Kibanda: Kinana ni Kimbunga

Kibanda: Kinana ni Kimbunga

anaomba msamaha,anaponda humohumo,anasifia humo humo..kesi inayomkabili imemfanya anunulike kirahisi sana,mwoga wa jela huyu.,anachonikera zaidi ni kujifanya genius kuliko wote sababu alisoma HGL.
amenunuliwa kwa bei nafuu sana,!!kibanda usiogope kwenda jela kwa kesi inayokukabili kama alivyofanya yule wa mwananchi na tume ya mwangosi..kwenye msafara wa mamba na kenge kama kibanda wamo

Nimeipenda hii..
 
Wakuu namuomba Kibanda anijibu yafutayo.
  1. kwa mujibu wa maelezo yake aliwahi kutilia mashaka utendaji kazi wa Ben Mkapa kwa upande wa CCM na kwa upande wa upinzani alitilia mashaka Mrema wa NCCR enzi hizo na hata kuwapinga wote wazi wazi,Je yeye kwa mtizamo wake na uwezo wa kuwapinga watu ambao kimsingi hawkufanya vizuri kama ubashiri wake ulivyokuwa,alipendekeza nani awe mgombea wa CCM 1995 na kwa uande wa upinzani instead of Lyatonga Mrema?
  2. Uchaguzi wa 2005 alipinga kuwa JK sio mgombea mzuri na hakufaa kwa nafasi kubwa kama ya kiongozi mkuu wa nchi,Je aliwahi kupendekeza mgombea mbadala ambae yeye kwa ujuzi wake wa kuwatambua viongozi wazuri na wasio wazuri?na kwanini amekuwa haandiki wale ambao kwa mtizamo wake aliona wangefaa kugombea ili taifa lipate viongozi mahiri wa kuwasaidia watanzania
  3. Hivi anaweza kufafanua ubora halisi wa kinana kiutendaji kiasi cha kumfanya unique kiasi hicho?je anadhani ni kwa namana gani Kinana ata-perfom kusafisha chama wakati Kinana huyu huyu ni mchafu tangu miaka ya 1993 na kuendelea na wenzake humohumo wanajua uchafu wake?je anadhani anaweza kuwavua magamba wenzie na wakati yeye ni ganmba pia?
  4. Je ni ushabiki upi wanaoufanya watanzania na tayari ameshawaelewesha kwa kuwapa njia mbadala za kutambua viongozi wazuri ama wakiwa CCM au Upinzani? hasa CDM,maana amesema watu wanaimba Dr Slaa,ni kweli hata mimi naimba hivyo lakini kama anauhakika naimba vibaya si atoke hadharani aseme huyu ndo bora kuliko Dr Slaa kiutendaji ana hata kwenye kugombea uraisi.unapotuambia tunaimba Slaa,Slaa halafu hutuambii mbadala wake kwa vigezo nasi tukapima kwa uelewa wetu na tukalinganisha na ulitueleza tutajuaje kama uko sahihi.
  5. Je kitendaji na vison ni kweli Dr Slaa ni wa kumlinganisha na Lyatonga Mrema?yapo aliyoyafanya Mrema kwa nafasi yake na kwa enzi yake,but you come into comparison,bado Dr Slaa yuko juu.weka vigezo tuone ni kwa vipi unawaza hivyo.
  6. Mwisho unawezaji kufikiri kwamba CDM hawakosoani?au wakikosoana mpaka iwe hadharani ndipo ujue wanakosoana,hawapendi kukosoana hadharani lakini hata wao wanajua kuwa they are not angels.
  7. Kinana mpambe ujuavyo kwetu sisi ni kichocheo cha kufanya kazi ya kukiunga mkono CDM lakini hakika nakuambia hana cha kufanya ndani ya CCM maana nayeye ni Gamba,tena siku hizi huyo ni WEKA MBALI NA TEMBO,Kibanda hujui hayo?
 
Ukitaka kujua kama Kinana ni kimbunga yeye ndio alifanikisha ushindi wa kishindo kwa CCM kuanzia mwaka 1995, 2000, 2005, 2010.

Kama aliweza kuratibu na kupanga ushindi wa CCM hakiwa amekabidhiwa dhamana ya muda mfupi ya kuongoza kamati ya taifa ya kampeni za chama hicho.

Tutalajie nini akipanga mikakati na kusimamia mwenyewe utekelezaji wa mipango ya chama kama Katibu Mkuu.

Hapo ndipo unatakiwa umsome vizuri Kibanda.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza ningependa unionyeshe mahali ambapo Kibanda anajaribu kuwapotosha watu kwa kumpamba Kinana,hilo ni moja Lakini Pili Siamini kama Kibanda ameonesha katika Andishi lake kwamba kutokana na Uteuzi wa Kinanan sasa CHADEMA haiwezi kufurukuta tena:Nadhani utakuwa umemuelewa vibaya tena sana Mkuu Kibanda

Wasiwasi wangu ni kwamba hukusoma makala ya kibanda ya wiki iliyopita, na kama uliisoma basi hukuielewa. Nadhani si vibaya ukarudia tena kuipitia ili ujiridhishe na hiki unachokiandika hapa.

namini hata baadhi ya viongozi wa CDM sio wasafi kama unavyomsemea Kinana kamba ni mchafu,kuna wakina Dk Slaa wamewahi kupata tuhuma nyinginyingi zikiwemo hizo hizo za ufisadi kwenye makanisa huko alikokua,na hata kenye masuala ya ngono!

Huko koooote ulikopita ulikuwa unazunguka mbuyu tu hapo kwenye nyekundu ndiyo ilikuwa target yako kwakuwa hiyo ndiyo kazi mliyokabidhiwa juzi wakati wa mkutano wenu mkuu wa dodoma.

Tuhuma za Dr. Slaa kanisani zimekuwa zikitungwa na ninyi ccm lakini kanisa Katoliki limekanusha hizo taarifa kwamba sio za kweli.
Kuzungumzia mahusiano ya kimapenzi ya mwanaume mwenzako ni dalili mbaya kwako wewe binafsi, kwani inamfanya mtu aanze kutathmini uwezo wako (urijali wako) katika mahusiano ya kimapenzi.
 
Ukitaka kujua kama Kinana ni kimbunga yeye ndio alifanikisha ushindi wa kishindo kwa CCM kuanzia mwaka 1995, 2000, 2005, 2010.

Kama aliweza kuratibu na kupanga ushindi wa CCM hakiwa amekabidhiwa dhamana ya muda mfupi ya kuongoza kamati ya taifa ya kampeni za chama hicho.

Tutalajie nini akipanga mikakati na kusimamia mwenyewe utekelezaji wa mipango ya chama kama Katibu Mkuu.

Hapo ndipo unatakiwa umsome vizuri Kibanda.
ushindi wa kishindo na Tume ya Uchaguzi ya Mh.Rais; Kinana alikuwa kampeni meneja bila kuwa na tume huru ni sawa na kufanya mazoezi ya kuua sisimizi wakati ukiwa na rungu ya tani 50 ??? Na kweli tumeshamsoma vema Kibanda!!
 
Kibanda "nkamu gwangu"this is too cheap!Kwenye nakala zake zote 2 Kibanda Kaeleza tu uzuri wa Kinana lkn HAJAGUSIA kabisa udhaifu wa Kinana!Kwa bahati nzuri tunamfahamu Kinana kama ni KIONGOZI ASIYE NA UWEZO!

Kibanda acha uvivu wa kutafuta habari kuhusu Kinana;nenda JWTZ makao makuu kaulize kuhusu madudu ya Kinana hasa alipokuwa Waziri wa Ulinzi,tafuta undani wa biashara zake na nenda Arusha kaulize jinsi alivyowatumikia wana Arusha hovyo hovyo alipokuwa Mbunge wao!Nasisitiza tena Kinana HANA LA KUJIVUNIA na HANA LOLOTE LA MAANA alilowasaidia WATZ kwa nafasi nono alizoshikilia serikalini;kama tu wenzake wa CCM na yy ni OPPORTUNIST tu!

Kibanda;kesi ile wamekutishia kama watakufunga usipowaandika vyema au?
 
ushindi wa kishindo na Tume ya Uchaguzi ya Mh.Rais; Kinana alikuwa kampeni meneja bila kuwa na tume huru ni sawa na kufanya mazoezi ya kuua sisimizi wakati ukiwa na rungu ya tani 50 ??? Na kweli tumeshamsoma vema Kibanda!!

Hiyo hiyo Tume ya Uchaguzi ya Rais ndio iliyowatangaza washindi John Mnyika, Joseph Mbilinyi, Halima Mdee, Godbless Lema, Freeman Mbowe na wengine.
 
jamani mnahangaika bule na kibanda alisha nunuliwa zamani sana, hamkumbuki alivyokuwa anamshambulia sita? Na alinchufua zaidi siku aliyo pata safasi ya kumuuliza swali la papo kwa papo jk nilitamani kilia eti ndo mweyekiti wa jukwaa la wahariri ni aibu kwa stania ya habari kuongwozwa na mchumia tumbo dizaini ya kibanda.
 
Sidhani kama ni sawa sana mtu kama wewe kuandika vitu kama hivi?!,labda nikwambie ukitaka kujua urijali wangu we nambie nikukute chumba namba ngapi ili ujue niko sawa au siko sawa,mimi nilikuwa naamini humu ndani tunakwenda kwa hoja lakini kumbe naona huna hoja umeanza matusi,wewe sema uko chumba namba ngapi mimi nije



Huko koooote ulikopita ulikuwa unazunguka mbuyu tu hapo kwenye nyekundu ndiyo ilikuwa target yako kwakuwa hiyo ndiyo kazi mliyokabidhiwa juzi wakati wa mkutano wenu mkuu wa dodoma.

Tuhuma za Dr. Slaa kanisani zimekuwa zikitungwa na ninyi ccm lakini kanisa Katoliki limekanusha hizo taarifa kwamba sio za kweli.
Kuzungumzia mahusiano ya kimapenzi ya mwanaume mwenzako ni dalili mbaya kwako wewe binafsi, kwani inamfanya mtu aanze kutathmini uwezo wako (urijali wako) katika mahusiano ya kimapenzi.[/QUOTE]

Sidhani kama ni sawa sana mtu kama wewe kuandika vitu kama hivi?!,labda nikwambie ukitaka kujua urijali wangu we nambie nikukute chumba namba ngapi ili ujue niko sawa au siko sawa,mimi nilikuwa naamini humu ndani tunakwenda kwa hoja lakini kumbe naona huna hoja umeanza matusi,wewe sema uko chumba namba ngapi mimi nije ili uone na katika hili sipepesi macho,nawaomba mods msiiondoe wala msiniban kwa sababu yake mmeiacha imekuja,so nipeni haki yangu na mimi!!
 
Kuna Mambo mawili hapa.... 1.Either Kibanda anataka wana chadema wakae chini na kuweka mikakati mipya baada ya safu ya uongozi CCM kubadilishwa, au 2.Kibanda kaamua kukubali yaishe na kufuata nyayo za Salva Rweyemamu!!

Kama sababu ni hiyo ya pili basi fani ya uandishi wa habari ina makanjanja wengi ambao wanatuangamiza
 
Si rahisi kihivyo kitu gani? Nani asiyejua kwamba usalama wenu ccm uko kwa vyombo vya dola? au unataka kupingana na mwenyekiti wako?

Maranya mbona unanihukumu kihivyo bila kunipa nafasi ya kunifahamu,sikia mimi siko huko uliko,mimi ni mwanaharakati na ndiyo maana nimekuwa nakuunga mkono kwenye coment zako nyingi,na vivbyo hivyo nitamuunga mkono mwingine yeyote yule ambaye nitaona anazungumzia utaifa ama hoja,na niko tayari kuchafuana na wewe vyovyote utakavyo kama nitaona unamshambulia mtu pasipo na hoja ya msingi,maranya umekuwaje wewe?,acha ujinga mkuu naona sasa tuanze kupeana za uso ila niwaombe Mods wawe makini kwa sababu kuna watu humu hawachelewi kuwaban wakipitiliza ila wengine wanachiwa tu wanatirirka watakavyo,wewe kama ni CDM endela ila siku likinuka uatafute pa kwenda sisi wanaharakati tuko KILA KONA YEYOTE YULE TUKO NAE MAADAM AMESIMAMIA UKWELI,Peleka ushbiki wako huko we unadhani kila anayepingana na wewe ni CCM,nyooooooo!
 
Ukitaka kujua kama Kinana ni kimbunga yeye ndio alifanikisha ushindi wa kishindo kwa CCM kuanzia mwaka 2010

Ushindi wa kishindo 2010?!CCM mbona ilipangua safu ya uongozi wake wote wa juu baada ya uchaguzi huo wakilalama kuwa ushindi wao umepungua sana?

Pls Ritz give me a break!
 
Halooh JF,
mimi naungana na hao wanaosema Kibanda kasema anayofikiri na kuamini hivyo tuheshimu hilo. Pia katoa tahadhari kuwa pengine Kinana siye wa KUBEZA aangaliwe kwa macho yote matano na kumfuatilia kwa karibu. Namna nzuri ya kumfuatilia ni kupeleka makamanda kila anapotoa mguu na kwenda kujibu kifasaha mapigo. Naungana na Kibanda, 'hiki Kinana' si cha kubeza. Tutafakari.
 
Huyu jamaa nilmpenda na alikuwa rafiki yangu hata fb, kuanzia makala yake ya mwanzo nimeshapoteza imani nae, sijui ni hii kesi ndo imemfanya hivi au, ngoja nimfuate nikampe makavu live
 
Abi Kibanda! Nakushangaa sana. Kwanza wewe ni mwongo msahaulifu na pia jua kuwa atakaye kukosoa hapa ni kijana mdogo.
UMESEMA mwaka 1995 hukuunga mkonn harakati za Mwl . Nyerere (udikteta katka demokrasia) ili Mkapa awe mgombea urais kupitia CCM, na umethibitisha kwa kusema utabiri wako ulitimia kwa Mkapa kuboronga mwishoni. Lakini pia umesema ulipinga 2005 Kikwete kugombea urais na hadi ukakwaruzana na Rostam, hata hivyo Kikwete alishinda na kwamba wote tunashuhudia kuboronga kwake.

Sasa huyu ndo Kikwete aliyepokonywa karata na Mwl. 1995 kwa kumpendekeza Mkapa, sasa 1995 wewe ulikuwa upo kwa mgombea yupi? Au Kikwete wa 2005 uliyempinga alikuwa sio yule aliyefanyiwa udikteta 1995?

Tukiendelea zaidi pia umesema, Mrema 1995 kupitia NCCR hukumkubali. Je mwaka huo basi wewe ulikuwa huna mgombea wa kumpa kura yako?
Au alikuwa wa chama kipi mbali na hivyo viwili.
acha uvivu wa kufikiri kumkataa mkapa hakumaanishi kumkubali kikwete.kama alimkataa mkapa the akamkataa kikwete means aliwakataa wote,
tumia kichwa kufikiri japo kidogo
 
Hi JF,

Kibanda katoa opinion yake na waungwana husikiliza na kuheshaimu wazo la mtu. Nadhani ametoa angalizo ambalo siyo sahihi kulibeza. Napendekeza lifanyiwe mkakati angalizo hilo, ili asije kujisifu kama afanyavyo sasa kuwa 'nalisema na angalia yametokea.' Ushauri wangu, makamanda CDM wamwandame Kinana, ili kila anapotoa mguu makamanda wafike mara na kusafisha uongo kwa kutoa ukweli kwa wananchi. TUTAFAKALI.
 
Maranya mbona unanihukumu kihivyo bila kunipa nafasi ya kunifahamu,sikia mimi siko huko uliko,mimi ni mwanaharakati na ndiyo maana nimekuwa nakuunga mkono kwenye coment zako nyingi,na vivbyo hivyo nitamuunga mkono mwingine yeyote yule ambaye nitaona anazungumzia utaifa ama hoja,na niko tayari kuchafuana na wewe vyovyote utakavyo kama nitaona unamshambulia mtu pasipo na hoja ya msingi,maranya umekuwaje wewe?,acha ujinga mkuu naona sasa tuanze kupeana za uso ila niwaombe Mods wawe makini kwa sababu kuna watu humu hawachelewi kuwaban wakipitiliza ila wengine wanachiwa tu wanatirirka watakavyo,wewe kama ni CDM endela ila siku likinuka uatafute pa kwenda sisi wanaharakati tuko KILA KONA YEYOTE YULE TUKO NAE MAADAM AMESIMAMIA UKWELI,Peleka ushbiki wako huko we unadhani kila anayepingana na wewe ni CCM,nyooooooo!

Kwanza nikuambie kwamba haimhitaji mtu kuwa mwanaharakati kujua kwamba ccm wanaweza kuendelea kuitawala nchi hii (maana kuongoza wameshindwa) kwa kuvitumia vyombo vyya dola tu. Sasa inapofika mahali unataka kupingana na mwenyekiti wa ccm aliyesema hadaharani kwamba sasa wanaccm waache kuwategemea polisi katika kukabiliana na hoja za Chadema nakuona kama si mwanaharakati kama unavyojipambanua. Na kama ni mwanaharakati basi ni wale wanaharakati njaa wanaoitwa GONGO (Governmental Non Governmental Organizations).


Pili nikuambie kwamba mimi sijawahi kuogopa vitisho, tena toka kwa mtu nisiyemfahamu, mojawapo ya vitu nilivyofundishwa nilipokuwa jandoni ni kutomuogopa mtu yeyote, hata awe mkubwa kama meli ya kinana. Kwahiyo mkuu usipoteze muda kujaribu kutoa vitisho, kama unajiamini una nguvu na uwezo wa kupambana nami we twende kazi.

Tatu nikwambie kwamba mwanaharakati makini hawezi kupoteza muda kuzungumzia masuala ya mahusiano ya kingono ya mtu yeyote awe kiongozi ama mwananchi wa kawaida. Nani asiyekuwa na mahusiano ya kingono? na hayo mahusiano ya kingono ya kiongozi wa chama ama serikali yanatusaidia nini sisi ama kutuathiri nini sisi kama Taifa? mbona watu mnakubali kupoteza uwezo wenu wa kufikiri kwa sababu ya chuki za kirejareja mnazopandikizwa na hao wanaowatuma na ninyi bila kufikiria mnaanza kuropoka tu? Kama unataka tuendelee kuwa na mijadala yenye staha ni lazima ujitanabahishe kwa kuandika vitu vyenye staha kwa wengine, vinginevyo ukubali kukutana na majibu usiyoyatarajia ama kuyapenda.
 
Back
Top Bottom