Kesi ya Thadey Kweka: Utawala wa sheria, hauruhusu vyombo vya uchunguzi na mahakama, kuvunja haki za kikatiba na sheria, katika utoaji hukumu zake

Rudi darasani kidogo uongeze ufahamu
 
Ukisoma pleading zao hakuna maombi ya Exparte and for that sake it was inter-Parte iliyofantika Exparte ili kutimiza nia ovu ya wanaoshitaki
 
Tunasafari Ngumu ya Kujifunga Mkanda Kupata Katiba Mpya itayoweka misingi ya Uhuru wa Mhimili wa Mahakama. Unapoona Mahakama inashirikiana na Wakamataji na Washitaki kwa kupuuza haki za binadamu ni hatari sana
It's true, tuna safari ndefu, ila kwa vile kumetokea fursa ya katiba mpya, twende na upepo huo kuboresha haki
, wajibu na uwajibikaji.

P
 
Tatizo zaidi viongozi wa kitaifa hawaoni najisi waliyoifanya.

Saa zingine kuna mambo unayaachia fate.
Kuachia 'fate', hilo ndilo tumaini zima wanalolisubiri hawa watawala waovu kabisa!

Hakuna 'fate' isiyokuwa 'influenced' na utashi wa watu. Fate ya hawa waovu itapatikana kupitia kwenye juhudi za waTanzania wasiokubali upuuzi huu.
 
Uko sahihi.
Polisi kiutendaji ni kama vile wako juu ya sheria.
Ukiangalia hata taarifa ambazo ilistahili zitolewe na waziri wa mambo ya ndani zinatolewa na polisi.
Kwa sababu huyu waziri hapo ni pambo tu; wahusika hasa wanaoendesha jeshi hilo ni wengine.
 
Rudi darasani kidogo uongeze ufahamu
Kwa bahati nzuri ninao ufahamu mzuri sana, mkuu 'Emekha Ikhe'; kwa hiyo ushauri wako huu unaonyesha bado huelewi nilichokieleza kwako.
Ukitulia na kutofakari vizuri ushauri niliokupa, utaona ukweli ulipo.

Haikuwa maana yangu ya kudharau ulichowasilisha; maana yangu ni kukustua uone upungufu katika uwasilishaji wako, jambo ambalo najuwa unaweza kulimudu.
 
UPDATE 6: Kesi ya Thadei Kweka

January 1, 2026

1. Mawakili wa Thadei wame—file Habeas corpus ili afikishwe mahakamani haraka. Matarajio Jumatatu kesi itasikilizwa

2. ⁠Pia, Mawakili wame—file revision (marejeo) ya maamuzi kumtaka Thadei atoe password ya simu yake kwani kuna suala la kukiuka haki ya kimsingi ya privacy.

3. Bado Thadei ameshindwa kutoa password kwa sababu haikumbuki baada ya kupitia unyanyasaji wa kisaikolojia tokea akamatwe. Zoezi la kutoa password limeshindikana hadi hapo Thadei akikumbuka password yake.

5. Polis bado wamemkatalia Thadei dhamana.

6. Leo Thadei amesaini form kutoka Ubalozi wa Marekani baada ya pressure kubwa kutoka Ubalozi wa Marekani.

7. Thadei anashtakiwa kuchapisha taarifa za uongo kwenye groups za ”what sup”. What sup hatujui ni Application gani haya Thadei mwenyewe haelewi!

8. ⁠Thadei yupo kwenye spirit nzuri na anawashukuru diaspora kwa kusimama naye na anatambua hii sijui vita dhidi yake, bali ni vita dhidi ya diaspora wote.

Tutaendelea kuwapa taarifa.

#FreeThadeiKweka

Asante
 
Waja hawana wema wanadai video ya hotuba ni AI generated inawezekana hata mukulu hakuongea kabisa
 
Kwa hiyo umekuwa ni hakimu
 
#UPDATE_ISSUE_THADEI_KWEKA

Anaandika Liberatus Mwang'ombe

January 3, 2026

1. Mwanzoni December 28, 2025 alipo kamatwa aliambiwa ana kesi ya kuingia nchini sio kihalali.

2. Jumatatu, December 29, 2025, Thadei alichukuliwa hadi uwanja wa ndege KIA kwa escort ya polis. Record za airport zikaonyesha Thadei aliingia kihalali December 20, 2025

3. Thadei alitolewa Boma Ng’ombe akiwa na tuhuma za kuingia bila kibali. Akahamishiwa Central Polis Moshi mjini na kuambiwa anatuhuma za kuchapisha habari za uongo “What sup”

4. Muda wote huu hakukuwa na proper charges.

5. Leo, Jumamosi, January 3, 2025 Thadei amepewa dhamana baada ya siku 7 kuwa ndani.

6. Jumatatu, kesho kutwa, kesi ya marejeo ya hukumu ya upande mmoja ili Thadei atoe Password inatarajia kusikilizwa. Pia, kesi ya dhamana.

7. Thadei hadi sasa ameshindwa kufungua simu yake kwa sababu haikumbuki password baada ya stress zilizosabaishwa na kukamatwa bila utaratibu. Simu yake bado ipo polis.

8. Thadei yupo kwenye spirit nzuri na anawashukuru diaspora kwa kusimama naye na anatambua hii siyo vita dhidi yake, bali ni vita dhidi ya diaspora wote.

#FreeThadeiKweka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…