Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Hao maaskofu mawazo yao yanawakilisha kundi moja la watanzania kwahiyo wasituburuze tutaingia oic kwa manufaa ya hao maaskofu na vizazi vya pia

Mkuu, mawazo yako nayo yanawakilisha kundi gani?
 
Masatu. Sensa ya 1967 inasema Waislamu 35% Wakristo 35% na wanaoamini imani za kijadi 30%.

Ni zaidi ya miaka 41 tangu sensa hiyo ya mwaka 67 na idadi ya Watanzania imeongezeka kwa kiasi kikubwa tangu 1967. Hao wanaoamini imani za kijadi naamini kabisa kwamba asilimia yao itakuwa imepungua sana.
 
Nina uhakika kwamba percent kubwa ya nchi hii ni waislamu na pia tuna haki ya kujiunga na OIC...kujiunga na OIC hakiwezi kuifanya nchi hii ya Kiislamu bali tutatambulika tu kwamba ni nchi ambaye ina waislamu wengi na imejiunga na umoja huu. Waziri Membe anachukua hatua hii kutokana na maslahi ya nchi, na pia nina uhakika kwamba referendum ikifanyika waislamu(ambaye ni majority) watashinda kwa hio tusibabaishane kwa swala ambalo ni obvious. Sisi wote tuna haki kama wananchi na tafadhali msilete udini au ukabila, tusonge mbele kama Wazawa wa nchi mmoja. UNITED WE STAND, DIVIDED WE FALL!

Kajifunze logic kwanza halaf urudi ..sawa?

Asante..
 
Mimi nashangaa hivi tulipoanzisha uhusiano na vatican nani alishauriwa.

Dah, sasa hapa kumegeuka Kariakoo au, maana kila mtu ansema linalomjia kichwani, sijui kuna mapepo hapa?

Naona mada tumeiweka pembeni..

Mi napendekeza tufanye kitu kimoja kwa manufaa ya kila mtu ..


NCHI IUZWE NA KILA RAIA APEWE URITHI WAKE ATAJIJUA MBELE KWA MBELE ..
 
Ni me google hii.

Roman Catholicism in Tanzania
From Wikipedia, the free encyclopedia
Jump to: navigation, search
This article does not cite any references or sources.
Please help improve this article by adding citations to reliable sources. Unverifiable material may be challenged and removed. (February 2007)

The Roman Catholic Church in Tanzania is part of the worldwide Roman Catholic Church, under the spiritual leadership of the Pope and curia in Rome.

There are around 9 million Catholics in the country - about a quarter of the total population. There are 31 dioceses, including 5 archdioceses:
 
mnapotezwa lengo. tarehe 31 oktoba imekaribia. watu mtatoana macho na oic
mnasahau umuhimu wa hiyo tarehe.
 
Inanikumbusha pale tulipohakikishiwa watanzania kuwa pamoja na Tsunami la kiuchumi linalozikumba nchi zilizoendelea, tusiwe na wasiwasi maana tumehakikishiwa kuwa MISAADA yetu iko pale pale! Humu namo tunataka tuingie ili tukakinge kibakuli. Lini tutaingia mahali kwa nia ya kutafuta soko na teknolojia? Halafu tunashangaa kwa nini bado tunaweka viraka kwenye kandambili zetu!
 
Hivi tunatakiwa kujiunga kwa sababu tunakubaliana na Katiba ya OIC au kwa sababu tunataka kupokea misaada ambayo tayari tunaipata kutoka kwa baadhi ya nchi ambazo ni wanachama tayari wa OIC?

Je tunaweza kujiunga na jumuiya hiyo bila kukubali Katiba yake?
 
''Kwa nini tunashikwa na uoga? Tukipewa msaada na Marekani tunaambiwa kuna mkono wa mtu, tukipewa na Iran tunaambiwa hivyo.

Niambieni mimi kama Waziri wa Mambo ya Nje niende wapi?, alihoji Membe na kumtaka mwandishi huyo amtajie japo nchi mbili duniani ambazo ni takatifu kwa asilimia mia moja ili Tanzania ijenge uhusiano nazo na iachane na nchi nyingine''-MEMBE


Ukiwa na viongozi wenye mtindio wa ubongo kama huyu, amabye uongozi wake anawaza aandike proposal gani ya kuomba msaada wapi basi tumekwisha!

Narudia uislamu usifanywe kama watoto wa ombaomba tunaowaona mabarabarani! hii ni aibu na matusi makubwa,

Hili swala ni aibu hata kuzungumzia, hivi Nyerere angeamua nchi iende sawa na dini yake tungekuwa wapi?

Kipindi cha Mwinyi-OIC!!,kipindi cha Kikwete OIC!!, hivi nyie wenzetu kulikoni? asilimia 80% ya kura zilikuwa za waislamu tu?

waberoya
 
Ina maana population ya Tanzania iko kwenye steady kuanzia mwaka 1967

Mama,
Assumption ni kwamba ukizaliwa katika familia ya Kiislamu unakuwa Mwislamu na ukizaliwa katika familia ya Kikristo unakuwa mkristo. Ingawa kuna wale waliobadilisha dini kwa hiari yao tu ukubwani lakini katika takwim sidhani hiyo italeta mabadiliko makubwa. Kwa hiyo kama tumeongezeka kutoka millioni 12 mwaka 1967 hadi millioni 41 hivi sasa logic ni kwamba tumeongezeka correspondingly, na hakujatokea mabadiiko makubwa ya kupunguza idadi ya kundi moja kulinganishwa na jengine. Unless utoe takwim kuwa Waislamu au Wakristo wamefanya kazi ya ziada kuwabadilisha wale wenye imani za kijadi wajiunge nao.
 
Mama,
Assumption ni kwamba ukizaliwa katika familia ya Kiislamu unakuwa Mwislamu na ukizaliwa katika familia ya Kikristo unakuwa mkristo. Ingawa kuna wale waliobadilisha dini kwa hiari yao tu ukubwani lakini katika takwim sidhani hiyo italeta mabadiliko makubwa. Kwa hiyo kama tumeongezeka kutoka millioni 12 mwaka 1967 hadi millioni 41 hivi sasa logic ni kwamba tumeongezeka correspondingly, na hakujatokea mabadiiko makubwa ya kupunguza idadi ya kundi moja kulinganishwa na jengine. Unless utoe takwim kuwa Waislamu au Wakristo wamefanya kazi ya ziada kuwabadilisha wale wenye imani za kijadi wajiunge nao.


vipi kuhusu kuzaliana, itakuwaje kama wakristo wamezaliana zaidi kuliko waislamu or the reverse? This percentages are provisional and not definite.
 
Habari zilizonifikia sasa hivi Maaskofu wa CCT na TEC wametoa kauli kali kuhusu kampeni ya Serikali ya Tz kuiepeleka nchi OIC na wamemtaka Membe ajiuzulu kwa kuchukua msimamo kuhusu Tanzania kujiunga na OIC. Wamemshutumu kuwa ametoa msimamo kabla Baraza la Mawaziri kukaa na kuamua kuhusu hilo.

Wakuu heshima mbele, hoja ya msingi ya hawa maaskofu ni kwamba Membe ameliruka baraza la mawaziri na kuanza kukampeni nchi yetu iingie huko OIC, hayo mengine mengi hayahusu anything na hoja ya maaskofu,

Membe ni lazima atueleze wananchi kwamba ni kwa nini sasa analilia sana kuingia huko kuna nini? Na pia atueleze wananchi faida na hasara ya kuingia huko, na akubali mbele ya public kwamba uamuzi ni wetu wananchi sio wake yeye au cabinet, halafu pia hii hoja lazima ifike bungeni.

Maaskofu walipaswa kumuuliza Membe kwanza kama huu msimamo ni wake kama mwananchi au? Maana kikatiba anayo haki kusema msimamo wake kama raia wa taifa letu. Membe apewe nafasi ili aweze ku-clarify exactly ametoa huu msimamo kwa what capacity, kukimbilia kumtaka ajiuzulu bila ya kua na uhakika ametoa vipi hayo maoni ni kushusha thamani ya kujiuzulu, period.

Membe lazima apewe due process kwanza!
 
Ni vema watu wakasome katiba na muongozo wa OIC ndiyo waje na hoja zao hapa. Inaonekana watu wengine wanapenda kuchangia hoja wakati hawana ufahamu mzuri hiyo jumuiya ya OIC.

Nina uhakika watu wakisoma watapata majibu yao na watagundua kuwa bwana mdogo Membe amelewa madaraka makubwa aliyoyapata na kuja na kauli kama hizi.

Ninaamini kuwa akiwa nje ya madaraka na au akiamua kutoa maoni yake binafsi atakuwa na msimamo tofauti kabisa.

Kwa mfano:

1. Jina - Organisation of The Islamic Conference[/B]. Tafsiri ya jina pekee lnatosha kuelewa maudhui ya jumuiya hii. Huu ni mkutano wa jumuiya ya Kiislam. Wakristo na Wapagani tunapelekwa kufanya nini huko??? Membe hajaliona hili???

JE, CHARTER YAKE INASEMAJE????

Angalia # 2, 8, 11, 12, 16,

Charter of the Organisation of the Islamic Conference

CHAPTER I

Objectives and Principles
Article 1


The objectives of the Organisation of the Islamic Conference shall be:
1. To enhance and consolidate the bonds of fraternity and solidarity among the
Member States;
2. To safeguard and protect the common interests and support the legitimate
causes of the Member States and coordinate and unify the efforts of the
Member States in view of the challenges faced by the Islamic world in
particular and the international community in general;
3. To respect the right of self-determination and non-interference in the domestic
affairs and to respect sovereignty, independence and territorial integrity of
each Member State;
4. To support the restoration of complete sovereignty and territorial integrity of
any Member State under occupation, as a result of aggression, on the basis of
international law and cooperation with the relevant international and regional
organisations;
5. To ensure active participation of the Member States in the global political,
economic and social decision-making processes to secure their common
interests;
6. To promote inter-state relations based on justice, mutual respect and good
neighbourliness to ensure global peace, security and harmony;
7. To reaffirm its support for the rights of peoples as stipulated in the UN Charter
and international law;
8. To support and empower the Palestinian people to exercise their right to selfdetermination
and establish their sovereign State with Al-Quds Al-Sharif as its
capital, while safeguarding its historic and Islamic character as well as the
Holy places therein;
9. To strengthen intra-Islamic economic and trade cooperation; in order to
achieve economic integration leading to the establishment of an Islamic
Common Market;
10. To exert efforts to achieve sustainable and comprehensive human
development and economic well-being in Member States;
11. To disseminate, promote and preserve the Islamic teachings and values based
on moderation and tolerance, promote Islamic culture and safeguard Islamic
heritage;
4
12. To protect and defend the true image of Islam, to combat defamation of Islam
and encourage dialogue among civilisations and religions;
13. To enhance and develop science and technology and encourage research and
cooperation among Member States in these fields;
14. To promote and to protect human rights and fundamental freedoms including
the rights of women, children, youth, elderly and people with special needs as
well as the preservation of Islamic family values;
15. To emphasize, protect and promote the role of the family as the natural and
fundamental unit of society;
16. To safeguard the rights, dignity and religious and cultural identity of Muslim
communities and minorities in non-Member States;
17. To promote and defend unified position on issues of common interest in the
international fora;
18. To cooperate in combating terrorism in all its forms and manifestations,
organised crime, illicit drug trafficking, corruption, money laundering and
human trafficking;
19. To cooperate and coordinate in humanitarian emergencies such as natural
disasters;
20. To promote cooperation in social, cultural and information fields among the
Member States.

PIA ANGALIA MAELEZO HAYA MACHACHE KWENYE CAPTER # IV, Items zote zinaanza na Islamic Summit????

CHAPTER IV
Islamic Summit
Article 6
The Islamic Summit is composed of Kings and Heads of State and Government of
Member States and is the supreme authority of the Organisation.
Article 7
The Islamic Summit shall deliberate, take policy decisions and provide guidance on
all issues pertaining to the realization of the objectives as provided for in the Charter
and consider other issues of concern to the Member States and the Ummah.
Article 8
1. The Islamic Summit shall convene every three years in one of the Member States.
2. The Preparation of the Agenda and all necessary arrangements for the convening
of the Summit will be done by the Council of Foreign Ministers with the
assistance of the General Secretariat.
Article 9
Extraordinary Sessions will be held, whenever the interests of Ummah warrant it, to
consider matters of vital importance to the Ummah and coordinate the policy of the
Organisation accordingly. An Extraordinary Session may be held at the
recommendation of the Council of Foreign Ministers or on the initiative of one of the
Member States or the Secretary-General, provided that such initiative obtains the
support of simple majority of the Member States.

Je, Haya yote yanahitaji elimu kubwa sana au uwe Waziri ndiyo uyaelewe????
 
hivi uungwaji au kutokuungwa mkono hoja ya kujiunga na oic imegawanyika kidini? yaani waislamu wote wa tz wanaiunga mkono na wakristo wote wanaipinga? hivi hakuna wakristo wanaounga mkono au waislamu wasiounga mkono. je hakuna ambao hawako huku wala kule?
je wale wasio waislamu wala wakristo wamesimamia wapi?

hivi msimamo wa wananchi kama niliotaja hapo juu hauwezi kuwa na impact na hizi takwimu zinazotolewa hapa jamvini?
 
hivi uungwaji au kutokuungwa mkono hoja ya kujiunga na oic imegawanyika kidini? yaani waislamu wote wa tz wanaiunga mkono na wakristo wote wanaipinga? hivi hakuna wakristo wanaounga mkono au waislamu wasiounga mkono. je hakuna ambao hawako huku wala kule?
je wale wasio waislamu wala wakristo wamesimamia wapi?

hivi msimamo wa wananchi kama niliotaja hapo juu hauwezi kuwa na impact na hizi takwimu zinazotolewa hapa jamvini?

Mimi, mmisheni, naunga mkono. Ninachopinga ni kudai kuwa si chombo cha kidini. Tuwe wazi kama alivyosema Membe, tunaenda huko kukinga kibakuli. Tujiunge, halafu baada ya miaka mitano tuone kama tutakuwa tumetoka katika huu umasikini tunaoendekeza!
 
Kujiunga au kutojiunga na jumuiya hii itokane na matwakwa ya wananchi na busara ya viongozi na sio vinginevyo. Pamoja na mazuri ambayo yapo ndani ya jumuiya hii ni vyema busara ikatumika kuona je wananchi katika makundi yao na imani zao wataendelea kuwa watanzania au kutatokea ufa. Tayari malumbano yanayoendelea yanaashiria arufu mbaya ya kujiunga. Serikali ikijiingiza sana kwenye mambo ya imani itakuja kuleta taabau baadaye. Muungano wowote ule unaohusu imani waachiwe viongozi wa dini, dhehebu liwe huru kufanya mambo yake na kikundi chochote kile duniani bila kuvunja sheria za nchi, na si serikali kuchukua nafasi ya dini.
Ni wazi chanzo cha OIC ni kueneza na kutetea imani ya kiisilamu kupitia uchumi na tamaduni, ni kweli zipo nchi nyingi zimejiunga na lazima ukubaliane na katiba ya chombo hiki sioni ubaya kama waumini wa dhehebu husika wakaungana na chombo hiki kwa manufaa ya imani na maendeleo ya waumini na washirika wake, serikali ikakaa pembeni.

Ni unafiki mkubwa wa serikali kusema itawauliza wananchi kuhusu kujiunga au kutojiunga. Ni wazi mwisilamu atakubali na wakristo watakataa kama inavyoendelea sasa. Na kuleta mijadala kama hii kwenye jamii iliyotulia na kuheshimiana ni kuazisha tafrani isiyonamaana kabisa.Huwezi kuleta maswali yenye manufaa ya kiimani kwa mtu ambaye sio wa imani husika.

Viongozi wetu lazima watumie ubongo kama bado wanao au waazime akili za watu wengine.
 
Back
Top Bottom