Kama unaomba hivi, imani yako itashuka na utamchoka Mungu mapema

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,596
15,391
Maombi ni moja ya njia ya kuondoa wasiwasi na kuongeza imani katikati ya changamoto na sintofahamu za maisha.

Lakini kama hujui kuomba vizuri unaweza kujikuta yanakuongezea stress, wasiwasi, hata kushusha imani yako kwa Mungu. Na hii imepelekea watu kucheza miguu miwili. Mmoja kwa Mungu mwingine kwenye utamaduni kificho.

Kosa liko wapi.
Unapoanza maombi unaanza kwa kutanguliza shida na masumbufu yako badala ya kutanguliza ukuu na uweza wa huyo Mungu kwanza.

Tumia muda mwingi katika utangulizi kumtambua Mungu, uweza wake, ukuu wake sifa zake na utukufu wake. Hii itakufanya akilini mwako uone Ukuu wa Mungu na katatizo kanafifia hata kabla hujakataja. Ukifika wakati wa kueleza unachotaka basi unakuwa na uhakika na huyo unayemuomba maana unajua akilini fika anauwezo gani.

Kutanguliza kuvurumisha matatizo yako kama kipaumbele, unayakuza kuliko uwezo wa Mungu akilini mwako. Hivyo unamkuza shetani na uwezo wake kwako Kuliko Mungu. Unampa nafasi kubwa kuliko Mungu. Hivyo maombi ya kumbrand shetani na uwezo wake huwa yanaarika majini badala ya malaika. Yanajaza hofu, mashaka na wasiwasi.

Mfano wa hili fundisho ni story ya Mfalme Yehoshafat 2Nyakati 20. Namna walivyoanza maombi ni kwa kumtambua Mungu na uweza wake kisha wakamsakizia matatizo yao. MUNGU ALIINGILIA KATI KWA KASI YA AJABU.

HII NDIO MAANA YESU ALIFUNDISHA TUANZA KUOMBA KWA KUSEMA " BABA YETU ULIYE MBINGUNI, JINA LAKO LITUKUZWE, UFALME WAKO UJE".
Hii ni kama frame work wewe hapo unatakiwa kujaza maneno mengi kwenye hii sentensi ya Yesu.


Ni hayo tu.


Kama umepata kitu, sema amina.
 
Haya maisha haya yanatesa watu sana!!

Binadamu Hana furaha coz ya matatizo na mashaka!!

Dunia haikupaswa kuwa na shida zinazotufanya kuwa watumwa wa maombi kwa mamlaka yasiyoonekana kwa macho,

Maombi yenyewe kwa mamlaka yasiyoonekana ni mateso tosha kwamuombaji ni vile watu ni waoga kusema ukweli tu!lakini Imani zinaongeza mateso zaidi kwa wahusika kulikuwa hakuna haja ya mateso kuumbwa wakati UWEZEKANO wa kuyaepuka na Dunia ikawa mahala pa Raha sana!!
 
Haya maisha haya yanatesa watu sana!!

Binadamu Hana furaha coz ya matatizo na mashaka!!

Dunia haikupaswa kuwa na shida zinazotufanya kuwa watumwa wa maombi kwa mamlaka yasiyoonekana kwa macho,

Maombi yenyewe kwa mamlaka yasiyoonekana ni mateso tosha kwamuombaji ni vile watu ni waoga kusema ukweli tu!lakini Imani zinaongeza mateso zaidi kwa wahusika kulikuwa hakuna haja ya mateso kuumbwa wakati UWEZEKANO wa kuyaepuka na Dunia ikawa mahala pa Raha sana!!
Asante kwa haya maoni pia. Na wewe ubarikiwe sana. Wewe nj mtu mwema.
 
Hapo kwny kuvurumisha matatizo hapo ndo penyewe..sasa tulishaambiwa tulete mizigo yetu atatupumzisha..ndo tunamshushia sasa kila aina ya matatizo...hahha
 
oh huwa nafanya hivyo bila kujua umuhimu wake,kumbe ndiyo maana naridhikaga kabla hata ya majibu. Mungu ni mwema sana ameniondolea vipepo mtu vyote kwa njia hiyohiyo, maana hivi vipepomtu ndiyo huwa vinatumwa na babayao ibilis kunifikia.
 
oh huwa nafanya hivyo bila kujuanumuhimu wake,kumbe ndiyo maana naridhikaga kabla hata ya majibu.Mungu ni mwema sana ameniondolea vipepo mtu vyote kwa nia hiyohiyo, maana hivi vipepomtu ndiyo huwa vinatumwa na babayao ibilis kunifikia.
Amina songa mbele. Hivyo ndivyo watakatifu wanaomba.
Sio maombi ya kilokole eti unapigana na shetani kwenye maombi. Ukiomba hivyo hata huyo shetani hasogelei hapo mahala.
 
Hapo kwny kuvurumisha matatizo hapo ndo penyewe..sasa tulishaambiwa tulete mizigo yetu atatupumzisha..ndo tunamshushia sasa kila aina ya matatizo...hahha
😀😀
Matatizo sio kipaumbele. Kibaumbele ni kiboko wa matatizo. Ukispend muda wa kutosha kumtambua utagundua vitatizo vyako ni viduchu sana kulinganisha na uweza wake. Hivyo utajikuta unavutaja bila wasiwasi au kuvikuza.

Haijakatazwa ila sio kitu cha kuanza nacho.
 
Back
Top Bottom