KERO: Bole International Airport - Addis Ababa

KERO: Bole International Airport - Addis Ababa

Aisee india nimewakubali zaidi na Airport zao pia na Malls zao za ukweli, Nilifika pale DELHI Airport FULL A/C mpaka chooni/ hakuna kelele wala nini na pametulia hakunaga vurugu kama BOLE sema inabidi uwahi uwanjani mapema maana, wadosi wanasafiri sana so foleni kubwa immigration.usipokuwa makini ndege inaondoka ukiwa kwenye foleni za immigration maana hakunaga maspika mule (ni kimya kimya) Ila dada zetu waafrika (Watanzania pia wamo wanauza nyappu mnoo Huko India mpaka aibu).

** Hiyo ndege ya ADD-DELHI ni tule tudogo tudogo sit kama school bus yaani sisi warefu kukaa masaa 6 kwenye zile siti ni mateso ajabu.
 
ATC hii ya marubani wetu hawa wazee? tuombe mola atupatie hikma na busara katika kuendesha shirika hili pendwa.
** Tubadilishe jina....KILIMANJARO AIRLINES
 
Nilipita pale April nikaunganisha ndege ya Entebbe, du! Kweli vyoo vichafu. Halafu uwanja wao ni mkubwa ila sio mzuri
 
tmp-cam--184807990.jpg

Dream Liner 787...Ethiopian hao
 
ethiopian ni watu wa ajabu kuanzia kwenye ndege kwenyewe, yaani vile vidada vichoyo balaa vinakupa chakula kiduchuu, hakuna kinywaji cha maana zaidi ya maji, maza fanta na cocacola abiria wa safari ndefu ukifika basi pale uwanjani kwao DUTY FREE shops zao wametandaza ile mitandio tu ya ki-ethiopia tu, sisi tunataka pombe tupotezee muda safarini mnatuuzia mitandio, ya nn sisi?
NB: WIFI mpaka kununua 10 USD dakika 30 tu. ***** wallahi!!

Aaaahaaaa niliacha kupanda Ethiopian airline mwaka2009 Iyo siku nilikutana Na kinyesi live chooni makoozi kwenye sink nikasema shida yote ya Nini khaa nikasema sipandi tena hili kopo kweli cheap is expensive aaaahaaaaaaa nimekimbilia Qatar
 
Cheap is expensive, hata bure sipandi EA
Nyinyi Watanzania Wenzangu mnaanzaje kuponda shirika lenye Flight 56 na dreamliner 6 wakati sisi tuna Ndege moja? Tanzania hapa mnatumia usafiri gani au magari gani mna drive Bongo mbona sioni magari ya hizo hadhi mnazozizungumzia wote iweje muiponde ET huku sisi choka mbaya kwa usafiri wa Anga...
 
Back
Top Bottom