Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kwani tulitegemea majibu ?

Toka lini Mtanzania akapata majibu bana ?

Tuna formulate maswali na ku brainstorm majibu wenyewe kila siku hapa, na the Zitto's of the world couldn't give a hoot kutafuta majibu.

Ukishabweteshwa na privileges za Tume za Rais na kuweza kutembea kwenye corridors na sebule za Magogoni bila kuulizwa we nani utakumbuka kutafutia wananchi majibu ?


Hivi ile tume imeshafanya direct slowness induction kwa Zitto katika ufuatiliaji wa mambo yanayohusu maslahi ya wananchi kwa ujumla?
 
You see, hicho ndio anachoogopa Zitto hicho.

That's what I'm talking about nikisema Zitto anataka kujijengea gravitas. Ile image ya back bencher truth teller na kukemewa kemewa na Spika haitaki tena. Ameshaingizwa kwenye wanaoaminiwa na Tume za Rais.

You see, this is why Dr. Slaa is the most ballsy leader in modern history of Tanzania.

Kaka nchi haijengwi na wanasiasa wa aina moja. Ndio maana kuna kina Slaa, Mrema, Seif Sharif, Mtikila, Mama Anna Abdala, Mkapa, Kikwete ect..

Hawa wote wana mitindo yao, uwezo wao, mazingira yao na miono yao ya nini na jinsi gani ya kufanya siasa. Na wote kwa pamoja wanajenga utamaduni wa kisiasa tulionao na hata kuinspire utamaduni mpya unaojijenga. Tusimlazimishe Zitto kufanya siasa za kubwatuka, insensitivity na zisizoendana na utashi wake, mazingira yake na hata nafasi yake kichama na kitaifa...

Tunapofanya kuwakejeli ama kuwatuhumu viongozi kama hawa wanaojitokeza hapa kujadiliana nasi tunasababisha ama walipo kujiondoa ama wengine kuogopa kuja hapa.

Ni muhimu tukawa strategic katika mijadala hii na kuthamini, kuheshimu na kung'amua hali na utashi wa wanajamii forum wa kada tofauti, mitazamo tofauti, imani tofauti na kadhalika..

Tanzanianjema
 
Kuhani, nadhani utakuwa humtendei haki Zitto katika hili. Tumeshaona hata kwa wenzetu walioendelea kwenye mahojiano yao na waandishi wa habari njinsi wanavyoweza kukwepa maswali ambayo huleta direct confrontation baina yao na waajiri. Sisi kama wananchi ni waajiri wa wabunge, lakini ili wawe wabunge ni lazima wale viapo ambavyo vitathibitisha maadili ya kazi zao kama vile ambavyo inatakiwa kuwa kulingana na miongozo tuliojiwekea sisi wananchi - Katiba.

Sasa kumlazimisha kiongozi kutamka maneno fulani ambayo yatafurahisha jamvi na kumfanya awe shujaa kwa dakika chache za JF hali zitakazo mfanya asiweze kuwakilisha wananchi wa jimbo lake kwa kipindi kisicho julikana, huko ni kutomtendea haki. Tukubali kwamba ameshataja mengi ambayo hamna kiongozi mwingine ameweza kutaja tayari kuhusiana na swala hili na kwenye thread hii.

Je, tuwe watu wa kulazimishana tu katika kila jambo, kwa kuchukulia kila neno linaloandikwa iwe kimakosa au bila makosa kwa dhati kwenye mtandao kama tamko la katiba? Hapana, huu utakuwa unyanyasaji wa kimtandao (cyber bullying). Jambo ambalo wote naamini tungependa kuepukana nalo. Tuko kwenye majadiliano ndugu yangu, basi pale mtu anapoenda mrama/mlama asihukumiwe jumlajumla. Ni mawaidha yangu, ahsante.
SteveD.

SteveD,

Nina hakika Kuhani means no harm na anajaribu tu kugonganisha vichwa - after all he is lucky to have the curiosity of a cat - which is not a bad thing. We are often reminded that at the frontiers of knowledge, it is the difference in the thinking that points the way. Kuhani is definitely having a field day - remember it is a weekend - I only hope he has the lives of the same cat 🙂
 
Hivi ile tume imeshafanya direct slowness induction kwa Zitto katika ufuatiliaji wa mambo yanayohusu maslahi ya wananchi kwa ujumla?

Mama,

Obviously alipoingizwa kwenye Tume ya Rais lile jambo limemjengea cachet. Anataka ku maintain hiyo gravitas. Anakunywa kahawa na Kikwete na Spika na Pinda.

Zitto anasema " Madini tena ni la kwangu? Soma ripoti ya Bomani. Kazi yangu nilimaliza na nimeridhika nayo. Tuendelee na EPA"

Unaona ? Yuko kwenye such a conundrum sasa hivi. Oh yeah, the Tume ya Rais thing moderated him in the worst way.


Kuhani, nadhani utakuwa humtendei haki Zitto katika hili. Tumeshaona hata kwa wenzetu walioendelea kwenye mahojiano yao na waandishi wa habari njinsi wanavyoweza kukwepa maswali ambayo huleta direct confrontation baina yao na waajiri. Sisi kama wananchi ni waajiri wa wabunge, lakini ili wawe wabunge ni lazima wale viapo ambavyo vitathibitisha maadili ya kazi zao kama vile ambavyo inatakiwa kuwa kulingana na miongozo tuliojiwekea sisi wananchi - Katiba.

Sasa kumlazimisha kiongozi kutamka maneno fulani ambayo yatafurahisha jamvi na kumfanya awe shujaa kwa dakika chache za JF hali zitakazo mfanya asiweze kuwakilisha wananchi wa jimbo lake kwa kipindi kisicho julikana, huko ni kutomtendea haki. Tukubali kwamba ameshataja mengi ambayo hamna kiongozi mwingine ameweza kutaja tayari kuhusiana na swala hili na kwenye thread hii.

Je, tuwe watu wa kulazimishana tu katika kila jambo, kwa kuchukulia kila neno linaloandikwa iwe kimakosa au bila makosa kwa dhati kwenye mtandao kama tamko la katiba? Hapana, huu utakuwa unyanyasaji wa kimtandao (cyber bullying). Jambo ambalo wote naamini tungependa kuepukana nalo. Tuko kwenye majadiliano ndugu yangu, basi pale mtu anapoenda mrama/mlama asihukumiwe jumlajumla. Ni mawaidha yangu, ahsante.

Steve D,

Hebu soma taarifa ya bandiko la Bubu Ataka kusema hapo juu kuhusu the illustrious Dr. Slaa, halafu njoo tuongee.
 
IGP Mwema, watu wanaisubiri Kagoda

2008-11-22 10:26:30
Na Mhariri

Juzi Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali (IGP), Said Mwema, akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano aliouitisha, alieleza kutokufurahishwa na kauli za malalamiko kwamba kuna vigogo wa wizi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambao hawajakamatwa.

Alisema kulalamika tu kwamba kuna watu hawajakamatwa bila kutaja majina na uthibitisho wa wanaolalamikiwa hakuna maana, kwa hali hiyo aliwapa changamoto wananchi kuwataja wahusika kuliko kubakia tu kulalamika.

Alionya kwamba suala la EPA lina mlolongo mrefu na uchunguzi wake unaweza kuchukua muda hadi kesi zote zifikishwe mahakamani.

Sisi tumeipokea kauli ya IGP Mwema kuhusu EPA kwa tahadhari kubwa, kwanza tunakubali kwamba suala hili linaweza kuwa na mlolongo mrefu, likihusisha vyombo vya ndani na vya kimataifa au vya nje katika uchunguzi. Pia tunatambua kwamba malalamiko tu kwamba kuna vigogo hawajakamatwa bila kuwapo kwa ushahidi wa vigogo hao hakuna maana.

Lakini, IGP Mwema anapaswa kukumbuka kwamba ushughulikiaji wa watuhumiwa wa EPA tangu awali umegubikwa na usiri wa hali ya juu.

Tangu kampuni ya Deloitte Touche ilipogundua wizi wa Dola milioni 30 kutoka EPA zilizochotwa na Kagoda Agriculture Limited na baadaye Gavana wa BoT wakati huo, Daudi Ballali, akavunja mkataba na kampuni hiyo kwa sababu ya kuhoji wizi huo, serikali ilijua kwamba kuna ufisadi ndani ya BoT.

Kadhalika, ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Serikali ya mwaka 2005/06 kuhusu hesabu za BoT ilieleza hali ya wizi huo; baada ya kupata shinikizo kutoka makundi mbalimbali ya ndani na nje ya nchi ndiyo serikali iliamua kuiteua kampuni ya Ernst & Young kufanya ukaguzi wa EPA.

Kila Mtanzania anafahamu kwamba makampuni 22 yaligudulika kuhusika katika ufisadi wa Sh bilioni 133 katika akaunti hiyo peke yake.

Lakini hata baada ya ugunduzi huu wa Ernst & Young, bado serikali iliteua timu ya watu watatu ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu (AG) kuchunguza EPA ili fedha zirejeshwe na kutazama jinsi ya kuchukua hatua za kisheria.

Pamoja na AG Johnson Mwanyika, wajumbe wengine wa timu hiyo ni IGP Mwema na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah.

Kwa maana hiyo, IGP Mwema anaifahamu kwa undani EPA. Tunaamini amesoma mara kadhaa ripoti ya Ernst & Young kuhusu EPA; tunaamini pia anajua mapapa ambao wananchi wanalalamika ni akina nani; analijua hili kwa sababu anayo majina ya wenye makampuni haya.

Tutamsadia IGP Mwema kwamba miongoni mwa kampuni inayopigiwa kelele sana ni Kagoda Agriculture Limited, wamiliki wake wanaelekea kuwa wanasaidiwa kukwepa mkondo wa sheria; IGP Mwema analifahamu hili, lakini anataka umma uamini kwamba eti hakuna mchezo wowote `mchafu` unaochezwa.

Ni kwa hali hii, tunamshauri IGP Mwema kutokukubali kutumbukia katika mitego mibaya na mibovu kama ya Kagoda. IGP Mwema ni miongoni mwa wakuu wa Jeshi la Polisi ambao wamejipatia heshima kubwa katika kipindi kifupi mno alichokaa madarakani. Wananchi wanamwamini kwa kuwa ni mtu wa haki.

Sasa katika sakata la EPA ambalo umma unaamini kwamba limeasisiwa na Kagoda; yaani baba na mama wa EPA ni Kagoda; watu wanapoona Kagoda ikikwepeshwa kwa mbinu chafu mkondo wa sheria, wanapiga kelele.

Hakika tunaamini sisi kama chombo cha habari tukiwa ni mdomo wa umma hatutaacha kuwapa nafasi wananchi wawasilishe hisia zao juu ya EPA na mama yao Kagoda. IGP Mwema ni vema akalijua hili kwamba bila Kagoda kushughulikiwa hakika sakata la EPA halitafika mwisho.

SOURCE: Nipashe
 
CCM by way of Mkapa, Apson, Rostam, Sijui kuhusu CS Lumbanga.. lakini zile hela ziliibiwa kusaidia election ya CCM lakini sas pale pale watu wakachukua a retirement pension ya ukweli na wengine wakapata hela kwajili ya further political gains... Ukweli ni kwamba whenever politicians (wakimaskini) get donations or get money from corrupt means... wanapiga 'panga'... Malecela did it when his presidential bid failed... the 1st one and the 2nd one... Freeman na ile USD $2million... Kina Mkapa na EPA, Ndege ile, Mkapa alipiga panga la pension..

Katika harakati za kubinafsisha... Lumbanga, Abdallah Kigodo na Mkapa wamepiga matukio makubwa sana... Retirement.lol

Mmoja wa wanasheria walishuhulikia contract za Richmond aliniambia Mkapa is worth 500million dollars sasaivi... Watu wanafikiria mafisadi ni kina Mwakale sijui Johnson yule mshamba tuu.. Bongo people are Mafia..

JF inachukuliwa kama 'watoto wakwenye intaneti'... That is why when the time comes I will run for office and from there ndio watanikolimba...
 
Kuhani,

..Warioba na Ulimwengu walianza kuwa critical kwa Mkapa baada ya kuachwa ktk teuzi za Tume mbalimbali.

..nimeshuhudia hizi Tume za Bunge na Raisi zikiwanyamazisha wanasiasa wengi machachari.
 
Fisadi Mkapa bado tunakula naye sahani moja mpaka kieleweke kuhusu kujimilikisha Kiwira na kuwashinikiza TANESCO kusaini na mkataba na 'kampuni' yake wa shilingi 326 billioni ambao unamlipa 146 millioni kwa siku. Ule mradi wake wa kuwaleta makaburu wa Net Group ambao uliiacha TANESCO katika hali mbaya zaidi. Ushiriki wake katika ununuzi wa rada ya kifisadi, magari na helicopters za jeshi, ndege ya Rais na pia kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa si ajabu hata kwenye Kagoda kuna mkono wake. Ameshaanza kuwa na wasiwasi hata anazikacha dhifa za kitaifa kama sherehe za uhuru na muungano sijui kama mwaka huu atahudhuria sherehe za kutimiza miaka 47 ya uhuru wa Tanganyika. Bado tunaye huyu mpaka kieleweke.
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Kwa taarifa nilizonazo, Lowasa kama mtu binafsi hahusiki na KAGODA. Ana matatizo yake lakini katika hili mtakuwa mnamwonea tu. Sasa tusionee watu. Tuwe wakweli. KAGODA, kwa taarifa nilizo nazo mimi ni state sponsored corruption.
Maoni yangu binafsi tu hayo

Hata mimi: deep down in my heart; Lowasa hahusiki katika hili.
Kinachoendelea hapa ni kile kuwa kwa vile mwanafunzi alifeli somo fulani basi mawazo ya mwalimu wake ni kuwa yeye nifelia kila somo.
 
SteveD,

Nina hakika Kuhani means no harm na anajaribu tu kugonganisha vichwa - after all he is lucky to have the curiosity of a cat - which is not a bad thing. We are often reminded that at the frontiers of knowledge, it is the difference in the thinking that points the way. Kuhani is definitely having a field day - remember it is a weekend - I only hope he has the lives of the same cat 🙂

Mag3

Unajua kina SteveD na kina TanzaniaNjema wanachohofia ni kupoteza watu kama Zitto kwenye jamvi kwa kuwa wanakuwa lambasted wakija. It's a misguided fear for any number of reasons.

Kwanza, the more fearful the forum the more formidable and credible it is. Ukiangalia hata discussion forums kama vile Meet the Press, zinaogopwa kama ukoma lakini hiyo ndio sababu zinaheshimika. Na mtu hajawa kiongozi Marekani kama hajaweza kufaulu acid test ya Meet the Press. Same here. Watakaoogopa kuja hapa ni vilazas in the first place, and we can do without them. Ok ?

Furthermore, the Zitto's of the world need JF no less than we need them. Ok ? They pick up an idea or two when they come here and the ideas end up in Parliament. Tena labda wangeanza kulipa royalties na ku-cite references za mawazo wanayoyapata JF! Kwa hiyo sidhani Zitto ataanza kuogopa kuja hapa. We need him, he needs us, OK ?

And then, tukisema viongozi watakaokuja hapa tuwe tunawalea lea ili wasije kimbia tutakuwa wanafiki, wazandiki na wazembe. Yani tuwe tunapiga kelele humu weee halafu wakija kujibu tuwapeteshe na kuwalea lea ? No pal, include me out!
 
Zitto,

Nyaraka zako zinaweza kabisa kuwa ziko 80% accurate na hiyo 20% ambayo huna ndiyo hiyo inayomuingiza Lowassa katika Kagoda. Haya mambo si rahisi kufikia conclusion bila ya kuwa na ushahidi uliokamilika.
Hata kama unamchukia Lowasa ,Zito ansema ukweli.Inawezekana kumbukumbu zako ni ndogo unajua kwamba wizi huu umefanyika kambla JK na EL hawajashika post hizo.sasa ushiriki wao ulikwa vipi wakati hawakuwa na maamuzi kuhusu benki kuu.
 
Hata kama unamchukia Lowasa ,Zito ansema ukweli.Inawezekana kumbukumbu zako ni ndogo unajua kwamba wizi huu umefanyika kambla JK na EL hawajashika post hizo.sasa ushiriki wao ulikwa vipi wakati hawakuwa na maamuzi kuhusu benki kuu.

Sina chuki na mtu yeyote yule bali ninachotaka kuona ni ushahidi unawekwa bayana bila woga wala kificho na wahusika wote wanafikishwa kunako husika na sheria ziachwe zifuate mkondo wake bila upendeleo wowote. Hatuwezi kukaa chini na kujadili mambo mbali mbali ndani ya nchi yetu bila kuitwa wenye chuki binafsi au wachochezi!!!! ili kuwatisha watu na kuwapa mafisadi nafasi ya kuendelea kupeta!!! Mwe!!! kazi kweli kweli!!!
 
Mag3

Unajua kina SteveD na kina TanzaniaNjema wanachohofia ni kupoteza watu kama Zitto kwenye jamvi kwa kuwa wanakuwa lambasted wakija. It's a misguided fear for any number of reasons.

Kwanza, the more fearful the forum the more formidable and credible it is. Ukiangalia hata discussion forums kama vile Meet the Press, zinaogopwa kama ukoma lakini hiyo ndio sababu zinaheshimika. Na mtu hajawa kiongozi Marekani kama hajaweza kufaulu acid test ya Meet the Press. Same here. Watakaoogopa kuja hapa ni vilazas in the first place, and we can do without them. Ok ?

Furthermore, the Zitto's of the world need JF no less than we need them. Ok ? They pick up an idea or two when they come here and the ideas end up in Parliament. Tena labda wangeanza kulipa royalties na ku-cite references za mawazo wanayoyapata JF! Kwa hiyo sidhani Zitto ataanza kuogopa kuja hapa. We need him, he needs us, OK ?

And then, tukisema viongozi watakaokuja hapa tuwe tunawalea lea ili wasije kimbia tutakuwa wanafiki, wazandiki na wazembe. Yani tuwe tunapiga kelele humu weee halafu wakija kujibu tuwapeteshe na kuwalea lea ? No pal, include me out!
Kuhani,
But don't you think that you have decided to judge Zitto prematurely na kumweka kwenye kundi la "cachet" etc?
 
Mh. Zitto, hilo swala la viongozi kuandika ni la muhimu sana. Nakumbuka Mkjj alimhoji SAS kuhusiana na kuandika biography yake... kama sikosei alisema analifikiria hilo jambo... ni kitambo sasa.

Maendeleo Tz na nchi nyingi Africa bila kuwa na documented evidence ya mawazo ya viongozi wetu ni kazi ngumu. Wenzetu hata wanajeshi wao wakiwa kwenye frontlines bado wanaandika progress za mapigano.... Yaani mwaka huu 2008 bado waweza kusoma mawazo ya mpiganaji aliyeshiriki Wild wild west, WWI, Trafalga battle n.k. Wakati sisi viongozi tena wa ngazi za juu kabisa hawana hata walichokiandika mpaka mauti zinawakuta... jamani tutafika kweli... bora hata ya wewe na baadhi ya wachache walioamua kushiriki kwenye majamvi kama haya... at least that way, mawazo yenu yatabakia yakijulikana katika jamii for generations to come...
Shukrani.

SteveD.
Kipindi cha mwisho cha maisha ya Mwalimu, Prof. Haruoub Othman aliwahi kupata baraka za Mwalimu ili aandike biography ya Mwalimu. Bahati mbaya Mwalimu akafariki kabla hilo halijafanyika.

Wakati mwingine umri ni kikwazo cha wazee waliokuwa viongozi kuweza kuandika historia yao ama ya nchi yetu, lakini wakifuatwa simulizi za kusisimua na maelezo yenye manufaa yatabubujika. Wanahitajika vijana wenye nia njema ya kutaka kuwepo kumbukumbu kuhusu viongozi wa taifa letu na historia ya Taifa kwa ujumla wajitokeze kufanya kazi hiyo, tena wajitokeze mapema.

Naamini wakati ule ni Watanzania wachache sana waliowaza kwamba Mwalimu atafariki kama walikuwepo basi walikuwa ni 'wachawi'. Katika vichwa vya wananchi wengi, wazo kwamba iko siku Mwalimu atafariki halikuwepo kabisa! Tumeishapata fundisho kwamba hakuna binadamu aliye immortal. Kwa maana hiyo, ni changamoto kwa wazee wenye nguvu bado na vijana wenye ujuzi na uwezo wa kutafiti na kuandika waanze kuifanya kazi hiyo kwa manufaa ya taifa letu. Wahenga walisema linalowezekana leo lisingoje kesho!
 
Tuombe Mungu haki itendeke ili KAGODA ipelekwe Mahakamani......"Haki ya Mungu" kila kitu kitakuwa wazi..Unajua huko Juu wanalaumiana nani karuhusu kesi ya EPA iende Mahakamani? Ile Hesabu waliyofikiria imetoa jibu Tofauti!! Kuna watumishi wakubwa serikalini wakiongozwa na Martin Lumbaga ni lazima wawajibike....Hapo awali tulisema Kagoda ni kubwa kuliko RA na sasa ukubwa wake utaonekana...iondolewe immunity kwa baadhi ya watu ili watu wote wafike Mahakamani bila kujali nyadhifa zao.....Hali ikienda hivi ni lazima uitishwe Uchaguzi mwingine(serikali itavunjwa)...kweli nani atapona kwenye walioko madarakani? Wapo wanaotaka kutoa ushahidi wa kubeba pesa za kugawa kwenye Uchaguzi wa 2005...Hivi Kikwete hakujua kuwa EPA itamlipua na yeye? atatoka kwa mtindo gani katika Mtego huu? Hiyo ni KAGODA tu.Bado Deep Green,Meremeta na Tangold kampuni hizo zote serikali ina mikono yake!!
 
Politics as usual..Nimeuliza swali uka ignore...Kuhani amekulima swali lile lile na bado unakwepa kisiasa.
Mfano niliotowa kuhusiana na kauli ya usalama wa Taifa ni similar in terms of ambiguity.
Unaposema state allowed the deal na huku ukisema Lowassa hakuwakilisha state bali chama ndipo naposhindwa kuelewa.
Kwenye execution ya hiyo deal si ni lazima kuna procedures za ku approve?
Unapothubutu kusema EL hakuhusika hata kidogo yeye binafsi una maana gani?
Kuna ubinafsi na u state hapo na sielewi vigezo vyako vya kumetetea EL na kumpakazia huyo state peke yake.

Kwenye masuala ya kuruhusu wizi wa fedha BOT kwa kufoji nyaraka ni hatua ipi inamwingiza waziri mkuu katika kuweka sahihi, kuandika dokezo au kutoa amri ya kimadaraka kuamuru malipo yapitishwe bila mizengwe.

Kwamba alijua fedha inaibiwa ili kusaidia CCM ishinde hilo sina ubishi.

Ukisikia taarifa kwamba " serikali imetoa uamuzi fulani" haina maana vyombo vyote vya serikali Polisi Jeshi,Bunge,Mahakama na Ofisi ya Rais vimefikia uamuzi na kutoa tamko la pamoja.

Vingunge wachache wasiofika 10 wana uwezo wa kukaa na kutoa uamuzi kama chama na kuamuru waziri muhusika atoe tamko kupitia redio ya taifa kuhusu maamuzi mapya ya serikali.

Vivyo hivyo wizi huu ulipikwa ndani ya chama na kubarikiwa kisha kondoo wa kafara wakapigwa shinikizo kuufanikisha. Wale wenye dhambi sasa wanarudi na kujaribu kumchinja kondoo aliyekufa ili kuondoa dhambi ile ile. Kafara siku haiendeshwi hivyo.
Richmond kondoo wake.
EPA kondoo wake, kama kondoo hawapatikani wahusika jiandaeni kufa kifo cha dhambi ni halali yenu.

State sponsered, State house, State ni maneno tata kama unatafuta utata.
Fedha tunajua kwa kiwango kikubwa ziliishia kugharimia uchaguzi wa CCM kwa kuingizwa kwenye mifuko binafsi ya viongozi wa CCM na siyo account za CCM kama chama, na nyingine ziliishia kwenye UFUKSA.
Tukisema State sponsered katika nchi ambayo chama tawala ni dola pia kiwingu cha watu kinapungua na kuacha kundi lisilozidi watu 12 kujibu maswali kuhusu Kagoda.

Naomba wana CCM, wapenzi wa CCM mashabiki na waganga wao wa jadi wasituvuruge, watulie kama wananyolewa kwa wembe.
Hii issue bado mbichi kabisa, tena kwa taarifa yenu mwakani ni lazima iingie rasmi mezani kwa Obama, hapo mtajua kama Mharage ni mboga au mlo kamili.
Jiandaeni kuva vilemba vya manyasi na mabua ya mpunga. Nahii zenu nyie(kumradhi).
 
Naomba wana CCM, wapenzi wa CCM mashabiki na waganga wao wa jadi wasituvuruge, watulie kama wananyolewa kwa wembe.
Hii issue bado mbichi kabisa, mwakani nilazima iingie rasmi mezani kwa Obama.
Jiandaeni kuva vilema vya manysi na mabua ya mpunga, nahii zenu nyie(kumradhi).
Khee usinchekshe. tulia wewe kama unanyolewa. kwani wewe si mtu wa kunyolewa tu. Njoo Zenji. Kikwajuni Juu.
 
Watu kama kina Zitto ni wapinzani njaa waliojawa na tamaa tu ya kuwa na madaraka hawana chochote na wala msikubali kudanganyika. Hawa siku zote wanailaumu serikali iliyoko madarakani kwa vitendo vyake kadhaa vya kuwanyima wananchi taarifa za msingi zinazohusu uendeshwaji wa nchi, leo hii Zitto anakuja hapa na kuwalingishia wanaJF kuwa ana taarifa za msingi ambazo wanatamani kuzijua lakini hatawapa!!! Sasa kama hauko tayari kusema unayoyajua ni nani alikwambia uanze kutoa fununu humu, watu wazima hawataki fununu wanataka taarifa kamili, na kama huwezi kutoa hiyo taarifa tutakuchukulia kuwa taarifa hiyo hauna. Huu upinzani njaa njaa ndio unaosababisha ukiritimba wote ulioko Tanzania. Sasa wewe Zitto hutoi hizo taarifa hapa in full kwa kumuogopa nani???anhaa kumbe na wewe huwa unaogopa kutoa taarifa za mambo muhimu kwa wananchi! Je siku ukiwa waziri unaweza kutoa siri za ufisadi unaofanywa na viongozi wa juu wa nchi??? kwa ujumla, wewe na the other so called wapinzani mnakera na kuchefua kwa unafiki wenu.
 
Back
Top Bottom