Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

we Mkandara ni mtu hatari sana (sorry to say that) ukweli ndiyo huo. umh...
Mkuu hapana mimi sii hatari isipokuwa nipo kijiweni na hapa ni mahala pa kuangalia pande mbili za shilingi kisha unapima uzito wa hoja zote..Bila kuwakilisha upande wa pili itakuwa hatujadiliani isipokuwa tunafanya ushabiki mtupu..
Kumbuka hili swala ni zito sana na linaweza tikisa nchi na kinachotakiwa ni kuelimisha Umma pande zote mbili, mazuri na mabaya yake (kama vile swala la mahakama ya kadhi OIC na MOU)
Taratibu na haki za ibada hizi kwani ndizo zinazofanya tofauti ya dini hizi. kama sote tungekuwa tunakubaliana basi sidhani kama tungekuwa na dini au madhehebu mengi..Kinachotushinda kuelewa ni hizi tofauti ambazo ndizo chanzo cha sisi kutengena ktk imani ya dini lakini tunajariobu kufikiria sawa mahala pasipokuwa na usawa huo..
Utasherehekea kuzaliwa/Kufa kwa Yesu kwa sababu ni ibada kubwa ya Mkristu, na sio lazima iwe pia ya Muislaam wala Muislaam kuweka shaka juu yake. Waislaam nao wanasherehekea Idd kwa taratibu zao kwa sababu ndiyo part ya ibada yao ktk mafundisho yao ukianza ku question wakati jibu lake ndilo lilikufanya usiwe Muislaam itakuwa kazi mpya..
Hizi zote ni ibada (sherehe) zinazokubalika kikatiba lakini huwezi kulazimisha ibada moja ya dini utumike ktk dini nyingine ukitumia reasoning ya mafundisho yako.
 
Tangu serikali ya awamu ya 4 iingie madarakani mwaka 2005 ilijigamba kulishughulikia suala la mahakama ya kadhi. Lakini leo ni takribani miaka 4 bado haina ufumbuzi wa tatizo hili huku ikiendeleza usanii na ubabaishaji.

Hakika serikali ya CCM ipo njiapanda isijue nini cha kufanya kwani inahitaji msaada mkubwa sana wa kundi hili la Waislam ili iweze kuvuka kizingiti cha mwaka 2010 kiulaini, wakati huo huo ikiogopa kuwaudhi wakristo kwa kuingiza masuala ya dini ndani ya serikali kinyume na katiba ya nchi. Suala hili linasukumwa na utashi wa kisiasa zaidi kuliko uhalisia na katiba

Mtizamo wangu:
Mahakama ya Kadhi ni sehemu ya ibada kwa waislamu. Hili ni jambo jema kabisa na ni muhimu ikawepo ili kutimiza nguzo za imani ya ndugu zangu waislamu. Lakini maswali yangu ni kuwa hii mahakama haiwezi kuwepo bila kuwa chini ya usimamizi wa serikali? Je ikiwa serikali itaanza kusimamia na kuhudumia/ kulipa gharama ya mahakama ya kadhi haitakuwa imekiuka na kuvunja katiba ya nchi? Je uanzinshwaji wa mahakama ya kadhi chini ya mwamvuli wa serikali ni kwa maslahi ya Taifa zima kwa ujumla au ni kundi moja la watu bila kujali ukubwa au udogo wa kundi hilo? Ikiwa serikali itaamua kuziingiza sheria za kiislamu na kuruhusu zitumike kwa mahakama zetu zitatumikatumikaje kwani hapa pia kuna utata mtupu.

Hii ni ibada, kwa hiyo wenye ibada yao waachwe waendeshe ibada yao kwa jinsi wanavyoona inafaa pasipokuleta shinikizo la kuvunja katiba ya nchi yetu. Serikali kutumia hela zetu kufadhili ibada ya kundi fulani ni uvunjaji wa katiba jambo ambalo litaleta mgawanyiko na uvunjifu wa amani.

MAHAKAMA YA KADHI IWE NJE YA UTARATIBU WA SERIKALI NA HAIPASWI KUJADILIWA NA SERIKALI WALA VYOMBO VYAKE KWANI NI IBADA YA WAISALAMU WAACHIWE WENEYEWE WATAFUTE NAMNA BORA YA KUITEKELEZA PASIPOKUISHIRIKISHA SERIKALI

Je Mwananchi na MwanaJF nini mtazamowako kuhusu mahakama ya Kadhi? Toa ushauri tu, Kashfa hapana.
 
Katika kipindi cha papo kwa papo leo wabunge walishindwa kumuuliza Mh Pinda Swala kuhusu mahakama ya kadhi. Jee inatokana na taarifa za Tz daima kutoa habari hii kabla ya kipindi hicho au Tz daiama walidanganya katika habari yao. habari yenyewe ni hii. Natoa Hoja

Hoja ya Kadhi sasa kumbana Pinda leo

  • Wabunge wataka afafanue bungeni alichomwahidi Mufti
na Edward Kinabo na Danson Kaijage


SUALA la Mahakama ya Kadhi, leo linatarajiwa kuchukua sura mpya bungeni, baada ya kuwapo kwa baadhi ya wabunge waliojipanga kukitumia kipindi cha maswali na majibu ya hapo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kumtaka afute kauli ya serikali iliyotolewa na Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe, kuhusu mahakama hiyo.

Akizungumza bungeni wiki iliyopita, Chikawe alisema kuwa serikali haitaunda Mahakama ya Kadhi na badala yake mahitaji ya Waislamu yatachanganywa katika sheria za nchi na kuamuriwa na mahakama za kawaida.

Taarifa ambazo Tanzania Daima imezipata kutoka katika vyanzo vyake vya kuaminika, zinasema kuwa mpango wa wabunge hao unatokana na Waziri Mkuu, Pinda, kuwakubalia viongozi wa Kiislamu wakiongozwa na Mufti wa Tanzania, Sheikh Mkuu Issa bin Shaaban Simba, kuwa ataifuta kauli hiyo ya Chikawe, iliyotolewa bungeni Juni 30, mwaka huu.

Jumatatu iliyopita, Mufti Simba, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alisema yeye na baadhi ya masheikh wengine walikutana na Pinda na kuzungumzia suala hilo kwa kina, na kuafikiana naye kuwa ataufuta msimamo wa awali wa serikali na kuacha suala hilo likifanyiwa kazi zaidi.

Wabunge hao, kwa sharti la kutotajwa majina yao, wameliambia Tanzania Daima kwa njia ya simu kutoka mjini Dodoma jana, kwamba watamuuliza Pinda swali la kumchokoza, kumtaka aifute kauli ya Chikawe, kama alivyomuahidi Mufti na masheikh wengine waliokutana naye.

“Yeye aliwaahidi masheikh kuwa ataifuta kauli ya waziri bungeni, na kauli ile ndiyo msimamo rasmi wa serikali ulioingia kwenye Hansard (kumbukumbu za Bunge), kuwa hawategemei kuanzisha Mahakama ya Kadhi. Mimi naona kama ameamua hivyo ni jambo jema na ni vema akaheshimu maafikiano yake na viongozi hao wa Kiislamu. Nafikiri wakati wa kipindi cha maswali kwake, nitapata wasaa mzuri wa kumuuliza suala hilo na kumkumbusha ahadi aliyoitoa kwa masheikh, ili aufute msimamo ule aliosema Chikawe. Naamini atafanya hivyo kesho (leo),” alisema mmoja wa wabunge hao.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mufti Simba, aliwataka waumini wa dini ya Kiislamu kuwa watulivu juu ya suala la uanzishwaji wa Mahakama ya Kadhi, kwani halijazikwa bali linaendelea kujadiliwa na serikali kwa msaada wa masheikh.

Mufti Simba alisema yeye na masheikh wengine walikutana na Waziri Mkuu, Waziri wa Sheria na Katiba, na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, William Lukuvi, Jumapili iliyopita usiku na kukubaliana baadhi ya mambo ambayo yataharakisha kuundwa kwa mahakama hiyo.

“Tumekubaliana kwamba hoja ya Mahakama ya Kadhi haijazikwa, ila serikali inahitaji msaada wa masheikh katika suala hilo na sisi tumekubali kutoa msaada huo.

“Hivyo jopo la masheikh litaundwa, na serikali itaunda jopo lake la wataalamu halafu tutakutana, ili kuratibu mfumo ambao utatumika katika Mahakama ya Kadhi nchini,” alisema Mufti.

Mbali ya wabunge hao, Taasisi ya Kiislamu ya Almallid mkoani hapa, nayo imemtaka Waziri Mkuu Pinda, kutoa kauli bungeni ya kubatilisha usemi wa Waziri Chikawe juu ya kutokuwapo kwa Mahakama ya Kadhi nchini.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, mwenyekiti wa taasisi hiyo, Kayumbo Kabutali, alisema kauli ya Pinda kwa Mufti inaweza kuwa ya kinafiki na ya kuwapumbaza Waislamu kama hatalizungumza bungeni.

Mwenyekiti huyo alisema, ili waweze kuwa na imani na Waziri Mkuu, matamshi na kauli yake hiyo, aizungumzie bungeni ili iweze kukaa kwenye kumbukumbu za Bunge na kauli hiyo inasubiriwa kwa hamu na Waislamu wengi nchini leo.

Alisema Waislamu wana hofu kwamba ile inaweza kuwa kauli ya kuwafariji kutokana na uzoefu wa viongozi wa serikali kutumia ulaghai kwa Waislamu ili wapate wanachokitaka kutoka kwao.

Kabutali alisema, wanakusudia kufanya kongamano kubwa mkoani hapa kwa ajili ya kutoa elimu kwa Waislamu, wajue umuhimu wa Mahakama ya Kadhi ili wawe na ujasiri wa kuidai.

Hatua ya serikali kutangaza kuzika mpango huo wa kuanzisha Mahakama ya Kadhi, ilipingwa vikali na Waislamu ambao walidai Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiliwahadaa wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2005, na hivyo baadhi yao kudai kuwa hawatakiunga mkono chama hicho kwenye uchaguzi ujao.

Aidha, baadhi ya Waislamu walikuwa wameshapanga kufanya maandamano kesho, kabla ya Mufti Simba kuwaagiza watulie kwani kikao kati ya viongozi wa Kiislamu na Waziri Mkuu, kilichohudhuriwa na wajumbe zaidi ya 20, likiwamo jopo la masheikh aliloliteua kutoka madhehebu yote ya Kiislamu, kilikubaliana kuwa suala hilo liendelee kushughulikiwa.

“Niliandaa jopo la masheikh kutoka madhehebu yote ya Kiislamu nchini. Nashukuru kwa kuitikia wito wangu. Tulienda kwa Waziri Mkuu tukazungumza kwa mapana zaidi kuhusu Mahakama ya Kadhi na amekubali kuwa mahakama haijafa na mchakato unaendelea,” alisema Mufti Simba.

Alifafanua kuwa, walikubaliana na Pinda kwamba atazungumza bungeni kukanusha kauli iliyotolewa na Waziri Chikawe Juni 30, mwaka huu kuhusu uamuzi wa kuzika hoja ya mahakama hiyo. Mahakama ya Kadhi hushughulikia hasa masuala ya mirathi na ndoa kulingana na misingi ya dini ya Kiislamu.
 
Ulichikisema ni kweli, mahakama ya Kadhi hasa ni kwa Waislamu na wala si kwa watu wa dini nyingine. Ila kusema kwanini serikali iingie ghalama kushughulikia baadhi ya kundi fulani katika jamii, mi hilo siliungi mkono kwa kuwa hao waislamu wanaichangia serikali yao katika michango mbalimbali na kodi mbali mbali ili mambo ya serikali na yao yende kwa ujumla na ufanisi. kwa hiyo sioni ubaya kwa serikali kuliendea na kulisimamia jambo hili lenye maslahi na taifa kwa ujumla wake.
Lakini tukija kwa upande mwingine, mara nyingi hata hizi mahakama za kawaida zinakusanya mapato kupitia uendeshaji wa kesi zikiwemo faini na ghalama zingine ambazo watu hua wanalipa katiaka mahakama, utafiti ulishawahi kufanywa na NGOs moja kuwa mahakama nyingi zinaweza kujiendeesha zenyewe hata bila ya msaada wa serikali kuu. Kwa hiyo hata hizi mahakama za Kadhi zitakuwa hivyo hivyo, kwamba badala ya kuwa mzigo kwa serikali zikawa ni sehemu ya mapato ya Taifa, mapato ambayo yakawafaidisha hata wale wasio waislamu!
Mi nafikiria baadhi ya ndugu zangu wasiobahatika kuwa Waislamu wache chuki na kusubiri kuvuna matunda mazuri ya mahakama ya Kadhi.Aksante.
 
Wengi wa Tz wanangojea kauli yake juu ya kufuta kauli ya Chikawe kuhusu uanzishwaji wa mahakama ya kadhi. Lkn navyoijua CCM itakua shughuli kama kweli Pinda ambae ni CCM damu kufuta kauli ya Chikawe Bungeni. na jee kama hakufuta ndani ya Bunge waislam watafanyaje?
 
Kushindwa miaka yote minne kuiingiza ni ishara kuwa kuna ugumu upo. Lakini ni kitu muhimu kwa waislamu hivyo, itakuwa vema jambo hili likaangaliwa na kutafutiwa namna bora ya kulifanya liwepo, nje ya mamlaka za serikali. Dola haina dini ati ila wananchi tuko sensitive na dini kupita maelezo. Mijadala inaonyesha hivyo
 
.... kwa hiyo sioni ubaya kwa serikali kuliendea na kulisimamia jambo hili lenye maslahi na taifa kwa ujumla wake.

Mi nafikiria baadhi ya ndugu zangu wasiobahatika kuwa Waislamu wache chuki na kusubiri kuvuna matunda mazuri ya mahakama ya Kadhi.Aksante.

Maslahi ya taifa au ya waislamu?
Kumbe kuwa muislamu ni kubahatika? na nini hasa, hebu fafanua....
 
Kimsingi nakubaliana na uwepo wa mahakama ya Kadhi katika nchi yetu, na pia naunga mkono serikali kuchangia katika uendeshaji wa mahakama hiyo kwasababu Waislamu kama kundi jingine lolote la jamii ya watanzania wanahitaji msaada wa serikali yao hasa ukizingatia kuwa nao ni sehemu ya walipa kodi. Tukianza kuhoji kundi moja kusaidiwa kuendesha shughuli zenye manufaa kwao kwa kodi za kundi jingine tutafika mahali ambapo tutashindwa kujibu baadhi ya maswali ya msingi. Mfano mdogo tu; waislamu wanalipa kodi na wakristo wanalipa kodi na wasio na dini wanalipa kodi, kodi zao zinatumika kufundisha wataalumu mbali mbali wakiwemo wa mifugo, katika hiyo mifugo kuna mbuzi, ngómbe na mheshimiwa kiti moto ambaye miongoni mwa walipa kodi kuna ambao kwao si riziki, ndo kusema kodi zao zimetumika kusomesha mtu ambaye anakuja kutibia kiti moto while wao hawali? Hapo tunasemaje?
 
Kimsingi nakubaliana na uwepo wa mahakama ya Kadhi katika nchi yetu, na pia naunga mkono serikali kuchangia katika uendeshaji wa mahakama hiyo kwasababu Waislamu kama kundi jingine lolote la jamii ya watanzania wanahitaji msaada wa serikali yao hasa ukizingatia kuwa nao ni sehemu ya walipa kodi. Tukianza kuhoji kundi moja kusaidiwa kuendesha shughuli zenye manufaa kwao kwa kodi za kundi jingine tutafika mahali ambapo tutashindwa kujibu baadhi ya maswali ya msingi. Mfano mdogo tu; waislamu wanalipa kodi na wakristo wanalipa kodi na wasio na dini wanalipa kodi, kodi zao zinatumika kufundisha wataalumu mbali mbali wakiwemo wa mifugo, katika hiyo mifugo kuna mbuzi, ngómbe na mheshimiwa kiti moto ambaye miongoni mwa walipa kodi kuna ambao kwao si riziki, ndo kusema kodi zao zimetumika kusomesha mtu ambaye anakuja kutibia kiti moto while wao hawali? Hapo tunasemaje?

kuna direct na indirect benefits, hiyo ya waganga kwa mtizamo wangu siyo direct, lakini kuna hii ya kuingiza na kuihudumia mahakama hii moja kwa moja si sawa hii ni sehemu ya ibada ya kundi moja hapa serikali itakuwa imeji confine moja kwa moja na udini pia tuangalie katiba inasema nini.
 
Ulichikisema ni kweli, mahakama ya Kadhi hasa ni kwa Waislamu na wala si kwa watu wa dini nyingine. Ila kusema kwanini serikali iingie ghalama kushughulikia baadhi ya kundi fulani katika jamii, mi hilo siliungi mkono kwa kuwa hao waislamu wanaichangia serikali yao katika michango mbalimbali na kodi mbali mbali ili mambo ya serikali na yao yende kwa ujumla na ufanisi. kwa hiyo sioni ubaya kwa serikali kuliendea na kulisimamia jambo hili lenye maslahi na taifa kwa ujumla wake.
Lakini tukija kwa upande mwingine, mara nyingi hata hizi mahakama za kawaida zinakusanya mapato kupitia uendeshaji wa kesi zikiwemo faini na ghalama zingine ambazo watu hua wanalipa katiaka mahakama, utafiti ulishawahi kufanywa na NGOs moja kuwa mahakama nyingi zinaweza kujiendeesha zenyewe hata bila ya msaada wa serikali kuu. Kwa hiyo hata hizi mahakama za Kadhi zitakuwa hivyo hivyo, kwamba badala ya kuwa mzigo kwa serikali zikawa ni sehemu ya mapato ya Taifa, mapato ambayo yakawafaidisha hata wale wasio waislamu!
Mi nafikiria baadhi ya ndugu zangu wasiobahatika kuwa Waislamu wache chuki na kusubiri kuvuna matunda mazuri ya mahakama ya Kadhi.Aksante.

Unapoita kuwa ni chuki ndio unapokosea. Naomba ujustify serikali kugharamia Ibada ya dini moja huku serikali hiyo hiyo ikawa haijavunja Katiba ambayo inasema kuwa uenezaji wa dini ni jambo la mtu binafsi na litakuwa nje ya mamlaka ya nchi! Chuki iko wapi hapo? Na unaposema habari ya mapato, hilo sio lengo la waislamu, wao wanacholilia ni uhuru wao na haki ya kuabudu ambayo wanatakiwa waigharamie wenyewe. Kwani Quran inasema lazima serikali igharamie mahakama hizi? Mbona BAKWATA inajigharamia yenyewe na hakuna ugomvi wowote?
 
Mimi naona na ni dhahiri kuwa Kilio cha Waislam ni muhimu kisikilizwe kwani wao ni sehemu ya wananchi wa tanzania. Na vile vile haki yao haitegemea ihsani toka kwa wakristu. Kwani wote wana daraja lililo sawa katika status za uraia.

Nategemea Pinda hatapindisha hilo.
 
Hivi Kenya imewezaje kuwa na mahakama ya kadhi na maisha yanaendelea kama kawaida? Je mahakama ya aina hii iliwahi kuwepo Tanganyika enzi zile na ikafanya kazi? Kama Kenya wameweza kwa nini Tanzania kuwe na kigugumizi?Kama ilikuwapo hapo zamani ilisabbaisha matatizo gani hadi ikaondolewa?
 
Kimsingi nakubaliana na uwepo wa mahakama ya Kadhi katika nchi yetu, na pia naunga mkono serikali kuchangia katika uendeshaji wa mahakama hiyo kwasababu Waislamu kama kundi jingine lolote la jamii ya watanzania wanahitaji msaada wa serikali yao hasa ukizingatia kuwa nao ni sehemu ya walipa kodi. Tukianza kuhoji kundi moja kusaidiwa kuendesha shughuli zenye manufaa kwao kwa kodi za kundi jingine tutafika mahali ambapo tutashindwa kujibu baadhi ya maswali ya msingi. Mfano mdogo tu; waislamu wanalipa kodi na wakristo wanalipa kodi na wasio na dini wanalipa kodi, kodi zao zinatumika kufundisha wataalumu mbali mbali wakiwemo wa mifugo, katika hiyo mifugo kuna mbuzi, ngómbe na mheshimiwa kiti moto ambaye miongoni mwa walipa kodi kuna ambao kwao si riziki, ndo kusema kodi zao zimetumika kusomesha mtu ambaye anakuja kutibia kiti moto while wao hawali? Hapo tunasemaje?

Usisahau kwamba Taasisi za Dini zimepewa misamaha ya kodi!
 
Kwa muda mrefu sasa Watanzania wamekuwa kwenye mjadala wa ama Tanzania ijiunge na OIC au isijiunge. Hoja za ufasaha zimekua zikitolewa na pande zote, wale wanaopinga wazo la kujiunga na wale wanaoukubali wazo la kuto jiunga. Kilichonivutia zaidi ni yale makala ya Prudence Karugendo iliyochapishwa kwenye gazeti lako la Alhamisi, Novemba 13 – 19, ukarasa wa 11.

Ameeleza mengi yanayoonesha kampeni zake za kutaka Tanzania isijiunge na OIC. Mfano, ametoa maelezo ya kikao cha OIC kilichofanyika Baghdadi mwaka 1984 ambacho kilihudhuriwa na Mzee Joseph Mihangwa na ambaye anasema kwamba katika kikao hicho, mjumbe kutoka OIC aliweka wazi kwamba lengo la Jumuiya yao ni kuhakikisha kwmba Uislamu ndio unaitawala duni. Mimi ningemwomba Prudence Karugendo atupatia ukarasa mmoja tu wa Katiba ya OIC ulioandikwa Malengo na Madhumuni (Goals and Objectives) ya Jumuiya hiyo ili tuone kama hilo analolisema Mihangwa linajitokeza. Kusema tu nikitu kimoja na ukweli wa unachokisema ni kitu chengine.

Katika maelezo yake amesema kwamba, nanukuu “nchi kuingia kwenye shirika la kidini ni kama inakuwa inawaingiza wananchi wake wote kwenye dini hiyo”. Kwa mantiki yake hiyo haoni kwamba nchi kufungua ubalozi wa kidini, kama Tanzania ilivyofungua Ubalozi wa Vertican nchini, ni kuiingiza nchi nzima ya Tanzania kwenye Ukatoliki? Prudence alipotoa mantiki hiyo hilo hakuliona? Kwani haitoshi Tanzania kua na Ubalozi wa Italia? Kwa nini ikaongeza ubalozi wa Vatican kama sio udini? Amezitaja Jumuiya kama vile CARITAS, AMECEA, CECAM na LWF kama ni jumuiya ambazo Tanzania ni mwanachama kupitia katika madhehebu ya kila kundi na kupendekeza kwamba, kwa hapa Tanzania, ni vyema BAKWATA ikajiunga na OIC badala ya Tanzania. Hapa na msifu kwamba ametoa hoja au pendekezo la msingi lakini hajapendekeza kwamba Ubalozi wa Vertican ufungwe na badala yake wapewe fursa Wakatoliki kujiunga na Ubalozi wa Vertican.
 
Tofautisha kuwa na ubalozi na kujiunga na Jumuiya au nchi fulani. Huu mfano haufai hapa, tafuta mwingine. Unataka kusema kuwa Vatican imejiunga na Tanzania kwa kuwa kuna ubalozi wao hapa? Au tuseme kwa kuwa Iran ina ubalozi hapa ndio tumejiunga nayo kama nchi ya kiislamu? Rejea katiba ya OIC kama haijasema kuwa moja ya malengo ya wanachama ni kueneza utamaduni wa Kislamu duniani then leta hoja tujadili uhalali wa Tanzania isiyokuwa na dini kusaidia kuueneza uislamu kupitia OIC!
 
Je ikiwa serikali itaanza kusimamia na kuhudumia/ kulipa gharama ya mahakama ya kadhi haitakuwa imekiuka na kuvunja katiba ya nchi? Je uanzinshwaji wa mahakama ya kadhi chini ya mwamvuli wa serikali ni kwa maslahi ya Taifa zima kwa ujumla au ni kundi moja la watu bila kujali ukubwa au udogo wa kundi hilo? Ikiwa serikali itaamua kuziingiza sheria za kiislamu na kuruhusu zitumike kwa mahakama zetu zitatumikatumikaje kwani hapa pia kuna utata mtupu.

Je Serikali hiyo ivunje katiba mara ngapi?

Kuna Balozi wa VATICAN huko nchini Tanzania. Kwa msingi balozi huyo anamwakilisha kiongozi wa kiroho wa kikatoliki Pope. sasa gharama zinazotumika katika kumuhudumia balozi huyu kiulinzi kwa mujibu wa status yake , Je hio sio kutumia kodi za wananchi kwa ajili ya kundi fulani katika jamii.

Vile vile Rejea kwenyye misamaha ya kodi kwa taasisi za kidini ( rejea bajeti ya 2007/2008 na ile 2008/2009 kwene majedwali ya misamaha ya kodi taasisi za kidini pg 58 iii na pg 76 ii.

Utaona waislamu wanatumia 4% tu na nyingine zote kwa wengine. Lakini yote kwa waislamu ni sawa. sasa haitakuwa ajabu serikali kuhudumia mahakama hii ya kadhi.

Kuchanganya sheria hizi katika katiba ni kuleta confusion katika katiba
 
Serikali kumbe nayo ina udini kamtindo (indirect) japo inajifanya katiba hai iruhusu.! Watupatie Mahakama yetu nasi tuwe kamilifu katika masuala yanayotuhusu na dini yetu.
 
Je Serikali hiyo ivunje katiba mara ngapi?

Kuna Balozi wa VATICAN huko nchini Tanzania. Kwa msingi balozi huyo anamwakilisha kiongozi wa kiroho wa kikatoliki Pope. sasa gharama zinazotumika katika kumuhudumia balozi huyu kiulinzi kwa mujibu wa status yake , Je hio sio kutumia kodi za wananchi kwa ajili ya kundi fulani katika jamii.

Vile vile Rejea kwenyye misamaha ya kodi kwa taasisi za kidini ( rejea bajeti ya 2007/2008 na ile 2008/2009 kwene majedwali ya misamaha ya kodi taasisi za kidini pg 58 iii na pg 76 ii.

Utaona waislamu wanatumia 4% tu na nyingine zote kwa wengine. Lakini yote kwa waislamu ni sawa. sasa haitakuwa ajabu serikali kuhudumia mahakama hii ya kadhi.

Kuchanganya sheria hizi katika katiba ni kuleta confusion katika katiba

Barubaru

Ninachokiona hapa ni kwamba Serikali ya TZ haiwajibiki kumhudumia balozi wa nchi yeyote hapa nchini. Balozi wa Vatcan ambaye anamwakilisha Pope anahudumiwa na Vatican. Hata siku moja hauwezi kusikia bungeni bajeti ya kuhudumia balozi za mataifa ya nje. Pia kwa sheria za kimataifa office ya Ubalozi ni sawa na nchi kamili katika mahali popote duniani ilipo. HATUHUDUMII BALOZI YOYOTE KWA PESA ZA WALIPA KODI.

Kuhusu misamaha ya kodi ikiwa wameshindwa kutumia fulsa hiyo hilo ni suala lingine tofauti na halina madhara yoyote kwa katiba ya nchi bali ni walengwa kushindwa kuchangamkia fursa hiyo. Msamaha unapotolewa hailamishwi kuupokea au kuukataa bali ni hiari ya mlengwa kuuchangamkia. Hawezi kuuchangamkia basi, lakini si suala tena la kuanza kulalamika, fulani anafaidika zaidi kuliko mimi... hebu jiulize kivipi na kwa nini na mbona sio wewe?

Bado naamini kuiingiza nguzo za ibada za dini katika dola ni uvunjaji wa katiba na tunapotaka kujenga taifa imara ni lazima tulitenganishe. MAHAKAMA YA KADHI WAACHIWE NDUGU ZETU WAISLAMU WAIENDESHE NJE YA SERIKALI ILI WAWEZE KUKIDHI NGUZO ZA IMANI YAO

 
Back
Top Bottom