Kifo cha Kapt. Komba, funzo kwa wanasiasa

Kifo cha Kapt. Komba, funzo kwa wanasiasa

Uko sahihi Mkuu! Safari ya kifo huanza mara tu mbegu ya kiume iunganapo na ya kike. So, suala la kifo sio suala la mjadala bali suala la muda tu; kwa wale wana-hisabati, death = f(time) where time is very unpredictable - hapa hakuna cha uzee, ujana, wala utoto - at any time (age) death is a sure event.

Kwa maana hiyo, mwanadamu (mwanasiasa) mwenye busara huchunga sana kauli zake akijua muda asiotarijia, kifo huja kama mwivi ajapo. Tuisjitungie sheria (Katiba) na kanuni nyingine za kulinda ka-kikundi ketu kana kwamba tutaishi milele humu duniani. Badala yake tufanye mambo kwa maslahi mapana ya taifa, kwa maslahi ya maskini walio wengi, kwa maslahi ya wananchi.

Hebu tuandae mabango yetu vizuri ili tuyabebapo wengine waone sifa njema kwenye mabango hayo ili ijapo siku ile tusiyoitajia wananchi watukumbuke kwa sifa nje badala ya kushukuru na kusema "afadhali". Hivi utapata faida gani kwa kuacha mabilioni ya ufisadi kwenye mabenki huku ukiondoka na sanda na jeneza tu wananchi wakishukuru kwa kuondoka kwako? Marehemu Komba alijaaliwa kipaji lakini kwa nyakati tofauti alitumia kipaji chake vibaya - hakuwa na sababu ya kuwatukana na kuwadharau wapinzani kiasi kile! Kwamba kama sio CCM wewe sio mtanzania!? CCM na wanasiasa wajifunzi siasa za staha na kuvumiliana

Kwamba Mzee Warioba na tume yake ni wazee wanaokaribia kufa hizo ni kauli za akina Komba, Ridhiwani, Paul Makonda, Kibajaji, na Nape. Kwa hakika Mungu akiamua mtatangulia wote mtawaacha wazee hawa; bahati nzuri wao wanalo bango lililo jema; ninyi mtapotea kama mbwa asiyekumbukwa tena baada ya kifo chake.

Hiyo nyekundu nimeikubali mtabe. It's real. Probability yake huwa ni kitu kizima siyo sehemu tena kama sikosei. safi sana kamanda.
Mimi huwa siwaelewi watu wanaosema eti mtu akishaaga dunia, basi hajadiliwi, mapokeo mabaya kabisa. Mtu sema upuuzi wake tu hata anapokuwa anazikwa. Alikuwa mwizi, sema sifa hizo, sio mbaya maana alikoandikiwa mtu baada ya kufa, hata ukimpamba vipi, hubadili mawazo ya aliye hai milele. Sasa sisi tunadanganyana tu. Unafiki tuache kwa kweli, suala la kufa kila mtu analijua kuwa lzima afe siku moja tu. But unakufaje? ndo swali
 
Makamanda wa ukweli huwaombea maisha maisha marefu maadui zao ili waje kuona mafanikio yao. Kinyume chake ni makamanda fisi ( waoga)

Ngoja nikuulize. Kwa kuwa Hitler amekufa huwa unasema alikuwa ni mtu mzuri sana ama huwa unamuita dictator? Kwanini ulazimishe kumnenepesha ng'ombe mnadani!?
 
Hukusikia bungeni mtoto wa mh furani akasema tumuache baba yake apumzike.
 
R.I.P Komba ngoja ifike zamu yakufa lema na TL sijui mtasemaje

Unaruhusiwa kuwasema upendavyo sio kuanza kuwapamba kwa sifa za kipuuzi. Utakachokisema watu tutajua ni kweli ama ni uwongo. Na ujue hali hiyo itakuwa fundisho kwa wengine kutokana na tabia utakazozisema. Ila kusifiana sifa za uwongo siafiki. Hivi kaburu Peter Botha wa S. Africa tulimsifia baada ya kufariki? Hii tabia ya kulazimisha sifa nzuri ambazo mtu akiwa hai hajali kama ana wajibu wa kujenga sifa njema tunaitoa wapi. Simply ni unafiki
 
umesahau alisema wapinzani wakishinda ataingia msituni,,,,ndio kaingia hivo
 
Mimi niko bado najiuliza, Captain Komba aliwezaje kutunga nyimbo za kuombeleza kifo cha baba wa taifa ndani ya muda mfupi tu tangu kifo kitokee, au alikuwa ni mnajimu aliyetabiri kuwa Baba wa Taifa atakufa na akaanza kutunga nyimbo na kuifundisha band yake?? Looh, kafa kabla hajatupatia majibu ya swali la kitendawili hiki!!! Vile vile alisema atakwenda msituni, hakufafanua kama angeenda msituni kujificha ili katiba asiyoipenda kama itapitishwa, au kwenda msituni kuongoza mapambano ya kijeshi kutetea katiba anayoipenda. Looh, kafa kabla hajatupatia majibu ya swali la kitendawili hiki kingine!!!

The guy was very talented musician...he could have been our Mozart or something. Instead of honing his skills on the talent he chose the easy path to get rich in Africa...becoming a politician.
RIP Capt Komba....ningependa kupata CD ya nyimbo zake toka 80's...they rejuvenate us and make us feel young again
 
Mnataka huyu nanii, nanii huyu bhana, yaani akifa tusiseme upuuzi wake, yaani kwa hawa ma- DC, haki tena tutasema sana!

Hadi nyimbo kama za nduli amini tutaimba!
 
Kila mtu atakufa na atakumbukwa kwa kutajwa yale aliyoyatenda wakati wa uhai wake yawe mazuri au mabaya.Mimi nakumbuka mara ya mwisho nilimuona Marehemu Komba akiwa anachangia hoja akisema"Muundo wa serikali 3 ukipitishwa nitaingia msituni", mwisho wa kunukuu.Matendo yako ndiyo mazungumzo baada ya kifo chako.
 
Flora Msoffe,
Hebu niambie kwa akili yako kumsema vibaya marehemu kunasaidia nini?? Arudi ajitete? Kama kuna mabaya alifanya wakati wa uhai wake mbpna mlikuwa kimya?? Tuna sheria na taratibu tumejiwekea dhidi ya watu watendao mabaya kwa jamii km polisi na mahakama
Mlikuwa wapi hadi msubiri afe? Hii siyo dalili ya udhaifu kweli??

Wewe Roho - mbaya, tatizo lako nini kwani?

Hatusemi haya kwa ajili yake bali kwa ajili yetu sisi tulio hai ukiwemo wewe ndiyo maana hukanushi ila una hofia kifo tu!

Si kweli kwamba mabaya au mapungufu yake hayakusemwa alipokuwa hai, yalisemwa sana lakini kiburi cha uzima kilimpofusha!!

Pia kumbuka huyu alikuwa kiongozi na kwa namna yeyote lazima yasemwe mengi juu yake mengine kama ninyi obviousily hamtayapenda!

Hata baba wa taifa Mwl J.K Nyerere mpaka leo anasemwa kwa namna hasi au chanya kila ajisikiaye kusema.

Muulize mtu mmoja humu jamvini anaitwa FAIZAFOXY atakuambia mengi tu mabaya juu Mwl Nyerere J.K kwa sbb ndiyo mtazamo wake!!
 
Wabunge wote wa mkoa wa Ruvuma wanaishi Dar. Komba ana nyumba mbinga mbambabay na lituhi. Zote amekodisha. nimestushwa kuona watu wa nyasa wamefurahishwa na msiba huu
 
.....kupitia msiba wa kpt John Komba ndio nimeanza kuthibitisha chuki kati ya watawala na watawaliwa,hasira kati ya 'wao na sisi',roho mbaya kati ya daraja la chini na daraja la juu....
Watu hawana huzuni tena...na kuna watu wanaongea maneno machafu.....
Nchi haipo salama sana....hasira za matabaka zinaongezeka...
 
Back
Top Bottom