Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

Kagoda Agriculture Ltd: Another BOT scandal

wakuu,msininukuu vibaya mkaniangushia huo mziki wa RA na Manji mimi jamani..sio mimi!
labda nipo nyuma mwenzenu,nielimisheni,[COLOR="Yellow[B]"]hivi kati ya waliochota vijisenti vya EPA ni mdudu Kagoda tu aliyebaki kufikishwa mahakamani[/B]?kwanini Mangi ataje hiyo tu?[/COLOR]na nani kati yetu asiyejua mtafaruku wa hao watu wawili?kwanini isi'raise question hapa kama ni kweli anapinga ufisadi kama tunavyolia wengi ama anaingiza personal interests kwenye hili suala?
.....ni hayo tu!


Semjato, Usimlaumu Mengi, yeye kataja Kagoda, wewe na mimi tutaje wengine. Maana si jukumu lake peke yake kutaja na kukemea mafisadi, bali ni jukumu letu wote.
 
...haya jamani,ngoja na mi nitafute adui yangu kati ya hawa wezi ambao hawajakanyaga Kisutu nimuulize Mh. mmoja ntakaempata kwanini hajafika mahakamani mpaka sasa!nimeliona pia kwenye magazeti ya guardian leo suala lilivyopewa kipaumbele cha kutosha...idumu vita dhidi ya mafisadi.
 
duh,naona Mangi anashindwa kabisa kuificha vita yake na Manji....kaaaz kwelikweli

Sidhani hivyo Mkuu, bali he smells something. Kagoda imekuwa ni wimbo kwa mwaka huu wote na bado Wakuu wa nchi wamebanisha kimya! Kwani hiyo Kagoda ni Mzimu gani wa kuogopa, kunani Kagoda? Hiyo inatufanya WaTZ tuwe na hofu na huo mzimu wa Kagoda kwa nini unaogopwa namna hiyo na tuna sababu ya kuhoji na kutaka kujua na ndo maana Mengi amehoji pia, kila MTz anataka kujua inashindikana vipi kushindwa kuwafikisha Wamiliki wa Kagoda kortini.

Isijekuwa tunaogapa vivuli vyetu wenyewe. Sisi hatujali kama Kagoda ni Manji au la tunachotaka na kuhoji ni kwa nini KAGODA hakamatwi.
 
Ibrah na wakuu wengine..heshima mbele!
Mi sikatai kabisa mangi kukomalia kama tufanyavyo wote wezi wa hela zetu wafikishwe kwa Pilato wote,yupo sahihi...ila kuwataja Kagoda pekee na historia ya matukio kadhaa ya sio muda mrefu sana uliopita baina ya mmoja wa wamiliki/wahusika wa huyo mdudu kagoda na bwana mangi ndio inayonipa mashaka kama kweli tunakemea kitu kimoja hapa.Nahisi mangi kwa upande mwingine anatafuta kuungwa mkono kunako vita yake binafsi na huyu mwizi ambayo haihusishi maslahi ya Taifa and therefore haituhusu kivile.
ni mashaka tu niliyonayo,naweza kutokuwa sahihi pia...
 
Ibrah na wakuu wengine..heshima mbele!
Mi sikatai kabisa mangi kukomalia kama tufanyavyo wote wezi wa hela zetu wafikishwe kwa Pilato wote,yupo sahihi...ila kuwataja Kagoda pekee na historia ya matukio kadhaa ya sio muda mrefu sana uliopita baina ya mmoja wa wamiliki/wahusika wa huyo mdudu kagoda na bwana mangi ndio inayonipa mashaka kama kweli tunakemea kitu kimoja hapa.Nahisi mangi kwa upande mwingine anatafuta kuungwa mkono kunako vita yake binafsi na huyu mwizi ambayo haihusishi maslahi ya Taifa and therefore haituhusu kivile.
ni mashaka tu niliyonayo,naweza kutokuwa sahihi pia...

Waweza kuwa sawa lakini Kagoda ndiye papa mkubwa aliyebaki katika Kesi ya EPA na ndiye tuansubiri kumwana akiburuzwa kortini. Kama kuna wengine wataje au wengine watawataja na si lazima awe Mengi (yawezekana Mengi hawajui kama mimi).
 
DPP atakiwa atoboe siri ya vigogo Kagoda

2008-11-19 10:21:33
Na Joseph Mwendapole

Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania, (CTI), limemwomba Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kuharakisha kuyafanyia kazi majalada ya watu wote wanaotuhumiwa kuhusika kuiba mabilioni ya fedha kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Kadhalika, shirikisho hilo limemtaka DPP aweke wazi nani mmiliki wa Kampuni ya Kagoda Agriculture Ltd, inayodaiwa kuhusika katika wizi huo.

Ushauri huo ulitolewa jana na Mwenyekiti wa CTI, Reginald Mengi, wakati wa uzinduzi wa miaka 10 ya kuanzishwa kwa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) na siku ya Viwanda Afrika.

Mengi alikuwa akitoa neno la shukrani kwa Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, ambaye alikuwa mgeni rasmi.

Mengi alisema rushwa ni adui mkubwa kwa ustawi wa viwanda nchini hivyo jitihada zinahitajika kuwashughulikia wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Alimwomba Makamu wa Rais kufikisha salamu za wenye viwanda kwa Rais Jakaya Kikwete kuwa wanafurahishwa na jitihada anazofanya kuwashughulikia watu wanaodaiwa kuhusika na wizi katika EPA.

``Sisi tulidhani waliorejesha fedha atawasamehe, lakini yeye ameagiza waliorejesha na wasiorejesha mafaili yao yaende kwa DPP huu ndio utawala wa Sheria ambao wenye viwanda tunautaka,`` alisema Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP na pia Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Afrika Mashariki (EABC).

Alisema kwa uzoefu alionao DPP wanaamini kuwa atayafanyia kazi kwa haraka ili watakaobainika kuhusika wachukuliwe hatua za kisheria.

``Ombi lingine kwa DPP ni kwamba tunataka atueleze huyu Kagoda ni kitu gani, kwa kweli CTI na wananchi wana shauku ya kujua huyu ni mdudu gani,`` alisema Mengi.

Mengi alimshukuru Dk. Shein kwa kuhudhuria hafla hiyo na kwamba ameonyesha kwa vitendo namna anavyowajali watu wa sekta binafsi.

Alisema kuuza malighafi nje ni sawa na kuuza ajira nje ya nchi kwani viwanda vya ndani haviwezi kukua.

``Ni kweli kama ulivyotushauri tujivunie bidhaa zetu kwani mtu usipojivunia chako hakuna mtu atakayejivunia chako,`` alisema Mengi.

Aidha, alimsifu Mkurugenzi wa CTI, Christine Kilindu, kuwa amekuwa nguzo muhimu katika maendeleo ya taasisi hiyo.

Alimwagia sifa pia Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania, Ester Mkwizu, kuwa ni mchapakazi na ameonyesha uwezo mkubwa katika kuendesha taasisi hiyo.

Mpaka sasa watuhumiwa 20 wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam kujibu mashitaka mbalimbali ya wizi wa fedha za EPA Sh. bilioni 133.

Hivi kribuni, DPP, Eliezer Feleshi, alisema kazi ya kuwashughulikia watuhumiwa wengine wa kashfa hiyo bado inaendelea.

Alisema majalada yote yanayohusu watuhumiwa wa EPA yaliyowasilishwa katika ofisi yake yanaendelea kufanyiwa kazi ikiwa ni pamoja na kuyafanyia uchunguzi zaidi kama ilivyoelekezwa na vyombo vya dola.

Makampuni 22 yaliyovuna mabilioni ya EPA kwa mujibu wa taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, aliyoitoa Januari 9, mwaka huu ni Bencon International Ltd of Tanzania, VB& Associates Ltd, Bina Resorts Ltd, Venus Hotels Ltd, Njake hotels and Tours Ltd, Maltan Mining Company na Money Planners and Consult.

Makampuni mengine kwa Mujibu wa Luhanjo ni Bora Hotels and Apartments Ltd, B.V Holdings Ltd, Ndovu Soaps Ltd, Navy Cuts Tobacco Ltd, Changanyikeni Residential Complex, Kagoda Agriculture Ltd, G&T International Ltd, Excellent Services Ltd, Mibale farm Liquidity Services Ltd, Clayton Marketing Ltd, M/S Rastash, Malegesi Law Chambers (Advocates), Kiloloma and Brothers na Karnel Ltd.

Naye Hellen Mwango anaripoti kuwa idadi ya washitakiwa wanaokabiliwa na kesi ya wizi wa Sh. bilioni 133 kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) waliopata dhamana imeongezeka na kufikia 13.

Idadi hiyo iliongezeka jana kutoka watuhumiwa 12 baada ya Kaimu Mkurugenzi wa Madeni katika BoT, Ester Komu, kuachiwa na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

Washitakiwa wengine saba bado wako rumande kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Komu aliachiwa kwa dhamana na Hakimu Mkazi, Victoria Nongwa, baada ya kutimiza masharti na kujidhamini kwa hati yenye mali ya thamani ya Sh. milioni 450 na wadhamini wawili wanaofanya kazi katika taasisi zinazojulikana.

Hakimu Nongwa alisema mshitakiwa huyo yuko nje kwa dhamana ya masharti hayo na kwamba wadhamini wahakikishe anafika mahakamani kusikiliza kesi dhidi yake.

Aliongeza kuwa endapo watakuwa na wasiwasi wa mshitakiwa kutoroka, wana haki ya kufuta udhamini dhidi yake.

Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa mshitakiwa akiwa mwajiriwa na kwa kutumia cheo chake alifanya uzembe na kusababisha wizi wa Sh. 3,868,805,737.13 mali ya BoT.

Ilidaiwa kuwa mshitakiwa na wenzake walighushi hati za kuhamisha mali kwa jina la kampuni ya Mwibare Farm ya Tanzania na Lakshmi Textile Mills Ltd ya Mumbai, India.

Mbali na Komu, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni, Rajabu Maranda, Bosco Ndimbo na Sophia Joseph.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Novemba 21, mwaka huu itakapotajwa tena.

Wakati huohuo, kesi inayowakabili washitakiwa Johnson Lukaza na Mwesiga Lukaza jana ilitajwa na kuaihirishwa hadi Januari 14, mwakani itakaposikilizwa kwa awali.

Johnson na Mwesiga wanadaiwa kuwa kati ya mwaka 2003 na 2005 walighushi, kuiba na kujipatia Sh. 6,300,402,224.64 kutoka BoT baada ya kudanganya kuwa kampuni ya Kernel Ltd ya Tanzania imehamishiwa deni na Kampuni ya Marubeni Corporation ya Japan.

Watuhumiwa hao wawili waliachiwa kwa dhamana na mahakama hiyo Ijumaa iliyopita.

Mbali na Mahakama ya Kisutu kuweka wazi dhamana kwa washitakiwa wa kesi ya EPA watakaotimiza masharti, pia inawataka kuwasilisha hati za kusafiria mahakamani, kutokutoka nje ya mkoa wa Dar es Salaam bila kibali cha mahakama hiyo pamoja na kuripoti Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi.

SOURCE: Nipashe
 
This EPA will cost them, kuna maajabu makubwa sana yatatokea na huenda watu wasiamini kitakachokuwa kinaendelea kwani wapo wazee wawili ambao wanahusika moja kwa moja na hawa jamaa na ndio waliomwambia Balali ali[pe pesa hizo kwani duniani kote ndivyo wanavyofanya sasa siku kesi zikianza kuna maajabu mengi sana subirini na hamtaamini kuwa yatakayowasilishwa mbele ya mahakama ni ukweli .
 
Watanzania bana hutawajua tu.
Mtu akisema tunataka kujua Kagoda ni ya nani wao wanakuja na vita ya Mengi na sijui na nani,akikaa kimya wanakuja na huu ukimya sijui wa nani unatisha.Yani wako as if wao haya mambo hayawahusu na wako tu pembeni kusikilizia nani kasema nini huku wakijua ukweli.

Sasa wewe unaejua hii kagoda ni ya nani umefanya nini au umesaidia nini dhidi ya vita hii ya mafisadi.Nyie mnataka Mengi aseme yoote halafu muanze tena yeye anasema yote hayo kwa kujibu wa nani.hamkawii nyie eti.Du
Bongo Daresalama
 
oooh nchi kiongozi wake anapokuwa mtumwa ni hatari maana mtumwa amezoea kukandamizwa akipewa nafasi atakula hata mtaji msitegemee kuwa atawataja wahusika wa kagoda hiyo ni sawa kumwambia mtoto ataje kama baba yake ni mwizi

asante kwa issue hii nzuri
 
hivi huyo Mengi amesahau hata yeye ni mmoja wa walioyoifilisi iliyokuwa Benki ya Nyumba tanzania??? atulie na aendeshe vita yake na Manji kimya kimya.
 
Inaonesha ugomvi uliopo hapa ni baab kubwa! Tusubiri tuone!
 
Sipendi kuona watu wanakwepesha hoja ya wizi wa Kagoda Agriculture Ltd na kuifanya ugomvi binafsi wa Manji na Mengi, huu ni uvivu wa kufikiri na kukwepa majukumu. Mengi alishajitetea siku nyingi kwamba yeye na Manji biashara zao haziingiliani kabisa, sasa 'conflict of interest' ya Manji na Mengi inatoka wapi? Kesi yao ilishasuluhishwa na mahakama kuu na hukumu ilitoka, sasa nyie mnaodai bado kuna bifu katika ya Manji na Mengi mna 'justifications' zipi? Ingekuwa wanafanya biashara moja tungesema labda wanagombania wateja! Mengi anapigia kelele suala la Kagoda kwa sababu ndio walioiba pesa nyingi za EPA kuliko kampuni yoyote ile na hawajafikishwa mahakamani mpaka leo, ndio sababu anahoji ukimya huo! Hata mimi napigia kelele suala la Kagoda kwa sababu zile zile za Mengi, sasa kama na nyie wachangiaji mnaomtetea Manji hapa JF ni wafaidika wa wizi wa Kagoda mjue Kisutu inawangoja.
 
Mengi anazungumza kwa niaba ya waTanzania wote kuwa vita dhidi ya hawa mafisadi ni lazima iwe kamili na sio kukamata dagaa na kuwaacha Kambale. Hawa mafisadi ni genge la "MAFIA" ambao kama halitateketezwa litakuja kuiangamiza nchi yetu; hata waziri mkuu alikili kuwa hawa jamaa sio wakuwaendea hovyo wanaweza kuiangamiza nchi; kwahiyo ni lazima washuhulikwe wote kikamilifu hasa wale waliokaribu na viongozi wa nchi kwani wanaweza kublackmail viongozi wa juu wa Serikali.
 
Jumatatu nilisema kwamba washtakiwa wa EPA,wote,kila mmoja wao,wasamehewe. Watu wengine wakauilza,kwa nini wasamehewe,wakaniambia,"You are a ***** for making that suggestion" Lakini sasa I am told kwamba Waziri Mkuu Mstaafu Lowassa na Mbunge Rostam Aziz ndio wamiliki wakuu wa Kagoda Agric. Co.. Sasa, siyo rahisi zaidi kuwaachia huru watu kama hawa badala ya kuwapeleka Mahakamani?

Jana Slaa,Mbunge wa Chadema aliongea katika mkutano na kuwataja tena hawa wahusika wa Kagoda Co. Sijui alimtaja nani,kwa sababu haikuandikwa kwenye gazeti,ingawa ilitajwa katika mkutano. Lakini,hawa Lowassa na Rostam Aziz,ndio ambao nimesikia from a relaible source,kwamba ndio wahusika wa hii Company.

Katika hali ya namna hii,ambapo watuhumiwa wanaweza kutajwa kwenye mkutano uliohudhuriwa na watu 1000,lakini hawawezi kuandikwa katika gazeti,inaonyesha kwamba kuna mazingira ya vitisho,a clear and present danger to national security,na ingekuwa siyo jambo baya kwa watu hao,kuwa rounded up,na kupelekwa Mahakamani,so that we may all speak freely,and breathe freely again.

Halafu nimesikia Lowassa aliwahi kumfanyia wema mkubwa Ndugu Rais. Nimesikia,again,from a reliable source,kwamba siku moja Mwalimu Nyerere alimwita Nd. Jakaya Kikwete aende Msasani. Alipofika kule,Mwalimu akamwamia Ndiugu Jakaya,kwamba,"Wewe kijana,ni hodari wa kazi,ni mwanamapinduzi.....,sasa ,nenda sasa hivi,kachukue form ugombee Urais" Sasa,Ndugu Jakaya Kikwete akakatoka pale,lakini alikuwa hana fedha za kufanyia hiyo kazi. Ndipo,akaenda kwa Lowassa,na akapata hizo fedha. Nimezipata hizi habari,from a reliable source,na,nadhani,zinaeleza kwa nini hawa watu hawajapelekwa Mahakamani mpaka sasa.

In conclusion,ningependa kusema,kwamba hawa watu,kama wanapelekwa Mahakamani wapelekwe,kama wanaachiwa huru,waachiwe huru,it is all the same to me. Rais ana uwezo wa kuwapeleka Mahakani,and The President can rescind the order at any time,at any time. Wale wanaosema Rais ana uwezo wa kupeleka watu Mahakamani,lakini hana uwezo wa kuwatoa watu Mahakamani,au kuwatoa jela,hao ndio wanaotaka kuzifanya kazi hizi ziwe ngumu,au zionekani kwamba ni ngumu.

Halafu nimepita Karatu,wiki chache zilizopita,nikasikia kwamba Ndugu Lowasa,anafanya matayarisho ya kugombea Urais mwaka 2010,au 2015,na anawaambia watu wote wanaotaka kugombea Ubunge katika Bunge lijalo,wawasiliane naye wapate msaada wa fedha. Hii ni chaos,kama watu watatumia ill gotten gains kutafuta Urais. Katika Mathematics,inaitwa Chaos. Kwamba ukianza vibaya,maendleeo yako ya badaye yatakuwa mabaya.

Mwalimu Nyerere alitaka kuwasaidia waongoze nchi. Lakini baadaye aliingilia kati na kumsaidia Ndugu Mkapa. Sijui kwa nini Mwalimu alibadili mawazo yake. Labda ni kwa ajili ya maneno yao ambayo walikuwa wanyazungumza,na yaliyokuwa yanazungumzwa kuhusu wao,kwamba wanataka "kuichukua nchi",ndio maneno ambayo hata sasa utayasikia ukienda kule Karatu,kwamba "Lowasa na rafiki zake wanataka kuichukua nchi" Maneno kama haya ukiyasikia kwamba watu wanataka "kuichukua nchi",ukiyasikilza yanakuwa kama ya kifisadi.

Again,I say,haya mambo hayanihusu mimi. As far as I am concerned,hili swala kwangu mmi limekwisha,kwa sababu nimeshawafahamu hawa mafisadi,ni akina nani,and that is all I wanted. Haya mambo yajadiliwe bila kujali nani atakasirika. Yajadiliwe kama timu ya mpira inavyojadili mambo wakati wa half time,bila ya kujali nani ataudhika. Muhimu ni kuwaondoa tu watu wasiohusika kabla ya kuanza kujadiliana.
 
Jumatatu nilisema kwamba washtakiwa wa EPA,wote,kila mmoja wao,wasamehewe. Watu wengine wakauilza,kwa nini wasamehewe,wakaniambia,"You are a ***** for making that suggestion" Lakini sasa I am told kwamba Waziri Mkuu Mstaafu Lowassa na Mbunge Rostam Aziz ndio wamiliki wakuu wa Kagoda Agric. Co.. Sasa, siyo rahisi zaidi kuwaachia huru watu kama hawa badala ya kuwapeleka Mahakamani?

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Kwa taarifa nilizonazo, Lowasa kama mtu binafsi hahusiki na KAGODA. Ana matatizo yake lakini katika hili mtakuwa mnamwonea tu. Sasa tusionee watu. Tuwe wakweli. KAGODA, kwa taarifa nilizo nazo mimi ni state sponsored corruption.


Halafu nimesikia Lowassa aliwahi kumfanyia wema mkubwa Ndugu Rais. Nimesikia,again,from a reliable source,kwamba siku moja Mwalimu Nyerere alimwita Nd. Jakaya Kikwete aende Msasani. Alipofika kule,Mwalimu akamwamia Ndiugu Jakaya,kwamba,"Wewe kijana,ni hodari wa kazi,ni mwanamapinduzi.....,sasa ,nenda sasa hivi,kachukue form ugombee Urais" Sasa,Ndugu Jakaya Kikwete akakatoka pale,lakini alikuwa hana fedha za kufanyia hiyo kazi. Ndipo,akaenda kwa Lowassa,na akapata hizo fedha. Nimezipata hizi habari,from a reliable source,na,nadhani,zinaeleza kwa nini hawa watu hawajapelekwa Mahakamani mpaka sasa.

Watu wamewahi kuandika kuhusu suala hili. Kikwete hakuwa mgombea wa Mwalimu Nyerere. Mwalimu hakuwahi kumwambia Kikwete agombee. Inawezekana Mwalimu alitumia wazee wengine kutuma salamu hizo lakni sio kwa ndugu Kikwete kwenda Msasani. Ndugu Kikwete aliambiwa akachukue fomu na Mzee Mwinyi Ikulu Dar es Salaam, wakati huo Kikwete ni Waziri wa Fedha - Jenerali aliwahi kuandika kuwa Kikwete alitembea kwa mguu kwenda ikulu kupata 'amri' hiyo majira ya saa moja jioni.

In conclusion,ningependa kusema,kwamba hawa watu,kama wanapelekwa Mahakamani wapelekwe,kama wanaachiwa huru,waachiwe huru,it is all the same to me. Rais ana uwezo wa kuwapeleka Mahakani,and The President can rescind the order at any time,at any time. Wale wanaosema Rais ana uwezo wa kupeleka watu Mahakamani,lakini hana uwezo wa kuwatoa watu Mahakamani,au kuwatoa jela,hao ndio wanaotaka kuzifanya kazi hizi ziwe ngumu,au zionekani kwamba ni ngumu.

Halafu nimepita Karatu,wiki chache zilizopita,nikasikia kwamba Ndugu Lowasa,anafanya matayarisho ya kugombea Urais mwaka 2010,au 2015,na anawaambia watu wote wanaotaka kugombea Ubunge katika Bunge lijalo,wawasiliane naye wapate msaada wa fedha. Hii ni chaos,kama watu watatumia ill gotten gains kutafuta Urais. Katika Mathematics,inaitwa Chaos. Kwamba ukianza vibaya,maendleeo yako ya badaye yatakuwa mabaya.

Hili laweza kuwa kweli!

Mwalimu Nyerere alitaka kuwasaidia waongoze nchi. Lakini baadaye aliingilia kati na kumsaidia Ndugu Mkapa. Sijui kwa nini Mwalimu alibadili mawazo yake.

Agenda ya Mwalimu has always been Salim Ahmed Salim. Hajawahi kuwa na ajenda ya Lowasa wala Kikwete. Na hili ndio tatizo la Tanzania, viongozi wetu hawaandiki na wasaidizi wao hawaandiki na hivyo zinabaki speculations na rumours tu.

Labda ni kwa ajili ya maneno yao ambayo walikuwa wanyazungumza,na yaliyokuwa yanazungumzwa kuhusu wao,kwamba wanataka "kuichukua nchi",ndio maneno ambayo hata sasa utayasikia ukienda kule Karatu,kwamba "Lowasa na rafiki zake wanataka kuichukua nchi" Maneno kama haya ukiyasikia kwamba watu wanataka "kuichukua nchi",ukiyasikilza yanakuwa kama ya kifisadi.

Again,I say,haya mambo hayanihusu mimi. As far as I am concerned,hili swala kwangu mmi limekwisha,kwa sababu nimeshawafahamu hawa mafisadi,ni akina nani,and that is all I wanted. Haya mambo yajadiliwe bila kujali nani atakasirika. Yajadiliwe kama timu ya mpira inavyojadili mambo wakati wa half time,bila ya kujali nani ataudhika. Muhimu ni kuwaondoa tu watu wasiohusika kabla ya kuanza kujadiliana.

Maoni yangu binafsi tu hayo
 
Mh. Zitto, hilo swala la viongozi kuandika ni la muhimu sana. Nakumbuka Mkjj alimhoji SAS kuhusiana na kuandika biography yake... kama sikosei alisema analifikiria hilo jambo... ni kitambo sasa.

Maendeleo Tz na nchi nyingi Africa bila kuwa na documented evidence ya mawazo ya viongozi wetu ni kazi ngumu. Wenzetu hata wanajeshi wao wakiwa kwenye frontlines bado wanaandika progress za mapigano.... Yaani mwaka huu 2008 bado waweza kusoma mawazo ya mpiganaji aliyeshiriki Wild wild west, WWI, Trafalga battle n.k. Wakati sisi viongozi tena wa ngazi za juu kabisa hawana hata walichokiandika mpaka mauti zinawakuta... jamani tutafika kweli... bora hata ya wewe na baadhi ya wachache walioamua kushiriki kwenye majamvi kama haya... at least that way, mawazo yenu yatabakia yakijulikana katika jamii for generations to come...
Shukrani.

SteveD.
 
Maoni yangu binafsi tu hayo


Mkuu Zitto umesema vyema sana .Lakini sasa if that is the case kwamba the State was behind and is behind Kagoda leo watu wakimtaja Lowasa then JK hapatakuwa na kosa maana wao ndiyo walikuwa wakubwa ndani ya State ama hapa ni mimi sijaelewa ?
 
Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni. Kwa taarifa nilizonazo, Lowasa kama mtu binafsi hahusiki na KAGODA. Ana matatizo yake lakini katika hili mtakuwa mnamwonea tu. Sasa tusionee watu. Tuwe wakweli. KAGODA, kwa taarifa nilizo nazo mimi ni state sponsored corruption.

Maoni yangu binafsi tu hayo

Ndugu Zitto nina swali hapo kwenye kuhusu Kagoda kuwa State sponsored...Je kuna ufafanuzi wowote ule kuhusiana na individuals walio na majukumu ya kufanya maamuzi on behalf of the state?

Kwasababu ukisema tu kwamba ni "State sponsored" na kuishia hapo hakuna tofauti na kutumia kauli ya "Usalama wa Taifa" Bila ufafanuzi wa kuwa ni usalama wa Taifa wa aina gani huo wa kuuza nchi ama ni kina nani hao "State" waliofuja pesa za wananchi na kulitumbuliza Taifa kwenye umasikini kwasababu ya corruption.

Ama "State" haiundwi na individuals ambao ni lazima wawe held accountable in case of violations of the rules that governs the state and its people? This time corruption?

Ama inawezekana na The Head of State must have beeen involved?
Kazi ipo....Kati ya JK na EL kuna kutupiana mpira wa lawama as to who is responsible for the "State Sponsored" Corruption? This time Kagoda?
 
Ndugu Ganesh, kidogo unachanganya. Kweli unaona ni vema mafisadi waachiwe kwa sababu wao ni wazito kulio mafisadi wengine? Kwani hizo hela za kagoda zilizochotwa na serikali zilitumiwa kwa maslahi ya nani, serikali, wananchi au mafisadi? Kama zilitumiwa na mafisadi kwanini wasishughulikiwe?
Unajua tukianza kuzungumzia chaguo la mwalimu leo, wakati tayari yuko rais madarakani sijui tutakuwa tuna maana gani. Inajulikana wazi Mwalimu hakumtaka Lowassa kutokana na vitendo vyake, lakini ni Lowassa huyohuyo amekuwa PM, na madhara yake tunayaona. sasa la muhimu ni namna ya kudeal na mess na sio kuanza kujutia kupuuza aliyosema mwalimu. Hakuna sababu ya kuwasamehe mafisadi kwa kisingizio chochote, kuwalinda mafisadi ni kupalilia ufisadi. So let us deal with them and see what comes there after If it will result to chaos let it be it, as long as hatutaendelea kuwa na viongozi wa aina hiyo.
 
Mh. Zitto, hilo swala la viongozi kuandika ni la muhimu sana. Nakumbuka Mkjj alimhoji SAS kuhusiana na kuandika biography yake... kama sikosei alisema analifikiria hilo jambo... ni kitambo sasa.

Maendeleo Tz na nchi nyingi Africa bila kuwa na documented evidence ya mawazo ya viongozi wetu ni kazi ngumu. Wenzetu hata wanajeshi wao wakiwa kwenye frontlines bado wanaandika progress za mapigano.... Yaani mwaka huu 2008 bado waweza kusoma mawazo ya mpiganaji aliyeshiriki Wild wild west, WWI, Trafalga battle n.k. Wakati sisi viongozi tena wa ngazi za juu kabisa hawana hata walichokiandika mpaka mauti zinawakuta... jamani tutafika kweli... bora hata ya wewe na baadhi ya wachache walioamua kushiriki kwenye majamvi kama haya... at least that way, mawazo yenu yatabakia yakijulikana katika jamii for generations to come...
Shukrani.

SteveD.

Heshima mbele,

Jamani kumbukumbu zangu zinaonyesha kama aliwafokea wote wawili. Kwamba wamepata wapi pesa za kukodi ndeg kwenda kuchukua fomu( I stand to be corrected katika hili). Nyerere alishaona tamaa ya viongozi wetu watarajiwa. Hatukosoma alama za nyakati enzi hizo na sasa tunapata kwikwi katika kufikiri kipi ni kipi.Lowasa ndo alipigwa stop siku nyingi...I tend to feel like kwamba Usalama wa taifa wanalo faili chafu la Lowasa hilo nawaachia wadau mlione make kama watu waliopewa kupambana na kulinda uhai wa taifa ndo washukiwa wakuu tunategemea nini mwisho??

Change we believe- Maisha bora bila CCM yanawezekana.

Shadow!
 
Back
Top Bottom