Kama nchi, ushoga tumeukataza na kuuadhibu kisheria. Kilichobaki ni utashi wa kuisimamia sheria husika, tuache porojo!

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Nimechukua muda wa kutosha kuisoma Sheria ya Kanuni ya Adhabu (Sura Na. 16 iyofanyiwa mapitio mwaka 2019) na kujiridhisha pasi na shaka kuwa, kama nchi-Tanzania, ushoga umekatazwa na kuadhibiwa vikali kwenye sheria hiyo. Ni vifungu vya 154 na 155 vya Kanuni ya Adhabu.

Wahusika wote wa ushoga (anayeingilia na yule anayeingiliwa) wote wamewekewa adhabu zao pale ambapo mashtaka yao yatathibitishwa mahakamani.

Kama hiyo haitoshi, hata kujaribu kutenda ushoga/kuingilia kinyume na maumbile ni kosa chini ya Kanuni ya Adhabu. Ndiyo kusema kufanya ushoga au kujaribu kufanya ushoga kote kunahesabika kosa chini ya Kanuni ya Adhabu.

Kwakuwa sheria, inayobeba kauli na msimamo thabiti ya nchi yetu juu ya masuala ya kufanya mapenzi kinyume na maumbile, kinachobakia ni mamlaka husika kuendelea kuisimamia sheria hiyo na kutokomeza tatizo hili. Ni utashi tu wa kimamlaka ndio uliobakia katika kuishinda vita hii.

Tuache porojo na tusimamie sheria. Wapo wanaojihusisha na mapenzi kinyume na maumbile wanaojulikana na wale wasiojulikana lakini wanaoweza kujulikana. Waanikwe; wakamatwe; washtakiwe na kuadhibiwa kadiri ya matakwa na taratibu za kisheria. Nchi imesema kupitia sheria, nchi iendelee kutekeleza kupitia sheria!

Vifungu husika ni hivi:

154.-(1) Mtu yeyote ambaye-
(a) anamuingilia mtu yeyote kinyume cha maumbile au,
(b) anamuingilia mnyama kimwili au
(c) anamruhusu mwanaume kumuingilia yeye mwanaume au mwanamke kinyume cha maumbile, atakuwa ametenda kosa, na atawajibika kwa adhabu ya kifungo cha maisha na wakati mwingine kifungo kisichopungua miaka thelathini .

(2) Ikiwa kosa limetendwa chini ya kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki dhidi ya mtoto wa chini ya miaka kumi, mkosaji atawajibika kwa adhabu ya kifungo cha maisha.

155. Mtu yeyote ambaye atajaribu kutenda kosa mojawapo katika makosa yaliyotajwa katika kifungu cha 154 atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia atawajibika kwa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka ishirini .
 
Lakini si sheria inasema akipatikana na hatia??
Unataka waweke camera kila nyumba wapate ushahidi wa kuwatia hatiani???
Mkuu, ushahidi si huo tu. Wengine hukamatwa 'in the act'. Halafu, kukutwa na hatia ni pale ambapo mashtaka yake yatapelekwa mahakamani na kuthibitishwa na upande wa mashtaka. Itakatyofuata hapo ni adhabu tu kwa mujibu wa sheria.
 
Mkuu, ushahidi si huo tu. Wengine hukamatwa 'in the act'. Halafu, kukutwa na hatia ni pale ambapo mashtaka yake yatapelekwa mahakamani na kuthibitishwa na upande wa mashtaka. Itakatyofuata hapo ni adhabu tu kwa mujibu wa sheria.

Si wamehukumiwa tayari ?mmoja Mbeya na mwingine wapi sijui..
Waliokamatwa na kukiri wamefungwa Kwa kujibu WA sheria .
Lawama Kwa serikali zinakuja vipi?
 
Kuna yule shoga alikamatwa Mbeya, juzi nikaona picha zake mitandaoni akiwa amevaa nguo ya kike alipokamatwa na sungusungu usiku akiwa mawindoni ndipo akapigwa picha.

Yule shoga alihukumiwa miaka 30 jela kwa kukiri kosa la ushoga, nikajiuliza huyu alikiri kwani wapi walimkuta akifanya hivyo vitendo? na kama alikutwa, huyo aliyekuwa nae yuko wapi?

Hapo ndipo naungana nawe mleta mada, huwezi kumkamata mtu kwa sababu ya kuingiliwa kinyume cha maumbile, lakini usimkamate huyo aliyemuingilia, hilo ni sawa na uonevu na ni kinyume cha sheria.
 
Hii sheria bado ina mapungufu kwani ni vigumu kumkamata mtu akitenda kitendo cha ushoga ndio maana wengi wamekamatwa kwa makosa ya ulawiti nafikiri tungeenda mbali na kuweka sheria ya kuwaadhibu wale wanaopromoti mambo ya ushoga ikiwemo kwenye mitandao, redio, magazeti na tv hata kumbi za muziki hapo kidogo hata wakifanya mambo yao watafanya kwa usiri mkubwa kuliko sasa wanajitangaza waziwazi.
 
Kuna watu kama yule shoga mwandamizi Nabii Tito alikiri mwenyewe kuwa ni shoga na akaeleza alivyoanza hadi kuwa kungwi huku na yeye akiwa anawaingilia wenzake lakini hadi leo yupo mitaani aranda randa tu kuendeleza ushoga wake kwa kuzuga kuwa anapinga ufiraji. Sheria ipo lakini haitekelezwi kuwaadhibu hao mabazazi.
 
Ajira hakuna kwanini Vijana wasiuze mikund*.
.
FB_IMG_1612012763868.jpg
 
Watu wamewaandama mashoga tu wakati hii sheria inahusu hata wale ambao wanapenda kuwaingilia wanawake wao kinyume na maumbile(na wanawake wanaokubali kufanyiwa hivyo). Na kuingilia kinyume cha maumbile kunahusu pia viungo vingine kama midomo, mikono n.k. Wote hao wanastahili kufungwa miaka 30, kama vile jambazi wa kutumia silaha.

Amandla...
 
Nimechukua muda wa kutosha kuisoma Sheria ya Kanuni ya Adhabu (Sura Na. 16 iyofanyiwa mapitio mwaka 2019) na kujiridhisha pasi na shaka kuwa, kama nchi-Tanzania, ushoga umekatazwa na kuadhibiwa vikali kwenye sheria hiyo. Ni vifungu vya 154 na 155 vya Kanuni ya Adhabu.

Wahusika wote wa ushoga (anayeingilia na yule anayeingiliwa) wote wamewekewa adhabu zao pale ambapo mashtaka yao yatathibitishwa mahakamani.

Kama hiyo haitoshi, hata kujaribu kutenda ushoga/kuingilia kinyume na maumbile ni kosa chini ya Kanuni ya Adhabu. Ndiyo kusema kufanya ushoga au kujaribu kufanya ushoga kote kunahesabika kosa chini ya Kanuni ya Adhabu.

Kwakuwa sheria, inayobeba kauli na msimamo thabiti ya nchi yetu juu ya masuala ya kufanya mapenzi kinyume na maumbile, kinachobakia ni mamlaka husika kuendelea kuisimamia sheria hiyo na kutokomeza tatizo hili. Ni utashi tu wa kimamlaka ndio uliobakia katika kuishinda vita hii.

Tuache porojo na tusimamie sheria. Wapo wanaojihusisha na mapenzi kinyume na maumbile wanaojulikana na wale wasiojulikana lakini wanaoweza kujulikana. Waanikwe; wakamatwe; washtakiwe na kuadhibiwa kadiri ya matakwa na taratibu za kisheria. Nchi imesema kupitia sheria, nchi iendelee kutekeleza kupitia sheria!

Vifungu husika ni hivi:

154.-(1) Mtu yeyote ambaye-
(a) anamuingilia mtu yeyote kinyume cha maumbile au,
(b) anamuingilia mnyama kimwili au
(c) anamruhusu mwanaume kumuingilia yeye mwanaume au mwanamke kinyume cha maumbile, atakuwa ametenda kosa, na atawajibika kwa adhabu ya kifungo cha maisha na wakati mwingine kifungo kisichopungua miaka thelathini .

(2) Ikiwa kosa limetendwa chini ya kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki dhidi ya mtoto wa chini ya miaka kumi, mkosaji atawajibika kwa adhabu ya kifungo cha maisha.

155. Mtu yeyote ambaye atajaribu kutenda kosa mojawapo katika makosa yaliyotajwa katika kifungu cha 154 atakuwa ametenda kosa na akipatikana na hatia atawajibika kwa adhabu ya kifungo kisichopungua miaka ishirini .

Hii Nchi!!
 

Attachments

  • 1679755198287.jpg
    1679755198287.jpg
    14.7 KB · Views: 2
  • 1679755198420.jpg
    1679755198420.jpg
    12.7 KB · Views: 2
Back
Top Bottom