Juu ya OIC na Mahakama ya Kadhi

duh.. !! hongereni Waislamu kwa kupata mahakama yenu ya kadhi ambayo ilikuwa inazuiliwa na serikali ya CCM. Jambo hili ni la kujivunia kwani mmepata kile ambacho ni sehemu ya ibada yenu. Kutokana na hilo, nina uhakika serikali itaanzisha kodi maalum kwa ajili ya kufadhili mahakama hii (kama nikweli serikali itaigharimia); kodi ambayo Waislamu tu watatozwa. Hii itaondoa mgongano wa mahakama ya dini ya Kiislamu kufadhiliwa na makafir.
 
waislam wengi mtaukimbia uislam wenu huo, yangu mie macho. Nilikuwa napenda mlivyokuwa bila mahakama hii, mlikuwa huru sana na sheria za serikali zilikuwa fair tuuuu
 
Je akina Askofu Malasusa na wenzao wakihamasisha wakristo wao wasipigie kura CCM hiyo 2010 hao viongozi wa CCM watafanyaje?

Kweli sera pekee ya CCM sasa ni aidha Kuanzishwa au Kutoanzishwa Mahakama za Kadhi, hakuna sera nyinginezo...

Waislamu sasa ni kujiandaa kwa ajira za kufa mtu...
Good move let them try...thobutu watapata wapi pesa zaidi ya CCM, 2010 wakishapewa fedha watasema ni CHAGUO LA Mungu au Mtume wa mwisho who care ..money first kwa maaskofu ndugu!
 
Habari zinazoingia sasa hivi ni kuwa serikali imekubali kuanzishwa kwa mahakama za Kadhi na itazi gharamia


Kama hili kweli ,basi ni wakati mwafaka kwa mafederalist kudai serekali tatu.Serekali imekuwa accommodating kweli kweli.
 
elmo-1-1.jpg

huwezi kuwa rais wangu wewe...na zaidi ya hayo kama unavivu jinyonge!


he! acha kichekesho...ni kipi hasa cha kujivunia ...kitachofanya uonewe wivu???

mimi nafikiri kwakuwa unauelewa utaacha kufanya ubishi [au utani]..kwenye mambo ya msingi...kuliko walio mitaani bila kuwa na opportunity ya mawasiliano kama hii??

come on ...you can do better than this GAME....afteral wewe unaheshimika sana ..nategemea solid arguments kutoka kwako!

ni wazi kuwa mahakama ya kadhi haitakuwapo kikatiba na wala haitagharamiwa na serikali.....TUNAIKARIBISHA ...TUNAIUNGA MKONO!!

nadhani hakuna anayetaka pesa ya kafir kugharamia masuala matakatifu ya kidini.....kama vivyo ilivyo kwa mapagani hawaombi pesa serikalini kwenda kuabudu miungu...,mfano ndugu zetu wamasai....wanagharamia wenyewe maeneo yao ya kuabudu...na wana mahakama zao za kimila..zinaendeshwa kwa misingi ya mila[kipagani]

kudai serikali itoe kodi kugharamia mahakama za kadhi ....itasababisha ubishi ambao hautaleta tija kwa nchi kwa ujumla ...hata ukiamua kubisha ...utabisha tu kwa kuwa ...vidole ni vyako...vinavyogonga key board!!
 
mnadai mnapiga vita ufisadi lakini walioimaliza pesa za EPA na waliofikishwa mahakamani ni akina nani?
kaangalie waislam wangapi na wakristo wangapi Mahakama ya kadhi inakuja na wenye wevu wajinyinge

Mimi nadhani Waislamu hawapelekwi Mahakamani, kwani hao wa KAGODA ni wakristo?
 
duh.. !! hongereni Waislamu kwa kupata mahakama yenu ya kadhi ambayo ilikuwa inazuiliwa na serikali ya CCM. Jambo hili ni la kujivunia kwani mmepata kile ambacho ni sehemu ya ibada yenu. Kutokana na hilo, nina uhakika serikali itaanzisha kodi maalum kwa ajili ya kufadhili mahakama hii (kama nikweli serikali itaigharimia); kodi ambayo Waislamu tu watatozwa. Hii itaondoa mgongano wa mahakama ya dini ya Kiislamu kufadhiliwa na makafir.

I thought you are smart!! However you changed my mind, I'm no longer believe you.
 
Mimi nadhani Waislamu hawapelekwi Mahakamani, kwani hao wa KAGODA ni wakristo?
teh teh teh

huenda Rostam ambaye ni injinia wa wizi mkubwa ni mkristo teh teh teh

Mwaka 2006 Septemba kulikuwa na hii habari,

Tume ya Kurekebisha Sheria yakabidhiwa jukumu
*Wananchi na wadau wote watakiwa kutoa maoni
*Waziri Nagu awaomba Watanzania waache malumbano
*Aonya yanaweza kuipeleka nchi yetu mahali pabaya


Na Julius Samwel

BAADA ya malumbano ya kuanzishwa kwa mahakama ya Kadhi Mkuu Tanzania Bara kupanda moto, serikali sasa imeamua kuirejesha hoja hiyo kwa wananchi ili waijadili na kutoa maoni yao kama inafaa kuwepo au la.

Hoja ya kuanzishwa kwa mahakama hiyo imezua mvutano mkubwa baina ya viongozi na waumini wa dini za Kikristo na Kiislamu kwa miezi kadhaa sasa.

Wakati waislamu wamekuwa wakipigania kutaka serikali ianzishe mahakama hiyo kupitia sheria ya Bunge, Wakristo kwa upande wao wamekuwa wakiipinga kwa maelezo kuwa itasababisha madhara makubwa katika jamii siku zijazo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba, Dk Mary Nagu, alisema serikali imeamua kulipeleka suala hilo kwa wananchi kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria, kutokana na malumbano juu yake kuelekea katika kuleta mvutano na mpasuko miongini mwa Watanzania.

"Serikali imeiagiza Tume ya Kurekebisha Sheria kuifanyia kazi hoja hii ili baadaye tume hii iishauri serikali kuhusu ufumbuzi halisi wa suala hili kwa kuzingiatia maslahi ya taifa, historia ya nchi yetu na matakwa ya wananchi," alisema.

Alisema wakati suala hilo linafanyiwa kazi na tume ya kurekebisha sheria, wananchi wote watashirikishwa kwa uwazi mkubwa wakati wote wa mchakato wa huo.

Waziri Nagu alisema serikali itahakikisha inatumia busara na hekima katika kulishughulikia suala hilo na wadau wote watashirikishwa kutoa mawazo yao.

Aliwataka wananchi kuacha malumbano yanayoendelea kwa sasa kuhusu suala hilo na waliachie serikali ilifanyie kazi kwanza.

"Ndugu wananchi, kwa unyenyekevu mkubwa, ninawaomba kwamba malumbano yanayoendelea na yanayoelekea kuleta mvutano na mpasuko miongoni mwetu, tuyaache na kuyaacha kwa maslahi ya taifa letu, ninawaomba sana," alisema.

Alisema ni wajibu wa serikali kushughulikia mambo ambayo yanayonekana kuwa kero, likiwamo suala la kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi kama ilivyoanishwa katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2005.

Nagu alisema historia ya jambo hili inaonyesha jinsi ambavyo serikali ilivyolipokea na hatua ilizozichukua na inazoendelea kuzichukua ili kulitafuatia ufumbuzi na kwamba mchakato wa kulitafuatia ufumbuzi bado unaendelea.

Suala la kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi mkuu nchini lilianza 1999 na lilitolewa na na Waislamu kwa Rais Benjamin Mkapa katika kilele cha Sikukuu ya Idd el-fitr na Rais aliahidi kulifanyia kazi.

Baadaye suala hilo liliwasilishwa bungeni kwa mara ya kwanza mwaka 2002 kama hoja binafsi na aliyekuwa Mbunge wa Moshi Vijijini, Thomas Ngawaiya.

Baada ya kuwasilishwa kwa hoja hiyo, Spika wa Bunge, kwa kutumia kanuni za Bunge aliliwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Sheria na Katiba, ambayo iliunda kamati ndogo kwa ajili ya jambo hilo.

Nagu alisema kamati hiyo ilifanya ziara katika nchi za Kenya, Uganda, Musumbiji na Afrika Kusini ili kujifunza namna suala la kadhi linavyoshughulikiwa katika nchi hizo.

Alisema ikiwa Kenya, kamati hiyo iliambiwa kuwa mahakama ya kadhi inatambuliwa na katiba ya nchi na kwamba kuna sheria maalum iliyotungwa ambayo inampa madaraka Rais kuanzisha mahakama hiyo.

Alisema mahakama hiyo ina madaraka ya kusikiliza mashauri ya yanayohusu hadhi binafsi, ndoa, talaka na mirathi pale ambapo wahusika wote ni waislam. Hata hivyo, mahakama hiyo inafanya kazi katika maeneo ya ukanda wa Pwani.

Alisema nchi za Uganda na Msumbiji hazijaanzisha mahakama ya kadhi na kwamba Afrika Kusini inatambua ndoa za Kiislamu na wanaoshughulikia masuala hayo ni viongozi wa kidini wanaoitwa Amir.

Malumbano kuhusu kuanzishwa kwa mahakama ya kadhi yalianzishwa na maaskofu wa Kanisa Katoliki katika mkutano wao na Rais Jakaya Kikwete miezi michache iliyopita.

Katika mkutano huo, maaskofu hao walimweleza Rais kuwa wamepata taarifa za kuandaliwa kwa muswada wa kuanzisha mahakama ya kadhi na wakaiomba serikali ichukue tahadhari kubwa katika suala hilo.

Siku chache baadaye, viongozi wengine wa kanisa hilo waliitisha mkutano na waandishi wa habari, nao wakieleza kwa kina athari zinazoweza kutokea iwapo mahakama hiyo itaanzishwa kwa sheria ya Bunge, wakisema inaweza kuleta madhara makubwa dhidi ya watu wasiokuwa Waislamu.

Hata hivyo, viongozi na waumini wa dini ya Kiislamu wamekuwa wakisisitiza waachiwe hoja hiyo kwa kuwa inawahusu wao na si waumini wa dini nyingine.

Mbali na Kanisa Katoliki, Kanisa la Kiinjili la Kiluthari Tanzania (KKKT), nalo limetoa tahadhari ya kaunzishwa kwa mahakama hiyo, likisema iwapo sheria itapitishwa na Bunge, inaweza kusababisha madhara makubwa katika jamii ya Kitanzania katika siku za baadaye.
 
I thought you are smart!! However you changed my mind, I'm no longer believe you.

Hivi kumbe wewe ulikuwa "mfungwa".......stop believe in a person/people........unaweza kuja zimia..........please jaribu kuwa huru katika fikra.......you will never regret............thats my simple advise.......

NOTE: your fikras zaweza kuwa sahihi/potofu.....so be ready for challenges
 
Sijui na wengine wakitaka Canon Law ziingie kwenye makanisa na serikali itakuaje au ndio baada ya kutishiwa kutopigiwa kura?? au ndio wanasubiri muda upite
 
duh.. !! hongereni Waislamu kwa kupata mahakama yenu ya kadhi ambayo ilikuwa inazuiliwa na serikali ya CCM. Jambo hili ni la kujivunia kwani mmepata kile ambacho ni sehemu ya ibada yenu. Kutokana na hilo, nina uhakika serikali itaanzisha kodi maalum kwa ajili ya kufadhili mahakama hii (kama nikweli serikali itaigharimia); kodi ambayo Waislamu tu watatozwa. Hii itaondoa mgongano wa mahakama ya dini ya Kiislamu kufadhiliwa na makafir.
a) Tatizo ni kodi? au fedha mkuu naomba nikupe chanzo:
Kwakuwa kesi nyingi za Mirathi na ndoa za waislamu zitapungua kutoka "kwenye mahakama za maintream (taifa) then maana yake ni kwamba cost ambazo mainstream court ilikuwa inapata wanazishift very simple...yaani ni pesa ileile ambayo ingetumika kukiwa na mahakama za kawaida mkuu fahamu hilo!!! usiwe blind kwani zingeenda mahakamni kungekuwa hakuna cost?
b) Kwanini kwenye katiba?
Kwasababu ni rulings kama ruling zingine ndugu, tatizo mnafikiria mahakama hizo kama NGO fulani hivi no...lazima zipate mandate (mamlaka) ili kila atakayeamua kuhukumiwa nayo aheshimu hukumu na ifahmike hivyo kwa jamii (kuna ugumu gani hapa?)
c) Hivi nyie wakristo wa Tanzania ni wakristo sana kupita kenya, uganda etc...kiasi kwamba inakuwa ngumu muslim request...I am afraid mna wivu, chuki au choyo...shame on you (anyway mna haki ya kufikiri mpendavyo)
 
Kama kuna athari ambazo zitatokea baadae sasa wanaogopa nini? Lete hizo athari zitokee ili zitatuliwe.
 
Kama kuna athari ambazo zitatokea baadae sasa wanaogopa nini? Lete hizo athari zitokee ili zitatuliwe.
 
wizi ni tabia binafsi ya mtu ...si dini wala kabila...wala taifa!!

sasa mtafanya watu waanze kufuatilia majina ya vibaka wanaokamatwa kila siku au wazembe na wazururaji...tutafika kweli!!
 
article-1197628-059ABF54000005DC-270_468x328.jpg


Just when you thought it was all over....Federer naye anazidi kutustaajabisha kama waislam na mahakama ya kadhi
 
Sasa nisitoe pongezi zangu? au tatizo ni nini kwamba Waislamu hawakustahili mahakama yao ya kadhi?
Sasa inabidi ukashushe hilo jembe kwa mzee na wanaharakati wengine wa Waislam kwa kulima mpaka mpini umetoka na pia sasa wajiandae kwa harakati za wakristo hata mtafaruku mkubwa sana katika mambo na sekta ya sheria Tanzania. Watu wengine wanasema kuwa Mahakama zetu zitakosa watu wa kwenda kuhukumiwa na kwasababu hiyo kuna haja ya kuona ni kipi kiende kwenye hizi mahakama
 
Hivi kumbe wewe ulikuwa "mfungwa".......stop believe in a person/people........unaweza kuja zimia..........please jaribu kuwa huru katika fikra.......you will never regret............thats my simple advise.......

NOTE: your fikras zaweza kuwa sahihi/potofu.....so be ready for challenges

I'm not a someone's prisoner. However, I believe his intellectual capabilities.
 
Back
Top Bottom