Hakuna kipindi katika maisha yangu nilichokuwa karibu na Mungu kama hiki

jamaikatz

Member
Jul 11, 2023
51
132
Hakuna kipindi katika maisha yangu nilichokuwa karibu na Mungu kama hiki. Sometimes mpaka najiona nimechelewa sana kuyafanya yale anayotaka kila siku niyafanye.

Mimi nilishakuwaga na mashaka sana na Mungu kwenye kujibu maombi, thats true bro lakini baadaye nikakaa na kujifikiria kwa nini? Watu wanasema Mungu anajibu, why kwangu hajibu? Sikutaka kuwasikiliza wachungaji wanasemaje, nikaingia chimbo.

Ndio! Nikaingia chimbo.

Nikapata elimu kuhusu Mungu. Huwa ninawaambieni humu kila siku. Kila ninachomuomba Mungu sasa hivi huwa anajibu kwa wakati ninaotaka anijibu.

Kitu cha kwanza lazima ukubaliane na dunia, hilo watu huwa wanalishindwa na lazima ujue kwamba shetani ana nguvu kuliko wewe, sio nguvu tu, bali anaweza hata kukuua.

Mungu aliporuhusu shetani amjaribu Ayubu, miongoni mwa mambo aliyomwambia asimfanyie ni kumuua. Why? Hata Mungu anajua kwamba shetani kwa nguvu alizonazo, anaweza kukuua.

So cha kwanza kubaliana na dunia, usijifanye match know sana. Mtu anakwambia mambo makubwa duniani yanaongozwa na watu wa kishetani, anakuuliza nafasi ya Mungu ipo wapi? Bro! Kwanza kubaliana na hii dunia.

Tunaposema uwe humble, hata kukubaliana na hii dunia ni dalili ya kuwa humble, baada ya hapo sasa, saidia watu, ondoa chuki moyoni mwako halafu la zaidi kila siku utakapotaka kulala, chukua hata dakika 2 kumshukuru Mungu.

Usimshukuru kimoyomoyo, toa sauti yako mshukuru Mungu.

Jumapili nilimwambia Mungu, mpaka inafika Ijumaa nataka hiki na kile, najua siwezi kuvipata na sijui nitavipata kwa staili gani. Ila wewe si ndiye Mungu ninayemshukuru kila siku? Wewe si ndiye Mungu ambaye namuabudu? Mungu basi kumbuka jinsi ninavyojitoa kwa watoto wa mitaani. Kama ninachokifanya ni sahihi, kwa nini usinipe sasa ninachokiomba?

Leo Jumanne... Mungu akanipa, hakutaka kusubiri mpaka Ijumaa.

Huyu Mungu muacheni tu.

Leo ukiniambia Mungu hakujibu maombi yako, maybe kuna sehemu unakosea, kuna codes bado hujazielewa.

Hebu wakati mwingine mjaribu Mungu. Si kwenye Biblia ameandika nijaribuni muone nitakavyowabariki? Sasa wewe mbona humjaribu? Unajitoa kwa watu, hebu mjaribu Mungu kwa kumwambia nataka hiki na kile, tena omba vile vilivyo nje ya uwezo wako.

Mimi huwa nipo hivi.

Mtu akiniomba 500, nikampa, halafu akasema nashukuru sana, huwa naweza kumuongezea hata 2000, nipo hivyo. Huwa nasikia raha sana mtu akinishukuru. Sasa najiulizaga, kama mimi nasikia raha hivi, vipi kuhusu Mungu? Akinipa hiki, nikamshukuru sana, kesho nikimuomba kingine hawezi kunipa? Lazima atakupa kwa kuwa una moyo wa shukrani.

Braza! Mimi ni kasela flani hivi ila nipo humble sana kwa Mungu. Mimi mjanja mno ila ujanja nauwekeaga mfukoni nikiingiaga kwenye mambo kuhusu Mungu.

Namwambiaga jamaa anayenitengenezea App... Bro usiwe na presha, yaani hata kama ipo tayari, just relax, muda wa Mungu ukifika, wewe mwenyewe utanikabidhi, lakini pia nikitaka unikabidhi wiki ijayo, nikamwambia Mungu wangu, wiki ijayo utakuwa umeimaliza na kunipa.

Nikijaga humu nakuwa kama fala, nakwambia ndugu yangu tujichange tukawasaidie watoto wa mitaani hata kwa chakula. Unaniona fala fulani.

Bro! Nikifikaga kule ndio najua kwa staili hii Mungu hawezi kukuacha hata iweje. Fikiria unawapa chakula watoto, wanachukua na kimoja kinabaki, kila ukitafuta mtoto, humuoni, unaamua kuondoka nacho. Tena unajikuta ukipita katika njia ambayo huwa hupitagi hata siku moja.

Njiani unakutana na jamaa tu wa mtaani ambaye kwa kumwangalia unaona hajala, unataka kumpa, unahisi kabisa uzito moyoni, unaondoka. Njiani unakutana na muokota makopo, unamsogelea na kumpa ile plate, anaipokea, anakushukuru mno na anakwambia ni kwa namna ameteswa na njaa siku hiyo, daktari alimwambia kwa jinsi anavyoumwa, ale ashibe, atakula wapi? Anaamua kuokota makopo akauze apate pesa ya chakula tu ili ale ashibe kama daktari alivyotaka.

Ghafla njiani anakutana na wewe, unampa chakula. Bro! Mtu huyo anavyokushukuru, mwanaume mtu mzima mpaka anataka kulia, hebu jifikirie Mungu atamfanyia nini huyu Nyemo na watu waliojichanga kwa ajili ya hao watu? Unadhani wakimwambia Mungu tunataka hiki na kile atashindwa kuwapa? Thubutu.

Nilimwambia mama nitakuwa bilionea wa kwanza kwenye familia yetu, nilipokuwa chumbani nikamwambia Mungu nataka nipige hatua moja hadi nyingine mpaka niwe bilionea, yaani nizione hizo njia.

Naongea hivyo na Mungu wangu, simu inaita, napokea na sauti ya dada mmoja inaniita, Mambo vipi bilionea! Of course ananiitaga hivyo lakini why ananipigia simu na kuniita hivyo muda niliotoka kumuomba Mungu? Ni miezi mingi hatujawasiliana.

Guys! Hizi ni code.

Unashangaa watu wanakuwa na pesa nyingi na wanaongoza kutoa. Wewe hauna pesa nyingi unakuwa mchoyo.

Majuzi nilitaka kupata ajali pale Ubungo, yaani kwa namna ilivyokuwa, nikajisemea aliyeniokoa hapa ni Mungu wala si ujanja wangu. Huyu ni Mungu dhahiri.

Codes ni hizi.

1. Saidia wasiojiweza.
2. Mshukuru Mungu kwa sauti kila unapotaka kulala.
3. Ondoa chuki moyoni mwako na ujaze upendo.

Fanya hivyo, mwezi ujao utaniletea majibu.

By the way... Pasaka hii tunakwenda kulisha wale watoto kama kawaida yetu.
 
Hakuna kipindi katika maisha yangu nilichokuwa karibu na Mungu kama hiki. Sometimes mpaka najiona nimechelewa sana kuyafanya yale anayotaka kila siku niyafanye.

Mimi nilishakuwaga na mashaka sana na Mungu kwenye kujibu maombi, thats true bro lakini baadaye nikakaa na kujifikiria kwa nini? Watu wanasema Mungu anajibu, why kwangu hajibu? Sikutaka kuwasikiliza wachungaji wanasemaje, nikaingia chimbo.

Ndio! Nikaingia chimbo.

Nikapata elimu kuhusu Mungu. Huwa ninawaambieni humu kila siku. Kila ninachomuomba Mungu sasa hivi huwa anajibu kwa wakati ninaotaka anijibu.

Kitu cha kwanza lazima ukubaliane na dunia, hilo watu huwa wanalishindwa na lazima ujue kwamba shetani ana nguvu kuliko wewe, sio nguvu tu, bali anaweza hata kukuua.

Mungu aliporuhusu shetani amjaribu Ayubu, miongoni mwa mambo aliyomwambia asimfanyie ni kumuua. Why? Hata Mungu anajua kwamba shetani kwa nguvu alizonazo, anaweza kukuua.

So cha kwanza kubaliana na dunia, usijifanye match know sana. Mtu anakwambia mambo makubwa duniani yanaongozwa na watu wa kishetani, anakuuliza nafasi ya Mungu ipo wapi? Bro! Kwanza kubaliana na hii dunia.

Tunaposema uwe humble, hata kukubaliana na hii dunia ni dalili ya kuwa humble, baada ya hapo sasa, saidia watu, ondoa chuki moyoni mwako halafu la zaidi kila siku utakapotaka kulala, chukua hata dakika 2 kumshukuru Mungu.

Usimshukuru kimoyomoyo, toa sauti yako mshukuru Mungu.

Jumapili nilimwambia Mungu, mpaka inafika Ijumaa nataka hiki na kile, najua siwezi kuvipata na sijui nitavipata kwa staili gani. Ila wewe si ndiye Mungu ninayemshukuru kila siku? Wewe si ndiye Mungu ambaye namuabudu? Mungu basi kumbuka jinsi ninavyojitoa kwa watoto wa mitaani. Kama ninachokifanya ni sahihi, kwa nini usinipe sasa ninachokiomba?

Leo Jumanne... Mungu akanipa, hakutaka kusubiri mpaka Ijumaa.

Huyu Mungu muacheni tu.

Leo ukiniambia Mungu hakujibu maombi yako, maybe kuna sehemu unakosea, kuna codes bado hujazielewa.

Hebu wakati mwingine mjaribu Mungu. Si kwenye Biblia ameandika nijaribuni muone nitakavyowabariki? Sasa wewe mbona humjaribu? Unajitoa kwa watu, hebu mjaribu Mungu kwa kumwambia nataka hiki na kile, tena omba vile vilivyo nje ya uwezo wako.

Mimi huwa nipo hivi.

Mtu akiniomba 500, nikampa, halafu akasema nashukuru sana, huwa naweza kumuongezea hata 2000, nipo hivyo. Huwa nasikia raha sana mtu akinishukuru. Sasa najiulizaga, kama mimi nasikia raha hivi, vipi kuhusu Mungu? Akinipa hiki, nikamshukuru sana, kesho nikimuomba kingine hawezi kunipa? Lazima atakupa kwa kuwa una moyo wa shukrani.

Braza! Mimi ni kasela flani hivi ila nipo humble sana kwa Mungu. Mimi mjanja mno ila ujanja nauwekeaga mfukoni nikiingiaga kwenye mambo kuhusu Mungu.

Namwambiaga jamaa anayenitengenezea App... Bro usiwe na presha, yaani hata kama ipo tayari, just relax, muda wa Mungu ukifika, wewe mwenyewe utanikabidhi, lakini pia nikitaka unikabidhi wiki ijayo, nikamwambia Mungu wangu, wiki ijayo utakuwa umeimaliza na kunipa.

Nikijaga humu nakuwa kama fala, nakwambia ndugu yangu tujichange tukawasaidie watoto wa mitaani hata kwa chakula. Unaniona fala fulani.

Bro! Nikifikaga kule ndio najua kwa staili hii Mungu hawezi kukuacha hata iweje. Fikiria unawapa chakula watoto, wanachukua na kimoja kinabaki, kila ukitafuta mtoto, humuoni, unaamua kuondoka nacho. Tena unajikuta ukipita katika njia ambayo huwa hupitagi hata siku moja.

Njiani unakutana na jamaa tu wa mtaani ambaye kwa kumwangalia unaona hajala, unataka kumpa, unahisi kabisa uzito moyoni, unaondoka. Njiani unakutana na muokota makopo, unamsogelea na kumpa ile plate, anaipokea, anakushukuru mno na anakwambia ni kwa namna ameteswa na njaa siku hiyo, daktari alimwambia kwa jinsi anavyoumwa, ale ashibe, atakula wapi? Anaamua kuokota makopo akauze apate pesa ya chakula tu ili ale ashibe kama daktari alivyotaka.

Ghafla njiani anakutana na wewe, unampa chakula. Bro! Mtu huyo anavyokushukuru, mwanaume mtu mzima mpaka anataka kulia, hebu jifikirie Mungu atamfanyia nini huyu Nyemo na watu waliojichanga kwa ajili ya hao watu? Unadhani wakimwambia Mungu tunataka hiki na kile atashindwa kuwapa? Thubutu.

Nilimwambia mama nitakuwa bilionea wa kwanza kwenye familia yetu, nilipokuwa chumbani nikamwambia Mungu nataka nipige hatua moja hadi nyingine mpaka niwe bilionea, yaani nizione hizo njia.

Naongea hivyo na Mungu wangu, simu inaita, napokea na sauti ya dada mmoja inaniita, Mambo vipi bilionea! Of course ananiitaga hivyo lakini why ananipigia simu na kuniita hivyo muda niliotoka kumuomba Mungu? Ni miezi mingi hatujawasiliana.

Guys! Hizi ni code.

Unashangaa watu wanakuwa na pesa nyingi na wanaongoza kutoa. Wewe hauna pesa nyingi unakuwa mchoyo.

Majuzi nilitaka kupata ajali pale Ubungo, yaani kwa namna ilivyokuwa, nikajisemea aliyeniokoa hapa ni Mungu wala si ujanja wangu. Huyu ni Mungu dhahiri.

Codes ni hizi.

1. Saidia wasiojiweza.
2. Mshukuru Mungu kwa sauti kila unapotaka kulala.
3. Ondoa chuki moyoni mwako na ujaze upendo.

Fanya hivyo, mwezi ujao utaniletea majibu.

By the way... Pasaka hii tunakwenda kulisha wale watoto kama kawaida yetu.
MARUDIO YA HII THREAD
 
Back
Top Bottom