KERO: Bole International Airport - Addis Ababa

KERO: Bole International Airport - Addis Ababa

Mkuu joshua_ok hongera kwa safari za majuu ILA niseme tu pale addis Ababa na hata Nairobi na kigali unaposafiri fanya Timing vizuri ILI usikae ON-TRANSIT kwa muda mrefu sana. Mfano kama unasafiri ondoka Dar kwa ndege ya Alfajiri Unless safari yako toka ddis Ababa , Nairobi au kigali kwenda "Ulimwenguni" inaanzia huko usiku wa Manane.

Mkuu joshua_ok kuhusu Addis ababa kuwa na watu wengi kama "Kariakoo" hilo ningetamani kama ungeongelea na upande wa pili wa hiyo Scenario. Watu wengi pale Addis Ababa maana yake hilo shirika lina connection nyingi sana kwa nchi za Afrika hivyo basi hao unaowaona wapo ON TRASIT. Mimi natamani siku moja kuiona hiyo hali ya wingi wa watu hapo Addis Ababa hapa kwenye uwanja wetu wa ndege wa JK Nyerere au pale. KIA.


Ahsante

Labda kama gharama, lakini kuna best airlines wanakuja Dar almost kila siku ambao wana facilities bora zaidi kama unaenda nje ya Africa. Emirates, Qatar, KLM. Achana na hao wengine
 
Wale wasafiri wenzangu tunatumiaga "SAI-BABA" ETHIOPIAN katika mihangaiko ya maisha huko duniani mtakubaliana na mimi jinsi pale Airport kunavyoboa kama una "Long Layover" yaani kumejaa kama kariakoo, restaurant bei za ajabu ajabu, cancellation kama kawa, vyoo vichafu, bora kukwea FLY DUBAI au kupitia KIGALI ama NAIROBI ukakwee CHINA SOUTHERN AIRLINES.

NB: Wizara - Mambo ya Nje tafadhali ongeeni na CHINA SOUTHERN AIRLINES waje mpaka DAR angalau.
Kumbe ulikuwa unajiita joshua
 
Very true hakuna cha uhaya wala nini Ethiopian Airline ni madaladala yaliyochangamka kama una akili sawasawa chagua Emirates ,Qatar etc hizo za wahabeshi ni takataka tu
 
Kweli mkuu, pale pako ajabu ajabu sijui kwa nini? Ila ndo hivyo bei zao ni cheap ila huduma ni zero…Bora hata Kenya airways ina afadhali hao wahabeshi noma
 
Wale wasafiri wenzangu tunatumiaga "SAI-BABA" ETHIOPIAN katika mihangaiko ya maisha huko duniani mtakubaliana na mimi jinsi pale Airport kunavyoboa kama una "Long Layover" yaani kumejaa kama kariakoo, restaurant bei za ajabu ajabu, cancellation kama kawa, vyoo vichafu, bora kukwea FLY DUBAI au kupitia KIGALI ama NAIROBI ukakwee CHINA SOUTHERN AIRLINES.

NB: Wizara - Mambo ya Nje tafadhali ongeeni na CHINA SOUTHERN AIRLINES waje mpaka DAR angalau.
Wachafu Kweli wale jamaa

Ukila pale lazima uwashe vespa

But they have a successful airline
 
Hata dubai international airport DXB ile reception yao sijaipenda ukifika wanakupotezea mda sana inabidi waiangalie vizuri
Jf kila mtu ana hela na kazi ila likitoka tangazo la kazi watu wanaruka nalo hyo ndo jf.
 
Bole international airport wameboresha Kwa kiasi huduma za maliwato. Japo Bei restaurants za pale airports kizunguzungu*
 
Mkuu acha hizo bana, wanyarwanda wasafi sana, hebu nipe utofauti wa usafi wa wanyarwanda na watz? Acha kudhalilisha nchi za watu.. Kwa usafi gani haswa unataka kusema watanzania wamezidi wanyarwanda?? Anzia kulinganisha dar na kigali kwanza.!
Na hapa tunaongelea Bole airport, Ethiopia sio Rwanda eboo.!
Wanyarwanda wanatumia tissue kujisafisha sehemu za Siri Watanzania wanatumia maji.Nani kati yao atakuwa msafi.
 
Back
Top Bottom