Kama kweli suala la DP World limewagusa basi nguvu kubwa ielekezwe kwenye kudai katiba mpya

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,563
50,415
Inakera, inaudhi na inauma sana kuona katiba yetu inawafanya wananchi kuwa wanyonge. Hawana sauti, hawana maamuzi na wala hawawezi kupindua chochote kilichoamuliwa na viongozi (serikali).

Chanzo cha upuuzwaji huu wa sauti za wananchi, uvizwaji wa nguvu ya wananchi na viongozi kutoogopa/ kutoheshimu hasira/ maoni ya wananchi ni katiba mbovu tuliyo nayo.

Katiba imempa mamlaka makubwa sana rais. Hakuna kiongozi au raia yeyote anayeweza kuukwepa mkono wa adhabu wa rais endapo ataenda kinyume naye kwa katiba yetu hii. Hii ndiyo sababu watu wameamua kujikomba, kuwa machawa na kushabikia hata upuuzi unaofanywa rais ili maisha yaende.

Magufuli alifanya mambo ya hovyo yasiyopaswa hata kuelezewa ktk zama hizi, lkn kulikuwa na kundi kubwa la watu walioimba na kusifu upuuzi wa Magufuli. Sababu tu katiba yetu ni mbovu.

Kwa katiba yetu hii tutakujq kumpata rais atakayeamua kuuza baadhi ya mikoa kwa nchi jirani au mabeberu na hatutamfanya kitu. Mzee Mwinyi aliuza pori la Loliondo tumemfanya nn? Kikwete amekabidhi gesi yetu ya Mtwara (ni kama kauza tu) kwa wachina, tumemfanya nn? Samia naye atafanya chochote anachotaka kufanya, wananchi mtapiga kelele lkn hakuna mtakachomfanya. Mf. Alianzisha tozo (huku akijua tunalipa Kodi). Tumelalamika lkn mpk leo tunaitoa na kiodi tunalipa. Hatujamfanya kitu.

Suluhu ya haya yote ni kuunda katiba itakayomfanya rais kuwa mtumishi wa wananchi na siyo mtawala wa wananchi. Katiba itakayounda mihili huru na taasisi zenye nguvu. Katiba itayomfanya rais kuwa chini ya sheria, yaani akingua anawajibishwa ama anaondoshwa.

Nawasihi watanzania tuipiganie katiba mpya ili sisi na vizazi vyetu tuishi vyema katikati nchi yetu.

Nimemaliza, kama hutaki kimpango wako.
 
Hao manafiki hawana uzalendo wowote nyooyo zao zimejaa chuki, hi nchi ilisha uuzwa kitambo kuanzia enzi za Mkapa lakini atavukiwambia mwarubaini ni katiba mpya utaona wakujitokeza
 
Hao manafiki hawana uzalendo wowote nyooyo zao zimejaa chuki, hi nchi ilisha uuzwa kitambo kuanzia enzi za Mkapa lakini atavukiwambia mwarubaini ni katiba mpya utaona wakujitokeza
Wahuni tu hawa. Wanapamabana na majani badala ya kushughulika na mzizi.
 
Inakera, inaudhi na inauma sana kuona katiba yetu inawafanya wananchi kuwa wanyonge. Hawana sauti, hawana maamuzi na wala hawawezi kupindua chochote kilichoamuliwa na viongozi (serikali).

Chanzo cha upuuzwaji huu wa sauti za wananchi, uvizwaji wa nguvu ya wananchi na viongozi kutoogopa/ kutoheshimu hasira/ maoni ya wananchi ni katiba mbovu tuliyo nayo.

Katiba imempa mamlaka makubwa sana rais. Hakuna kiongozi au raia yeyote anayeweza kuukwepa mkono wa adhabu wa rais endapo ataenda kinyume naye kwa katiba yetu hii. Hii ndiyo sababu watu wameamua kujikomba, kuwa machawa na kushabikia hata upuuzi unaofanywa rais ili maisha yaende.

Magufuli alifanya mambo ya hovyo yasiyopaswa hata kuelezewa ktk zama hizi, lkn kulikuwa na kundi kubwa la watu walioimba na kusifu upuuzi wa Magufuli. Sababu tu katiba yetu ni mbovu.

Kwa katiba yetu hii tutakujq kumpata rais atakayeamua kuuza baadhi ya mikoa kwa nchi jirani au mabeberu na hatutamfanya kitu. Mzee Mwinyi aliuza pori la Loliondo tumemfanya nn? Kikwete amekabidhi gesi yetu ya Mtwara (ni kama kauza tu) kwa wachina, tumemfanya nn? Samia naye atafanya chochote anachotaka kufanya, wananchi mtapiga kelele lkn hakuna mtakachomfanya. Mf. Alianzisha tozo (huku akijua tunalipa Kodi). Tumelalamika lkn mpk leo tunaitoa na kiodi tunalipa. Hatujamfanya kitu.

Suluhu ya haya yote ni kuunda katiba itakayomfanya rais kuwa mtumishi wa wananchi na siyo mtawala wa wananchi. Katiba itakayounda mihili huru na taasisi zenye nguvu. Katiba itayomfanya rais kuwa chini ya sheria, yaani akingua anawajibishwa ama anaondoshwa.

Nawasihi watanzania tuipiganie katiba mpya ili sisi na vizazi vyetu tuishi vyema katikati nchi yetu.

Nimemaliza, kama hutaki kimpango wako.
Ulisemalo ni sahihi kabisa kwamba dawa ya matatitzo ya nchi yetu, wakati huu, ni wananchi sote kuamka na kuwa na ujasiri wa kudai haki ya kuwa na katiba sahihi ambayo, kwanza, itatambua Serikali tatu za Mungano (Serikali ya Muunga o, Serikali ya Tanganyika, na Serikali Zanzibar). Lakini wzkati huohuo I've Kstiba inayowapa wananchi mamlaka (uwezo) ya kuwawadhibisha viongozi wa Serikali zote tatu. Kwa kadiri ya kumbukumbu zangu, kazi ya kutengeneza Rasimu ya Katiba hiyo ilifanyika chini ya uongozi wa Jaji Joseph Sinde Warioba, tena kwa gharama kubwa ya pesa za kodi yetu (Wananchi), kwa kukusanya maoni yetu wananchi. Cha ajabu, kilichoitwa Bunge la Katiba, chini ya Spika (marehemu Samweli Sita) na Makamu Spika (Samia Suluhu Hassani -ambaye ndiye Rais wa sasa anayesema asilizwe swala la Katiba mpya, bali aachwe kwanza aiuze nchi - kwa mikataba mibovu), kwa makusudi, na bila kujali gharama kubwa ya fedha za kodi ya wananchi iliyotumika kukusanya maoni ya Wananchi kuandaa Rasmu hiyo, waliitupilia mbali bila maelezo yoyote ya kitaalam (na kusitisha kabisa ajenda ya utungaji wa Katiba Mpya). Nasi wananchi, kama kwamba tumelogwa, tulikaa kimya bila kuhoji kwa nini Serikali iliyadharau maoni ya wananchi, na hivyo kufanya gharama iliyotumika kukusanya maoni hayo ionekane kuwa ni ubadhirifu wa fedha za umma. Sasa, ninadhani, ndiyo muda mwafaka, wakati huu tunapolalamikia mkataba wa kifisadi wa DP World, tudai (siyo tuombe) serikali iheshimu maoni yetu yaliyo katika Rasimu ya Tume ya Jaji Warioba, yaidhinishwe kuanza kutumika kama yalivyotarajiwa kuwa Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tananyika na Zanzibar.
 
Samia Suluhu Hassani -ambaye ndiye Rais wa sasa anayesema asilizwe swala la Katiba mpya, bali aachwe kwanza aiuze nchi - kwa mikataba mibovu)
Serious?? Katoa kauli ya kwamba asiulizwe kuhusu katiba mpya??
 
Back
Top Bottom