Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Umesema ukweli mtupu

kwa hiyo wale wanaharakati watatu wa kikristu wakiongozwa na JULIUS KYARUZI kuishtaki Tanzania kwenye umoja wa mataifa ili serikali yetu iruhusu ushoga ndio mafundisho ya kanisani? soma mwananchi la jana.
 
huyu rais wa wetu inaonekana ni muoga; freedom of speech is one thing na inciting divisions is another. na hawa mashee sijui; mapadre washamjua ya kuwa ni muoga ndio maana sasa wanamshambulia na kumnyanyasa na upuuzi wao. kwanza ni wanafiki wote neno ambalo Mh. ameogopa kulitumia.... kama mwanasiasa lakini mwanakijiji keshaongelea humu humu ndani hawana lolote bali wana uchu na power na kutaka kuweka influence zao katika katiba ya serikali ambayo aina dini. hila wanacholeta ni mchezo wa hatari sana kwa taifa mi nadhani labda lugha inayotumika humu ndani ni ngumu baadhi kuitafakari vizuri.

lakini huu mchezo mi nadhani sasa unaenda mbali na umeendelea vya kutosha hawa watu wamungu au wa melo tu wasio rizika na kutaka kuupa umma mawazo ya kuanza kuambatanisha siasa na dini zao. wengi humu ndani mtabishana na maneno na chuki za ndani lakini rajabu na ray wa kule wapi sijui wao hawana line za kubishana hivyo chuki itakuja kisa padri kasema au sheikh kasema. kwa kweli nni wakati wa serikali especially rais wetu na washauri wake wakae chini na kumalizana na hawa watu for good warudi wanapo usika kuwapa watu imani ya mungu siasa wawachie wanasiasa na wahusika wakuriport abali ama sivyo ....... kuna mengi muheshimiwa ameonya ebu soma vizuri anachokisema alafu interpret sio usome juu juu tu nyie mnaozani hawa wanafiki wana njia njema na tanzania yetu.
 
kama sheria zilizopo za kitaifa haziwatosherezi waislamu katika
ina maana dini yao haifai na ina matatizo inawabidi wabadili
dini wawe wakristo au wasiwe na dini kabisa lakini hatutaki
ubabaishaji nchi hii sio lazima kuiga kila jambo hata kama ni la
kipumbavu.
* Mmoja asema serikali kuanzisha taasisi za dini ni kuvunja katiba

NYALANDU,Lazaro.jpg


Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu (CCM) ni miongoni mwa waliotoa tahadhari ya udini.


Exuper Kachenje, Dar na Kizitto Noya, Dodoma

HOJA ya Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kiislamu (OIC) na mijadala mingine ya dini imezidi kuwa moto baada ya wabunge watatu kuionya serikali kuwa masuala hayo yataigawa nchi katika vipande vipande.

Waliotoa onyo hilo ni pamoja na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu (CCM), Mbunge wa Maswa (CCM), John Shibuda na yule wa Bukene (CCM) Teddy Kasela-Bantu walipokuwa wakichangia hotuba ya makadirio, mapato na matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyowasilishwa na Waziri Bernard Membe.

Aliyekwenda mbali zaidi ni Nyalandu aliyetangaza nia ya kuwasilisha muswada binafsi kulitaka bunge kuzuia mjadala wa suala lolote la dini.

Kauli hizo zimekuja katika kipindi ambacho taifa limeshuhudia mijadala mikali inayochukua sura ya kidini, kuhusiana na uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi Tanzania Bara, nchi kujiunga na OIC na waraka wa Wakatoliki unaoelekeza Watanzania namna ya kupata viongozi bora katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Nyalandu aliitahadharisha serikali kuwa hatua yoyote ya kushiriki katika uanzishwaji wa mamlaka au taasisi yoyote ya dini nchini ni uvunjaji wa katiba ya nchi na inaweza kuligawa taifa.

Huku akipinga kuendelea kwa mjadala wa Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC); na kutoa mifano mbalimbali ya mataifa yaliyofuata misingi ya dini na athari zake na kunukuu vifungu vya Katiba ya Tanzania, Nyalandu alisema serikali ya Tanzania haina dini na hivyo haina mamlaka ya kusimamia uanzishwaji wa taasisi au mamlaka yoyote ya kidini.

“Itakuwaje tuanze kujadili masuala ya dini katika nchi ambayo haiongozwi kwa misingi ya dini?” alihoji Nyalandu na kuongeza:

“Serikali kimsingi hairuhusiwi kuwa na dini, lakini pia hairuhusiwi kusaidia uanzishwaji wa chombo chochote au mamlaka yoyote, yenye misingi ya dini ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.”

Aliongeza kuwa, “haitakuwa jambo la busara na itakuwa ni kukiuka misingi ya katiba ya nchi, kuruhusu aina yoyote ya michakato inayohusu masuala ya dini moja dhidi ya dini nyingine.”

Nyalandu alimkumbuka Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere alipokataa lilipoibuka suala la Zanzibar kujiunga na OIC.

Alisema suala jingine linalofanana na hilo ni la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi au nyingine yoyote inayofanana na hiyo na kueleza kuwa, pia litakuwa ni uvunjaji wa katiba iwapo litajadiliwa bungeni.

“Suala la dini ni nyeti sana, nchi hii ilikaa na watu wa dini zote. Dini au kabila vitaligawa nchi vipande. Tumeona ukabila ukiitafuna Kenya na sasa udini umeanza kuingia Tanzania,” alisema Nyalandu na kuendelea:

“Katika hilo, nakusudia kuleta muswada binafsi kupiga marufuku Bunge kujadili mambo ya dini na matumizi ya fedha za walipakodi katika kusaidia uanzishwaji wa taasisi yoyote ya dini hapa nchini,” alisema.

Aliendelea, “Ninaonya wanasiasa kunyemelea masuala ya dini na kuyajadili bungeni, wakuu wa dini kutaka mambo yao yaje kwenye siasa. Tufute kabisa kujadili OIC, hili ni shirika lao huko. Hakuna mchakato hapa, Tanzania sio nchi ya dini.”

Msimamo wa Nyalandu kupinga OIC, uliungwa mkono kwa nyakati tofauti na mbunge wa Maswa (CCM), John Shibuda na Mbunge wa Bukene (CCM) Teddy Kasela-Bantu waliosema kuwa, kufanya hivyo, ni kukiuka Katiba na misingi iliyowekwa na waasisi wa Tanzania akiwamo Mwalimu Julius Nyerere.

“Wabunge turejee na kufuata matakwa ya katiba tuliyoapa kuilinda, hifadhi ya amani ya Tanzania inategemea maneno yetu sisi wabunge, tuzungumze kwa masilahi ya Taifa,” alisema Shibuda na kuonya:

“Tusitumie lugha za tafrani, tusiwe wanaharakati wa dini hapa bungeni. Tusiwe ndondondo za tafrani kwa nchi yetu, tusiwe misumari ya jeneza la amani ya Tanzania, tukumbuke hakuna atakayetawala kwa kutegemea dini moja.”

Naye Mbunge wa Bukene, Teddy Kasela- Bantu aliwataka wabunge kuendelea kuitetea Katiba ya nchi akionya kuwa endapo viongozi wakianza kuivunja kwa makusudi, nchi itasambaratika.

“Kama viongozi tunaivunja Katiba tuliyoapa kuitetea, wananchi wafanya nini?” alihoji Kasela- Bantu na kuendelea, “Katiba inasema serikali haina dini, sasa kama humo ndani tunaanza kuzungumzia mambo ya dini ni wazi tunavunja katiba.”

“Mimi naomba hata kama mchakato wao huo utachukua miaka mingapi, Tanzania tuache kufikiria jambo hilo la kujiunga na OIC. Kila mtu anatakiwa kuamini anachoamini, cha Kaisari tumpe Kaisari ambaye ni serikali na cha roho kibaki rohoni, nchi hii haina dini,” alisisitiza.

Awali, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe aliwataka Watanzania wasitishe kwa muda mjadala wa Tanzania kujiunga na Jumuiya hiyo kwa kuwa OIC sasa ipo kwenye mchakato wa kubadilisha sheria na kanuni zake za namna ya kupata wanachama wapya.

“OIC ipo kwenye reform ya kuundwa upya, inafanyiwa mabadiliko ya muundo, taratibu, kanuni za kuwapata wanachama wapya. Naomba Bunge na Watanzania kuelewa mabadiliko hayo ili mjadala huu usitishwe hadi mwaka 2012 utakapokamilika mchakato huo,” alisema Membe na kuendelea.

“Hatuwezi kuendelea na mjadala wakati chombo chenyewe kinapitia mfumo na mabadiliko katika kipindi cha miaka miwili ijayo. Tukiendelea kujadili, tutakuwa tunajadili mambo yatakayopitwa na wakati. Haya sio maneno ya Membe, ni maelekezo ya kikao cha OIC kilichoketi mjini Damascus, Syria mwezi Mei mwaka huu.”

Membe alibainisha kuwa mchakato huo unafanywa na nchi nne ambazo zitatakiwa kumaliza kazi mwaka 2010 na kutoa taarifa yake kwenye baraza la wataalamu wa OIC mwaka 2011 kabla ya kufikisha taarifa kwa nchi wanachama.

Akieleza hasara za nchi kujiingiza katika masuala ya dini, Nyalandu alisema, machafuko yaliyotokea Zambia katika siku za hivi karibuni na mapigano ya Kitaleban nchini Pakistan ni matokeo ya uamuzi huo ambao Tanzania inataka kuufanya.

Hoja ya Nyalandu kwamba wanawake wa Saud Arabia wanakatazwa kuendesha magari kutokana na tamaduni za dini zao iligusa hisia za mbunge wa Mchinga (CCM) Mudhihir Mudhihir ambaye alisimama na kuomba mwongozo wa Naibu Spika akisema:

“Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mheshimiwa mbunge afute kauli yake kwamba dini ya Uislamu inakataza wanawake kuendesha magari ili asiamshe jazba zetu.”

Hata hivyo, Naibu Spika Anne Makinda alipuuza mwongozo huo akisema, “Mimi naamini mheshimiwa hakutaja dini, alisema Uingereza ukioa mke wa pili unafungwa; na Saud Arabia wanawake wanakatazwa kuendesha magari kwa mujibu wa tamaduni na dini zao,” alifafanua Makinda na kuomba Hansard kuthibitisha kauli yake.

Akihitimisha mjadala wa hotuba ya bajeti yake, Waziri Membe alisema serikali itaendelea kutokuwa na dini (secular state) huku akifafanua kuwa, “Si kwamba serikali inataka kuondoka katika “secular state” bali OIC inataka serikali za nchi kuwa wanachama na si taasisi, lazima serikali itoe kibali ndipo nchi iwe mwanachama, lazima tuwe na `tolerance` (tuvumilie).

Wakati hayo yakijadiliwa ndani ya Bunge, nje ya Bunge huko huko Dodoma, Habel Chidawali anaripoti kuwa, Waislamu mkoani humo wamesema kuwa wamechoka na kitendo cha serikali kuwadanganya kama watoto wadogo na sasa wanataka Mahakama ya Kadhi kwa nguvu zote.

Kauli hiyo waliitoa jana wakati wa kongamano la Waislamu wa mkoa huu lililofanyika katika Ukumbi wa Maktaba mjini chini ya udhamini wa shirika lisilo la kiserikali la Al-Mallid la mjini humo.

Waislamu hao walisema kuwa umefika wakati ambao wanaamini kuwa serikali inatoa haki kwa upendeleo kwa kuwajali zaidi Wakristo huku masilahi ya Waislamu yakisahaulika kabisa.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi
 
kwa hiyo wale wanaharakati watatu wa kikristu wakiongozwa na JULIUS KYARUZI kuishtaki Tanzania kwenye umoja wa mataifa ili serikali yetu iruhusu ushoga ndio mafundisho ya kanisani? soma mwananchi la jana.
Hapa hatuzungumzii ushoga. Kama unataka tuzungumzie hilo wewe anzisha thread hiyo tuwape ukweli chanzo cha ushoga na dini ipi inaruhusu hata kwenye vitabu vyao.
Usitake kupotosha mjadala hapa.
 
“Itakuwaje tuanze kujadili masuala ya dini katika nchi ambayo haiongozwi kwa misingi ya dini?” alihoji Nyalandu na kuongeza:

“Serikali kimsingi hairuhusiwi kuwa na dini, lakini pia hairuhusiwi kusaidia uanzishwaji wa chombo chochote au mamlaka yoyote, yenye misingi ya dini ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.”

upande mwingine kikatiba ohhh..serikali haina dini na hivyo kusadia taasisi ya dini ni kiuka katiba, upande mwingine tena ohh serikali itoe misamaha ya kodi kwa taasisi za kidini. kigezo gani kinatumika kuzisamehe taasisi za dini wakati serikali haiana dini na kusadia ni kuvunja katiba? kwanini hizo taasisi za dini zisiwe treated kama NGO zingine? unasamehe kodi kwa kigezo cha dini au umuhimu wa kinacho ombewa msamaha?

Aliyekwenda mbali zaidi ni Nyalandu aliyetangaza nia ya kuwasilisha muswada binafsi kulitaka bunge kuzuia mjadala wa suala lolote la dini.

Nyalandu alimkumbuka Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere alipokataa lilipoibuka suala la Zanzibar kujiunga na OIC

Sasa na hawa wa Zenji hoja yao ya kujiunga na OIC wapeleke wapi kama siyo bungeni? au waachiwe waamue wenyewe kwenye baraza la wawakilishi? Hivi Nyerere amekuwa marking scheme ya kila kitu? cant we think beyond Nyerere? Kipindi cha utawala wa Nyerere, Tanzania ilikuwa kama North Korea na akili za waTZ wengi zilikuwa zimeganda kama zawanorth Korea vile, every thing is Mr. Kim. Tanzania imebadilika, utawazuia vipi watu kujadili masuala yao ya msingi?

Nani alikwambia kuwa NGO zisizokuwa za dini hazinufaiki na msamaha wa kodi????? hapa unalako jambo tu. Hivi kwani haziko NGO za kiislamu ambazo pia ufaidi misamaha ya kodi?
 
muisla alielimika yupi huyo? acha ujinga sio kama mkiristo wanaopigania ushoga. waislam wote wenye kujua wapi watafika siku ya malipo wanataka mahakama ya kadhi. lkn akina Nyie wanafiki, wapenda starehe, waongo, wajinga na wapumbavu ndio msiotaka mahakama ya kadhi

Duu kazi kweli kweli. hii ndiyo lugha ya kudai mahakama ya kadhi!!!!
mod. nadhani huyu ana - polute jamvi. nadhani pia hata mahakama anayoidai inaweza kumgeuka kwa polution hii
 
Lwakatare wenzio wote wa Chadema wanaingia kwa majina yao ni wewe tu unayetumia pen name.
hisia zako za kidini zimechangiwa na wewe kunyimwa ukatibu mkuu msaidizi wa CUF.ulitaka uwe naibu wa kudumu?
Ulipojiita kanda mbili ulikuwa sahihi maana upeo wako ni mdogo kweli.
Hivi kweli hapa unaweza kujua kila mwanachama ni nani just depending on his/ her posts?
Umenoa mimi si Lwakatare, ila Lwakatare namfahamu sana. Kama ni kujaribu, jaribu tena🙂
 
huyu rais wa wetu inaonekana ni muoga; freedom of speech is one thing na inciting divisions is another. na hawa mashee sijui; mapadre washamjua ya kuwa ni muoga ndio maana sasa wanamshambulia na kumnyanyasa na upuuzi wao. kwanza ni wanafiki wote neno ambalo Mh. ameogopa kulitumia.... kama mwanasiasa lakini mwanakijiji keshaongelea humu humu ndani hawana lolote bali wana uchu na power na kutaka kuweka influence zao katika katiba ya serikali ambayo aina dini. hila wanacholeta ni mchezo wa hatari sana kwa taifa mi nadhani labda lugha inayotumika humu ndani ni ngumu baadhi kuitafakari vizuri.

Ni kweli umeongea, Rais wetu yuko kimya masaa yote akiona yamezidi ndo atakaa na wazee wa CCM; hawezi kukemea mara moja mtu yeyote kuacha hii biashara ya dini, na ndo maana kila mtu anaongea anavyotaka, nakumbuka nikiwa mtoto ulijawa na uwoga kutaja jina na Nyerere; sasa hivi nchi hainawa nidhamu mkubwa,mdogo wote sawa ni kujiachia tutafika?

Kama JF humu tumeshindwa hata kuelewana kila mtu maoni yake ni tofauti !!!! kweli wabunge wataelewana??? Jibu ni moja tu Rais wa Nchi atoe kauli yake.
 
CHADEMA kama chama kinachojiita chama mbadala ni lazima watu wajue msimamo wao kwenye hizi issues

huwezi kupewa nchi huku hutaki kueleza msimamo kwenye masuala ya kitaifa kama haya

Nani kakudanganya suala la dini moja likawa la kitaifa?
 
Binafsi ni mkristo lakini ningeunga mkono uanzishwaji wa MAHAKAMA YA KADHI nchini, hii ni kuzingatia umuhimu wake lakini siungi mkono kujiunga na OIC.
 
muisla alielimika yupi huyo? acha ujinga sio kama mkiristo wanaopigania ushoga. waislam wote wenye kujua wapi watafika siku ya malipo wanataka mahakama ya kadhi. lkn akina Nyie wanafiki, wapenda starehe, waongo, wajinga na wapumbavu ndio msiotaka mahakama ya kadhi

Haya matamshi yamejaa dharau,kebehi, chuki na roho mbaya aliyonayo mwandishi dhidi ya Ukristo.Lugha hii haitakiwi hapa jamvini kwa kuwa sio ligha ya kistaarabu.

Wewe kama unachuki zako binafsi basi baki nazo kwani kwa kuzileta hapa Jamvini haisaidii chochote wala hazitabadilisha mitazamo na misimamo ya watu juu ya kile wanachokijua na kukiamini.

Wewe toa hoja wala sio kusambaza chuki na dharau juu ya madhehebu mengine.

Nafikiri umefika wakati muafaka wa Serikali kuchukua hatua zinazopasa kwa kuwa hali kama itaendelea kuwa kama hii hakika mustakabali wa Taifa letu utakuwa hatarini kama hali hii haitadhibitiwa mapema.

Inaonekana tumefikia mahali ambapo baadhi yetu watanzania tumekosa uvumilivu dhidi ya imani ya watu wengine na kwa kuwa hatuna hoja tuaishia kutoa lugha kama hizi zinachoashiria kuja kwa machafuko tuu na sio kitu kingine.
 
muisla alielimika yupi huyo? acha ujinga sio kama mkiristo wanaopigania ushoga. waislam wote wenye kujua wapi watafika siku ya malipo wanataka mahakama ya kadhi. lkn akina Nyie wanafiki, wapenda starehe, waongo, wajinga na wapumbavu ndio msiotaka mahakama ya kadhi


Pole Saana angalia sehemu za mwambao waisilamu ni wengi na hapa Bongo ndiko waliko MASHOGA WENGI ,hata ZNZ siku mmoja waliojiwa na BBC walikubali na wakasema Hako kamchezo wamezoea na wanakapenda pia haiwazuii kuwa na Mke na watoto sasa wao wanaona POA !!

Wajinga ,Wapumbavu & Wanafiki Nyie msikubali kuwa mwaweza anzisha Mahakam ya KADHI bila kushirikisha Serikali kwani haina Dini ni hilo mwalijua wazi !

Wapenda Starehe angalia wakati wa Mfungu KITIMOTO inabaki saana , Bar hakuna watu saana na GUEST HOUSE Vyumba vipo tele tuu !
 
[/COLOR][/B]

kumbuka Chadema ni chama cha siasa, si kikundi cha madrasa au kwaya ya injili so hakuna ulazima wowote kuzungumzia jambo hilo

Nakuunga mkono Kamuzu chama chochote makini hakitakimbilia issue hii ya kadhi Court,Chadema wana sera zao na kadhi Court sio sera yao hivyo hawana ulazima wowote wa kutoa msimamo juu ya jambo hilo.

Walioliweka kwenye ilani yao washatoa tamko sasa ubishi ni wa nini.Kama kuna hoja zitolewe tena kwa uzito uaostahili bila kubeza wengine.

Ikumbukwe kwamba watanzania wanaishi katika nchi inayoheshimu katiba na katiba inasema wazi kuwa watu watakuwa huru kutoa maoni yao tena kwa hiari kabisa lakini bila kwenda kinyume na sheria nyingine za nchi.
 
muisla alielimika yupi huyo? acha ujinga sio kama mkiristo wanaopigania ushoga. waislam wote wenye kujua wapi watafika siku ya malipo wanataka mahakama ya kadhi. lkn akina Nyie wanafiki, wapenda starehe, waongo, wajinga na wapumbavu ndio msiotaka mahakama ya kadhi

Huwezi kumtenganisha muislam na kulawitiana pamoja na ugaidi, sijui hilo unalisemea vipi.
 
Naona wanaopenda maswala ya udini tayari wamesha vamia anga hii.
 
Kuna issues zitasemwa lakini si hii ya upande mmoja kila mara Uislam , Waislam, OIC , Kadhi , kuonewa waislam nk now way .Ndiyo maana Makinda alikanyaga mafuta leo na kumwacha Mdhihiri analia lia .Hii ni ishara kwamba watu wamechoka kupindishiwa hoja .Kesho kadhi watasema mtoto wa Mdhihiri kaiba akatwe mkono yeye atakubali ?Wakubaliane pembeni huko na si kutuhusisha sisi .

Mdhihiri haogopi mahakama ya kadhi wala kukatwa mkono. kwa sababu yeye hana mkono. anataka watu wa kuwa nae sare sare..WAONGEZEKE!
 
sio suala la mahakama ay kadhi na OIC peke yake, ....kwa sasa hayo pamoja na mambo ya ufisadi, muungano, uchaguzi huru ni mambo yanayowagusa jamii moja kwa moja hivyo kama chama cha siasa wanapaswa kutoa msimamo wao kwa kila moja ya hili.
wanaweza chadema moja kwa moja wakasema hawataweka mahakama ya kadhi, nafikiri itakuwa bora zaidi kuliko kunyamaza kmya.....kwa kuwa kimya chao kinaweza kuonekana kuwa hawana msimamo kwa hili na kwa mengine.
 
Naunga mkono hoja kwamba CHADEMA iendelee kutoa msimamo wake kwa masuala ya kitaifa na yenye maslahi kwa taifa zima. Vyama vyote vya siasa vingefanya hivi ili kuwaunganisha Watanzania wote.

OIC na Kadhi si masuala ya kitaifa. Ni propaganda ya kuwanufaisha watu wachache mno.

Waislam tusidanganyike. Watanzania tusidanganyike.
 
Back
Top Bottom