Kero ya kuripoti kazini baada ya kupangiwa ajira na sekretarieti ya ajira, halafu unaambiwa urudi nyumbani mpaka upigiwe simu kuitwa!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Feb 17, 2015
13,664
18,039
Inawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine!

Hii inamfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!!

Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!!

Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko Tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya Tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar.

Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watu na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!!

Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa!

Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!
 
Huwezi kuamini!! Vijana wanapambana sana na kujipa moyo kuwa kwa kuwa ni wanaume acha wapambane!! Kwa wale vijana wa kike wengine wao hujikuta wamelazimika kujirahisisha ili kupata ufadhili wa malazi na chakula wakati wanangoja hizo simu za miungu watu!! Wale wakiume wengine hushindia mkate wa buku na maji ya viroba na kulala popote hata kwenye stendi ya bus!! Ni mbaya sana na sijui kama huu utaratibu una baraka zote za serikali!! Wanaoga kwenye vibanda vya vyoo za kulipia!
Wewe fikiria kwa mfano yule aliyekuwa anabangaiza Dar na kisha kupata ajira Tabora!! anakopa nauli kwa ahadi kuwa akipata posho ya kujikimu atarudisha bpesa za watu!! Halafu anaripoti tabora na kuambiwa asubiri hadi apigiwe simu!! Nauli ya kurudi hana!! Hizo pesa kidogo alizobakiza anaona ni afadhali azitumie kwa kula chochote ili mradi aendelee kuwa hai na hajali analala wapi!! sawa wanavumilia hasa kwa kuwa wanajua mateso yanaelekea mwisho. Lakini je ni lazima watendewe hivyo? Haiwezekani kuwa na utaratibu ulio rafiki?
 
Bora umepata I'll nakutonya fanya Mara kwa .Mara kutembelea ofc kila baada ya siku tatu ,

Kuna kijan alilamika hapa ajira yake kupewa mtu mwingine Kisha yey akambiwa arudi nyumbano hvyo Ni vyema San uwe makini daile fika na unana na hr kuwa mm Niko najitoleaaa na kuzoea mazingiraaa
 
Inawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine! Hii inmfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!! Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!! Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar. Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watun na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!! Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa! Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!
Hii ni mpya sijawahi hata kuifikiria achilia mbali kuisikia. Sasa kwanini walitangaza nafasi km walikuwa hawamhitaji? mimi navyojua kuripoti ni kuanza kazi. Unajaza form na hapo hapo unaomba pesa za kujikimu ambayo inatakiwa upewe ndani ya wiki moja.

Ila sishangai halmashauri kuna miungu watu hasa maafisa rasilimali watu, ni wanyanyasaji sana. Huwezijua pengine kuna mazingira wanajenga.
 
Inawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine! Hii inmfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!! Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!! Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar. Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watun na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!! Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa! Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!
Nawaza natoka dar mpaka kigoma alafu ndio unanieleza huo upuuzi mbona kitawaka!!
 
Kukiwa hakuna ajira kelele mkipata kelele. Mama kanyaga twende
Haiwezekani kukubaliana na uonevu eti kwa kuwa tu umepata ajira!! huu ni utumishi ni utumishi wa umma na haikubaliki watu kujifanyia utaratibu unaonyanyasa na kutesa watu!! Mtu aliitwa kwa vitisho kuwa ukichelewa nafasi yako atapewa mwingine! lakini alivyoripoti bado anazungushwa, hilo halikubaliki!
 
Huwezi kuamini!! Vijana wanapambana sana na kujipa moyo kuwa kwa kuwa ni wanaume acha wapambane!! Kwa wale vijana wa kike wengine wao hujikuta wamelazimika kujirahisisha ili kupata ufadhili wa malazi na chakula wakati wanangoja hizo simu za miungu watu!! Wale wakiume wengine hushindia mkate wa buku na maji ya viroba na kulala popote hata kwenye stendi ya bus!! Ni mbaya sana na sijui kama huu utaratibu una baraka zote za serikali!! Wanaoga kwenye vibanda vya vyoo za kulipia!
Wewe fikiria kwa mfano yule aliyekuwa anabangaiza Dar na kisha kupata ajira Tabora!! anakopa nauli kwa ahadi kuwa akipata posho ya kujikimu atarudisha bpesa za watu!! Halafu anaripoti tabora na kuambiwa asubiri hadi apigiwe simu!! Nauli ya kurudi hana!! Hizo pesa kidogo alizobakiza anaona ni afadhali azitumie kwa kula chochote ili mradi aendelee kuwa hai na hajali analala wapi!! sawa wanavumilia hasa kwa kuwa wanajua mateso yanaelekea mwisho. Lakini je ni lazima watendewe hivyo? Haiwezekani kuwa na utaratibu ulio rafiki?
Wabunge wetu kazi yao ni nini, si juzi tu walipitisha bajeti ya wizara ya utumishi na utawala bora? na vilevile bajeti ya TAMISEMI? Wanataka kutuambia hawajui hayo madhila? Maana ndiyo sehemu tungepata majibu ya serikali directly.
 
Hii ni mpya sijawahi hata kuifikiria achilia mbali kuisikia. Sasa kwanini walitangaza nafasi km walikuwa hawamhitaji? mimi navyojua kuripoti ni kuanza kazi. Unajaza form na hapo hapo unaomba pesa za kujikimu ambayo inatakiwa upewe ndani ya wiki moja.

Ila sishangai halmashauri kuna miungu watu hasa maafisa rasilimali watu, ni wanyanyasaji sana. Huwezijua pengine kuna mazingira wanajenga.
Sema tu ni kwa kuwa vijana wenyewe wameteseka sana kwa kuhudhururia usaili mara nyingi kwa gharama zao!! Wameteseka sana kiasi cha kuyaona mateso kama ni sehemu halali ya maisha yao, hata hawawezi kulalamika!! Lakini watanzania wapenda haki lazima tupige makelele kwa ajili yao!!
 
Nawaza natoka dar mpaka kigoma alafu ndio unanieleza huo upuuzi mbona kitawaka!!
nilikuwa nawaza km wewe ili jamii ijue, ni bora ulazwe kituo cha polisi baada ya kukataa kutoka ofisini mwao mpaka wanieleze pakulala na chakula. Muwe mnaenda na hawa waandishi wa online TV waturushie video ya huo mtanange. Tuache unyonge uliopitiliza ndugu zangu.
 
Inawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine! Hii inmfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!! Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!! Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar. Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watun na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!! Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa! Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!
umegusa ishu sensitive sana kwa vijana wa taifa hili ,kifupi jobless hasaminiwi . afadhali yake huyo ambaye kaambiwa atapigiwa simu hata tumaini analo kuwa yuko mzigoni tayari
 
Inawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine! Hii inmfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!! Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!! Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar. Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watun na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!! Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa! Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!
Naomba nijibu kama ifuatavyo....unakuwa bado hujaingizwa kwenye mfumo, na mpaka uingizwe kwenye mfumo anaweza kuchukua mwezi au ndani ya miezi miwili ili upate mshahara wako, ili upate mshahara wako inabidi utumishi wa approve taarifa zako, kwa kuzikagua kiundani ili tusipate udanganyifu......kwa kuwa hakuna bajeti Yako ya kujikimu kwa mda ule,ndio maana tunakwambia kuwa kakae kwanza nyumbani mpaka tukupigie simu....jamani sio kwa ubaya,maana hakuna wa kukulisha hapa mjini.....kama hamuamini kawaulize walimu wanavyopata ajira,wanakaa zaidi ya mwezi ndio wanaingiziwa mshahara wao..muda wote huwa wanahudumiw na wakuu wa shule mpaka wanapopata mishahara Yao kwa mara ya kwanza.....alisikika HR mmoja wa michango.
 
Back
Top Bottom