Hiyo Barabara ya Dar Mwanza imeanza kujengwa toka mwaka 1982 na Wataliani wakaondolewa, sijii wakaja kina nani lakini hadi leo hii jamani hata hizo single lane bado nasikia ndio kwanza zimevuka Dodoma na Upande wa Mwanza zimefika karibu na Nzega... lini Zitapanuliwa hata kufikia hadhi ya Highway? Mungu ndio anajua..
Nimesafiri hivi karibuni toka Dar kwenda Mwanza, barabara ni nzuri na ipo katika hali nzuri katika kilometa zaidi ya elfu ni kilometa 90 tu ambazo hazina lami na zipo kati ya wilaya ya Singida vijijini na Manyoni.
Barabara toka Mwanza hadi Shinyanga ipo katika hali nzuri ingawa inahitaji matengenezo katika sehemu chache sana. Matuta katika barabara hiyo ni makubwa na tahadhali kuwa kuna tuta mbele yako inatolewa mita chache kabla ya kukutana na tuta lenyewe. Hii ni hatari kwa dereva ambaye hana uzoefu na barabara hiyo aidha ni hatari zaidi kwa dereva anayesafiri kwa spidi ya zaidi ya km 160 kwa saa. Barabara hii inafaa kwa kwa mwendo wa sio zaidi ya Km 110 kwa saa huku ukiweka taadhali kubwa kwenye matuta.
Barabara toka Shinyanga hadi Singida haina tofauti sana na MZA-SHY, tofauti unapokaribia tuta kuna vituta vidogo maarufu kama rasta hii inasaidia kwa gari ambalo lipo katika mwendo kasi. Zaidi mipaka ya barabara na sehemu za wakaazi imewekwa. Hii inasaidia naitasaidia sana kuhifadhi eneo la barabara na iwapo kunahitajika upanuzi pasiwepo habari ya nyumba kuvunjwa au kulipa fidia.
SGD-DOM, barabara bado inajengwa na inaonekana itakapokamilika itakuwa katika kiwango cha hali ya juu. Mipaka ya barabara ipo, matuta yapo na ni makubwa kama ya SHY- SGD kuna sehemu wameweka rasta na kuna sehemu hakuna, hivyo taadhali ni muhimu. Katika barabara hii ndio kuna km 90 ambazo hazipo katika kiwango cha lami. Ni katika kipande hiki ambacho kinarefusha safari nzima ya DSM-MZA, kwani kukivuka kinahitaji zaidi ya masaa mawili na nusu kwa gari linalotembea kwa km 40-60 kwa saa.
DOM-MOR hii wengi wamepita na hali yake bado ni nzuri, matuta yake sio makubwa hivyo kufanya madereva wengi kwenda spidi kubwa, ni pana,na haina msongamano mkubwa wa magari.