Just in: UDSM wafukuzwa

Just in: UDSM wafukuzwa

Wadanganyika wameanza amka, tusichoke kupiga kelele[hata msolla akin'oka], JF imekuwa ni kisima, watu wengi wanachota humu na kuamsha isiha mitaani, mfano mzuri ni suala la Richmond hakuna magazeti yaliyochambua kama JF na watu wengi wamesoma humu.

Tuendelee kupiga kelele, huku tukiweka mkakati wa kelele hizi kusikiwa na watu wengi zaidi
 
We have to set standard! na sio fedha kuweka standard!..[/QUOTE]

Its so unfortunate but thats the case! Iam not sure how we can reverse this!
 
Mikuki,
Very unfortunate indeed!..
Yet, it is possible...'cause ignorance and selfishness has always been ahead of traits of an effective leadership. I sometimes wonder if we do have good leaders at all...
Our leaders do not have vision, structure or values and they are not accountable for anything!. They can't communicate, see forces and ecosystem, sythesize viewpoints e.t.c on the other hand we do have the society which is driven by the force of evil.... MONEY! - Again, always wonder if we were/are fit to have Independence!...

Where to start - At those schools!... next time around thing will be different. Not this generation but self-fulfilling prophesy will come from these schools. A new generation of leadership...2nd time around Independence.
I do hope this is a lesson learned!
 
Mikuki,
Very unfortunate indeed!..
Yet, it is possible...'cause ignorance and selfishness has always been ahead of traits of an effective leadership. I sometimes wonder if we do have good leaders at all...
Our leaders do not have vision, structure or values and they are not accountable for anything!. They can't communicate, see forces and ecosystem, sythesize viewpoints e.t.c on the other hand we do have the society which is driven by the force of evil.... MONEY! - Again, always wonder if we were/are fit to have Independence!...

Where to start - At those schools!... next time around thing will be different. Not this generation but self-fulfilling prophesy will come from these schools. A new generation of leadership...2nd time around Independence.
I do hope this is a lesson learned!

....its true kwamba....chungwa huzaa chungwa!

hao watoto watakaosomeshwa...kwa pesa zipi...hizi za rushwa?,halafu wanajuwa wanasomeshwa nazo....hapo ilimu yake ni kuwa nao kesho wale hiyo ili wawasomeshe wa kwao!

barabara wanazopita ni zipi?hizi mbovu,tena kwa magari ya kifahari...kwahiyo deal hapo ni lipi?...kujenga barabara akishika madaraka au kununua gari kama hilo ili atese kwenye barabara mbovu?

babaye halimi vya kutosha hilo shamba...halafu anashinda klabuni,lakini chakula kinapatikana[subsistence],sasa...deal lipi, kuchoshwa na jembe au plau...au kuburudika komoni baada ya kazi ya kivivu?

babaye hakusoma...eti aliishia la pili....ila pesa anazo,si ana biashara ya ng'ombe....sasa,deal lipi....kwenda shule au kukuza mifugo na kuiuza na bado ukawa na fedha kuliko profesa!

mamaye alikuwa akiwafahamu wazungu ma-tx,yeye anakawaita uncle...amejenga,anakausafiri kazuri...pesa hazipigi chenga.....yeye kasomeshwa lakini uzalendo ukamshinda...kitabu hakilipi ka pale jolly's!

sasa,mi ntakwambia...tukifanyakazi tulizopewa[kwani,kusawazisha barabara za udongo tunahitaji grants toka china?]au kuziomba,tena kwa ufanisi na kama za kwetu binafsi[utamshangaa mtu akiwa na chake,cha wenzake aagh!]maendeleo yatapatikana.

ndio nakubali...tuache UBINAFSI!
 
DAR si LAMU,
nadhani tunachosema ni kwamba mabadiliko yanaweza kuanzisha ktk hizi shule!...hapa hatutaki kufuga kizazi hiki ambacho kinaweza leta matokeo kama uliyoyasema. Ni kizazi ambacho wewe na mimi tumekulia.. Kwa hiyo kama kuna mabadiliko basi yaanzie katika shule zetu.... ndiko iwe mlengwa wa somo lolote tunalojadili humu.
Hao ndio watakuwa viongozi bora zaidi ikiwa mabadiliko yameanza kwao wao!
 
DAR si LAMU,
nadhani tunachosema ni kwamba mabadiliko yanaweza kuanzisha ktk hizi shule!...hapa hatutaki kufuga kizazi hiki ambacho kinaweza leta matokeo kama uliyoyasema. Ni kizazi ambacho wewe na mimi tumekulia.. Kwa hiyo kama kuna mabadiliko basi yaanzie katika shule zetu.... ndiko iwe mlengwa wa somo lolote tunalojadili humu.
Hao ndio watakuwa viongozi bora zaidi ikiwa mabadiliko yameanza kwao wao!

maana yangu ni kuwa,tutawapeleka shule nzuri,lakini kama sisi wenyewe hatujajirekebisha na kuwajibika....watatufata nyayo zetu hawa!...na ndo litakalotokea....ilimu vitendo, maalim wangu.

kama unafundishwa halafu matendo hayo hayapo,haisaidii.

tutawaze kwanza,tujiondoe hii najsi halafu ndo tusonge mbele...itakuwa vicious circle tusiporekebisha.

ushan'fahamu maalim wangu?
 
tatizo moja ni hii imani tuliyonayo kuwa kwenda shule peke yake ni suluhisho la matatizo yetu. Hivi katika serikali yetu ya sasa ni mawaziri wangapi wana shahada ya kwanza na zile za juu (kina Nchimbi et al tusiwahesabu). Je ni vitengo vingapi vinaongozwa na "wasomi"? Mwenye kusimamia Wizara ya Sayansi na Elimu ya Juu si Profesa? Je dili ni kusoma sana halafu kufuja sana au kutosoma sana lakini kuwa mwaminifu kwa mali ya umma? Au kusoma na kuwa mwaminifu? Inaonekana mara nyingi wale "tuliosoma" tukipewa nafasi ya kura na kula, basi tunakula kisomi zaidi!!
 
i) Sasa wanafunzi wazuiwa hata kukusanyika na kufanya mkutano. Wakati huohuo walimu wataenda madarasani kuhubiri uhuru wa watu kukutana na kutoa mawazo.

ii) Kituko kingine eti wanafunzi wamepewa masharti ya kutokugoma tena!

Yaani unaweza kuwa na mamlaka na moyo wa kupora haki na uhuru wa watu kwa kiasi hiki

iii) Halafu wanafunzi waliosimamishwa wamepewa barua za 2004! They couldn't be more reckless

Haya yote yanatokea katika kisima cha elimu nchini mwetu na kinafanywa na maprofesa! Wakati mwingine Nungwi yuko sawa, bora kuwa na uprofesa wa Waryoba ukafanya mambo sawa kuliko hawa jamaa zetu wa mlimani! very disgusting

Soma hapa chini-Mwananchi
________________________________

Wanafunzi wawapigwa marufuku kukutana
*Chuo chanyofoa matangazo ya wanafunzi

Na Waandishi Wetu

HALI katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam eneo la Mlimani bado si shwari baada ya mgogoro kuibuka upya baaina ya wanafunzi na uongozi kuhusiana na hatua ya wanafunzi kutaka kufanya mkutano.

Mapema jana asubuhi, wanafunzi walibandika matangazo katika maeneo mbalimbali ya chuo hicho kwa ajili ya kufanya mkutano katika Ukumbi wa Nkurumah saa saba mchana, lakini ghafla uongozi wa chuo ulinyofoa matangazo ya wanafunzi na badala yake ukaweka mengine ambayo yalipiga marufuku wanafunzi kufanya mkutano.

Hali hiyo ilidhihirika jana baada ya uongozi wa Serikali ya Wanafunzi (Daruso) kupinga amri ya utawala ya chuo na kusisitiza kwamba mkutano wao lazima ufanyike. Katika mkutano huo wanafunzi walipanga kuzungumza masuala kadha hasa ya wanafunzi 56 ambao wamezuia kurejea masomoni.


Pia walikuwa wanatarajia kuongelea hatua ya uongozi wa chuo kuwasainisha mkataba kwa wakili, ambao unawataka kutogoma tena. Katika maeneo ya chuo, wanafunzi walionekana wamejipanga katika makundi huku wakijadili masuala kadhaa yanayohusu kurejea kwao.

Kutokana na hali hiyo, hofu ya kuzuka mapambano baina ya askari wa FFU na wanafunzi imetanda miongoni mwa wanachuo wengi.

Makamu wa Rais wa Daruso, Bernadeta Rushahu, alisema baada ya kushikilia msimamo wa kufanya mkutano wao, amepokea ujumbe mfupi wa maandishi kupitia simu yake ya mkononi kutoka kwa mtu wa karibu yake serikalini kuwa askari wa FFU walikuwa njiani kwenda chuoni hapo kuwatawanya iwapo watafanya mkutano huo.

Amri hiyo ya UDSM iliyosainiwa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo hicho anayeshughulikia Taaluma, Utafiti na Ushauri, Prof. Makenya Makoko na kubandikwa katika ubao wa matangazo chuoni hapo imetolewa saa chache baada ya uongozi wa chuo kung'oa tangazo la Daruso lililokuwa limewataka wanafunzi kuhudhuria mkutano huo.

Katika hatua nyingine, barua walizoandikiwa wanafunzi 56 waliosimamishwa masomo na utawala wa Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM) zikiwataka kukutana na Kamati ya Nidhamu ya Chuo hicho leo, zimebaini utata hali inayofumbua hoja kuhusu umakini katika uendeshaji wa chuo hicho.

Gazeti hili lina nakala ya moja ya barua hizo ikionyesha kuandikwa Mei 15, 2004, huku ikibainisha makosa ya wanafunzi hao kufanywa miaka minne baadaye yaani mwaka 2007.

"Kinachoonekana hapa ni hali ya mtu kuchukua barua za huko nyuma na kisha kuzichapa bila kutazama. Hali hii ni kukosa umakini hasa kwa taasisi kubwa kama hii," alisema mmoja wa wanafunzi waliokabidhiwa barua hizo na akaongeza;

"Inaonyesha walishajiandaa kutuhukumu na kama hivi ndivyo watuambie walikuwa na maana gani kutuandikia barua kuanzia mwaka huo na kisha kuzitoa sasa. Hali hii inaonyesha maamuzi ya kukurupuka," alisema

Katika barua hizo zenye makundi kadhaa, zipo ambazo zinatolewa nakala kwa Makamu Mkuu wa Chuo, huku zingine zikiwa hazina nakala kwa yeyote.

Kuna hali ya mashinikizo ya ndani na nje ya chuo ambayo yamesababisha Kamati hii kukaa mapema. Katika migomo iliyowahi kutokea huko nyuma, Kamati hii ilikuwa ikikutana baada ya muda fulani na wanafunzi wanaosimamishwa kurejeshwa chuoni kwa masharti ambayo hutoka kwa Makamu Mkuu wa chuo.

Kukaa kwa Kamati hii mapema kuna athari mbili. Moja ni kuwatoa katika kesi wale wanaoonekana kutohusika na pia baadhi yao kubakia kafara ya mgomo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala, alikaririwa na chombo kimoja cha habari akisema kuwa wanafunzi watakaobainika kutohusika na mgomo wataachwa huru.

Katika mgomo uliofanyika Aprili 15-16, 2007, kulikuwa na baraka za kisheria na kitaratibu kufuatia Bunge la wanafunzi kuuidhinisha. Kitendo hicho kilionyesha tayari kuwepo wahusika waliouhamasisha ambao ni viongozi wa wanafunzi kutokana na nguvu za uwakilishi wa wanafunzi wenzao.

Kutokana na utaratibu huo, kila aliyehusika alifanya hivyo kufuatia kubaini uhalali wa serikali ya wanafunzi Daruso kuwa na uwezo wa kuitisha mgomo.

Kama kutakuwa na kuathiriwa kwa baadhi ya wanafunzi, huenda kukawa na hali tete zaidi chuoni hapo. Kumekuwa tayari na taarifa za fujo chuoni hapo kufuatia kusimamishwa kwa wanafunzi hao 56 huku wakitakiwa kuanza mitihani ya mwisho ya semista wiki ijayo.
 
Dar Si Lamu,
Hawa vijana waliopo Vyuoni wanalazimishwa ibada!... wanafahamu vizuri haki zao na wimbi lao la kuikataa dini hii linaanza kujitokeza tofauti na wakati mwingine wowote. Kutawadha kwetu hakuondoi ubovu wa imani yetu ambayo kila siku ndio adhana. Hawa vijana bado ni bikra wa maisha kama yetu na ndio maana nakubali kwamba fedha itaendelea kuweka standard zetu badala ya sisi watu kuweka standard.... Hili ni somo pana zaidi ya kutawadha na kutoa najisi ikiwa ndani ya ibada zetu shetani katawala mafundisho...
Sisi ambao tayari tumeisha toa bikra tunachoweza kufanya ni kuwapa moyo hawa vijana na imani zao, hatuwezi kurudisha bikra zetu wala kuwaacha wake zetu...Mmoja mmoja anaweza kuwa anasali nyumbani mwake lakini ukweli ni kwamba dini nzima ni mbovu. Ibada haikomei msikitini ama kanisani.

Mzee Mwanakijiji,
Siku zote elimu inatanguliwa na IMANI....hata katika dini zetu kwanza unatakiwa Kuamini ambayo ina misingi yake kisha Elimu ambayop inakuonyesha jinsi ya kufanya Ibada. Tupo wengi sana wenye elimu hiyo iwe ya dini ama elimu dunia isipokuwa tumekosa Imani. Katika dini hawamwogopi MUNGU na katika serikali zetu hawaogopi SHERIA...

NI bora sana kuwa na waumini wasiokuwa na elimu lakini wana imani kuliko kuwa na wasomi wasiokuwa na imani. Hii ndiyo Tanzania ya leo, Tanzania ambayo inatanguliza mahitaji yake mbele ya imani.
Kwa hiyo labda wapo waliokwisha kata tamaa ya pepo na hivyo the ONLY way for them (ubinafsi huo) ni pepo ya hapa duniani... FEDHA!
 
soko lenye deal ni mabibo hostel....upo hapo!

Ebwana Mabibo hostel si mchezo lakini.
Mi napaita mbuga ya wanyama au serengeti....maana kuna wanyama wa kila aina i.e. twiga, pundamilia, ngedere, vicheche......n.k.

Bob Mkandara ulipitia hapo?
 
fist_of_glory_icon.JPG

Hakuna kitu kinachoudhi kama ubabe wa serikali. Inasikitisha kuona kuwa katika Tanzania tunatikiwa kuinama na kupigwa bong'oa kwa vile serikali imesema jambo fulani. Katika suala hili la wanafunzi wa vyuo vikuu kufukuzwa na serikali kushikilia msimamo wake wa kuwataka walipe fedha za chuo kikuu, wakati umefika kuwaonesha serikali kuwa "nguvu iko kwa watu"!!

Nyinyi wanafunzi wa vyuo vikuu ambao mmekubali kuburuzwa na serikali na utawala wa vyuo kwa vile mnaona hamna njia nyingine nawasihi mtulizane na kutafakari upya. Mtaendelea kusukumwa sukumwa kwani baadaye wakiwaambia "tumeona mnaweza kulipa asilimia 40, sasa itabidi mlipie asilimia 60" mtakataa!! Ni lazima mchore mstari ardhini na kuiambia serikali kuwa hakisomeki kitu hadi suala hili la malipo linatafutiwa ufumbuzi once and for all!!

It is about time to put your feet on the ground and don't you dare move! Viongozi wa Daruso na wengine wenye maslahi nawashaurini mfanye kile ambacho hufanywa mara nyingi kwenye nchi za kidemokrasia, siyo maandamano na mabango bali kukaa chini (Sit Ins)

a. Wanafunzi wote rudini vyuoni kwenu kwa makundi (siyo mtu mmoja mmoja) Mkishikilia mabango yasemayo yenye kuhamasisha serikali kuwaruhusu wote kurudi shuleni na kukabili tatizo zima la kulipia elimu ya juu. Mmekubali kugawanywa, hamuwezi kufika mbali! La maana wale walioruhusiwa kurudi wagome kurudi hadi wenzao wote nao wamerudi!

b. Jifungeni vitambaa midomoni (ishara ya kunyamazishwa!). Na mnaweza kuvaa nguo nyeusi kuonesha msiba mkubwa wa elimu ya juu Tanzania.

c. Nendeni na kukaa kwenye maeneo ya vyuo (hasa kwenye milango ya madarasa) na msiondoke hadi muondolewe kwa nguvu huku kamera zinaroll na picha zinapigwa ili kuionesha serikali mbele ya umma!


Mbinu hii ya kukaa chini, imetumiwa tangu wakati wa Mahtma Gandhi, na wakati wa kutafuta haki za raia kule Marekani. NI mbinu ambayo haina uchokozaji kwa serikali. Lengo kubwa la kutumia mbinu ni hii ni kulazimisha hoja ya watu isikilizwe na kuonesha hadhara kubwa kuwa kutotumia nguvu kwaweza kujibiwa kwa matumizi ya nguvu. Nina uhakika mkiamua kukaa chini kwenye milango na viwanja vya vyuo vyetu, watawaleta polisi na kuwasomea "Riot Act".. msibabaike, wala msikimbie, kaeni chini kama watawabeba na kuwapeleka kwenye makarandinga wawabebeni... mtazijaza mahakama, na jela, lakini wakati wa kuchukua msimamo umefika... woga wenu ndio umewaponza hadi hivi sasa!!

Wanafunzi wenzenu kwenye vyuo vikuu vingi duniani ndio wamekuwa chachu ya mabadiliko.. katika kupiga vita Ubaguzi wa Rangi Afrika ya Kusini, Sera ya Utenganisho wa Rangi huko Marekani, Vita vya Vietnam, kule Ujerumani mwaka 1968 n.k

There comes a point in a relationship between the State and the People when the people have to take a stand. Hili suala la kulipia asilimia 40 ni wakati kama huo, na watanzania tuwaunge mkono kuhakikisha kuwa vijana wetu wanarudi shuleni bila kubaguliwa kwa sababu ya uwezo wao wa kifedha!! Lengo la "kukaa chini" ni kuhakikisha Msolla anaondolewa na bodi ya Mikopo inavunjwa ili apatikane Waziri mpya na Bodi mpya yenye uwezo wa kukabiliana na matatizo ya elimu ya juu na kuyatafutia ufumbuzi wa kudumu!

let there be a showdown.. yes, this looming showdown between the state and unarmed, peaceful body of students!! Let the Kikwete's government take a stand and make a choice!!

u don't know what u are talking about. Besides umesoma Detroit kijana, elimu ya juu ya bongo unaisoma kwenye IPP media tu.
 
Nyani Ngabu,
Hiyo ndio lugha ya mjini siku hizi... Ukipita sehemu utasikia Punda milia haoo!..eeh eeh bwana wee!..Twiga kakatisha.
Eeeh mwenzako mwenyeji sana mji ule!...Mabibo Hostel tena. Kumbuka nilikuwa Mtalii nimeongeza hesabu ya watalii nchini, usifanye mchezo.
 
barua za Mei 2004!!!!!

Mhh.. mlimani kuna vitukooooooo......lakini daima nitakupenda tu.

Yaani hizo barua ni zilezile walizotumia wakati wa ule mgomo wa 2004 ambao ulikuwa kuzuia kupitishwa kwa sheria ya mikopo ambayo ni mfululizo wa uchemshaji uligubika zoezi zima la utekelezaji wa dira ya elimu ya juu nchini. wakati ule mzee Luhanga alipopoa mahasira yake akayamaliza ki-aina.

Lakini hili linadhihirisha kuwa uongozi mpya mlimani ambao umejaa damu changa zenye upeo wa hali ya juu (ni vichwa kwelikweli) katika dunia yetu umerithi tabia ya kutumia mazoea badala ya mbinu endelevu kutatua matatizo lukuki yanayokikumba chuo chetu.

Well,angalao mwaka huu hawa vijana hawajabakishwa nje ya chuo hadi wakose wiki tatu ambazo zitawalazimisha kurudia mwaka hata kama watkutwa hawana hatia. Lakini kwa upande mwengine hii inaonyesha dalili ya kuwa chuo kinampango wa kuwaachia kama sio wote basi wengi wao lakini kinataka kutoka na sura kidogo.

Ni wazi kuwa kwa kutowapa muda wa kujiaanda kwa utetezi ambao huwa unahitaji si chini ya wiki mbili na pamoja na kuwapa vigezo vyote vilivyotumika kuwashitaki na kuwafikisha katika kamati hiyo ya nidhamu, basi wanafunzi wanakuwa na nafasi nzuri kisheria kuushitaki utawala wa chuo kwa kuwahukumu kinyume cha taratibu za kisheria. Hii inaweza kuwasaidia wanafunzi kwa kuwalazimisha utawala "kuwasamehe" wote watakao patikana na "hatia". Hata hivyo hali yote naweza sema ni mtego mkubwa ambao ni busara zaidi ya maguvu ndio inayohitajika.

Mkumbuke kuwa wengi wao ni wa mwaka wa tatu ambao ni wa mwisho kama sio wanafunzi wa sheria, ualimu, uhandisi na kozi zingine za miaka minne. Hivyo kupoteza mwaka mwengine mmoja ni adhabu kubwa mno kwao na kwa watanzania ambao wangelifaidika na usomi wao hata kiduchu tuu.

tanzanianjema
 
Kaka mkandara,

inaelekea upo katik stage ya kujichambua kimaisha na unajaribu kupata, kujenga ama kuimarisha dira ya maisha yako. Ama nakosea?

Ombi langu ni kuwa ujitahidi tu isije mwisho wa siku usije uka amua kujiunga na "timu ya ushindi" ili ujitengenezee "maisha yako kiulaini" kama watanzania tunavyodai. Huku nyumbani huwa tunasema kuwa "smart" ama "kukubali ukweli".

Nakutakia kila la heri kaka Tanzania yetu inahitaji sana kichwa chako.

Tanzanianjema
 
Siku zote elimu inatanguliwa na IMANI....hata katika dini zetu kwanza unatakiwa Kuamini ambayo ina misingi yake kisha Elimu ambayop inakuonyesha jinsi ya kufanya Ibada. Tupo wengi sana wenye elimu hiyo iwe ya dini ama elimu dunia isipokuwa tumekosa Imani. Katika dini hawamwogopi MUNGU na katika serikali zetu hawaogopi SHERIA...

NI bora sana kuwa na waumini wasiokuwa na elimu lakini wana imani kuliko kuwa na wasomi wasiokuwa na imani. Hii ndiyo Tanzania ya leo, Tanzania ambayo inatanguliza mahitaji yake mbele ya imani.
Kwa hiyo labda wapo waliokwisha kata tamaa ya pepo na hivyo the ONLY way for them (ubinafsi huo) ni pepo ya hapa duniani... FEDHA!

Kaka Mkandara,

Maneno mazito hayo ... heshima juu yako
 
Back
Top Bottom