Kasoro kubwa katika video ya Lwakatare

Kasoro kubwa katika video ya Lwakatare

Wana mapinduzi wanaamini kuwa ukiona mambo kama haya tambua kuwa ukombozi upo karibu. Uhuru na Ruto walifanya kama haya na sasa wameingia ikulu, aibu kwa ICC na mafia wao. Nadhani ni muda wa kushangilia ushindi na mapinduzi ya kweli, watanzania wenye akili, na hasa hawa wanaotumia mitandao ya kijamii na forum makini kama JF watatumia akili zao kuchambua hili. Maana mengi yamesemwa kuhusu CHADEMA yameshindwa....walianza na ukanda ukashindwa, wakaja na dini wakashindwa, wakaja na kadi ya dokta Slaa wakashindwa, sasa wemeibuka na mauaji...hakika MUNGU ni yule yule jana, leo na hata milele, ataendelea kutupigania wana CHADEMA.

Tualianza na MUNGU, tunaendelea na MUNGU, tutamaliza na MUNGU
Ikiwa MUNGU, yupo upande wetu, nani atanyanyuka kinyume chetu?
naamini nakuapia wakitukosa hapa mwisho wao utakuwa umerejea rasmi maana hakuna watakachokisema watu wakawaelewa,watu watahoji hata ujinsia wao maana wamekuwa kama sio riziki wote
 
wa Tz kwa kutafuta vichaka, msitumie clip ya obama kujifichia humo
 
Mkuu wangu Patriote,
Waingereza wana msemo wao kwamba "A BLACK CAT MAY BE A BAD LUCKY ONLY IF YOU ARE MOUSE!" Chambilecho wewe sio panya, yanini kuingiwa taharuki pindi umwonapo paka?! Naona wapwa mmekazana sana kulikanusha hili jambo....pamoja na post kadhaa za kukanusha, bado hivi sasa kuna new threads za kukanusha...!! Hofu ya nini? I believe Lwakatare is smart enough ku-prove beyond reasonable doubt kwamba ile video is just a fabricated material; sasa nyie hofu yenu nini mkuu wangu Patriote? Mnatutia mashaka sie wengine; a black cat may be a bad luck only if you're mouse! Wewe majani, hofu yako nini kuingizwa kwenye banda la mbwa wakati unafahamu mbwa hali majani?! Unakumbuka pale Uhuru Kenyatta alipojipeleka mwenyewe ICC? Kenyatta alifahamu he's not a mouse so he'd no reason to get scared of a balck cat ICC!! Wewe kama ni majani, pigana kufa na kupona, ikibidi kanusha kwa nguvu zote kwamba wewe si majani ikiwa umegundua unataka kupelekwa zizi la mbuzi, lakini kwenye banda la mbwa; aaaargh, hofu ya nini!!!

mkuu unakumbuka Mwigulu bungeni kuwa ameletewa sms na wabunge wa chadema kuwa ametishiwa kuuawa?Spika na mwanasheria mkuu wakalivalia njuga,kama si watetezi na wapenda haki kuelezea kuna teknolojia ambayo baadhi ya makada wa ccm wanayo inayoweza kuingilia mfumo wa mawasiliano ya simu,wote hata mwanasheria mkuu aliyeagiza vyombo vya dola vishughulikie akawa bubu.
Coincidental toka mwaka jana the same person Mwigulu akadai ana video inayoonyesha viongozi wa chadema wakipanga mauaji,leo miezi takriban 5 tunaletewa video inayoonyesha kiongozi wa chadema akipanga mauaji.
Kwa nini uwadiscredit wanaoonyesha mapungufu ya hii serious allegation?na ni kwa maslahi ya nani unafanya haya.
Angalia sakata la Ulimboka tumeonyeshwa mkenya na waliofanya investigative journalism mwanahalisi wamefungiwa lkn mkuu wa nchi Ethiopia amediriki kudanganya sababu za kulifungia.
Tunaona juhudi za kudhoofisha upinzani bungeni kwa kutumia kamati batili,kama wewe ni mzalendo huwezi kushabikia na kutaka wapenda haki kutotetea upuuzi unaofanywa na watawala.
Bunge haliaminiki,ikulu haiaminiki,polisi nayo pia.Tuachieni waliamua kutupa ukweli hatutegemei kupata kwa Kova.
 
hatari sana,i am glad kwakatare is not a Muslim
tungeskia mengi sana katika hilo,
wala hatuskii akinyooshewa kidole kutokana na iman yake hapo..!
Kama kina shekhe ilunga,ila tutafika tuh
Upo sahihi DULLAH MSAVIVOR,
Stori nzima ingebadilika na kuwa si issue ya kisiasa tena bali ya kidini...!!!
 
Last edited by a moderator:
Alichoongea/kupanga Lwakatare sicho kilichomtokea Kibanda. Hakuna uhusiano wowote.
 
Kwa namna hii naona bado sana, wanakazi kubwa sana hiki si kizazi cha kuoneshwa filamu la Rwanda ili usichague wapinzani.
 
Hakuna suala la kutetea mkuu CANCER09,
Issue ni kwamba, if your conscious is clear, yanini kuweweseka?! I am certain Lwakatare can prove kwamba the whole thing is fabricated kama kweli ni fabricated!!! My concern ni zile nguvu kubwa mnazotumia kukanusha wakati none of you has evidence that can prove otherwise....you all rely on assumptions kwamba ni fabricated material na kutumia other fabricated materials to prove your arguments!! You all come with online tutorials on how to fabricate videos and example of those of fabricated videos but none amekuja kutoa technical proof kwamba the Lwakatare video is just fabricated material.Is like mtu ametumia risasi ya mpira, kisha aliyepigwa akafa....anakuja mwingine anasema, no; a rubber bullet can never kill na ili ku-prove madai yake, anakuja na lists of people who were previously shot with rubber bullets but didn't die badala ya ku-prove medically kwamba the died guy si kwa sababu ya rubber bullet aliyopigwa!
 
Last edited by a moderator:
Baada ya single ya shoza na mwambapa kubuma mmekuja na mpya ..,,..,.sikio la kufa alisikii dawa ehe poleni mwigulu+nape+ridhiwani
 
Wana mapinduzi wanaamini kuwa ukiona mambo kama haya tambua kuwa ukombozi upo karibu. Uhuru na Ruto walifanya kama haya na sasa wameingia ikulu, aibu kwa ICC na mafia wao. Nadhani ni muda wa kushangilia ushindi na mapinduzi ya kweli, watanzania wenye akili, na hasa hawa wanaotumia mitandao ya kijamii na forum makini kama JF watatumia akili zao kuchambua hili. Maana mengi yamesemwa kuhusu CHADEMA yameshindwa....walianza na ukanda ukashindwa, wakaja na dini wakashindwa, wakaja na kadi ya dokta Slaa wakashindwa, sasa wemeibuka na mauaji...hakika MUNGU ni yule yule jana, leo na hata milele, ataendelea kutupigania wana CHADEMA.

Tualianza na MUNGU, tunaendelea na MUNGU, tutamaliza na MUNGU
Ikiwa MUNGU, yupo upande wetu, nani atanyanyuka kinyume chetu?

Ameeeeeeeeeeeeeeen mkuu! hakuna wa kushindana na Mungu! waache watapetape sisi akina Daudi 2015 Kabaang! kwenye paji la CCM! kwisha habari yake hapo ndipo watakapoamini hawawezi kushindana na MUngu! waache watengeneze video kibao badala ya kuangalia changamoto kibao zinazokabili nchi na kuangalia njia ya kuzitatua! Mungu yu upande wa CDM kwa sababu ni wapigania haki! hakika Mungu atawaumbua sasa hivi! wanafanya mchezo hawajui hii nchi kila nukta ipo madhabahuni!!!
 
Sio kulikanusha, ila kuelimisha watu waelewe. Hauwezi kukaa kimya wakati unaona watu wanapotosha kwa maslahi ya taifa. Elewa hii ni mikakati ya kishenzi ya kisiasa.
Mkuu wangu Bill,
Mtu pekee mwenye uwezo wa kulikanusha kwa sasa, ni Lwakatare mwenyewe! Inakuwaje mtu mwingine akanushe suala linaloonekana kufanywa na Lwakatare wakati mtu huyo hatembei na Lwakatare?! Mkuu wangu wewe unafahamu hivi sasa Lwakatare anafanya nini na yupo wapi?! By the way, hakuna anayebisha kwamba hamna video manipulation technology, lakini uwepo wa teknolojia hiyo kusitufanye kuzikataa video zote zilizo na side effect kwetu wakati hakuna uchunguzi wowote ambao ume-prove otherwise!! What you all do hapa ni ku-paste online tutorials on how to fabricate videos.....hiyo peke yake haiwezi kuwa ushahidi tosha kwamba Lwakatare's video is also ni fabricated!
 
Last edited by a moderator:
polisi wetu wako shalow sana inaonekana hata mimi nikigombana na mtu akiweza kuingia studio akaandaa movie nimekwisha, tena wala hawamhitaji huyo aliyeipost you tube, wao wanaichukua kama ilivyo wanakupandia huko uliko.

inanipa wakati mgumu kuelewa, yani ushahidi kama wa dr Uli kuwataja baadhi ya wahusika wa sakata lake,
Kabanda naye kuwaanika baadhi ya vigogo, ushahidi huo wa maneno na mtu anayeutoa ukiwa unamwona physically unaupuuzia unadeal na ushahidi wa you tube, vid shop.?????

najua ni upeo wa geshi letu la polisi ulipofikia, na naamini hawajui kama kuna video shopn, baada ya muda kidogo ndo watabaini kumbe tulikurupuka kumkamata Lwaka.

Inamana hawa wangekua marekani wangeshampelekea Bush ile colabo yake na Blair, na Obama ile clip yake ya siku anakula kiapo kuwa U.S President

naamini polisi wetu wakiona ile movie ya Idd Amini wataamini hawajui imetengenezwa
 
Ukiwa mnafiki uwe na kumbukumbu, na wewe umetumia teknolojia gani kumlisha maneno Riz wan na Nape kuwa wamesema Chadema wanahusika, Wengi wetu tulipitia Wall paper ya Ridh na Nape hakuna neno Chadema walipotaja, Alama za Mtu mnafiki ni 3 na moja wapo ni Uongo.Lwakatare kesha nasa kwenye mtego hateguliwi kwa manati mtazid kumuumiza! Yeye ndo atathibitisha sio kukimbilia kwenye Google Engine kutafuta namna ya kumtoa!

Mkuu!

Hakuna kitu pale! Licha ya upoliccm kudandia hoja bila kutumia weledi wa kazi yao, ngoma itatoka kapa. Ni kuzidi kujiabisha tu. Wameacha kumkamata Mwigulu aliyesema anayo video hiyo, wanakamata mtu ambaye kimetumika kivuli fake kutengeneza ujinga wa namna hiyo!!!
 
Upo sahihi DULLAH MSAVIVOR,
Stori nzima ingebadilika na kuwa si issue ya kisiasa tena bali ya kidini...!!!

tatizo la kutojiamini hiyo ni inferiority complex jadilini issue at hand.
Au mnatafuta sympathy ya upuuzi wa akina Ilunga?
 
Last edited by a moderator:
Nadhani wenye maamuzi ya mwisho ni polisi, pamoja na kwamba mtuhumiwa ametokea upinzani, nitawaomba polisi wetu wasitumie upinzani kama kigezo cha kumhukumu mtuhumiwa. Lwakatare apewe haki yake kama Lwakatare na kama raia mwingine yeyote wa nchi hii.. Nadhani aliyeweka hii video alikuwa na mawazo hasi na upinzani ndiyo maana anawauliza wa "CHADEMA, hapa Lwakatare anamaanisha nini?.. Kwa uelewa wangu huyu mtu hana dhamira njama kwa Nchi yetu ya Tanzania, anaweza kuwa mtu hatari sana katika mipango na mikakati yote ilyokwisha ripotiwa ya mauaji, utekaji na uumizwaji wa raia, waandishi na wanaharakati mbalimbali hapa Tanzania. Nadhani Polisi wangeanza na huyu mtu angeweza kuwasaidia sana katika utekelezaji na upelelezi wa makosa yanayofanana na haya. Nachoona hapa ni hiki,.

  1. Mweka video alishiriki katika kuiandaa clip hii kikamilifu.
  2. Anatumiwa na watu wasiyoitakia mema Nchi yetu ya Tanzania,
  3. Ana mtandao ambao huratibu uchafu wote unaofanywa na hawa magaidi ndiyo maana anahisisha mambo ya utekaji yanayoendelea hapa nchini na vyama vya upinzani hususani CDM.
  4. Anaweza kuwa ni mtu wa system mwenye dhamana ndiyo maana hakupeleka hii clip sehemu husika kama kituo cha polisi akiogopa atatoa ushirikiano ambao utamfanya ajulikane..
  5. Anaweza akawa anajua ukweli wa mambo mengi sana maovu yanayotokea hapa nchini ya kihalifu na kigaidi, na kama ni mwandishi wa habari, anafaa zaidi katka upelelezi.
Rai yangu njema, nawaaomba polisi wamsake huyu mtu atawasaidia sana katika kubaini njama mbalimbali za uovu zinazoendelea hapa nchini.. Kama ni mtu mwenye nia njema atajitokeza ili awasaidie polisi katika kufahamu mambo yafuatayo.
  1. Hizo video nyingine za mikakati ya mauaji
  2. Sehemu ilitumika katika kurekodia video hizi,
  3. Mtu/taasisi iliyo nyuma yao katika kufadhili mpango huu,
  4. mbinu nyingine chafu ambazo wameshafanikisha na ambazo ziko kwenye pipeline.

Nawasilisha...
naamini taasisi na kila kitu vinajulikana,ila nasikitika hakuna litakalofanyika na kama lwakatare pamoja na cdm wakikomaa vizuri utashangaa yanafukiwa fukiwa mwisho yanaisha.
 
Kitu cha ajabu hata
mkubwa anafurahia propaganda kama hizi za kitoto na za kipuuzi kweli
mabwepande wameishiwa mbinu

kama ni hivi itabidi tuzikubali na zile video clip za kwenye Ze Utamu zilizomwonyesha mkulu akinanihiwa.....
 
Patriote,

Nimekubali. Ni kweli aisee!!! Maneno yanayosikika utadhani yalitamkwa na Obama kabisa kumbe fake. Ile video ya Lwakatare ni fake kabisa!!!

Angekuwa ametepiwa NAPE ungesema Fake? pumba*f mumeshikwa pabaya na mbinu zenu chafu.
 
Back
Top Bottom