Basi hata benki zingefungiwa kwa kutoa siri ya viroba vya sandarusi na vijisenti vya mboga,kama kukataa kataa mwenyewe na siri gani hizo,kama unataka kuisaliti serikali utadukuliwa hata isipokuwa Voda,mara nyingi muovu huogopa hata kivuli,pia kudukuliwa mawasiliano si lazima yadukuliwe kutoka Vodacom tu hata kwenye kompyuta watu hudukuwa hao ndio hackers,kuwalaumu Vodacom ni kuwaonea
Tusishabikie uovu .
Usilinganishe tishio la usalama wa nchi na tishio la vyeo vya makabila ya watu na marafiki za watu.
Watu wakijipanga kumtoa madarakani MTU kwa mtutu wa Bunduki hao ni wahaini na wanatakiwa wakamatwe na kushitakowa mahakamani au kukaa kizuizini lakini watu wakipeana taarifa za kutumia Demokrasia kumkataa mtu( na serikali yake ya watu wachache waliojawa na roho za za ubinafsi ,Chuki ,uroho wa madaraka ,uuaji na ukabila) na kumnyima kura wakati wa uchaguzi ukifika hawawezi kamwe kuwa Maadui wa Nchi.
Maadui wa nchi ni hao wanaotumia mitandao kuwatafuta watu ,kuteka,kutesa na kuua watu.
Kwa nini hawakutumia mitandao kujua waliompiga Lisu Risasi ili haki ya kiusalama itendeke kwa wote,? Kwa nini hiyo mitandao haikutumika kujua waliomteka Ben,Azori na wengine wengi?
Kwa nini vyeo vya watu waovu vimegeuka kuwa ndio usalama wa nchi?
Hivi ni nani mwema kiasi cha kujitwika Jukumu la kutoa hukumu bila kumpeleka mtu mahakamani?
Hivi huoni kuwa huu mtindo wa kuwaua na kuwapoteza watu utafikia siku pa kulipizana visasi kwa jino kwa jino wakati ambapo hata mitandao itakua haitumiki tena mana hata hiyo mitandao yao watu hawata itumia tena.?
Hivi wanavyopigana wakulima na wafugaji ni kwa sababu ya usalama wa nchi au wanatetea Mali zao na maisha yao?
Kwa nini hatujifunzi kwa Watu wenye maarifa kama wazungu kuwa ,ulinzi ni jukumu la kila mtu kuwa na amani na uhuru. Ukiwa na amani huwezi kuwaza kumuua mwenzako.
Wasio na amani siku zote ni wale waroho na wabinafsi wenye vyeo. Hofu yao kubwa ni kukosa madarakani na kuona wenzao wanapata na wanadhani kuwa wenzao watakula na kujilimbikizia Mali kama wao walivyofanya.
Angalia wote wanaotumika kuhujumu Demokrasia ni wale wale ambao angetokea Malaika akaambiwa aangalie Mali walizojilimbikizia na mapesa wanayonyanganya watu na kujilimbikizia na ufahari wa kila aina hakika wangeomba milima iwaangukie ili wajifiche wasiumbuliwe.
Hakuna mtu mwema mwenye hofu ya kukosa.
Mtu mwema akikosa anamshukuru Mungu na kujipanga tena wakati wake ukifika atamuinua tena.
Watu waovu wakipandishwa wanamsahau Mungu na kutupa ngazi iliyowapandisha.Wanaamini nguvu zao ndizo zitakazowasaidia kudumu kwenye madarakani yao.
Nchi ikiwa na Uhuru na Demokrasia ya kweli adui wa nje na ndani hawezi kuingia. Ndio maana nchi nyingi za magharibi hazina vita vya wenyewe kwa wenyewe visivyoisha kama Afraka na Asia.
Hivi Mtu ambaye wazazi wake wamepotezwa na magenge yasiyojulikana lakini hayatafutwi atakuaje na amani na kuipenda nchi yake. Bora mtu apotezwe kwa Uhalifu kama wizi ,ujambazi na uuaji lakini sio kwa sababu anakosoa watawala ambao ni binadamu wenye makosa.