Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,565
- 7,988
Maranya we kumbe KILAZA kabisa nilikuwa nadhani una timamu kumbe haim kabisa,yani kweli unashindwa kutambua kwamba kiongozi ambaye ameshindwa kulea na kuitunza familia yake hana uwezo wa kuingoza nchi?,hivi na hili ni jambo ambalo linakutaka kuwa na Masters moja au mbili kulifahamu?!,hebu nenda kwenye Biblia angalia hata maandiko matkifu yanvyosema juu ya mtu kama Dr.Slaa,hivi umeshinda kusimamia na kuiendesha na kuiongoza nyumba yenye watu watano,utaweza nchi yenye zaidi ya watu milioni 45?.
Hata lile ombi lako la Asubuhi kamba niendelee kukuheshimu naachana nalo moja kwa moja kwa sababu nimegundua wewe ni 'Kimburu',unachojua ni kula tu lakini kutafuta wala kuwinda hujui unsubiri wenzako wakutengenezee ndio wewe ufike na kubugia mwisho wa siku ndiyo hivyo tena unakula kisha unambiwa unatkiwa kulipa na mlipo yenyewe unachaguliwa namna y kulipa!
Sitaki kufikishana mbali sana na wewe lakini wito wangu kwako ni kwamba jifunze kukubali kukosolewa,hakuna mtu asiyempenda Slaa,lakini ili tumfanye akubalike na kuonekan ni kiongozi mzuri tumshauri na kumueleza madhambi yake ayajue.
Kwa taarifa yako mimi siko hapa JF kutafuta heshima kutoka kwa misukule ya ccm ama waganga njaa kama wewe. Hiyo heshima ichukue halafu tuone kama nitakuwa nimepungukiwa nini. Watu wanaoniheshimu na ninao waheshimu wanatosha kwahiyo sihitaji heshima toka kwa misukule ya ccm. Na kwa taarifa yako heshima yangu inaongezeka kila siku hapa JF na hata huko mtaani.
Kama ungekuwa na akili timamu ungetambua kwamba hata katiba yetu haijaweka masharti ya kumtaka mtu kuwa kiongozi lazima awe ameoa ama kuolewa kwakuwa katika kutekeleza majukumu yake ikitokea anaumwa ama ana udhuru wowote hatuwezi kumkabidhi majukumu mke wake au mme wake. Ndio sababu tunakuwa na nafasi ya makamu wa raisi kwa mfano ukizungumzia nafasi ya raisi na wasaidizi mbalimbali ndani ya ofisi ya raisi ikulu.
Tunayo mifano iliyo dhahiri inayoonyesha maraisi kadhaa wa nchi mbalimbali ambao walipata kuongoza nchi zao tena kwa mafanikio makubwa huku wakiwa hawajaoa, sasa sijui hapo utasemaje. Tunachohitaji kama nchi ni kiongozi mwenye vision, mzalendo wa kweli na anayefahamu mahitaji ya wananchi na nchi yake. Hatuhitaji raisi aliye na mke lakini hajui sababu ya umasikini wa nchi yake. Hatuhitaji raisi aliye na mke na mke wake ndiye anaongoza serikali kupitia mlango wa uani. Hatuhitaji raisi mwenye mke lakini fisadi, anatumia mamlaka yake kuiibia nchi kwa kutumia kampuni ya mkewe ama ya mtoto wake kujilimbikizia mali.