Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Hao vijana wa kiislam wakiandamana usiku na mchana watasoma saa ngapi? Haya wasubirie sup.na disco huku vyuoni. Km si kuendelea kuukumbatia ujinga badala ya kupigania elimu ambayo ndo msingi wa maendeleo ya Taifa lolote.
 
Uanzishwaji wa mahakama ya kadhi una uhalali wowote kua na usimamizi wa serikali wakati huo huo serikali haina dini? Mi sijaelewa hapa uhalali wake mwenye kujua zaidi afunguke basi nimuelewe vizuri
 
Kwa mujibu wa kauli ya JK, serikali haitashiriki kuanzisha Mahakama ya kadhi!
Sasa kwa namna yoyote, kuanzisha maandamano ya suala hilo ni fujo, na wahusika watastahili kuzuiliwa!
Kwanini msikae msikitini mkapanga na kuratibu mahakama hiyo?..Tafuteni hata mwekezaji basi awasaidie kama shida ni fedha!
Kuanzisha mahakama ya DINI kwa fedha za walipa kodi mchanganyiko(waislamu na wasio waislamu), wakati mahakama hiyo itawahukumu waislamu tu, hiyo ni kosa la kaburi!...tusilinganishe mahakama hii na Hospitali bana!
 
bahati nzzuri sisi waislam linapokuja swala la kudai haki zetu za msingi hatuogopi kupigwa , wala kufa ikibidi... kitaeleweka tu,
"mwembechai" ya mwaka huu atawalipua muislam mwenzenu kikwete, sio Mkapa. sijui mtachakachua vipi propaganda zenu za 'tunaonewa'.
 
Mimi kwa mtazamo wangu hawa waislamu wanapaswa kuelemishwa. Wameshaambiwa waanzishe mahakama. Hawakatazwi, lakini mahakama hiyo iwe nje ya mfumo wa serikali. Wakatoliki wana mahakama yao. Tena Hakimu alikuwa wakati huo paroko wa kipawa, Padre Kimario ambaye sasa ni Askofu wa Same. Anglikana wanayo mahakama na waruteli wanayo. Sina uhakika makanisa ya kakobe na mwingira. Sasa ili mahakama ya kadhi iwekwe kwenye katiba basi, ziwekwe zote. Mie nawashauri waanzishe kwanza ili yale mapungufu ya kutokuwemo kwenye katiba yaonekane.
 
"mwembechai" ya mwaka huu atawalipua muislam mwenzenu kikwete, sio Mkapa. sijui mtachakachua vipi propaganda zenu za 'tunaonewa'.
You are wrong. Mwembechai ilisimamiwa na ustaadh Yusufu Makamba akiwa mkuu wa mkoa wa DSM (rais wa DSM ktk lugha ya mtazamo), Kama unafahamu hierarchy za kiserikali huyu alikuwa ni nani ktk kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa. Nadhani jibu utakuwa umelipata sawa bin sawia.
 
wanataka waingie kwenye payroll ya serikali...mahakim wanamenyeka miaka kibao kusomea..eti wanataka waitwe mahakimu bila shule,..duh!!
 
Labda mimi sijaelewa jamani, kwani nani kawanyima kuanzisha mahakama? si wameambiwa waanzishe kwa taratibu zao? au hio content ya habari sijaelewa? au wanatafuta sababu ya kuhalalisha uovu wao? aliesema hivyo si muislam mwenzao? au ni "kafiri"? Mbona ndugu zangu wanakosa msimamo? nani kawanyima mahakama? mmh tuone sasa Rais Muislam, IGP muislam, Judge Mkuu muislamu, makam wa Rais wa kwanza na wa pili waislam, wakurugenzi wa idara nyeti waislam! Mahakama ya kadhi imegoma...kuna tatizo, si bure. Watulie sasa
 
JK keshasema waislam mnaweza kuanzisha mahakama ya kadhi kwa utaratibu wenu ndani ya dini yenu, kwa gharama zenu na kuzisimamia nyie wenyewe na sio serikali. Kwa kuwa mahakama hiyo ni ya kidini na itatatua mambo yenu ndani ya dini yenu (Ndoa, Talaka, Wakfu, Mirathi, Urithi) na serikali ya Tanzania haina dini. Hii ni kutokana na utafiti & ushauri ambao serikali imeupata kutoka kwa wataalam wa kisheria (za kawaida& kiislam). Sasa hili la hawa waislam kutaka serikali ndio iwaanzishie, izisimamie & inziendeshe mahakama za kadhi, linaleta utata mkubwa, nina uhakika kuna jambo lilikuwa limejificha nyuma ya mpango wa kudai mahakama ya kadhi.

Nina hamu kubwa kumsikia Shekh mkuu Mufti Simba akitoa kauli ya kupinga au kuunga mkono mpango huu, kwa kuwa mara nyingi amekuwa akiwabeza wapinzani wanaoandamana dhidi ya utawala wa JK, akidai kuwa JK anaandamwa kwa kuwa tu ni muislam na huku akiwahamasisha waislam wamuunge mkono JK kwa kuwa ni muislam mwenzao!!
 
kupenda vya bure. Badala ya kukusanyana ili waandamane wangekusanyana wachangishane Pesa na kuandaa mkakati wa Kuanzisha mahakama yao.
 
Nadhani waislamu kwa hili wameshindwa kusoma alama za nyakati. Wanajazana propaganda za kiharifu na kuona kana kwamba hii mahakama itapunguza ukali wa maisha? au itapunguza mgao wa umeme? mbona wakatoliki wana mahakama yao tena ipo kurasini na huwa hawapigi kelele, pia mbona serikali yetu haina dini kwa nini ianzishe hii kitu, nadhani kwa hili waislamu wanaolisimamia kamwe kwa Tanzania nasema halitawezekana hata siku moja!!!
 
Mimi kwa mtazamo wangu hawa waislamu wanapaswa kuelemishwa. Wameshaambiwa waanzishe mahakama. Hawakatazwi, lakini mahakama hiyo iwe nje ya mfumo wa serikali. Wakatoliki wana mahakama yao. Tena Hakimu alikuwa wakati huo paroko wa kipawa, Padre Kimario ambaye sasa ni Askofu wa Same. Anglikana wanayo mahakama na waruteli wanayo. Sina uhakika makanisa ya kakobe na mwingira. Sasa ili mahakama ya kadhi iwekwe kwenye katiba basi, ziwekwe zote. Mie nawashauri waanzishe kwanza ili yale mapungufu ya kutokuwemo kwenye katiba yaonekane.

Hili ndio tatizo kubwa, wanadhani taratibu za ibada za kiislamu zi aweza kuwa sawa na za kwao. Kwanza kwa wakristo sheria si muhimu! Munadai mutaokolewa kwa neema au mtu fulani kutundikwa msalabani! No wonder wakristo hawana sheria madhubuti za kuzifuata. Kwa waislamu kuhukumiwa nje mwa sheria za Muumba ni kufur, na kunamtoa mtu kwenye uisilamu wake. Hivyo kama katiba inatoa uhuru wa kuabudu..kwa waislamu uhuru huo ni mpana zaidi ya kupiga gitaa! Hili siamini kama mnaweza kulielewa!.

Kuanzishwa mahakama y kadhi ndani ya dola n i muhimu ili ruling zake ziwe binding! Hata mabaraza ya usuluhishi ya kata yameanzishwa ndani ya dola!

Kama vipi tufuate ile sera ya CHADEMA, tugawane majimbo, wengine waanzishe hizo mahakama wengine wasianzishe kama ilivyo NIGERIA..
Hii nchi yetu wote na hatuwezi kulazimishwa kufuata mila za kiyahudi!
 
Kwenda shule ni muhimu
hawa jamaa waislam wanataka mahakama ya kadhi na wanajua serikali haina dini
labda wanataka na sisi wakristo tudai mahakama yetu??
Kuna mambo mengi ya kushughulikia kipindi hiki kuliko ili.
 
Uanzishwaji wa mahakama ya kadhi una uhalali wowote kua na usimamizi wa serikali wakati huo huo serikali haina dini? Mi sijaelewa hapa uhalali wake mwenye kujua zaidi afunguke basi nimuelewe vizuri

Wanataka ianzishwe na serkali ili mahakama hiyo iwe inagharamiwa na serkali ikiwa pamoja na kadhi kulipwa mshahara na serkali. Waislamu hawana uwezo wa kuigharamia. Hapa ndipo serkali inapokataa kujiingiza kwenye mambo ya dini, kwa sababu ikifanya hivo maaskofu nao watadai walipwe mishahara na serkali.

Wanawaza kwa kutumia masaburi yao!!!
 
bahati nzzuri sisi waislam linapokuja swala la kudai haki zetu za msingi hatuogopi kupigwa , wala kufa ikibidi... kitaeleweka tu,
.

Sasa haki ya msingi mnayodai ni ipi hapo? mbona nataka kufanya hii nchi kama Nigeria? kila kukicha makundi ya kiisilau yamefanya mauaji. mnataka mahakama yenye nguvu ya kisheria ya nini? hapo kuna agenda gani ya siri? mmesema hiyo mahakama itahusu mirathi na ndoa, kwani hizi mahakama nyingine haziwezi kuyashungulikia hayo? kwani tangu awali huko misikitini mlikuwa hamtatui matatizo ya ndoa ya waumini wenu?
 
Kwenda shule ni muhimu
hawa jamaa waislam wanataka mahakama ya kadhi na wanajua serikali haina dini
stupid idea labda wanataka na sisi wakristo tudai mahakama yetu??
Kuna mambo mengi ya kushughulikia kipindi hiki kuliko huo upuuzi wao

Aende shule then aache Uislam,kwani akienda shule akabaki Muislam,hata angeelimika vipi ni tatizo linabaki palepale...Wanataka mahakama ya kadhi kama ilivyo kwenye Quran yao,wanaficha makucha kuwa wanakubaliana na swala la kuanzishwa kwa ajili ya ndoa,mirathi na talaka ili ionekane kweli hawana nia mbaya,ukweli ni kuwa baada ya kuianzisha watataka waitumie kwa kadri ya maalisho ya Allah na Mohammad,napo wataleta maandamano kuonyesha kuwa mahakama yao inaminywa kutotendekazi kwa muujibu wa Quran.
Watanzania tusikubari kuingizwa mkenge na hawa jamaa...
 
WaIslamu wanapinga BAKWATA kwasababu wanadai imeanzishwa na serekali ???.Wanataka kuanzisha chombo chao amabacho hakitakuwa na mkono wa serekali wakati huo huo wanadai kwa nguvu zote serekali iwaanzishie mahakama ya kazi ohoo sorry mahakama ya kadhi ?.Je huu si unafiki !.


Kuna watu hawana kazi za kufanya wanatafuta umaharufu wa kipuuzi.Nashauri serekali itumie vyombo vyake vya dola kukomesha masheikh ubwabwa.Mohamed said ajiandae kuandika kitabu kingine Tanzania hatutaki udini wenu pelekeni Somalia.
 
  • Kuandamana usiku na mchana kushinikiza Mahakama ya Kadhi
JUMUIYA ya Taasisi za Kisilamu, imesema utatumia maandamano ya usiku na mchana, kushinikiza kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na kwamba hatua hiyo inakuja baada ya kushindikana kwa njia ya kidiplomasia, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Hayo yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Shehe Issa Ponda, alipokuwa akisoma tamko la msimamo wa Taasisi za Kisilamu kufuatia kauli ya Rais Kikwete katika Baraza la Idd el Fitri, lililofanyika Septembe mosi mwaka huu mjini Dodoma, kuhusu kuanzishwa kwa mahakama hiyo.

Shehe Ponda alizitaja taasisi zilizokutana na kuazimia kutoa tamko hilo kuwa ni pamoja na Baraza Kuu, Jopo la Mashehe, Baraza la Vijana wa Kiislamu na Basuta.

Soma zaidi hapa Waislamu sasa kuandamana kushinikiza Mahakama ya Kadhi

Tuandamane kudai ustawi wa taifa letu.............mahakama ya kadhi wakati watu wanakufa njaa hakuna tija...tatizo viongozi wa dini ni wanafiki,wakati wa baraza la idd kabla ya hotuba ya JK hawa mashehe waliponda sana kusema,amani ni jambo la msingi tuitunze na kuviponda vyama vya siasa na watu wanaotaka kuvunja amani(kumbuka nchi hii mtu anaedai haki na ustawi wa nchi hii ni mvunja amani)wakadhani wanamuonga JK hakubali mahakama ya kadhi,jamaa alipofika akafumba macho hakawapa vidonge vyao....kama uliangalia kupitia TVs au ulikuwepo pale ungeona jinsi mashehe walivyoshikwa na butwaa wasiamini kuwa yale ni maneno ya JK au?
 
Back
Top Bottom