Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Simply hii ni akili ya madrasa shule ndogo kaongeze elimu dunia kwanza ndipo uje kujadili.
 
Kinachobainishwa hapo ni kuingiza mfumo wa mahakama ya kadhi ndani ya mfumo wenu wa Mahakama ili kusilete mgongano wa maamuzi yake na mahakama za kawaidia kama walivyoweka hata wenzenu Kenya.

Nitakupa mfano mdogo sana wa mabaraza ya ardhi ya kata na mahakama za mwanzo. haya hayaingiliani katika mamuzi sababu yamewekwa pale kisharia. Sasa kwanini unakwepa mahakama ya kadhi.

Mimi naamini wazi watakao pata hudima kwenye mahakama hizi ni raia wa Tanzania kama walivyo raia wengine wa Tz na hivyo kupunguza msongamano wa kesi nyyingi sana za madai kama talaka na miradhi katika mahakama zenu.

Suala langu hapa. Je Serikali ya JMTz ipo tayari kuwalipia wa TZ kama raia wake watakaoamua kutumia mahakama hizi kutafuta haki zao?

Fungukeni kiakili na mjitoe katika mental slavery.

Hapo kwenye nyekundu ndo umeniacha hoi,unazungumzia mahakama ya kadhi unatolea mfano mahakama ya ardhi ambayo ni secular court haina uhusiano na dini yeyote.
Jaribu kufikiri nje ya uislam uweze kuona ukweli bila chenga. Anzisheni hizo mahakama zenu,Dini ni mapenzi na hiari ya mtu,aliyechagua kuwa muislam anayo hiari ya kutumia mahakama ya kadhi kwa ajili ya yale aliyoahidiwa na allah wake,serikali haina sababu ya kumlipia kwani kwa faida au hasara yake ya maisha baada ya haya ndiyo kaamua kuwa mwislam.
 
tunachotaka ni kuingizwa ktk katiba kitendo cha kutoingiza katika katiba ni hatari kwa makadhi watakao kuwa wanaamua kesi, wanaweza kuja kufungwa endapo mtu asiporidhishwa na hukumu ya kadhi, akaenda ktk mahamaka za kisecular, hii ni hatari hata mimi siungi mkono mahakama kuanzishwa bila kutambuliwa na KATIBA, Lete Maandamano.
 
Ingawa waswahili husema ASIYEJUA MAANA USIMFUNZE MAANA lakini mimi nitavunja mwiko huo kwa kukujuza.

Mahakama ya Ardhi inashughulikia masuala yanayohusiana na mambo ya ardhi tu na si vinginevyo.
Mahakama ya kadhi itashughulikia masuala ya waislam hususan mirathi, talaka n.k na si vinginevyo.
Mahakama ya Biashara halikadhalika inashughulikia masuala yanayokhusu biashara tu.

Sasa kama una hoja , karibu.
Poor thinking.....hivi ardhi ni ya dini gani.
 
Kuanzishwa mahakama y kadhi ndani ya dola n i muhimu ili ruling zake ziwe binding! Hata mabaraza ya usuluhishi ya kata yameanzishwa ndani ya dola!

Ushasema mahakama ya kadhi ni ibada. Sasa unataka nini iwe ndani ya dola ili iwe binding. Yaani ibada inapewa uhalali wake na dola/katiba ama imani ya kiroho ya muislam mwenyewe? Kama kweli mahakama ya kadhi ni ibada kama unavyodai basi maamuzi yake mtayaheshimu wenyewe bila kushurutishwa na serikali. Na by the way authority pekee inayoshangaza wataalam ni ya kidini haihitaji sanctions ili ifuatwe bali ni imani ya wahusika wa dini husika. Lakini mamlaka za kiserikali huhitaji sanctions ili watu waziheshimu. Halafu wewe unakuja na hoja dhaifu eti iwe ndani ya katiba ili iwe binding. Kwa hiyo unasema indirectly waislam hamtaiheshimu ibada ya kadhi hadi mshurutishwe na serikali?
 
bahati nzzuri sisi waislam linapokuja swala la kudai haki zetu za msingi hatuogopi kupigwa , wala kufa ikibidi... kitaeleweka tu,

utakuwepo kwenye maandamano lakn mkuu,...au jf ndio mpango mzima?
 
Tusikurupukia mambo.. nafikiri lazima inshu ziwekwe mwezani.. kwamba tunataka mahakama ya kadhi.. yes fine.. sasa je kipi kimepungua kwenye utawala uliopo kiasi kwamba tunataka jambo jingine?? na mahakama ya kadhi ni nini, inafanya kazi na nani na nini, na kama mahakama zozote zina sheria zake, je sheria za mahakama hii ni zipi kwa lipi na washtakiwa wanahukumiwaje na wapi na adhabu zake zikoje kwa nini.. Sheria za jamhuri ya muungano ambazo hukasmiwa mahakama hutungwa na Bunge, je hizi hutungwa na nani na hukasmiwa kwa nani kwa mpango upi.. mie nadhani maswali haya na mengine mengi bado hayajajibiwa na walengwa. Kusema kwamba tunataka mahakama ya Budha au ya wakristo au ya waislam, si hoja sana ni kama ushabiki tu. hoja ni kuweka inshu zote mezani, kisha jamii ikapima kipi kiwe vipi. kwa kweli.. TUACHE USHABIKI WA KIDINI. Kusema tu nataka mahakama ya kadhi kwa dini fulani bila kuweka kila kitu bayana ni ushabiki.. nami siwapendi washabiki, huongozwa na mamluki za hisia za Kiimani ambazo madhara yake huwa kwa vizazi watavyoviacha.


Na mimi sipendi kutajataja imani za watu, mara hawa waislam, wale wakristo, wale mabudha.. embu tuzungumzie matatizo yetu na uchumi wa taifa letu..
 
Ushasema mahakama ya kadhi ni ibada. Sasa unataka nini iwe ndani ya dola ili iwe binding. Yaani ibada inapewa uhalali wake na dola/katiba ama imani ya kiroho ya muislam mwenyewe? Kama kweli mahakama ya kadhi ni ibada kama unavyodai basi maamuzi yake mtayaheshimu wenyewe bila kushurutishwa na serikali. Na by the way authority pekee inayoshangaza wataalam ni ya kidini haihitaji sanctions ili ifuatwe bali ni imani ya wahusika wa dini husika. Lakini mamlaka za kiserikali huhitaji sanctions ili watu waziheshimu. Halafu wewe unakuja na hoja dhaifu eti iwe ndani ya katiba ili iwe binding. Kwa hiyo unasema indirectly waislam hamtaiheshimu ibada ya kadhi hadi mshurutishwe na serikali?
Mkuu hawa jamaa wangekuwa na uelewa angalau kidogo tu wangeelewa ulichoandika hapo juu.
Tatizo lao wanafikiri ndani ya box la uislam tu
 
hahahah.... watoto wa mamam mdooogoooo.. watoto wa mama mdogo bwana. they never fail to amaze me..... wananipa raaaaaaha. yaani kila siku watakuja na jipya.
 
Mbona imeanzishwa mahakama ya Ardhi na mahakama ya Biashara. Sasa kwanini isiwe hii ya kadhi?

Kweli wee unawaza kibarubaru. Haya ngoja nikuongezee na nyingine

1. Mahakama ya kazi (labour court)
2. Mahakama ya katiba

Nakushauri soma kisomo cha manufaa (ngumbaru) uongeze ufahamu wako.
 
Tatizo linalowasumbua waislamu ni elimu ndogo za maimamu wao hawa-judge mambo critically wanachukulia kirahisi tu na mara nyingi kwa jaziba.

Ttatizo nililolibaini huko Tanganyika kwa wakristo ni CHOYO na CHUKI dhidi ya haki za waislam. Ikiwa pamoja na kujiona wao ni first citizen na waislam ni second citizen.

Sioni sababu yoyote ya msingi na khasa ukiangalia hata wenzenu Kenya wameanzisha hivyo na ukitazama Kenya ina zaidi ya 75% ukristo ukilinganisha na tanganyhika ambao mnakaribiana kiidadi.

Kama JMT ina nia ya kweli kuanzishwa kwa mahakama hizo basi ni wajibu wao kuzifanya Ruling zake ziwe binding katika sheria za nchi ili zisilete mgongano na mahakama za kawaida.

na lazima muelewe mahakama hizo zitakuwa huru kwa kila mwenye kutaka kutuzitumia katika kutafuta haki yake na zitakuwa kwa raia wote wa TZ wanaotaka.

Poleni sana
 
Tusiwajibu kwa ukali, ni vyema tukawaeleimisha; wana matatizo makubwa ndugu zetu. Tunawapenda pia
 
Hao vijana wa kiislam wakiandamana usiku na mchana watasoma saa ngapi? Haya wasubirie sup.na disco huku vyuoni. Km si kuendelea kuukumbatia ujinga badala ya kupigania elimu ambayo ndo msingi wa maendeleo ya Taifa lolote.


wakisha-sup na ku-disco watakwambia wanafelishwa...
 
Kweli wee unawaza kibarubaru. Haya ngoja nikuongezee na nyingine

1. Mahakama ya kazi (labour court)
2. Mahakama ya katiba

Nakushauri soma kisomo cha manufaa (ngumbaru) uongeze ufahamu wako.

Nakushauri soma andiko langu lote na kuelewa nimejenga hoja gani sio kuchukua baadhi ya maneno na kujenga hoja dhaifu.

lete hoja sio kudandia train kwa mbele.
 
Mpwa kwani tatizo liko wapi endapo mtaanzisha wenyewe? ni lazima sana ianzishwe na serikali? Je kama itaanzishwa na serkali si mtakuja na hoja kuwa serikali inainglia uhuru wenu kama mnavyofanya kwa Bakwata sasa? Kuwa Bakwata haina maamuzi kwasababu ilianzishwa na serikali? tuamini lipi sasa toka kwenu? mara mnaitaka Serikali ianzishe wakati huo huo Bakwata haina maamuzi kwasababu ilianzishwa na Serkali? iweje serikali kuanzisha Bakwata iwe kosa kwenu lakini iwe safi ikianzisha Mahakama ya Kadhi ya watu wale wale wanaoipinga? Au kuna lingine zaidi ya Hilo? Na sula kwamba wakristo hawataki haki zenu na lenyewe halieleweki maana Rais Muislamu, Makamu zake ni waislamu, IGP muislamu, Mnadhimu wa Jeshi Muislam, Judge Mkuu Muislamu, Mkuu wa usalama Muislamu; so you have everything in your hand, mkristo kakaaatje hapo au anaingiaje hapo? Tumia busara kujenga hoja Mpwa
Ttatizo nililolibaini huko Tanganyika kwa wakristo ni CHOYO na CHUKI dhidi ya haki za waislam. Ikiwa pamoja na kujiona wao ni first citizen na waislam ni second citizen.

Sioni sababu yoyote ya msingi na khasa ukiangalia hata wenzenu Kenya wameanzisha hivyo na ukitazama Kenya ina zaidi ya 75% ukristo ukilinganisha na tanganyhika ambao mnakaribiana kiidadi.

Kama JMT ina nia ya kweli kuanzishwa kwa mahakama hizo basi ni wajibu wao kuzifanya Ruling zake ziwe binding katika sheria za nchi ili zisilete mgongano na mahakama za kawaida.

na lazima muelewe mahakama hizo zitakuwa huru kwa kila mwenye kutaka kutuzitumia katika kutafuta haki yake na zitakuwa kwa raia wote wa TZ wanaotaka.

Poleni sana
 
UWATAPO HAKI YAKO

Namba nawe mlimwengu, pulikiza matamko
Nikweleze neno langu, uzinduwe bongo lako
Nayo nda M'ngu si yangu, na ayani haya yako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

2
Simama uitete, usivikhofu vituko
Aliyo nayo mwendee, akupe kilicho chako
Akipinga mlemee, mwandame kulla endako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

3
Amkani mulolala,na wenye sikio koko
Isiwe mato kulola,natutizame twendako
Tuwate na kuduwala,usingizi si mashiko
Uwatapo haki yako,utaingiya motoni

4
Teteya kwa kula hali, usiche misukosuko
Siche wingi wala mali,sabilisha roho yako
Unyonge usikubali, ukaonewa kwa chako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

5
Siche kifaru na ndovu, wangazidi nguvu zako
Wapempe kwa uwekevu, unusuru haki yako
Siandame wapumbavu,kilicho chako ni chako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

6
Cha mtu hakifitiki,kikafungiwa kiliko
Huzuka kikawa hiki,kazana utwae chako
Uwatapo yako haki,fahamu ni dhara kwako
Leo na kwa Mola wako,utaingiya motoni

7
Fumbuwa unyang'arize, uone duniya yako
Bure sijiangamize,kuangalia wendako
Utatupa upoteze,wende ambapo si pako
Uwatapo haki yako,utaingiya motoni

8
Kadhalika nako pia,huko ambako sikwako
Huwezi kujitetea,wala huwi na mashiko
Basi iwaze duniya,kwani ya kale hayako
Uwatapo haki yako ,utaingiya motoni

9
Kadi tamati shairi,sitii la ongezeko
Mwanati iwa tayari, utete haki yako
Unyonge usiukiri,Jifunge ufe kwa chako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni
 
Labda nikuulize kwani mkristo akienda kudai haki yake kwa kutumia mahakama ya kadhi atakataliwa? Mbona Islamic banking huko Tz nasikia kuna wakristo wengi sana wanajiunga.

Kwanini Mkristo aende kudai haki kwenye mahakama inayohukumu kwa kutumia sheria za Kiislam? Kama unaona hii ni sawa then hakuna haja ya mahakama ya Kadhi kwani Waislam wanaweza tumia mahakama zilizopo sasa.

Mbona aulalamiki ruzuku kubwa sana kutoka Serikalini zinazopewa shule na hata vyuo na mahospitali ya taasisi za kidini kama KCMC na Bugando?

Mmeshaambiwa anzisheni shule zenu, vyuo vyenu na hospitali zenu then mkadai ruzuku. As far as I know waTanzania wa dini zote wanapata huduma sawa kutoka hizo taasisi ulizozitaja kwani sijasikia Muislam akinyimwa huduma KCMC au Bugando kwaajili ya dini yake.
 
Mimi naungana na shemeji zangu ccm hawawezi kuwafanya wajinga.serikali ya ccm isigine katiba na iwape waislamu ilichowaahidi na kama haitatoa mimi naungana na shmeji zangu na waif katika maandamano na ikizingatia ni usiku na mchana hata chadema tutakuwa tumewafunika.
Na ole wa dini yoyte inayolaani maandamano au inayofikiri kulaani.
Magamba mmeisha tumewashtukia.
Sasa tunawaomba wale waliokwishadanganywa na ubwabwa,kanga,chumvi,kofia,bukutano mje tuungane na waislamu tuwaondoe hawa matapeli wa siasa na haki za watanganyika.
 
Mpwa kwani tatizo liko wapi endapo mtaanzisha wenyewe? ni lazima sana ianzishwe na serikali? Je kama itaanzishwa na serkali si mtakuja na hoja kuwa serikali inainglia uhuru wenu kama mnavyofanya kwa Bakwata sasa? Kuwa Bakwata haina maamuzi kwasababu ilianzishwa na serikali? tuamini lipi sasa toka kwenu? mara mnaitaka Serikali ianzishe wakati huo huo Bakwata haina maamuzi kwasababu ilianzishwa na Serkali? iweje serikali kuanzisha Bakwata iwe kosa kwenu lakini iwe safi ikianzisha Mahakama ya Kadhi ya watu wale wale wanaoipinga? Au kuna lingine zaidi ya Hilo? Na sula kwamba wakristo hawataki haki zenu na lenyewe halieleweki maana Rais Muislamu, Makamu zake ni waislamu, IGP muislamu, Mnadhimu wa Jeshi Muislam, Judge Mkuu Muislamu, Mkuu wa usalama Muislamu; so you have everything in your hand, mkristo kakaaatje hapo au anaingiaje hapo? Tumia busara kujenga hoja Mpwa
Nafikiri soma mzizi wa khoja yangu.

Je waislam wakizianzisha. Je Serikali ya Muungano ipo tayari ruling zake ziwe binding na sheria za Muungano? kwani kama hawako tayari kuziweka kisheria mahakama hizo basi itakuwa ni useless na kupoteza muda kwa waislam kuanzisha chombo hicho ambacho kitakuwa hakina meno.

Kenya zimebainishwa wazi katika sheria zao za nchi yao na zimewekewa mipaka yake. Vipi Tanganyika mpo tayari. Hilo ndio suala la waislam kwa Serikali ya JMT
 
Back
Top Bottom