Kifo cha Kapt. Komba, funzo kwa wanasiasa

Kifo cha Kapt. Komba, funzo kwa wanasiasa

Inakuaje hadi maprofesa wanatumia neno kubwabwaja? Hili ni neno linaleta picha nzuri au linatafsiri aina ya mtu anayeliongea? Mh Rais kwa mfano anaweza tumia neno hili,au ni la wahuni wahuni.Nielimisheni
 
heri kaondoka kuliko angeingia msituni kwani madhara yangekuwa makubwa zaidi. wajane, watoto na vilema wangetaabika kwa kuingia kwake huko.
 
Hivi komba alikua mtu mwema!!!??ktk jamii au ndio kama alivyomwambia warioba!
 
Issue siyo kushangilia!! Hapa watu wana andika wasifu wa marehemu hiyo ndiyo ilikuwa Tabia yake. Unataka wamsifu kwa vile sasa ni marehemu?? By the way huu in ujumbe kwa walio baki wenye tabia kama ya Komba. Mnatakiwa mjifunze kwa kupitia kifo cha Komba. Ccm wenye Tania na uropokaji kama was Komba mko wengi. Jirekebisheni.
Alivyo sema Mh anakaribia kufa mbona hamkumuambia afute kauli yake?? Sasa katangulia kamuacha Mzee wa watu.

Natumaini Bunge lijalo atakayeleta kejeli mfano hai upo
 
Wazazi wamefikaje huku tena jamani? Si mmalizane wenyewe tu!

Hapana huwa sipendi mtu kuwa na ad hominen arguments! One has to put forward arguments sio kutukana. ukinitukana nitakutukana kwa tusi lolote. mimi sikumtukana nimetoa hoja, angelijibu hoja! This is my modus operand!
Pole kama nimekukwaza ndugu. nami sipendi kuingiza wazazi, lakini ukitanguliza tusi tegemea kujibiwa lolote
 
Inakuaje hadi maprofesa wanatumia neno kubwabwaja? Hili ni neno linaleta picha nzuri au linatafsiri aina ya mtu anayeliongea? Mh Rais kwa mfano anaweza tumia neno hili,au ni la wahuni wahuni.Nielimisheni
Kwani unafikiri hakuna maprofesa wahuni.
 
Khaa!! Hivi nyie mna akili kweli? Kumsema vibaya marehemu kuna wasaidia nini?? Yule hayupo nasi tena wala hasikii tena. Hapa mnachokifanya hakuna zaidi ya kuwatia majonzi ndugu na wapendwa wake tu ambao ndiyo haohao wanaoipigia kura ccm, cuf, cdm etc Mnachoonesha ni utoto katika siasa. Eti wanasiasa wengine wajifunze, wajifunze nin? Nani asiyejua kifo? Ndiyo maana mtu akifa husemwa kwa mazuri hata kama ni ya uongo ili kuifariji familia na hata ukisema mabaya yake atajitetea vipi naye kisha kufa?
Jamani hata akili kidogo ya kuliona hili hamna? Ndiyo shida ya kuwa na wanasiasa njaa kali wengi kuliko wazalishaji



Wewe Binti Vipi? Mleta mada anataka nyie MABWANYENYE mliobaki mjifunze kutokana na kifo cha mwenzenu!!! Alitenda kana kwamba ataishi milele. Kwahiyo wewe na hata familia yake ambayo iliishi kwa unafiki wa marehemu mjifunze na muepuke uzandiki huo.
 
Hakuna mtu yeyote anayejua kuwa maneno/matamshi yake yanaweza kuwa hasara au faida hadi siku atakaporudi alipokuwa (mauti).
Na siku hiyo ni walio hai tu ndio uendeleza kuzungumzia/kukumbuka kauli hizo na kuzichambua/kuzitafakari vyovyote vile waonavyo na kadri walinvomfahamu marehemu.
Pamoja na mapungufu ya kiubinadamu aliyokuwa nayo,Hayati Kpt.J Komba alikuwa ni mtu muhimu sana ndani na nje (kwa wanachama na wakereketwa) ya CCM.
Sote tumsaheme kama alitukwaza kwa namna moja au nyingine,lakini pia tumuenzi kwa ushujaa na umahili wa kutumia kipaji chake kwa manufaa ya wote.
 
Back
Top Bottom