Kifo cha Kapt. Komba, funzo kwa wanasiasa

Kifo cha Kapt. Komba, funzo kwa wanasiasa

Ngoja nikuulize. Kwa kuwa Hitler amekufa huwa unasema alikuwa ni mtu mzuri sana ama huwa unamuita dictator? Kwanini ulazimishe kumnenepesha ng'ombe mnadani!?

Kuna mwimbo tuliimbaga 'eid amini akifa mimi siwezi kuliia nitamtuuupa kageera awe chakula cha mambaa'
 
Marehemu asiwe kinga ya kufumbia macho maovu yanayoendelea kufanywa na watu wa namna hiyo! Sote tunapita hapa duniani, lakini ujumbe umefika kikamilifu tumuombee tu!

Aliye msafi na awe wa kwanza kumtupia jiwe
 
Hivi huyu mzee hakuwa na watoto wa kiume.maana naona ndugu ni wanawake tupu
 
siku zote marehem hasemwi wala hatajwi kwa mabaya, wahenga walikuwa na hekima kubwa sana, sababu merehmu keshafumba mdomo hana uwezo wa kujitetea kwa kwa kusemwa vibaya na kushutumiwa ingawa inahisiwa anasikia na kuona kila kitu.

Hivyo kutosema mabaya ya marehem haimaanishi watu hawajui mabaya na maovu yake ua wamesaahu la asha, bali wanataja mazuri yake tu ili mwenyewe marehemu asikie na aone akitajwa kwa mazuri.

Mwisho kumbuka kila mtu atakufa na hata ww na mimi tutakufa tu, hatujui mwisho wetu kama utakuwa ni mwema au utakuwa ni mwisho mmbaya, vyovyote iwavyo hautajisikia viuri kama tukitajwa kwa mabaya na ili hali tukishindwa kujitetea.

Mkuu inabidi tuache unafiki tuwe wa kweli. Mauti hata siku moja hayasafishi roho ya mtu. Huwezi kuwa jambazi halafiu ukifa unakuwa mheshimiwa.

NI vizuri kama mtu mzuri akifa tuka muomba mungu amlaze pema peponi, lakini alikuwa mbya atusema wazi tu rot to hell you evil person, we thank God for taking you.
 
nilisikia jana kwenye taarifa ya habari kuwa ana watoto kumi na moja sasa hapo kujua wa kiume wapo wangapi ndo sheeeeedeeer
Hivi huyu mzee hakuwa na watoto wa kiume.maana naona ndugu ni wanawake tupu
 
Nauliza tu kwa mzee wa WAPIGWE TU , sijui nn kitatokea
 
Khaa!! Hivi nyie mna akili kweli? Kumsema vibaya marehemu kuna wasaidia nini?? Yule hayupo nasi tena wala hasikii tena. Hapa mnachokifanya hakuna zaidi ya kuwatia majonzi ndugu na wapendwa wake tu ambao ndiyo haohao wanaoipigia kura ccm, cuf, cdm etc Mnachoonesha ni utoto katika siasa. Eti wanasiasa wengine wajifunze, wajifunze nin? Nani asiyejua kifo? Ndiyo maana mtu akifa husemwa kwa mazuri hata kama ni ya uongo ili kuifariji familia na hata ukisema mabaya yake atajitetea vipi naye kisha kufa?
Jamani hata akili kidogo ya kuliona hili hamna? Ndiyo shida ya kuwa na wanasiasa njaa kali wengi kuliko wazalishaji

Kauli ya kipimbi hii..! Mbona Idd Amin alikuwa anaombewa afe na hata alipokuja kufa baadae wakasema good riddance..?
 
Kwani nikipi kibaaaaya alichofanya komba, maneno ya bungeni mbona ni kawaida sana mtu kuroppka chochote, alikuwa anatetea sera za chama chake tu, tatizo liko wapi?
 
Kwani nikipi kibaaaaya alichofanya komba, maneno ya bungeni mbona ni kawaida sana mtu kuroppka chochote, alikuwa anatetea sera za chama chake tu, tatizo liko wapi?

Kutabilia wenzake vifo unaona kuzuri si ndiyo?
 
Marehemu huenziwa.Husifiwa na kukumbukwa kwa mema yake. Isiwe haramu kusema na alipoteleza pia.Aliposema au kufanya tofauti ya matarajio ya wengi au wote. Maneno ya tahadhari au ya mafunzo wakati wa msiba si kwa ajili ya marehemu.Yeye hausiki tena.Kusema na kutenda.


Alichoposti mtandaoni J.J.Mnyika ni kukumbusha tu kauli ya Hayati Kapteni John Damian Komba aliyoitoa katika Bunge la Katiba. Kauli ya kumsimanga na kumtabiria kifo Waziri Mkuu Mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,Jaji Joseph Sinde Warioba. Hayati Komba alimwita Warioba 'mzee anayekaribia kufa'. Haikuwa kauli rafiki.Ilikera na kukwaza kwelikweli.

Kukumbusha kauli hiyo wakati wa msiba wa mtoa-kauli si matusi wala kejeli.Ni mafunzo kwa sisi tuliobakia.Tunaaswa kusema na kutenda kwa mipaka hata pale tunapoghadhibika.Tujitahidi sana kuzuia kughafilika. Kifo ni fumbo. Kujua haiwezekani. Tunaaswa kuwa makini na kauli na matendo yetu hasa kuhusu masuala ya kifo.

Tukimtetea Hayati Komba kwa kauli yake,Mzee Warioba atajisikiaje? Misiba itufunze zaidi ya kuhuzunika na kuomboleza kwetu. R.I.P. Captain (Rtd.) John Damian Komba!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Wenzako hawataki kuyasikia maneno hayo

Kwao kumtukana warioba na kumkata vibao vya mgongoni kuliwanufaisha mfano mmoja alipata ukuu wa wilaya na mmoja tuko hapa tunamuaga,ama kweli ya Mungu mengi ya shetani machache
 
nadhani kati ya watanzania wote, kauli chafu kwa marehemu imetoka kwa mnyika mnatetea ujinga ili iweje? Mnyika anajua yeye atalazwa wapi? anakumbuka alivyomtukana rais?
 
...
Alichoposti mtandaoni J.J.Mnyika ni kukumbusha tu kauli ya Hayati Kapteni John Damian Komba aliyoitoa katika Bunge la Katiba. Kauli ya kumsimanga na kumtabiria kifo Waziri Mkuu Mstaafu na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,Jaji Joseph Sinde Warioba. Hayati Komba alimwita Warioba 'mzee anayekaribia kufa'. Haikuwa kauli rafiki.Ilikera na kukwaza kwelikweli.

...

Mungu wa Mbinguni ni mwema. Amlinde na kumpa maisha marefu Mzee Joseph Sinde Warioba na Tume yake. Mwanadamu u nani wewe utabiriye vifo vya wenzio? Ni mpumbavu tu wa kushupaza shingo atakayethubutu kujiinua kujifananisha na wewe Mtakatifu wa Mbinguni; ambaye ndiwe peke yako mwenye kujua majira na nyakati.

Hata Shetani na milki yake hawajui siku ya mwanadamu kufa; sembuse sisi wa mwili wa nyama na damu. Komba ametimiza wakati wake, amekwenda. Hatumsemi vibaya wala kumjadili yeye kama yeye bali tunajadili mawazo yake ambayo kimsingi hayafi bali yanaishi. Yale mema tuyachukue; yasiyo mema tuachanne nayo na yawe fundisho kwa vizazi.
 
Back
Top Bottom