<br /><img src="http://www.mombasa-event.com/PICS/FashionLinzy7293.jpg" border="0" alt="" /><br />
<br />
Kanga zina mambo mengi, zina mengi hizo kanga,<br />
Kanga zinaficha vingi, vinavyofichwa na kanga,<br />
Kanga zina siri nyingi, zina siri hizo kanga,<br />
Kanga unapoachiwa, ana penzi mwenye kanga!<br />
<br />
Kanga zinaona mengi, chumbani ziliko kanga,<br />
Kanga zahifadhi vingi, vyasitiriwa na kanga,<br />
Kanga zafunika mengi, visivyoonwa bila kanga,<br />
Kanga unapoachiwa, ana penzi mwenye kanga!<br />
<br />
Kanga zinagusa vingi vinavyoguswa na kanga,<br />
Kanga zapangusa pengi, papanguswapo na kanga,<br />
Kanga zina hisa nyingi, za wadau wenye kanga,<br />
Kanga unapoachiwa, ana penzi mwenye kanga<br />
<br />
Kanga zinaganda vingi, visivyoganduka bila kanga,<br />
Kanga zinashinda nyingi, kweli vitenge si kanga,<br />
Kanga zina rangi nyingi, na misemo kwenye kanga,<br />
Kanga unapoachiwa , ana penzi mwenye kanga. <br />
<br />
Kanga hata kama nyingi, atakupa moja kanga,<br />
Kanga itasema mengi, kubwa ni hilo la kanga,<br />
Kanga yatangaza vingi, hakuna kuzidi kanga, <br />
Kanga unapoachiwa, ana penzi mwenye kanga.<br />
<br />
<br />
UKIMPENDA ITUNZE.<br />
<br />
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji) <br />
(picha kutoka Mombasa Events)
Ahahah...asante ASKOFU!!Lizzy....
Hongera
:A S 41::clap2::A S 41:
Hapa kazi ipo.... Mwanakijiji mambo mashallah naona.
Mzee mwanakijiji, naomba ufafanuzi
majibu nayahitaji, niyafanye maamuzi
ninaomba nikuhoji, nisijefanya ajizi
Kanga unayoisema, ni ndege au ni nguo?
Mimi nawafuga kanga, ni kitoweo kizuri
ukila wa kukaanga, watamu kama asali
watalaamu wa kuunga, hili watalikubali
kanga unayemsema, ni ndege au ni nguo?
Kanga ina raha zake hata kwake mvaaji..
Acha we huko pembeni ulobaki mwangaliaji..
Unaetamani kuona kila saa ikiwa maji..
Hakika kanga jamani...mi naipenda sana!
Yampendeza mnene hata nae mwembamba..
Utashangaa wanaume jinsi inavyowabamba..
Mimacho itawatoka hauwaishi ushamba..
Hakika kanga jamani...mi naipenda sana!
Naifunga kibwebwe shereheni nikienda..
Ikikamata kiuno hakika utaipenda..
Nikiifunga kifuani kesi nimeshaishinda..
Hakika kanga jamani mi naipenda sana!
d! Kumbe kanga inavutia kiasi hiki,mbona sasa wengine wanavaa jeans chumban?
kanizidi urefu
mzima wewe?
jana mwenye tukio aligomea kuruhusu picha kuwekwa nikaamua kuipotezea sredi.
Kanga inaniuwa, kifo cha mende jamani
Kanga yanizuzuwa, hata njia siioni
Kanga iliyovaliwa, mimi huku hamkani
Kanga ilobenuliwa, akh! hivi naitwa nani?
Kanga yanipagawisha, yanikosesha amani
Kanga wakijivalisha , napayukwa hadharani
Kanga yanipa mkesha, akivaa wa pembeni
Kanga inavyonikosha, naweza honga milioni
Kanga ya kifuani , pumzi nusu hupotea
Kanga ya kiunoni, huishia kuzimia
Kanga hizi si utani, asifiwe alovumbua
Kanga akiwa chumbani, burudani yatulia.
By Klorokwini a.k.a kibaka mzoefu
Mi hunioni ehhhhhh?!
Kanga ina raha zake hata kwake mvaaji..
Acha we huko pembeni ulobaki mwangaliaji..
Unaetamani kuona kila saa ikiwa maji..
Hakika kanga jamani...mi naipenda sana!
Yampendeza mnene hata nae mwembamba..
Utashangaa wanaume jinsi inavyowabamba..
Mimacho itawatoka hauwaishi ushamba..
Hakika kanga jamani...mi naipenda sana!
Naifunga kibwebwe shereheni nikienda..
Ikikamata kiuno hakika utaipenda..
Nikiifunga kifuani kesi nimeshaishinda..
Hakika kanga jamani mi naipenda sana!