadhi).

Alisema ana ushahidi wa kutosha wa jinsi vigogo hao walivyoshiriki kutekeleza mauaji hayo aliyoyaita ya kinyama.
Alimuomba Rais Jakaya Kikwete kukiajiri Kikosi Maalum cha Upelelezi cha Uingereza cha Scotland Yard kufanya uchunguzi wa kifo hicho kwa madai kuwa Wangwe alikuwa kiongozi wa kitaifa.

Source: Global Publishers Global Publishers - Tanzania Newspapers
 
Kubwajinga,
Bado ningali hai kwa hiyo naomba usiniwekee maneno kinywani mwangu. Hakuna mahali popote pale niliposema au kukubali kuwa Mzee Slaa ni mropokaji.

Jasusi,
Kama aliyosema Dr.Slaa kuwa anaushahidi wa Mtikila kupewa 50m na Makamba, yameshaitwa kuropoka na wewe ukasema unayakubali sijui tuseme nini tena. Au wewe unayaonaje hayo aliyobwabwaja Dr. Slaa, hayafanani na kuropoka?
 
Ushahidi wa Mtikila kulingana na mahojiano yako ni wa watu alioongea nao. Kulingana na yeye huo ni ushahidi ambao bado unahitaji kufanyiwa kazi. Whewther ni kweli au sio, lakini kuna point moja aliyosema kuwa polisi walitakiwa kuwabana zaidi watu wanaowezekana kufaidika na kifo cha Wangwe na sio kurahisisha kifo chake kama ajali tu ya barabarani kutokana na dereva asiye na leseni.

Kwa mara nyingine tena ninapenda kuuliza mkuu MMJJ, ni lini utamhoji Mbowe maana ana mambo mengi sana ya kujibu, including huu msiba wa Wangwe, lakini inaelekea ni vigumu sana kwako kumhoji? Can't you be fair and balanced jounalist?

KJ, you worry too much; hivi naweza kumfunga mtu kamba aje kuzungumza na mimi? Kama mtu hataki au hayuko tayari what do I do? Nimkabe?
 
chakaza;

Hapo nimekuelewa mkuu, lakini mbona huyo Mtikila hajafika hapa nyumbani Tarime? tunamsubiri kwa hamu aje atujuze hayo anayoyafahamu na kisha tutamuuliza maswali akishindwa kuyajibu tu. hapo ndipo atujua kanga anafanana na kuku

mwambieni sisi wana tarime tuna msubiri sana.
isayamwita!
Wa Tarime nawapenda sana kwa misimamo yao na sio watu wa kudanganywa kwa Tshirt wala kanga/vitenge na hawamung'unyi maneno kama waoga na ndivyo alivyokuwa Marehemu Wangwe (mbunge kupitia Chadema). Sasa Mtikila na wenzake wabwabwaje wakiwa huko Dsm kwa wamesahau yule aliyeleta hayahaya jukwaani majuzi alipatwa na nini? alisahau hata usafiri. Mwageni sera na sio upupu Tarime na watawakaribisha.Acheni njaa za kuendekeza.
 
Jasusi,
Kama aliyosema Dr.Slaa kuwa anaushahidi wa Mtikila kupewa 50m na Makamba, yameshaitwa kuropoka na wewe ukasema unayakubali sijui tuseme nini tena. Au wewe unayaonaje hayo aliyobwabwaja Dr. Slaa, hayafanani na kuropoka?

Hapana. Kuropoka ni kutoa kauli bila kufikiria. Sidhani Ustaadh Dr. Slaa alifanya hivyo.Na ni nani aliyesema kuwa Mzee Slaa ameropoka kama si wewe?
 
KJ, you worry too much; hivi naweza kumfunga mtu kamba aje kuzungumza na mimi? Kama mtu hataki au hayuko tayari what do I do? Nimkabe?

MMJJ,
I will be a sycophant if I were to worry not. This guy want to be my president.

Ina maana huyu kamanda anayevaa magwanda ya mgambo na kuruka hewani anaogopa kuhojiwa na MMJJ? CNN itakuwaje? Hivi umeshawahi kumtafuta akakataa? Kwa nini usiandike au hata kuanzisha thread ili tumshurutishe aje kuongea na vijana wake utitiri wanaoipigania CHADEMA hapa mtandaoni and beyond? Why are you so soft or somehow afraid of him?
 
Hapana. Kuropoka ni kutoa kauli bila kufikiria. Sidhani Ustaadh Dr. Slaa alifanya hivyo.Na ni nani aliyesema kuwa Mzee Slaa ameropoka kama si wewe?

Huyu uliyempa wasifu wa ustaadhi, ambaye aliyekuwepo wakati Mtikila akihongwa 50m sijui ni wa wapi. Kama hajaropokwa basi angalau atupatie video ya hayo makabidhiano au ushahidi mwingineo, bila hivyo, yeye na Mtikila sawa sawa. Dr. Slaa kachemsha, na kama definition yako ya kuropoka ni kuongea bila kufikiri, sijui hiyo ya kwake tuiiteje, kuropoka x2 ??
 
Huyu uliyempa wasifu wa ustaadhi, ambaye aliyekuwepo wakati Mtikila akihongwa 50m sijui ni wa wapi. Kama hajaropokwa basi angalau atupatie video ya hayo makabidhiano au ushahidi mwingineo, bila hivyo, yeye na Mtikila sawa sawa. Dr. Slaa kachemsha, na kama definition yako ya kuropoka ni kuongea bila kufikiri, sijui hiyo ya kwake tuiiteje, kuropoka x2 ??

Bado swali langu linasubiri jibu ndugu yangu, wewe ni msemaji wa Mtikila?
 
Bado swali langu linasubiri jibu ndugu yangu, wewe ni msemaji wa Mtikila?

Huu ndio ninaoita u-pr school. Ustaadhi anapokosa hoja, huamua kuropokwa.

The bottom line ni kuwa hata kipenzi cha watu akichemsha ni lazima na yeye afahamishwe.
 
Hata na mimi nilikuwa ninamthamini sana Dr. Slaa, ingawa bado namheshimu, lakini sio uongo kila siku zinavyosonga, ninamuona kuwa na yeye hana maana kabisa sawa sawa na wanasiasa wengine wenye uchu wa madaraka. Inaelekea yuko radhi kusema au kumsupport yeyote yule as long as ni kwa manufaa ya mtandao wao ndani ya Chadema.

Kwa jinsi alivyoshiriki katika kumpiga vita marehemu Wangwe na kumsingizia kuwa amenunuliwa, kama anavyosema sasa kuhusu Mtikila na Makamba, inaonyesha wazi kuwa kuna upande ambao ameamua kuulinda ndani ya Chadema, kwa hali na mali na wala sio CHADEMA as a whole. Inabidi huu mtandao wa ndani ya CHADEMA tuuibue maana utakiua chama, kama tulivyoubaragaza ule wa CCM. Mungu ibariki Tanzania.

Mkuu Kubwajinga,

Hapo kwenye Slaa kuwa na uchu wa madaraka hapo nina tatizo napo. Sema yooote, mkurupukaji, hata asemwe kala ruzuku, kamuua Wangwe, si Mkatoliki mtakatifu, lolote lile, lakini sio uchu wa madaraka. Madaraka gani hayo, Uwaziri, au ubunge, au katibu wa CHADEMA ? Wenye madaraka na uchu wa madaraka hawaji hapa kukosoa watoa madaraka. Na kuvumilia kupigwa madongo. Wako huko wanapiga parapanda wakisema "Mali za nchi hazilindwi...patakuwa hapatoshi" lakini "Rais ana nia nzuri...." What crock! Waliojichukulia hela wamesamehewa na bado panatosha, tena panatosha kufanya pati ya kushangilia na kuandamana kumuunga mkono Kikwete. Give me a break. Wanajibaraguza na kujishabadua kwa Rais. Sio Dr. Slaa.

Kikwete ndio anajibaraguza kwa Slaa. Kama juzi alivyomletea utani utani eti atamkamata akitaka. Ungefikiri Slaa ata mu entertain. No, fikiri tena. Kesho yake Slaa akakataa kuombwa undugu, akasema Spichi ya Rais ni bomu, kachemka, kateka nyara kazi za Bunge kwa kusema hela za Serikali ziende anako taka yeye Kikwete, kajitungia sheria za kusamehe Wezi ambao ilibidi washitakiwe kwa jinai, mengi mengine, so horrific a speech, mpaka leo Slaa anadai nakala yake, ambayo, as far as he knows, imefichwa.

Slaa hata mimi mara nyingi nimemkosoa nilipoona amechemsha, kama mwingine yeyote yule. Lakini jina lake halitatajwa katika orodha ya wenye uchu wa madaraka. Hana hatia hapo.
 
MMJJ,
I will be a sycophant if I were to worry not. This guy want to be my president.

Ina maana huyu kamanda anayevaa magwanda ya mgambo na kuruka hewani anaogopa kuhojiwa na MMJJ? CNN itakuwaje? Hivi umeshawahi kumtafuta akakataa? Kwa nini usiandike au hata kuanzisha thread ili tumshurutishe aje kuongea na vijana wake utitiri wanaoipigania CHADEMA hapa mtandaoni and beyond? Why are you so soft or somehow afraid of him?

We anzisha mada ya kumtaka afanye hivyo, sijawahi kumpigia mtu magoti kumbembeleza azungumze nami. Siku akipata nafasi or whatever basi atazungumza. Naendelea kumtafuta though kwa sababu mimi kama wewe kuna mengi ningependa kusikia toka kwake.
 
Mkuu Kubwajinga,

Hapo kwenye Slaa kuwa na uchu wa madaraka hapo nina tatizo napo. Sema yooote, mkurupukaji, hata asemwe kala ruzuku, kamuua Wangwe, si Mkatoliki mtakatifu, lolote lile, lakini sio uchu wa madaraka. Madaraka gani hayo Uwaziri, au ubunge, au katibu wa CHADEMA ? Wenye madaraka na uchu wa madaraka hawaji hapa kukosoa watoa madaraka. Na kuvumilia kupigwa madongo. Wako huko wanapiga parapandanda wakisema "Mali za nchi hazilindwi..." lakini "Rais ana nia nzuri...." What crock! Wanajibaraguza na kujishabadua kwa Kikwete. Sio Dr. Slaa.

Kikwete ndio anajibaraguza kwa Slaa. Kama juzi alivyomletea utani utani eti atamkamata akitaka. Ungefikiri Slaa ata mu entertain. No, fikiri tena. Kesho yake Slaa akakataa kuombwa undugu, akasema Spichi ya Rais ni bomu, kachemka, kateka nyara kazi za Bunge kwa kusema hela za Serikali ziende anako taka yeye Kikwete, kajitungia sheria za kusamehe Wezi ambao ilibidi washitakiwe kwa jinai, mengi mengine, so horrific a speech, mpaka leo Slaa anadai nakala yake, ambayo, as far as he knows, imefichwa.

Slaa hata mimi mara nyingi nimemkosoa nilipoona amechemsha, kama mwingine yeyote yule. Lakini jina lake halitatajwa katika orodha ya wenye uchu wa madaraka. Hana hatia hapo.

Mkuu Kuhani,

Hili nafikiri ni suala linaloanza kujitokeza hivi sasa ambalo linatufanya wengine tuanze kukagua sana mienendo ya Dr. Slaa et al.

Mimi bado ninajiuliza ni kwa nini wapiganaji kama Dr. Slaa na Zitto hawakuona hata 1% ya aliyokuwa anapigania marehemu Wangwe kuwa yana umuhimu? Kwa nini walishiriki kumpiga mawe badala ya kutafuta njia ya ku-accomodate maoni yake?

Hapa ndio ninapobakia na conclusion moja tu, madaraka. Hawa mabwana hakuna atakayewaelewa endapo wataondoka CHADEMA na kuingia CCM. Hivi sasa sio kuwa wanasota ndani ya CHADEMA, wako Ok tu ingawa sio kama akina Lowassa ndani ya CCM.

Kwa hiyo, uchu wao wa madaraka sio serikalini kwa hivi sasa, bali ni ndani ya mtandao wao waliojijengea ambapo Mbowe ndie supreme being ingawa na wao wanaelewa kuwa hana the best qualities za kuongoza chama.

Wote wameamua kufungia macho matumizi mabaya ya pesa ndani ya chama, ukabila, nepotism n.k. ili tu wasiwe against Mbowe. As long as hapigi kelele kama marehemu Wangwe basi yuko Ok. Hiki ndio kigezo changu cha uchu wa madaraka. I might be wrong, but time is a good story teller, and we will have the story well told in a short while.
 
We anzisha mada ya kumtaka afanye hivyo, sijawahi kumpigia mtu magoti kumbembeleza azungumze nami. Siku akipata nafasi or whatever basi atazungumza. Naendelea kumtafuta though kwa sababu mimi kama wewe kuna mengi ningependa kusikia toka kwake.

Sidhani kama hao wengine uliwapigia magoti. Au hao akina Mtikila, Ms. Malecela n.k., uliwapataje? Hii ya kwako ya kuendelea kumtafuta Mbowe naona karibu tutaifanyia birthday, maana na sababu za yeye kutoshikika sasa huwa zinabadilika. Kama kweli na wewe una mengi ya kuuliza, nafikiri yeye angekuwa priority kuliko kuleta wababaishaji kama Mtikila n.k. Tufahamishe ulikokwama ili tutafute dawa.
 
Naona mkuu umeanza kashfa sasa,

Mambo ya Pr School?
Kuzidiwa hoja? hoja gani uliyonizidi hiyo?
Kubatiza wewe msemaji wa Rev?

Nimekuuliza swali rahisi tu lililohitaji jibu rahisi, hayo mengine na historia yako hapa JF ni juu yako mkuu lakini katika hii thread ambayo inahusu maisha ya wanaTarime mimi nitakemea unafiki wowote ninaoona bila kujali historia ya watu hapa JF (wewe) au Tanzania (Mtikila).

Natumaini tumeelewana katika hili, kama huwezi kujibu swali langu unaweza tu kusema hivyo na sio kuniambia cha kuandika hapa.

Asante.

Poti
Lakini hili swali lako sijui msingi wake ni nini?

Mda utafika tu siku hili swali litakapokugeukia na kukuuliza mfano wewe ni msemaji wa SLAA ,ZITO,MBOWE ama chadema.

Haya mkuu .
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom