Hapa hakuna ukweli ispokuwa Wabunge hao wapo hapo kuhakikisha mikakati ya Wakiristo kupinga na kuzizuia hoja za Waislamu inafanikiwa.
Nasema hivyo kwa sababu kama Wabunge hawa si waongo basi watakuwa ni wanafiki wa kutupwa ndani ya siasa za Tanzania ,hii inatokana na wao kuitetea na kuona KATIBA ya NCHI HII inavunjwa ,ilihali KATIBA hii sio imevunjwa tu bali imevurugwa na haifuatwi kabisa ,ipo tu na kuwepo kwake kunafaidisha baadhi ya mambo kama walivyofanya na kuinukuu juu ya kupinga mambo yahusuyo dini ya Kiislamu ,Katiba kwao wao itatumika kusitisha na kusimamisha mambo ya Kiislamu ,kwa wakati huo wataiona KATIBA ndio ya kufuatwa na kuabudiwa kwa hali na mali.
Sasa wabunge hawa vichwa maji kama kweli wanailinda KATIBA na ni wafuasi wa Baba yao Nyerere ,waende kaburini kwa Nyerere wakamlilie ,kuwa KATIBA ya Nchi inavunjwa.
Sasa mimi sitataka kuingilia hayo mambo ya kidini ,najua kabisa kuwa Tz haina dini ila wananchi wake ndio wamo ndani ya dini ,mimi ninatatizo na hawa wabunge wanaokuja na kujiweka kimbelembele kuwa ukifanya hivi au vile unavunja KATIBA.
Uchaguzi wa Tanzania unasemwa unaendeshwa kwa kufuata KATIBA ,malalamiko mengi yametolewa na vyama vya upinzani kuwa KATIBA inavunjwa katika kuendesha uchaguzi huu ,hivi Wabunge hawa wanakuwa wapo wapi ? Kama huu wanaouonyesha sasa si unafiki ni kitu gani ? Ukiangalia sana utaona kuwa wao ndio wanaotaka kuigawa jamii ,hiyo ya Kadhi na OIC ni mikakati katika sera zao na wao ndio wenye kuongoza nchi hivyo wapo katika kutimiza sera zao ,waachwe kama walivyo.
Kama wanavunja KATIBA ni CCM ndio wanaovunja katiba kwa kuruhusu mambo ya kidini ,aidha wangenifurahisha sana kama wangedai zile jumuia zote za kidini zilizojifunga na serikali zivunjwe mara moja na serikali isijihushe nje wala ndani ya nchi.Na yeyote anaeleta harakati za kidini na kutaka kuihusisha Serikali ni adui wa Nchi hii.
Katika Nchi hii KATIBA iimevurugwa na haifuatwi kikamilifu ,maandamano ni haki ,kuandikisha uraia ni haki ,leo hii wananchi kwa maelfu wameshindwa kupata vitambulisho vya uraia kule Zanzibar ,hilo hawalioni maana KATIBA inavunjwa lakini wao wamenyamaza kimya (Iwe KATIBA ya Zanzibar lakini ni ndani ya Jamhuri ya Muungano)
Hawa wanaweka ngumu kutokana na mikakati ya kanisa ambayo imo ndani ya waraka uliokamatwa Zanzibar ,kuzima mambo ya Waislamu kwa kutumia vyombo vya serikali na si kulinda KATIBA wala kulinda amani iliyopo ,na huyo aliesema kuhusu madereva kuwa haikutanjwa dini ya kiislamu inaonyesha akili yake ni finyu,sijui amepataje cheo hicho cha Unaibu.