Kandambilimbili ametutoka RIP

Mwenzetu Kandambilimbili alitutoka tangu 26/12/2010 jumapili na amezikwa jana kwao Bukoba.

Alizaliwa mwaka 1971 hivyo ametutoka akiwa bado kijana. Alikuwa na tatizo la kisukari tangu muda mrefu lakini halikuwa kubwa sana na aliweza kulimudu vema kwa muda wa zaidi ya miaka 10. Wiki iliyopita sukari ilisumbua na kusababisha 'stroke' na akalazwa mikocheni hospital na ndipo umauti ukamkuta.

Poleni wana JF wote kwa kuondokewa na mmoja wetu.

RIP Kandambilimbili ( Real Name: Baruti, formely TAA member of staff).

R.I.P Dear Kandambilimbili.
 
RIP kamanda Kandambilimbili..nenda baba ukapumzike baada ya kumaliza kazi yako ngumu hapa duniani pasipo na chembe ya huruma. Nenda baba ukawasilimie makamanda wote walitutangulia mbele ya haki. Usisahau kuwastua watuombee ili hawa viroboto na kunguni waliotuvamia wasitumalize.. Kawasalimie wote akiwemo Baba yetu (Mwalimu JKN) aliyetuachia watoto feki wanaotunyonya damu.

Kazi ya Mola haina makosa...Tunaamini siku moja tutakutana nawe katika makazi yako ya Milele,

Bwana alitoa...........AMEN!
 

I Salute you broda...IAM SHAKING!



RIP Kamanda Mwesiga Baruti, Pole sana mama Kaila au Mrs Baruti wa Tabata Kimanga (Mwisho wa lami) na wanafamilia wote, Poleni sana wafanyakazi wote wa Tanzania Airports Authority na Mwenyezi Mungu awabariki sana kwa kujitoa kwenu wakati wote wa matatizo haya, Poleni sana wanafunzi wa IFM MBA-IB kwa kuondokewa na mwenzenu akiwa amebakisha mwezi mmoja tu kutunukiwa shahada yake ya MBA-IB.

Poleni sana wana JF kwa kuondokewa na mmoja wa 'great thinkers'.

RIP KANDAMBILIMBILI, RIP MWESIGA BARUTI.
 
Do your best before they do their best...safari hii ni yetu sote, tofauti ni wakati na sababu tu! poleni wafiwa.
 
What a loss in JF family and Kandambilimbili familiy.

May he Rest In Peace and wish comfort to JF family and Baruti family
 
Tangulia Kandambili, hapa jamvini tulikupenda lakini Bwana anakupenda zaidi!
 
I dont know how many days,
of life are mine to spend...
bt I know u r now resting in |His hands!!!!
R.I.P bro...!
 
hizi fake names za jf sio nzuri. Sikujua kandambilimbili ni mtu namfahamu. Tuliwahi kutofautiana kidogo hapa jamvini. May ur soul rest in peace. Very sad news.
 
Back
Top Bottom